Leo jioni nimepanda mwendokasi baada ya kupata breakdown lakini kilichonitokea aisee wanawake hizo nywele muwe mnaosha

Leo jioni nimepanda mwendokasi baada ya kupata breakdown lakini kilichonitokea aisee wanawake hizo nywele muwe mnaosha

Hapa leo hadi nimeshindwa kwenda bar najiuliza hii choking naitoaje maana nahisi bado ile harufu ipo puani mwangu.

Ilikua hivi, nimepata breakdown mahala nikalazimisha limp mode hadi garage ila gari imebidi kuiacha hapo. Ili kufika ninakokwenda ikabidi nichukue mwendokasi jioni hii, mule ndani palikua pamejaa lkn sikujua nikaingia tu. Mbele yangu alikua amesimama binti mmoja mfupi kiasi kaweka nywele style moja nzuri tu.

Lakini baada ya sekunde kadhaa nikaanza kuhisi hewa kuwa nzito sana kuja kugundua kumbe pua yangu imeangaliana kabisa na na kichwa cha huyo binti aliepo mbele yangu. Aisee nywele zile zilikua zinatoa harufu moja mbaya sana kama upo karibu, na ni harufu kitaalamu tunaweza iita pungent au choking smell.

Staili ya nywele nzuri ila sasa kaa karibu usikie mziki wake. Nimevumilia hadi ikabidi nishuke tu kituo kinachofuata ili nitoke nibadili usafiri.
Dungadunga kakutanana na kiama aisee🤣
 
Sasa habari ya gari yako ilipata brakedown mbona hapa haina umuhimu ? Au baada ya nywele za dada kuwa chafu ulienda kumchukulia wigi la ziada kwenye gari yako?
Basuras
 
Kwanini uangaike na mwendokasi jioni kama hiyo wakati unajua kuna lundo la watu wanatoka kwenye shughuli zao ulishindwa nini kurequest makampuni binafsi ya usafiri, itoshe kusema wewe huna hela mkuu hayo mambo ya breakdown ni stori za kufikirika tu
 
Tengeneza gari...
Ya mwendokasi utajaza threads humu kila siku
Kuna siku utapakwa ukwaju na wale watoto wa Bunge primary....
Bado kuna wamama wauza samaki wale na ndoo zao...
Hahahaa ndo narudi garage mida hii kucheki
 
Hawaoshi zinakaa kichwani wiki kadhaa wategemea nini..
Rasta mtu anakaa nazo mwenzi mzimaa na joto la dar hiloo
Huwa nadhan wanaosha kumbe wakishaweka vile hamnaga kuosha?
 
Na wewe inaonesha ni mtoto wa mama sana. Watu wametoka michakatoni na kila mtu na shughuli anayoifanya, wametoka jasho siku nzima ikiwa pamoja na kichwa, sasa mida hiyo ulitaka anukie???
Nywele zinazoshwa vizuri hazitoi harufu za ajabu. Nywele zinafukizwa na kuwekewa al oud zitaanzaje kunuka. Kuhangaika gani mpk nywele zitoe harufu. Dddaaaahhhh
 
swala la breakdown

Yaweza kuwa kamba ,ila kupanda mwendokasi siokamba
Aiseee omba yote ila sio roho au akili ya kimasikini.

Yaan ukiwa na roho ya kimasikini hata ukiona tu matajiri wanatumia hela zao unahisi wanafanya ili wajioneshe kwako kumbe hakuna mtu hata mwenye muda na wewe.

Roho ya kimasikini inafanya hata ukiona mtu anaongelea gari yake unadhan kafanya makusudi wakati gari ni kitu cha kawaida sana

Kuwa masikini ni sawa lakini kuwa na roho au akili ya kimasikini ni janga ndugu, omba sana uepushwe
 
Back
Top Bottom