Che mittoga
JF-Expert Member
- Mar 28, 2017
- 12,658
- 16,205
Sijawahi kushuhudia shabiki wa Simba mwenye uelewa mkubwa hivi hongera sana mkuu wangu [emoji120]Kuna muda tuache tu ubishi usio na maana yeyote tuongee tu sport...Sapong Jana hakufunga? hukuona movement zake mkuu? Hao Prisons unaowaona msimu uliopita achana na kushinda Simba hatukupata hata goli...kweli ni kipimo sahihi cha kuipima Yanga Leo kama ni mbovu?
Fanya hivi...Yanga ulioiona Jana inafanana na Yanga ya misimu mitatu iliyopita?
Na si kila mchezaji akicheza Yanga basi akija Simba atakua average...mkuu kuna watu wana Universal quality...unamtaja Ajib na Gadiel kama mifano na humtaji Morison huoni kama unakua biased?
Sometimes tujadili football tu...si kila kilichopo Jirani ni kibaya au kitaendelea kuwa kibaya milele...
For the first time leo Gentamycine umeongea positive kuhusu YANGA Safi sana kiongozi wangu [emoji120]Michael Sarpong
Leo niseme tu ukweli wangu nimewahi Kuwashuhudia Washambuliaji mahiri sana hapa nchini Tanzania kutokea Timu mbalimbali za Ligi Kuu yetu hii ila kwa Kumtizama Kwangu katika Mechi zake Mbili huku nami nikiwa 'namtathmini' kwa Jicho langu la Kiuchezaji Mpira hasa miaka yangu ya nyuma kama Beki wa Kulia, Namba Nne na Kiungo wa Chini ( Namba Sita ) leo nitayasema machache ila yenye Umuhimu juu ya huyu Mchezaji.
Huyu Mchezaji ana yafuatayo mazuri tupu....
Ni Mpambanaji muda wote awapo Uwanjani
Ni Mwenye Uroho na Goli ( Goal Poacher )
Ni mwenye Kujiamini muda wote
Ni mwenye Uwezo mkubwa sana wa Kumiliki mpira
Ni mwenye Kupiga Pasi zenye Tija kwa Timu
Ni mwenye Nguvu za Kutosha
Ni mwenye kutumia vizuri uwezo wake wa Kichwa na Miguu katika Kufunga
Pongezi zangu nyingi sana kwa Uongozi wa Watani zangu wakubwa Yanga SC kwa 'Kumsajili' huyu Mshambuliaji kwani pamoja na kwamba GENTAMYCINE ni Simba SC 'lia lia' kabisa Kwangu Mimi nadhani huyu Mchezaji kwa Kushiriki Kwetu Mashindano makubwa basi huenda ndiyo angetufaa kwa 100% kuliko huyu Mshambuliaji wetu Chris Mugalu tuliyemtoa nchini Zambia.
Na nawaonya mapema sana 'Mabeki' wa Timu zote za Ligi Kuu kuwa kama hawatamuundia 'Kamati' ya 'Roho Mbaya' ya 'Kumdhibiti' asilete 'Madhara' Kwao GENTAMYCINE natabiri mapema leo hii kuwa huenda Mshambuliaji huyu wa Yanga SC Michae Sarpong akaja Kufunga Goli / Bao hata 50 ( Hamsini ) kwa Msimu huu na Kuvunja hadi Rekodi inayoshikiliwa na aliyewahi kuwa Mshambuliaji wa Yanga SC Mohammed Hussein 'Mmachinga' na niseme tu kuwa hapa Yanga SC imelamba 'Dume' hasa.
Tuisila Kisinda
Kama kuna Mchezaji ambaye nina uhakika anaenda 'Kuwakera' na 'atawakera' mapema tu wana Yanga SC endapo tu 'hatobadilika' upesi ni huyu. Nikiri tu hapa kuwa huyu Tuisila Kisinda ni Bernard Morrison ndani ya Yanga SC na naweza Kudiriki kusema hapa kuwa amemzidi vitu kadhaa muhimu Mchezaji wangu wa Simba SC Bernard Morrison na hili wala halihitaji Mjadala.
Kitu pekee tu ambacho kinaenda 'Kummaliza' huyu Kijana wa Kikongo Tuisila Kisinda ni Makosa yake ya Kitoto ( Schoolboy Mistakes) pia ameshalewa 'Sifa' tayari, anataka Kuutafuta kwa haraka sana 'Ufalme' ndani ya Kikosi cha Yanga SC, ni Mchoyo ( Mbinafsi ) na kibaya zaidi anapenda mno Kucheza na Jukwaa na hata Nidhamu yake pia sidhani kama iko vyema ukianza tu Kuangalia jinsi ambavyo hupenda Kuvalia Jezi kwa Kuzikunja na huku Bukta yake nayo akiikunja ikiashiria kuwa huenda ama ana 'Ushamba' au amekulia katika 'Mazingira' ya 'Kiuswahili' sana huko Kwao Congo DR.
Kama si ule 'Upuuzi' wake alioufanya Jana pale Uwanjani nina uhakika ile Mechi Yanga SC ingeibuka 'Mshindi' tena kwa Goli / Bao nyingi sana kwani Tuisila Kisinda alikuwa anaingia kabisa katika eneo la Hatari la Wapinzani na kutakiwa kutoa tu Pasi ya mwisho kwa Wenzake ili wafunge Yeye hakuwa akifanya hivyo na badala yale alitaka asifiwe tu Yeye kama Yeye na siyo Yanga kama Timu.
Angalau sasa kwa Msimu huu Simba SC tutapata 'Upinzani' wa kweli kutoka kwa Yanga SC na tuwe nao 'Makini' kwani sasa nao ni Wazuri sana tu.
[emoji3][emoji3]Wanivumilie tu kwa 'Ukweli' wangu Mkuu.
Hahahaha nimecheka sana [emoji23][emoji23]Na wala sikufichi GENTAMYCINE nimeshawahi pia kuwa katika Kamati 'Maalum' ya 'Kuiroga' Yanga SC tena ile 'mliyopigwa' zile Goli / Bao 5 Taifa.
Achana na takataka hizo mkuuunaaribu uzi kwa kuweka kamasi zako za kishabiki,mtoa mada kaeleza mpira haswa na sio ushabiki.
Mikia kwa kuiba wachezaji,mkachukua Ajib,Gadiel,Morrison sasa mnawamezea mate kina sarpong jitu la miraba minne shingo ya kiboko hatari kichwa jiweakitoka yanga anakuja simba
Mikia kwa kuiba wachezaji,mkachukua Ajib,Gadiel,Morrison sasa mnawamezea mate kina sarpong jitu la miraba minne shingo ya kiboko hatari kichwa jiwe
Unasajili wa nini sasa?Mchezaji wa Yanga akija Simba tunamuweka bench tu kama Man City[emoji16]
Ubora upi kwa mpira huo mbovu wa Mikia fc.Kwani huyo sarponho jana hakuwepo? Hata ajib aliyokuwa yanga alikuwa mkali sana il@ huku simba amekuwa average,
Gadiel alikuwa hatari kule uto ila huku simba amekuwa average,mifano ni mingi sadney, lamine nk
Kama hujui hata ukimchukua ndemla umpeleke pale uto lazma atakuwa mfalme pale, yaani sawasawa udondoshe silva katika mkaa, pale simba sc kuna rundo la wachezaji bora.
Yanga au nyani au mbwa mnachezeshwa kwata na mbeya city mbovumbovu mkiwa home mnabebwa na refa[emoji24][emoji23]. YUbora upi kwa mpira huo mbovu wa Mikia fc.
hivi mnaposhiriki kusambaza hizi video halafu inagundulika baadae video imehaririwa au sio yeye huwa mnakumbuka kuomba radhi?
hiyo editing mkuu...hapa kimewekwa kichwa tu mwili wa mwanamke.hivi mnaposhiriki kusambaza hizi video halafu inagundulika baadae video imehaririwa au sio yeye huwa mnakumbuka kuomba radhi?
wanakosea sana. huu sio ushabiki ni kuvunjiana heshima na utu.hiyo editing mkuu...hapa kimewekwa kichwa tu mwili wa mwanamke.
Ule ni utoto mtu mwenye akili timamu hawezi kuwa na ushabiki wa kipumbavu vile.wanakosea sana. huu sio ushabiki ni kuvunjiana heshima na utu.
Kwani kuna mtu ametajwa hapo au umekuja na matokeo yako mfukoni?hivi mnaposhiriki kusambaza hizi video halafu inagundulika baadae video imehaririwa au sio yeye huwa mnakumbuka kuomba radhi?
dhamira.Kwani kuna mtu ametajwa hapo au umekuja na matokeo yako mfukoni?