Leo nimekumbuka namna mpenzi/ mama wa watoto wangu alipoanza kunishinda kipato baada ya kupata kazi kila kitu kikaparaganyika

Usiongee ukamaliza ndugu.......

Hakuna mtu anayependa maumivu na hakuna anayependa mateso

Watu wanafanyiwa unyama na watu ambao hata hawakuwategemea......

Sisi kama binadamu wenye mapungufu kuna nyakati tunateleza kimaamuzi na kujikuta kwenye mikono ya watu makatiri.........

Maisha ni safari ndefu sana na jambo la msingi ni kumuomba Mungu atuweke mbali na watu wanaoonekana wanatuchekea Hali ya kuwa wametupangia mabaya........

NB;
HUWEZI KUJUA KUWA DUNIA INA MAMBO MPAKA LIKUKUTE JAMBO........
 
Ulitakiwa usimpe talaka, ungetafuta mwanamke mdogo na mrembi kuliko yeye then akifanya maendeleo nenda mahaksmsni mgawane mali
 
Ukipigwa tukio mara moja either la wewe kupigwa au kupiga red card,likitokea next time huwezi babaika.
Ni kama mtu ambaye alisha achwa/acha na Mke/Mme siku akiishi na Mme au Mke halafu akamlete kuchi kuchi lazima kumuacha ni swala la sekunde.
Basi mm ndio nmepatwa na tukio sshv wallah ni mwezi sasa bado sijawa sawa kbs muda wote nmefura naskia kulia tu kazi sifanyi nmejaribu kusafiri nkaenda Mwanza lbd nkazubae kdg bado tu hali ya maumivu ipo.

Imebdi nirudi tu Dodoma lbd ipo siku nitakuwa sawa, Kusalitiwa hasa na mwanamke uliekuwa unamuamini na una mpa muda wako na kila kitu aseeh ni tafrani yani unaweza toa machoz na uanamume wako wote.
 
Imekuwaje mkuu? Mapenzi bhuana ukiona ni kama huyo mtu ulieko NAE ana dalili za kuja kukupa gonjwa la moyo kimbiaaaaa vunjika mguu kuliko uvunjike moyo...naogopa sana kuvunjwa moyo
 
Jipe mda mkuu utasahau, pia tafuta mdada wa kukuweka bize kidogo ila kua makini usimpe moyo
 
Imekuwaje mkuu? Mapenzi bhuana ukiona ni kama huyo mtu ulieko NAE ana dalili za kuja kukupa gonjwa la moyo kimbiaaaaa vunjika mguu kuliko uvunjike moyo...naogopa sana kuvunjwa moyo
Tumekuwa pamoja kwenye mahusiano since 2020 tumepanga kila kitu mwaka huu ndio ilkuwa namuweka ndani kwao wananijua na kwetu anajulkana.

Tumeishi vzr mno kwa muda wa 3yrs nlikuwa kama nmeoa tu maana nilkuwa nagharamia kila kitu aseeh, shida ilkuja mwez wa 4 tu hapa tumekaa akawa kapigiwa Simu nikaona anaongea kwa wasiwasi sana si ndio nkasema ngoja tuulzane akawa mbishi kusema huyo ni nani nkanyakua Simu nkatazama charting zao nkajua hawa ni wapenzi tena walioshibana kbs.

Kumuulza akawa amekiri ni mtu wake na wako wana date since 2022 aseeh nilichoka na nilishindwa nmfanye nn ,bas bana nlijikaza kiume sana ila maumivu ninayopitia hayaelezeki nlfuta nmba yke akantafuta akidai tuonane anahtaji kunpa namba ya yule jamaa tuzungumze ili nijue ndio ameachana nae ili tuendelee na mipango yetu but hapana nmeumia sana nkiishi nae sitakuwa na amani wala imani nae, aseeh sjui km hili jeraha litawahi kupona.
 
Ni suala la muda tu litapona kabisaaaaa tena utakuja kujiuliza ni mimi kweli?...
 
Pole kwa maumivu ndugu yangu.....lakini maumivu hayo ni ya muda tu...na baadae ya muda kila kitu kitabakia kuwa historia.......

Sisi sote tulishapitia purukushani za mapenzi......

Mimi niliwahi kuwa na mwanamke na date naye napanga kupeleka barua kwao na yeye namshirikisha lakini akaja akanikana kwao na kumpeleka mtu mwingine....na kibaya zaidi huyo mtu mwenyewe ni rafiki yangu kabisa..... unaweza kuona nilipitia machungu kiasi gani.......


Hayo ni moja ya mitihani kwenye maisha......piga moyo konde yatapita.....

Pole sana ndugu.....hakuna ushauri utakao kuponya zaidi ya kuwa mvumilivu
 
Heeee imagine na umeshasahau hata huyo litapita,
 
Usifikie huko mkuu
Huu ulimwengu una viumbe makatili sana mpaka unajiuliza kuwa na wao wameumbwa kwa mfano wa MUNGU au kuna version nyingine ya wanadamu........

Kuna wanadamu wenzetu wanatupitisha mapito magumu sana.....

Mapito yanayozibadilisha nyoyo zetu kutoka kwenye ubinadamu na kuuvaa unyama ili kuishi kwenye dunia wanavyotaka wao........

Unapitishwa mapito magumu mpaka unamwaga chozi bila wewe mwenyewe kujua.....mpaka mtu anakuletea leso unabaki kumshangaa kwani nani analia....

Maumivu yameupa ganzi mwili wako mpaka unapoteza ya kitu chochote mwilini mwako.....kila ukiangalia kosa lako lililofanya ustahili hiyo adhabu ya kikatili hulioni zaidi ya wema uliotamalaki uliowatendea watesi wako.......

Ukifikia hatua hiyo ni roho wa Mungu pekee ndio wa kukubadilisha na kuwa mtu wa kawaida........

Kitu ambacho watu wengi hawajui au wanachelewa kujua ni kuwa mioyo ya walimwengu imebadilika na imekuwa migumu mithili ya jiwe.......

Watu wema na wenye mioyo ya ubinadamu hawapendwi wamewekwa kwenye kundi la wajinga.....kila jema wanalofanya wanalipwa maumivu, majuto na machungu yasiosha mioyoni mwao......

Watu wema wanatumika badala ya kupendwa......unafiki umetamalaki kuliko uhalisia......

Aliyetangaza anakupenda na hawezi kuishi bila wewe ndiye anayekuwa wa kwanza kukuachia msiba wa nafsi......

Uovu umekithiri kiasi kwamba ukifanya wema au jambo jema linakuwa la kushangaza na kugonga vichwa vya habari......

Jamii iliyojaa uovu inawasukuma watu wema kwenye ukatili........

SIKU WATU WEMA WAKICHOKA KUUFANYA WEMA..... WAKICHOKA KUTUMIKA NA KUONEKANA WAJINGA....DUNIA ITAKUWA SEHEMU MBAYA SANA YA KUISHI.......
 
Mwanamke mwenyewe ni wa singida tena barmedi😁
 
Hela ndio nguvu zako ndio mamlaka yako. Ukioa mwanamke kama ana kazi mfanye mshikaji wako sana halafu tengenezen bajeti elekezi ya familia. Yaan mnaweza kusema kila mwez tuweke milion 2 chini then mwakan tununue kiwanja tujenge jumba letu la kifahar. Jitahd awe mshikaji kweli kweli na usiwe mtu wa kukariri makosa yake na muda mwingi uwe tayar kusikiliza umbea wake. Wana umbea mwingi kuwa shosti wake na wewe mpe kidogo kidogo. Utaona cku zinaenda. Tumia akili zaid ukiish na mwanamke. Zijue mapema tabia zake ukaziishi accordingly. Muombe Mungu kila wakat
 
Hayo ndio mapenzi mkuu
 
Tafsiri yake ni kuwa ili uishi na mwanamke mwenye kipato unatakiwa uishi kama anaishi na mwanamke mwenzake na sio uishi kama mume wake........
 
ndioooooo
 
So ikawaje
Mapicha picha yalivyozidi, mshikaji akafunga safari hadi huko mlimani akakaa na wazazi wa mke wake.

Wazazi baada yakuona ndoa ya mtoto wao iko matatani, wakamfungia safari pia.
Binti akaelezwa facts zakutosha, licha ya msaada mkubwa aliokuwa anawapa wazazi wake. Wale wazee wakamkumbusha alikotoka, wakajitahidi sana kushusha kiburi chake.

Walimchana kabisa kuwa akitoka hapo, ajue kila biashara inayompa pesa, itapukutika kwasababu msingi wake ni hiyo ndoa.

Mungu saidia aliwaelewa sana wazazi wake.

Pia naona ndoa nyingi zinazovunjika kwasababu ya pesa, wazazi/ndugu wa ukeni huwa wanamchango mkubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…