Leo rasmi nimeanza kutumia dawa kwa ajili ya pressure. Naanza staili mpya kuishi

Leo rasmi nimeanza kutumia dawa kwa ajili ya pressure. Naanza staili mpya kuishi

Ziroseventytwo

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
8,581
Reaction score
15,618
Nimekuwa nasumbuliwa na pressure kwa muda sasa. Leo nimepima ilikuwa 187 juu na chini 115.
Baada ya mashauriano na dr nimeamua kuanza kutumia dawa.

Nimepewa dawa za kutumia wiki moja then nirudi kucheck tena.

Ndio kwanza nina 44 yrs. Nitazimiss sana lite, na lager.
 
pole sana mkuu jitahidi kuwa makini na nini unakula katika mlo wako wa kila siku. Chakula bora ni tiba ya kwanza kabisa.
Ndio maana nikasema maanza life style mpya. Hata zile coca baridi za kushushia supu napumzika.

Pressure ikirudi nomal naanza tiz kabisa. Kukimbia na kuruka kamba. Mdogomdogo ntazoea.
 
Nimekuwa nasumbuliwa na pressure kwa muda sasa. Leo nimepima ilikuwa 187 juu na chini 115.
Baada ya mashauriano na dr nimeamua kuanza kutumia dawa. Nimepewa dawa za kutumia wiki moja then nirudi kucheck tena.
Ndio kwanza nina 44 yrs. Nitazimiss sana lite, na lager.
American College of Cardiology na European Society of Cardiology wanashauri kama ulikua mlevi basi walau unywe Bia moja kwa siku.

Na kwa wanawake walau bia mbili kwa siku na sio zaidi ya Hapo.

Tunawalazimisha wagonjwa wetu kuacha pombe ila kitafiti haizuiliwi moja kwa moja
 
karibu kwenye ulimwengu huu!u can controll it mimi yangu sasa imefika 124/80 na ilikuwa mbali 177/110 nikawa nahangaika sana nayo.pole controll ur diet.
Ahsante mkuu. Ndio safari inaanza. Nashangaaga wakati mwingine inaweza kuwa juu lakini najisikia kawaida tu. Leo nilikuwa vizuri tuila miliamua kucheck ndio nikakuta 187/115.
Ndio nikafanýa maamuzi.
 
Kwanza pole mkuu, you will be better..Nini chanzo chake au haijulikani ?
 
Ahsante mkuu. Ndio safari inaanza. Nashangaaga wakati mwingine inaweza kuwa juu lakini najisikia kawaida tu. Leo nilikuwa vizuri tuila miliamua kucheck ndio nikakuta 187/115.
Ndio nikafanýa maamuzi.
Ulikuwa na dalili zipi zilizokufanya mpaka uende kupima pressure? Si nilisikia ukishaanza dawa ndio hauwezi kuacha? Wanasema kwamba ukiwa na pressure au kisukari mtalimbo unakuwa doro?
 
Ulikuwa na dalili zipi zilizokufanya mpaka uende kupima pressure? Si nilisikia ukishaanza dawa ndio hauwezi kuacha? Wanasema kwamba ukiwa na pressure au kisukari mtalimbo unakuwa dolo?
😁😁😁😁 nilikuwa vizuri tu. Niliamua tu kwenda kucheck kwakuwa ni muda mrefu sikuwa nimecheck. Na siku zote nipo kawaida tu.

Kuhusu mtarimbo bada hiyo hali sijainona. Bed perfomance naiona kawaisa tu. Ref nipo ndani ya ndoa kwa mika 17 sasa.
 
😁😁😁😁 nilikuwa vizuri tu. Niliamua tu kwenda kucheck kwakuwa ni muda mrefu sikuwa nimecheck. Na siku zote nipo kawaida tu.
Kuhusu mtarimbo bada hiyo hali sijainona. Bed perfomance naiona kawaisa tu. Ref nipo ndani ya ndoa kwa mika 17 sasa.

Kama ni hivyo basi watu wengi wana pressure sema tu hawajapima.
 
Kwanza pole mkuu, you will be better..Nini chanzo chake au haijulikani ?
Chanzo chake kwa kweli sijui. Sababu za hili tatizo zipo nyingi. Inaweza kuwa mojawapo. Kifupi sivuti sigara, pombe nakunywa ila sio mlevi. Uzito wangu ni kg 78. Urefu ni 6 kasoro inchi kadhaa.
 
Kwa ushauri, kama ni first time kugunduliwa na tatizo yapo mambo ungestahili kuyafanyia kazi kwanza kabla ya kufikia kiwango cha Dawa, hatukatai PDx ya Dr.

Lakini jitahidi kabla hujapimwa upate nafasi ya kupumzika si kulala bali kutuliza akili kabla ya kupimwa pia pendelea upimwe nusu saa baada ya kufika kwenye taasisi husika.....

Vijana tutumie lishe kama dawa, maana kuna siku tunaweza kutumia dawa kama lishe
 
Nimekuwa nasumbuliwa na pressure kwa muda sasa. Leo nimepima ilikuwa 187 juu na chini 115.
Baada ya mashauriano na dr nimeamua kuanza kutumia dawa...
Ninashukuru Mungu nina 58 yrs sina Pressure ya aina yoyote ile na wala sina kilo nyingi mwilini mwangu. Pole sana bado kijana una Pressure?

Utatumia dawa za Hospoitali maishani mwako na pressure haito ondoka kamwe. Nitafute kwa wakati wako nipate kukutibia presha yako upate kuisikia katika Radio na TV upate kupona maradhi yako uguwa pole.
 
Yaani ulivyoenda kucheki tu ukaanza na dawa,
Laiti ungejua hizo dawa zinavyotesa ungesubiri kidogo kwa kuanza mazoezi na kubalance diet yako.

44 yrs mdogo sana kuanza hayo madawa unless iwe inakusumbua sanaaaa.

Ni vizuri kufanya hayo ukiwa umeikontrol na dawa. Maana mabadiliko yake/faida huchukua muda mrefu wakati huo athari ya presha ikiendelea kuumiza viungo vya mhusika.
 
Ulikuwa na dalili zipi zilizokufanya mpaka uende kupima pressure? Si nilisikia ukishaanza dawa ndio hauwezi kuacha? Wanasema kwamba ukiwa na pressure au kisukari mtalimbo unakuwa dolo?

Msingi wa kutokusitisha dawa kwenye presha si kwa sababu umezianza bali ni kwa sababu ni ugonjwa wa kudumu.

Kwa wachache ambao presha yao huwa haijawa kubwa sana huweza kurudi sawa kwa kurekebisha mtizamo na utaratibu mzima wa kimaisha, mambo hayo huusisha:
1: kupunguza uzito uliopindukia na kurudi sawa
2: kupunguza sana matumizi ya chumvi
3: kupunguza matumizi ya mafuta ya kuunga na yale yatokanayo na nyama.
4: kufanya mazoezi/aerobic
5: kusitisha uvutaji sigara
6: kupunguza matumizi ya pombe
7: kupunguza matumizi ya vyakula vya wanga
8: Matumizi mazuri ya vyakula vyenye asili ya protini, mboga za majani, matunda na samaki.
9: kontrol nzuri ya sukari pamoja na cholesterol.
10: matumizi mazuri ya kahawa

NB: Haya pia hutakiwa kuwa sehemu kuu ya maisha yako kwa utakapozembea presha au sukari hurejea tena. Na pia huu ndo unatakiwa kwa ujumla kuwa msingi wa maisha yetu.
 
Bibi yangu aliniambia kuna wakati inabidi upunguze kula baadhi ya vitu kabla daktari hajakukataza.

Over 40 ukianza kupunguza ulaji wa nyama na pombe na kuongeza ulaji wa mboga matunda na maji. Matokeo yake huwa ni 99% mazuri.

Kutembea kwa lisaa limoja kila siku ni tip nzuri pia.
 
Back
Top Bottom