Leon Spinks alifungwa mkono wa kushoto ili apambane na Mohammad Ali?

Leon Spinks alifungwa mkono wa kushoto ili apambane na Mohammad Ali?

Haahaaahaaaaaaa...
Hizo story zote nilikumbana nazo udogoni
mwishoni mwa miaka ya 80 nikiwa shule ya msingi.
Kuna braza wa zama hizo kitaa alikuwa akishatoka kwenye mishe zake anatukusanya 'madogo' na kuanza kutulisha hayo 'madini' pamoja na mamovi ya mbele ya kina Freddy Williamson,basi tulikuwa tunamkubali msela balaa.
Namkumbuka sana yule 'braza' nikiwa naitazama movie ya kihindi ya Sholay zama hizi za utu uzima wangu,kwani alichonisimulia yeye na nilichokuja kukiona kwenye hiyo muvi sasa dahhhh!.
Hahahaha
 


Wazee wa Zamani walikuwa waongo sana sijui kwanini, au kwa vile zamani ilikuwa ukidanganya ni ngumu MTU kutafuta ukweli ni UPI?No google, no you tube , TV changamoto, intaneti hakuna.Angalia pambano hilo


Ndiyo maana tumebaki nyuma kiuchumi sababu ya uongo uongo wa viongozi wetu tangu zamani.
 
Wazee wa Zamani waongo sana, Utasikia kina Gibson Sembuli walikuwa wakichana nyavu, Nyavu zenyewe za katani sijui zimeoza hazina ubora.Eti Kuna mchezaji gani sijui Alikuwa anapiga Kona halafu anaiwahi mwenyewe anakuja kufunga kumbe unaweza kukuta alipiga kona akawahi sekeseke golini akafunga, kingine eti Golikipa Omary Salehe Ombopa alikuwa ana uwezo wa kugeuka hewani, eti anaruka kulia akiwa hewani anajigeuza anarudi upande wa pili.

Kuna moja ya Pele kumfunga kipa aliyeshindikana, tuliambiwa Pele alilegeza kiatu akapiga mpira kiatu pia kikaenda, golikipa akafata kiatu. Kuja kushtuka ndo kufata mpira upande wa pili ila alichelewa kidogo.
 
Kuna moja ya Pele kumfunga kipa aliyeshindikana, tuliambiwa Pele alilegeza kiatu akapiga mpira kiatu pia kikaenda, golikipa akafata kiatu. Kuja kushtuka ndo kufata mpira upande wa pili ila alichelewa kidogo.
Hii story alinidanganya mwanangu mmoja hivi mwaka 91 kisa kwao kuna tv kwetu hakuna
 
Haahaaahaaaaaaa...
Hizo story zote nilikumbana nazo udogoni
mwishoni mwa miaka ya 80 nikiwa shule ya msingi.
Kuna braza wa zama hizo kitaa alikuwa akishatoka kwenye mishe zake anatukusanya 'madogo' na kuanza kutulisha hayo 'madini' pamoja na mamovi ya mbele ya kina Freddy Williamson,basi tulikuwa tunamkubali msela balaa.
Namkumbuka sana yule 'braza' nikiwa naitazama movie ya kihindi ya Sholay zama hizi za utu uzima wangu,kwani alichonisimulia yeye na nilichokuja kukiona kwenye hiyo muvi sasa dahhhh!.
Madini = matini.
 
Hahahah dah noma sana! Story ziolikuwa tamui sana hizi..Kina Tom kipese.. mashuti ya Sembuli. kipa wa simba yule ilipigwa penati akakwepa mpira maana aliona kama ni kisu kinamfuta..kufika kwa nyavu ikageuka mpira..

Kitengo noma
 
Hahahah dah noma sana! Story ziolikuwa tamui sana hizi..Kina Tom kipese.. mashuti ya Sembuli. kipa wa simba yule ilipigwa penati akakwepa mpira maana aliona kama ni kisi kinamfuta..kufika kwa nyavu ikageuka mpira..

Kitengo noma
Hahahaha kwamba wazee wa kitengo ndio waasisi wa hizo story ?

Na zote zilikua sawa dah kweli Noma
 
Ndiyo maana tumebaki nyuma kiuchumi sababu ya uongo uongo wa viongozi wetu tangu zamani.
Imagine Hashim Rungwe anasema akichaguliwa kuwa Rais ataweka mashine za kutoa ubwabwa na kuku kwenye mitaa ya jiji bure,ukiwa unapita ukiwa na njaa unajisevia [emoji1787]
 
Kuna story za kitoto mida ya miaka ya nyuma huyo mwamba alikuwa na nguvu mpaka Mohamed Ali aliomba afungwe mkono wa kushoto.

Nilisikia alifungwa mkono wa kushoto, alivyo fungua alivunja nondo ya ring.

Kuna ukweli hapa?

View attachment 1556223
Na Mohamed Ali akawa chizi kabisa kwa kukesha tu na ile Ngumi.
Dah utoto raha sana
 
Hahahaha kwamba wazee wa kitengo ndio waasisi wa hizo story ?

Na zote zilikua sawa dah kweli Noma

Haha propaganda... hiyo conclusion hiyooo..

Kuna moja hiyo Baba wa Taifa alisahau kile kifimbo chake juu ya meza. Watu kibao wakijaribu kukibeba ila walishindwa. Njemba zilizoshiba haswa zilikivuta kuki-iba ila zikafeli. Mwalimu akarudi kukichukua..ile amefika mezani tu pale akanyoosha mkono na kifimbo kikamrukia mkononi akakitia kwapani akasepa zake.. hahaha dah noma sana.
 
Imagine Hashim Rungwe anasema akichaguliwa kuwa Rais ataweka mashine za kutoa ubwabwa na kuku kwenye mitaa ya jiji bure,ukiwa unapita ukiwa na njaa unajisevia [emoji1787]
Hawa watu hatari sana uongo uongo mwingi tu,ikiisha miaka 5 wanatunga uongo mwingine.

Na wananchi wakishapewa T-shirts na Kanga wanasahau shida za miaka 5.
 
Ukipata jibu ni-tag
HIZO HADITHI ZA WATOTO TU ACHANA NAZO
wapo waliosema Nduli Idd Amini alifungwa mkono mmoja wa kulia na akapigana na Mwl Nyerere (RIP wote) vijana wanaamini hata vijiweni ukiwabishia wanaweza kukupiga
 
Back
Top Bottom