Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Nguruvi3,
Unajua mkuu wangu ktk swala hili la Utengano Wa -Zanzibar wajanja sana. wanajua sana kwamba Muungano Ukivunjika bado watapata hisani zote kutokana na kuwepo kwa EAC maana kila wanachokihitaji toka kwetu kitakuwa ktk EAC hivyo huwana sababu ya kuendelea kuwepo ktk muungano wakati Jumuiya ya EAC inawapa advantage zote wanazozihitaji toka bara. Hao Wazanzibar waliopo Bara watalindwa na ushirika huu lakini sidhani kama hii Jumuiya inaweza kulazimisha Zanzibar kupokea wageni wasiowataka...

Mkuu Mkandara

Kwa mchango huu umeonesha kuwa unaweza kufanya uchambuzi na upembuzi. Nilifikiri kuwa mwanzoni unaona moves za UAMSHO (wa-zanzibar)ni za kidini na ubaguzi. Wengine na nyimbo yao "usultani, upemba, unguja, mwalabu, gozi"

Sasa kwa uchambuzi huu unaonesha kuwa Wazanzibar wanatizama maslahi yao kinchi, na sisi wengi wetu hapa JF tunakoleza udini tu na chuki miongoni mwa watanzania.

Tokea ilipofufuliwa EAC kama tungefuata ushauri wa mwanzilishi wa Muungano mwenyewe,hakuna UAMSHO au nani angepata mwanya kuparaganya udugu,uhusiano na mshikamano wa Tanzania (Tanganyika na Zanzibar).

Mwalimu alitoa rai kuwa itakapoanzishwa tena jumuiya ya Afrika Mashariki basi Tanzania iwe na serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.

(
"Kwa kweli hata kesho Nchi za Afrika ya Masharikizikiamua kuungana, na Tanzania ikawa ni mshiriki, naamini kuwa ni rahisi zaidi kushirikisha Tanzania yenye Serikali Mbili- ya Zanzibar na ya Tanganyika ..." Uk 11 .link ya kitabu hii )

Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere)

Tanzania ingekuwa na sauti kubwa katika EAC kwa uwepo wa Tanganyika na Zanzibar kama serikali zanazojitegemea. Wabunge 9 kila mwanachama,ingefanya 18 kwa Tanzania. Influencial voting block.

Kitafute kijarida cha shirikisho ndani ya shirikisho ukipitie kwa utuo.


 
Nguruvi3,
Unajua mkuu wangu ktk swala hili la Utengano Wa -Zanzibar wajanja sana. wanajua sana kwamba Muungano Ukivunjika bado watapata hisani zote kutokana na kuwepo kwa EAC maana kila wanachokihitaji toka kwetu kitakuwa ktk EAC hivyo huwana sababu ya kuendelea kuwepo ktk muungano wakati Jumuiya ya EAC inawapa advantage zote wanazozihitaji toka bara. Hao Wazanzibar waliopo Bara watalindwa na ushirika huu lakini sidhani kama hii Jumuiya inaweza kulazimisha Zanzibar kupokea wageni wasiowataka...

Kinachonisikitisha zaidi leo hii ni kwamba sio tena swala la kero za muungano limeshika moto bali ati sisi bara ni bomba la mavi tunapeleka uchafu wetu Zanzibar kwa mtazamo wa Udini na ustaarabu wakati vitu hivi vipo Zanzibar kwa uwekezaji wa Wazanzibar na wageni (Wataliani) walowakaribisha wenyewe na kujisifia kwa Utalii. Muungano haukuanza jana mbona haya ya kuuza bwimbwi, kubuyaUnga, kamari na uchafu wote hayakuwepo miaka ya 60 na 70 hadi mwanzo wa 80. Iweje leo wawekeze wenyewe ktk kujenga guest house halafu walalamikie wageni wapangaji wanaokuja kulala?

Mkandara,

..wa-Zanzibari wanataka "mkataba" na wa-Tanganyika kabla ya kwenda huko kwenye EAC, au SADC.

..wanajua tukikutana kwenye EAC basi Mzanzibari atakuwa sawa na Mkenya,au Mganda, anapokanyaga ardhi ya Tanganyika.

..wakati wa kampeni Maalim Seif aliulizwa kama akipewa madaraka atapendekeza Zanzibar iwe na Central Bank na sarafu yao wenyewe akakataa.

..ukichunguza utaona kwamba wa-Zanzibari wanataka na dola yao lakini wakati huohuo wanataka kuendelea kutunyonya wa-Tanganyika. Ndiyo maana unasikia mapendekezo ya kuwa na "muungano wa mkataba."

..napenda kuwaonya wa-Tanganyika kwamba tusikubali mkataba wa aina yoyote ile na Zanzibar bila kushirikisha mataifa mengine.
 
Nonda Pleeease, Huyo rais wenu mwenyewe Dr. Shein ana kadi ya bara, iwe kujiandikisha kupiga kura ama account zake sasa haya ya kujenga Uzanzibar kwa uzawa kusema kweli sidhani kama tunaijenga nchi hamjawa wayahudi....
Mkandara

Hawa Nonda wako wawili?
Mmoja Mtanganyika, mmoja mzanzibar?
Au wa Tatu, Nonda mtanzania?

Huyu naye ni Mzanzibari? link https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/277714-zanzibar-is-gone.html#post4040193

Nonda huyu anaendika hapa ana "chogo" cm 20 ishirini mkuu!

Turudi kwenye mada na hoja.
 
Nonda said:
Kwa mchango huu umeonesha kuwa unaweza kufanya uchambuzi na upembuzi. Nilifikiri kuwa mwanzoni unaona moves za UAMSHO (wa-zanzibar)ni za kidini na ubaguzi. Wengine na nyimbo yao "usultani, upemba, unguja, mwalabu, gozi"
Nonda said:
Sasa kwa uchambuzi huu unaonesha kuwa Wazanzibar wanatizama maslahi yao kinchi, na sisi wengi wetu hapa JF tunakoleza udini tu na chuki miongoni mwa watanzania.

Tokea ilipofufuliwa EAC kama tungefuata ushauri wa mwanzilishi wa Muungano mwenyewe,hakuna UAMSHO au nani angepata mwanya kuparaganya udugu,uhusiano na mshikamano wa Tanzania (Tanganyika na Zanzibar).

Mwalimu alitoa rai kuwa itakapoanzishwa tena jumuiya ya Afrika Mashariki basi Tanzania iwe na serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.



Nonda,

..UAMSHO ni ma-radical na hoja zao zimejikita ktk ubaguzi,chuki,na upotoshaji.

..kuna kauli nyingi sana za upotoshaji na chuki ambazo zinatolewa ktk mihadhara yao.

..hata ukiangalia ktk Mzalendo.net utakutana na wachangiaji wengi sana wenye chuki na ubaguzi.

..kuna MODERATES ambao wanajenga zaidi hoja ya KIUCHUMI na KIJAMII wakizingatia kwamba kuna manufaa ambayo Zanzibar inayapata ktk muungano huu na wangependa waendelee kunufaika nayo.

..moderates hao ambao wanajumuisha wasomi wa Kizanzibari pamoja na jumuiya kama ZANZINET wamekuja na mapendekezo ya kuwepo kwa "MKATABA" baina ya Tanganyika na Zanzibar.

..sasa mkataba huo in essence ni mrija wa Zanzibar kuendelea kuinyonya Tanganyika kwasababu inajulikana bila shaka yoyote kwamba kwamba Tanganyika does not need Zanzibar kiuchumi wala kijamii.
 
Mkuu Mkandara,
Ni kweli kabisa wanataka wawe ndani ya EAC ili waendelee na kunufaika na Tanganyika.

Kuna matatizo mawili nayaona.
1. Kwa vile watakuwa wamewabagua Watanganyika, chuki hiyo itaendelea hadi kwa Wakenya na Waganda. Katika nchi radical kama Kenya huwezi kumzuia asifanye shughuli zake Zanzibar wakati wewe upo Mombasa.
Ni lazima wazanzibar watabaguliwa. Hakuna nchi katika EAC inayokaribiana sana kiutamaduni kama tulivyo na hapo watarudi tu.

2. Mkuu Joka kuu kasema hakuna kukubali mkataba wa aina yoyote. Hata EAC itakapokuwepo bado kila nchi itakuwa na mambo yake ambayo mengi yanaiathiri Zanzibar. Sasa hivi hakuna mkataba wala muungano, tunasubiri tu waondoke kabla ya July 1 2012 au Dec 2012!

3. Kuondoka kwa Zanzibar katika muungano katika hali ya matusi, ubaguzi na kejeli itaacha makovu ambayo yataendelea tu kuwaumiza. Unajua, kuna Wazambia wengi na wamalawi nchini, kuna Wakongo na Warundi, wote wanaishi vema kwasababu hatuna ugomvi nao. Waganda wanaishi vizuri sana hata baada ya vita kwasababu hakuna mganda aliyemkosea Mtanzania ukiacha Idd Amin na genge lake. Lakini angalia makovu ya mwaka 1977 ya Kenya. Nadiriki kusema Wakenya pengine wana wakati mgumu kuliko raia wengine kwasababu za ugomvi wa mwaka 1977 dharau na kejeli pamoja na ubaguzi.

Zanzibar kwa mwendo wa chuki watakuwa victim number 1 ndani ya EAC, hilo linakuja na litawaumiza. Litawaumiza kwasababu kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni Zanzibar haiwezi kukwepa kivuli cha Tanganyika hata siku moja. Kama itafanya hivyo ni kwa gharama kubwa sana.

Ukitaka kuona chuki ilivyotanda dhidi ya Wazanzibar ni pale jana uwanja wa taifa vijana wlipobeba bendera ya Tanganyika. Hatua inayokuja ni kuwatoa maofisini kwa mwikaju, na kisha wamachinga kusimika bendera katika maduka ya wapemba. Mzanzibar ataonekana mhalifu hata kama hana hatia na hilo naliona hata kama watu watafumba macho.
Hiki ndicho UAMSHO isichokiona na madhara yake ukisikika na lafudhi ya kizanzibar hata ndani ya EAC utakuwa victim
Time will tell

Kwa mantiki hiyo ni bora waende zao mapema sana ili watuache na matatizo yetu. Kenya ilipovunja EAC tumebaki kama taifa na sasa tupo strong pengine kuliko wakati mwingine.

LET ZANZIBAR GO!
 
Hivi bado wapo tu???? Wataondoka lini hawa zanzibar??? Kelele nyiingi lakini hawatoki
 
zanzibar2.jpg


Msitunyonye bana nyie! Msitunyonye mnatudhiri! Tuachaneni angalau tujikung’ute kidogo! Tumekuwa mafukara; mtu mwenye miaka kumi na tatu amepinda mgongo kama mtu wa miaka sabini na tano! … tunachotaka sasa hivi mtuachie tupumue!
– Mhadhara wa Uamsho Zanzibar Machi 4, 2012.


Nimekuwa mtetezi wa Muungano kiasi kwamba nimegundua nimebakia peke yangu. Wengine wanautetea Muungano kwa kutumia vitisho na wengine wanautetea kwa kutumia dharau. Binafsi ninaamini muungano unaweza kutetewa kwa hoja maridhiwa zenye kuonesha kuwa Zanzibar na wananchi wa Zanzibar wananufaika na wataendelea kunufaika zaidi katika Muungano kuliko nje ya Muungano. Kwamba hoja za kupinga muungano kwa madai kuwa Wazanzibari wanaonewa na kuwa Zanzibar inakaliwa kama koloni na Tanganyika haina mshiko, ni ya kupuuza na ina uwezo wa kuteka akili za watu wasiotaka kufikiria.


Baada ya muda mrefu kuwa mtetezi pekee wa Muungano kelele za hivi karibuni zimenibadili kabisa mawazo yangu na sasa nimekuwa na nitaendelea kushakizia muungano uvunjwe ili wale wanaoitaka Zanzibar yao wapewe na ili watu wa bara tuhangaike mambo mengine kuliko kuonekana tunawakandamiza Wazanzibari. Ile hofu ya Mwalimu kiasi cha kuachilia mambo mengi ya Zanzibar kuwa tukiungana kuwa nchi moja kamili kabisa Zanzibar watajiona wamemezwa imetimia kwani pamoja na kuwapa kila kitu Zanzibar bado wapo ambao wanaona wanamezwa!


Ni kutokana na ukweli huu kwamba hakuna kiongozi au mwanasiasa wa Tanzania awe mzee au kijana mwenye uwezo wa kuutetea Muungano kisomi na kisiasa na kuwapinga wenye hoja dhaifu ndio maana leo naendelea na hoja yangu ya kuwasaidia Wazanzibar watoke kwenye Muungano, wawe na nchi na taifa lao na zaidi ya yote waweze baada ya kutoka kwenye Muungano kuanza mahusiano mapya na bara kama nchi mbili zilizo sawa. Ninaamini tunaweza kuhusiana vizuri zaidi baada ya Zanzibar kutoka na kuwa taifa lao wenyewe kuliko ilivyo hivi sasa ambapo Muungano hauteteleki – zaidi ya kutumia vitisho vya dola.


Tunawapenda sana ndugu zetu Wazanzibari kiasi kwamba hatutaki kuwang’ang’ania. Wapo kwao wenye kutuchukia sana kiasi kwamba hawataki hata kufikiria sisi ni ndugu zao. Wanatuangalia kwa dharau na kebeki wao wakiamini utukufu wao wa “Zanzibar” isiyokuwepo ndiyo tunu waliyonayo. Ukiwaskiliza sana baadhi ya wapinga muungano kwa kweli kabisa wamejawa chuki isiyo na kifani na chuki hiyo imezaa matunda meusi katika madhihirisho ya chuki dhidi ya watu wa Bara na Wakristu.


Lakini kitu kimoja ambacho watu wengi hawataki kukifikiria ni kuwa hawa watu wanaopinga Muungano wao wanadai “nchi”. Sasa hakuna aliyewauliza kwamba mbona katiba ya Zanzibar imefanyiwa mabadiliko na kuitangaza kuwa Zanzibar ni nchi? Sasa kama tayari Zanzibar ni nchi wanachodai hawa ni nini? Haiwezekani kuwa wanachodai ni nchi kwani nchi tayari wanayo na Katiba ya Zanzibar inasema hivyo! Wanachotaka siyo nchi! Wanachotaka ni kuwa nje ya Muungano! Hivi ni vitu viwili tofauti.


Ndio maana basi katika makala ya leo nataka kuwasaidia Wazanzibari hawa na wale ambao wanaamini kuwa muungano haustahili kuteteewa kwa hoja bali kwa vioja. Pendekezo langu ni njia nyepesi za Wazanzibari kujiondoa kwenye Muungano bila kufanya maandamano, mihadhara wala kuwashtumu watu wa Tanganyika. Wazanzibari wakitaka kutoka kweli kwenye Muungano wanaweza kufanya hivyo ndani ya wiki chache tu na wakawa nchi. Nina uhakika serikali ya Muungano haitotumia nguvu kuwalazimisha kubakia! Nyerere mwenyewe alishasema kuwa hawezi kuwalazimisha Wazanzibari kubakia kwenye Muungano.


Njia ya kwanza
Njia ya kwanza na nyepesi zaidi ya kuweza kujitoa kwenye Muungano ni kwa wananchi wa Zanzibar wakiongozwa na hawa wana- uamsho wawatake watendaji wote wa Muungano wenye asili ya Zanzibar kuachia nafasi zao mara moja na kurudi Zanzibar!


Hii ni pamoja na majaji, wabunge, mawaziri, maafisa wa polisi na vyombo vingine vya usalama, na wantedaji wengine ambao wako kwenye Muungano. Badala ya kuililia Tanganyika kila kukicha kuwa inawabana mashehe wa Zanzibari wenye kuongoza vuguvugu la kutoka kwenye Muungano waanzishe mihadhara ya kuwataka Wazanzibari wenzao ambao wanatumikia Muungano waachilie nafasi hizo.


Binafsi ningependekeza kama wataniruhusu waanzishe harakati hizo ili viongozi wote hawa waachilie nafasi zo ifikapo Disemba 10, 2012. Hii ni pamoja na Makamu wa Rais Ghaib Bilal, jaji mkuu na wengine.
Hawa wote wakishawishiwa kuondoka Wazanzibari wajiandae ama kuwapatia pensheni au kuwatafutia nafasi kwenye serikali ya nchi ya Zanzibar.


Sasa hawa wote wakikubali kuondoka kwenye nafasi zao za Muungano Zanzibar itapata wataalamu wengine wengi ambao wamekuwa wakitumikia Muungano na hivyo kujiongezea hazina ya wataalamu mbalimbali. Lakini pia itafungua ajira za Watanganyika wengi ambao wangeweza kushika nafasi zinazoshikiliwa na Wazanzibari hasa kwa vile Wazanzibari hao wako kimya na hawajitokezi kuutetea Muungano ambao wanautumikia.


Pamoja na kuwataka viongozi wao na watendaji mbalimbali watoke kwenye Muungano katika harakati za mwanzo za Zanzibar kujitenga wana uamsho hawastahili kulalamikia Watanganyika. Hawahitaji kuendelea kuwaghilibu vijana wa Kizanzibari kuwa inanyonywa na sasa wanahitaji kupumua. Mashehe wa uamsho waende mbali zaidi katik akudai nchi yao. Waanze kuwahamasisha Wazanzibari walioko bara kuamua kuondoka bara na kurudi Zanzibar ili kuendesha shughuli zao huko.


Watu kama kina Bakheresa wenye biashara kubwa bara itabidi watiwe hamasa waamue kuondoka bara. Siyo hawa tu bali pia wale Wapemba na Wazanzibari waliona maeneo ya ardhi Bara. Hivi ndivyo ilivyotokea Sudan ya Kusini ambapo baada ya nchi hiyo kujitenga Wasudan ya Kusini waliokuwa wanafanya kazi Khartoum waliacha kazi zao na wengi wao wameamua kurudi kwenye nchi yao kuanza kuijenga.


Wengi tunakumbuka kuwa baada ya Rwanda chini ya Kagame kutulia kwa kiasi Wanyarwanda wengi ambao wengine waliishi kama Watanzania waliacha kazi zao na kurudi kwao Rwanda kuijenga nchi y ao. Nakumbuka baadhi ya wahadhiri kwenye taasisi mbalimbali nchini ambao tuliwadhania ni Wahaya au Waangaza walipoamua kuacha kazi zao kumbe walikuwa ni Wanyarwanda.


Hili pia litakuwa na faida kubwa sana kwa Zanzibar kwani itapata watu wengi zaidi wenye uwezo na utajiri mkubwa na vile vile itabidi iwaandalie viwanja vipya vya kilimo na makazi maana vile vya bara itabidi waviachilie kuwapisha Watanganyika ambao wanalalamikia kukosa ardhi au kupatiwa ardhi isiy nzuri. Na pia wafanyabiashara hao wa Kizanzibari watakaporudi Zanzibar na kama watataka kuja kufanya biashara Tanganyika itabidi waje kama wawekezaji na hivyo watasaidia katika ukuaji wa uchumi wa Tanganyika kama wageni wengine. Na kama watakuwa wajanja kama wageni wengine wanaweza kutengeneza mamilioni zaidi kuliko wanavyofanya sasa kama raia wa Tanzania!


Hivyo hilo ni jjambo la kwanza nawashauri wana uamsho; hamasisheni Wazanzibari waondoke Tanzania bara ili warudi Zanzibar ambako watapatiwa nafasi bora zaidi za ajira. Mtakapofanya hivyo, na watu wa Bara nao itabidi waanze kuondoka Zanzibar japo hapo nina uhakika kutakuwa na kazi kidogo. Watu wa Bara ni kina nani Zanzibar?


Njia ya pili
Kuna maneno na kauli za baadhi ya watu wachache wakizungumza kana kwamba wanawakilisha "wengi". Utasikia mtu anayepinga Muungano anasema,"Wazanzibari hatuutaki Muungano" na wakati mwingine kudai "Wazanzibari wengi hawautaki muungano". Sasa mara nyingi wanaposema "wengi" mtu wa kawaida (asiyetaka kufikiri sana) anaweza kuamini kabisa kuwa ni kweli "wengi" hawautaki Muungano.


Mfano unaotolewa siku za hivi karibuni ni "sahihi 500,000" za wanaodaiwa "Wazanzibari" wasiotaka Muungano.
Sasa kwenye mahali ambapo pana watu milioni 1.5 hivi idadi hiyo ni kubwa sana; ni theluthi moja ya watu wote wa Zanzibar. Sasa kama kweli wapo watu wengi hivi njia rahisi ya kutaka kujitoa kutoka kwenye Muungano siyo mihadhara wala hawahitaji kabisa kuwalalamikia watu wa Bara au Serikali ya Muungano.


Kwa wanaokumbuka wananchi wa Zanzibar walishinikiza vyama vyao viwili vya CCM na CUF kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na waliweza kufanya hivyo baada ya kupitisha sheria ya kura ya maoni ambayo hatimaye iliandika upya Katiba ya Zanzibar.


Wananchi wakaweza kujitokeza na kupiga kura ya maoni. Walifanya hivi bila kuomba kibali Muungano na kiasi cha kuweza kuandika kwenye Katiba Yao vitu ambavyo ni kinyume na Katiba ya Muungano.

Sasa kama waliweza kufanya hili ni kitu gani kinawashinda kutaka viongozi wao wa kisiasa kuandia sheria ya kupiga kura ya maoni kama wanautaka Muungano au la?


Kwa vile hoja ya kupinga MUungano inadaiwa inakubaliwa na watu wa vyama vyote ni wazi kuwa ni rahisi sana kwa watu wa Uamsho na Wazanzibari wengine kuhakikisha kuwa BLW linapokaa linaazimia kupitisha kura ya maoni kuhusu Muungano na kutaka sheria iletwe ya kuuliza swali la Muungano.


Swali liwe rahisi tu:
Je unataka Zanzibar ibakie kwenye Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?


a. Ndio ibakie - Ikibakia kero na matatizo ya Muungano kutatuliwa ifikapo Julai 1, 2014 na yasipotatuliwa basi kipengele cha “b” kitatimia.

b. Hapana isibakie - isipobakia Zanzibar itajitoa kwenye Muungano ifikapo Julai 1, 2014.



Ijulikane mapema kuwa ikisemwa kuwa "ndio ibakie", maana yake ni kuwa masuala ya muundo na mfumo wa Muungano yatajadiiliwa na kushughulikiwa kwenye Katiba Mpya na yatakuwa tayari kumalizwa yote ifikapo 2014. Baadhi ya watu ambao wamesoma hoja yangu hii ya pili wamedai – na mimi nikakubali – kuwa mwaka 2014 ni mbali sana. Hivyo, Wazanzibari wakitaka kujitenga wanaweza kuja na sheria kwenye kikao kijacho cha baraza la wawakilishi na ninapendekeza Mjumbe Jussa alete muswada wa swali la kura ya maoni ili Wazanzibari wafanye hima ya kujitoa kwenye Muungano.


Nina uhakika wapo Watanganyika ambao watashukuru sana kwa wao pia kupewa nafasi ya kupumua kuliko kila siku kuimbiwa “Zanzibar, Zanzibar”; kama kweli inavyosemwa Muungano ni kama koti likibana unalivua ni wazi kuwa wanaobanwa na koti hilo sasa siyo Zanzibar tena bali ni watu wa bara na sasa wameamua kuwapa Wazanzibar uwezo kamili (absolute power) kujitoa kwenye Muungano bila kufanya mihadhara mingi wala kushindana na dola.
Njia hizo hapo juu zitawasaidia Wazanzibari wanaotaka kujitoa watoke salama hasa kwa vile inaonekana hakuna Wazanzibari wanaoutaka Muungano. Watu wa Bara hatutaki kuonekana tunawang’ang’ania Wazanzibari wakati nguvu yote ya kutoka kwenye Muungano wanayo wao.


Ni matumaini yangu serikali ya Rais Kikwete ambayo imeshindwa kujenga hoja na kuwajibu kwa hoja wana uamsho haitotumia nguvu kuzima harakati za kujitoa kwenye Muungano. Tena ningependa kabisa kutoa pendekezo kwa serikali ya Muungano kukataza kabisa Polisi na JWTZ kuingilia kati mikutano ya wanauamsho na badala yake waache kazi hiyo kwa Valentia, JKU na KMKM.


Vikosi vya Muungano vikae pembeni kabisa kwani vitaonekana vinalazimisha watu kuupenda Muungano. Kama Muungano haupo moyoni, muungano hauwezi kuwepo ulimini! Kama watu wanataka mfumo wa Muungano au mambo fulani yabadilike basi tungeona juhudi za haraka za kutatua kero zote za Muungano badala ya hili la “subirini mkatoe maoni kwenye tume”. Watanzania wameshatoa maoni ya kutosha kuhusu Muungano kiasi kwamba kama CCM na serikali yake wangekuwa na uwezo wa kuyatatua basi wangekuwa wamekwishayatatua.


Nidhahiri kuwa hakuna mwenye uwezo huo na sasa kilichobakia ni sote kwa pamoja kutoka Bara tuseme nasi pasi ya shaka kuwa LET ZANZIBAR GO- Iacheni Zanzibar iende.


Itaenda wapi zaidi ya kuwa kwenye kivuli cha Tanganyika ndani au nje ya Muungano


HUU NI MWANZO WA "LET ZANZIBAR GO MOVEMENT 2012"; Kama unaunga mkono kuwaacha Wazanzibar wajitoe kwenye Muungano weka kwenye sahihi yako "I support Let Zanzibar Go Movement 2012"! Tuwasaidie waharikishe wajitoe kwani hakuna kiongozi yeyote ambaye amekuwa na uwezo wa kuutetea Muungano kwa hoja maridhawa badala ya kutumia vitisho na mikwara.

kwanza nakupongeza mleta hoja.
Pili kuna sehemu moja ambayo umeizungumza na nzito sana,hoja hio wengi wanaifahamu kuwa tayari zanzibar ishakuwa nchi kwa marekebisho yaliofanyiwa na smz,lakini ufahamu kuwa marekebisho yake kwa hatua ile imeipa zanzibar hadhi ndani ya muungano tu na sio nje ya muungano,kilicho baki kwa wazanzibari kudai zanzibar yao nje ya muungano kuwa nchi huru ni kiti cha umoja wa mataifa.
Kama unafahamu kuwa kiti ambacho kinachotumiwa kwa tanzania ndani ya UN ni kiti cha wazanzibari, kimeondolewa na kuitwa tanzania,kama haufahamu hilo nakupa kazi fanya hio kisha rudi hapa tena.
Kwa kumalizia jamuhuri ya watu wa zanzibar itarudishwa na wazanzibari wenyewe tena wananchi na sio viongozi kwa kikatiba viongizi wote hadi znz wapeapishwa kuulinda muungano kwa gharama zote.
 
Mkuu Mkandara,
Ni kweli kabisa wanataka wawe ndani ya EAC ili waendelee na kunufaika na Tanganyika.

Kuna matatizo mawili nayaona.
1. Kwa vile watakuwa wamewabagua Watanganyika, chuki hiyo itaendelea hadi kwa Wakenya na Waganda. Katika nchi radical kama Kenya huwezi kumzuia asifanye shughuli zake Zanzibar wakati wewe upo Mombasa.
Ni lazima wazanzibar watabaguliwa. Hakuna nchi katika EAC inayokaribiana sana kiutamaduni kama tulivyo na hapo watarudi tu.

2. Mkuu Joka kuu kasema hakuna kukubali mkataba wa aina yoyote. Hata EAC itakapokuwepo bado kila nchi itakuwa na mambo yake ambayo mengi yanaiathiri Zanzibar. Sasa hivi hakuna mkataba wala muungano, tunasubiri tu waondoke kabla ya July 1 2012 au Dec 2012!

3. Kuondoka kwa Zanzibar katika muungano katika hali ya matusi, ubaguzi na kejeli itaacha makovu ambayo yataendelea tu kuwaumiza. Unajua, kuna Wazambia wengi na wamalawi nchini, kuna Wakongo na Warundi, wote wanaishi vema kwasababu hatuna ugomvi nao. Waganda wanaishi vizuri sana hata baada ya vita kwasababu hakuna mganda aliyemkosea Mtanzania ukiacha Idd Amin na genge lake. Lakini angalia makovu ya mwaka 1977 ya Kenya. Nadiriki kusema Wakenya pengine wana wakati mgumu kuliko raia wengine kwasababu za ugomvi wa mwaka 1977 dharau na kejeli pamoja na ubaguzi.

Zanzibar kwa mwendo wa chuki watakuwa victim number 1 ndani ya EAC, hilo linakuja na litawaumiza. Litawaumiza kwasababu kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni Zanzibar haiwezi kukwepa kivuli cha Tanganyika hata siku moja. Kama itafanya hivyo ni kwa gharama kubwa sana.

Ukitaka kuona chuki ilivyotanda dhidi ya Wazanzibar ni pale jana uwanja wa taifa vijana wlipobeba bendera ya Tanganyika. Hatua inayokuja ni kuwatoa maofisini kwa mwikaju, na kisha wamachinga kusimika bendera katika maduka ya wapemba. Mzanzibar ataonekana mhalifu hata kama hana hatia na hilo naliona hata kama watu watafumba macho.
Hiki ndicho UAMSHO isichokiona na madhara yake ukisikika na lafudhi ya kizanzibar hata ndani ya EAC utakuwa victim
Time will tell

Kwa mantiki hiyo ni bora waende zao mapema sana ili watuache na matatizo yetu. Kenya ilipovunja EAC tumebaki kama taifa na sasa tupo strong pengine kuliko wakati mwingine.

LET ZANZIBAR GO!

Nasikitika na wewe umeingika katika kundi la wapotoshaji!

Kwa nini ifikie hiyo hatua ya kuachana kwa chuki? kwani wanachokitaka wazanzibar ni nini? si kura ya maoni itakayoamua mustakabari wa wazanzibar! Mbona vitisho vingi sana?
 
Naunga mkono hoja ila kinachonisumbua ni kuwa ujue kuna wazanzibar wengi wanafanya biashara bara na wengine wengi wameajiriwa bara kwenye sector binafsi na wengine bado wako vyuoni ukiongea nao hawa yaani hawana majibu ya kuridhia hawaupingi wala kuunga mkono sasa sijui wanahofu kuwa muda si mrefu watakosa keki huku bara? halafu ukweli usiopingika nimeishi zanzibar siku 40 nilikuwa kwenye training u kweli usiopingika kabisa mimi nilikuwa silijui hili kuna ubaguzi kati ya unguja na pemba halafu na umri wangu wote nilikuwa sijui pemba ni wapi na unguja ni wapi. niliona kabisa mtu wa unguja anamdharau mtu wa pemba na nilipouliza wanasema kuwa watu wa pemba hawafanyi kazi eti kukaa kwenye kahawa hapo nikagundua kitu kuwa kumbe kuna tatizo hapo nimesoma kwenye blog ya zanzibar kuwa watu wabara tunania mbaya ya kuwatengenisha waunguja na wapemba eti hakuna kitu kama hicho lakini ukweli kutoka mioyoni mwao wanalijua hilo kuwa kuna ubaguzi kati yao na kuna mzanzibari mmoja alijibu kuhusu hilo akasema ni kweli sisi waunguja tuna ubaguzi na hata kule pemba kuna barabara za kupitisha gutta tu gari hazipiti, alishambuliwa sana na waunguja kisa kasema ukweli. ILA CHA MSINGI TUWAACHE WAENDE WAKAJENGE NCHI YAO NA TENA WATAKUWA NDANI YA EAC. kwa walioa tanzania bara wanabahati watabaki il sidhani kwa walioa zanzibar watabaki huko maana walivyowabaguzi ni balaa.
 
Mkuu Mkandara,
Ni kweli kabisa wanataka wawe ndani ya EAC ili waendelee na kunufaika na Tanganyika.

Kuna matatizo mawili nayaona.
1. Kwa vile watakuwa wamewabagua Watanganyika, chuki hiyo itaendelea hadi kwa Wakenya na Waganda. Katika nchi radical kama Kenya huwezi kumzuia asifanye shughuli zake Zanzibar wakati wewe upo Mombasa.
Ni lazima wazanzibar watabaguliwa. Hakuna nchi katika EAC inayokaribiana sana kiutamaduni kama tulivyo na hapo watarudi tu.

2. Mkuu Joka kuu kasema hakuna kukubali mkataba wa aina yoyote. Hata EAC itakapokuwepo bado kila nchi itakuwa na mambo yake ambayo mengi yanaiathiri Zanzibar. Sasa hivi hakuna mkataba wala muungano, tunasubiri tu waondoke kabla ya July 1 2012 au Dec 2012!

3. Kuondoka kwa Zanzibar katika muungano katika hali ya matusi, ubaguzi na kejeli itaacha makovu ambayo yataendelea tu kuwaumiza. Unajua, kuna Wazambia wengi na wamalawi nchini, kuna Wakongo na Warundi, wote wanaishi vema kwasababu hatuna ugomvi nao. Waganda wanaishi vizuri sana hata baada ya vita kwasababu hakuna mganda aliyemkosea Mtanzania ukiacha Idd Amin na genge lake. Lakini angalia makovu ya mwaka 1977 ya Kenya. Nadiriki kusema Wakenya pengine wana wakati mgumu kuliko raia wengine kwasababu za ugomvi wa mwaka 1977 dharau na kejeli pamoja na ubaguzi.

Zanzibar kwa mwendo wa chuki watakuwa victim number 1 ndani ya EAC, hilo linakuja na litawaumiza. Litawaumiza kwasababu kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni Zanzibar haiwezi kukwepa kivuli cha Tanganyika hata siku moja. Kama itafanya hivyo ni kwa gharama kubwa sana.

Ukitaka kuona chuki ilivyotanda dhidi ya Wazanzibar ni pale jana uwanja wa taifa vijana wlipobeba bendera ya Tanganyika. Hatua inayokuja ni kuwatoa maofisini kwa mwikaju, na kisha wamachinga kusimika bendera katika maduka ya wapemba. Mzanzibar ataonekana mhalifu hata kama hana hatia na hilo naliona hata kama watu watafumba macho.
Hiki ndicho UAMSHO isichokiona na madhara yake ukisikika na lafudhi ya kizanzibar hata ndani ya EAC utakuwa victim
Time will tell

Kwa mantiki hiyo ni bora waende zao mapema sana ili watuache na matatizo yetu. Kenya ilipovunja EAC tumebaki kama taifa na sasa tupo strong pengine kuliko wakati mwingine.

LET ZANZIBAR GO!

ndugu yangu.
Naona ume base sana upande wako eti ubaguzi,nakuuliza hivi ushawahi kuwa zanziba uchaguzi wa 95,2000,maandamano ya 2001,2005,kama ulikuwepo miaka hio yote,zanzibar ilikuwa na utawala wa kibaguzi,wazanzibari wananyanyaswa kwa kutumia jeshi la muungano,watu waliuwawa hapa zanzibar,walibakwa,kuna walikuwa walemavu,kuna walikuwa mayatima,yote hayo kulinda ccm madarakani na ndio muungano wenyewe,hivi kwa aliki yako kama ni wewe mzanzibari utakuwa na imani na mtu kutoka bara ? Nakupa mfano ,ingekuwa nyinyi wazanzibar na sisa watanyanyika tukawafanyia haya yote mungekubali ? Tungeacha masualaya kiuchumi ? Hapa zanzibar sijaona police wala jwtz mtu mwenye asili ya kiarabu kwa nini ? Mpaka uwonekane una asili ya bara,iwe baba au mama au babu? Kwa nini ? Ubaguzi wa kutosha kwa muungano juu ya wazanzibari,hata mwalimu nyerere alishatamka kuwa angekuwa na uwezo angeviondowa visiwa vyetu,why ? Chuki na roho mbaya. Ukweli huo.
 


Nonda,

..UAMSHO ni ma-radical na hoja zao zimejikita ktk ubaguzi,chuki,na upotoshaji.

..kuna kauli nyingi sana za upotoshaji na chuki ambazo zinatolewa ktk mihadhara yao.

..hata ukiangalia ktk Mzalendo.net utakutana na wachangiaji wengi sana wenye chuki na ubaguzi. ........

JokaKuu

Sauti za Zanzibar zinapokuja na malalamiko yao , tunawapuuza au huwa tunawapiga-date.
Ile sauti moja inayozimwa, baada ya muda inaibuka nyengine kali zaidi. Tunawa-radicalise! na kuwabeza.

Hoja yao ya msingi UAMSHO ni kura ya maoni juu ya kuutaka au kuukataa Muungano. Kuna kikundi ambacho kinataka kuwa-sabotage waonekane ni wahuni, ma-radical, wabaguzi kwa kuwabambikizia "uchomaji wa makanisa" ili kuua dai lao. Leo hakuna anaezungumzia au kuunga mkono kura ya maoni badala yake tunazungumzia, UAMSHO wadini, ma-radical, wanataka usultani, wanatuita machogo nk.

Unapoau hoja yao ya msingi katika upeo huu wa kuwadharau au kuwabambika majina ni kuwa hushughulikii kero wanayoiona, au tatizo wanaloliona bali tunawajengea jina ambalo jamii wakilisikia watawatoa maanani. Kwa tabia hii ni sawa na kufanya usafi nyumbani halafu unaweka uchafu chini ya zulia kuna siku, maradhi yatatuumbua.

Link https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/277714-zanzibar-is-gone-2.html#post4041423


Chuki niisomayo ktk Mzalendo.net naisoma pia ktk JF

afrodenzi, ni kweli unachosema kwasababu tumejitolea sana katika muungano........

Wametupiga marufuku mambo mengi ingawa wao ni wanufaika. Hakuna wanachodai na hawajapewa lakini bado wanalalamika.
........
Lakini la muhimu zaidi tutapata nafasi ya kushughulikia matatizo yetu wenyewe.
Tunayo mengi na muda wa kubembeleza mtoto mgongoni hatuna.
Kwanini tusifikirie matatizo ya watu milioni 40, tubaki tunacheza mdumange na watu laki tisa na nusu

LET ZBAR GO

Hawa UAMSHO (wazanzibari),watu laki tisa wanajaribu kutuonesha njia ya kupata nafasi na muda wa kushughulikia matakwa na matatizo ya watu milioni 40 lakini sisi au miongoni mwetu tunalazimisha, tunang'ang'ana na kuwang'ang'ania watu laki tisa na ushee!

Ni uendawazimu au ni ukichaa? 48 miaka haijatosha kucheza hide and seek? Na kuacha kila upande unalalama?

Ni wazi kama Matola na Mungi wanavyoona kuwa Watanganyika wakitaka within 24 hrs Muungano uvunjike/ uvunjwe basi hakuna wa kuzuia hilo lisitokee. Au tunasubiri ije kutoana pua na macho kwanza ndio lifanyike hilo?
Links 1. https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...tta-nyerere-na-wa-tz-bara-12.html#post3071074
link 2. https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/277714-zanzibar-is-gone.html#post4040193


Faida na hasara ya kuvunjika kwa muungano, kila upande utapiga mahesabu yake baadae lakini kwa hivi Muungano unavyoendeshwa na kulelewa utatuletea majanga.
 
ile chilisosi inakuchengua bado ??
Kamwewe mie nashangaa kuona bado hamjajitenga. mkitaka kujitenga si mumuambie shein tu atangaze zanzibar nchi hata kesho??. mie sioni sababu ya maandamano, mihadhara ,na kelele nyingine nyingi, nyie si muanze tuuuu!
 
kamwewe mie nashangaa kuona bado hamjajitenga. Mkitaka kujitenga si mumuambie shein tu atangaze zanzibar nchi hata kesho??. Mie sioni sababu ya maandamano, mihadhara ,na kelele nyingine nyingi, nyie si muanze tuuuu!

tumekosa mboga ya chilisosi
 
JokaKuu

Sauti za Zanzibar zinapokuja na malalamiko yao , tunawapuuza au huwa tunawapiga-date.
Ile sauti moja inayozimwa, baada ya muda inaibuka nyengine kali zaidi. Tunawa-radicalise! na kuwabeza.

Hoja yao ya msingi UAMSHO ni kura ya maoni juu ya kuutaka au kuukataa Muungano. Kuna kikundi ambacho kinataka kuwa-sabotage waonekane ni wahuni, ma-radical, wabaguzi kwa kuwabambikizia "uchomaji wa makanisa" ili kuua dai lao. Leo hakuna anaezungumzia au kuunga mkono kura ya maoni badala yake tunazungumzia, UAMSHO wadini, ma-radical, wanataka usultani, wanatuita machogo nk.

Unapoau hoja yao ya msingi katika upeo huu wa kuwadharau au kuwabambika majina ni kuwa hushughulikii kero wanayoiona, au tatizo wanaloliona bali tunawajengea jina ambalo jamii wakilisikia watawatoa maanani. Kwa tabia hii ni sawa na kufanya usafi nyumbani halafu unaweka uchafu chini ya zulia kuna siku, maradhi yatatuumbua.
Chuki niisomayo ktk Mzalendo.net naisoma pia ktk JF
Nguruvi3: Hawa UAMSHO (wazanzibari),watu laki tisa wanajaribu kutuonesha njia ya kupata nafasi na muda wa kushughulikia matakwa na matatizo ya watu milioni 40 lakini sisi au miongoni mwetu tunalazimisha, tunang'ang'ana na kuwang'ang'ania watu laki tisa na ushee!
Ni uendawazimu au ni ukichaa? 48 miaka haijatosha kucheza hide and seek? Na kuacha kila upande unalalama?
Ni wazi kama Matola na Mungi wanavyoona kuwa Watanganyika wakitaka within 24 hrs Muungano uvunjike/ uvunjwe basi hakuna wa kuzuia hilo lisitokee. Au tunasubiri ije kutoana pua na macho kwanza ndio lifanyike hilo?
Faida na hasara ya kuvunjika kwa muungano, kila upande utapiga mahesabu yake baadae lakini kwa hivi Muungano unavyoendeshwa na kulelewa utatuletea majanga.
Sisi hatulalamika kuwa ni koloni, hatujawahi kuchoma moto watu na mali zao. Kama hivyo ndivyo una 'advocate' nachelea kusema ni hatari.
Kama unadhani UAMSHO style ni njia muafaka basi hebu sema uone balaa! mungu pishilia mbali!!!!!!

Pili, hakuna jina lingine la UAMSHO kama si boko haram, alshabaab kwasababu matendo yao kauli zao, ubaguzi wao na mtazamo wao ni phoyocopy. Anayekataa hili akamuone Psychiatrician

Tatu, JF hakuna chuki kuna darasa la kuwasadia njia rahisi ya kuondoka katika muungano.
Chuki za kuchoma wanadamu na majengo moto zinaanza kujitokeza kwa majibu kama yale uwanja wa taifa.
Ni vema mkawahi maana chuki hizi zikichukua sura ya UAMSHO, hakika wazazibar wataumia

Tunatoa nafasi Zanzibar wajitoe, vinginevyo hatunyanyua hata njiti ya kibiri au usufi kumwadhibu Mzanzibar.
Tutawaondoa kwa njia moja tu! Serikali moja ya JMT
 
sisi hatulalamika kuwa ni koloni, hatujawahi kuchoma moto watu na mali zao. Kama hivyo ndivyo una 'advocate' nachelea kusema ni hatari.
Kama unadhani uamsho style ni njia muafaka basi hebu sema uone balaa! Mungu pishilia mbali!!!!!!

Pili, hakuna jina lingine la uamsho kama si boko haram, alshabaab kwasababu matendo yao kauli zao, ubaguzi wao na mtazamo wao ni phoyocopy. Anayekataa hili akamuone psychiatrician

tatu, jf hakuna chuki kuna darasa la kuwasadia njia rahisi ya kuondoka katika muungano.
Chuki za kuchoma wanadamu na majengo moto zinaanza kujitokeza kwa majibu kama yale uwanja wa taifa.
Ni vema mkawahi maana chuki hizi zikichukua sura ya uamsho, hakika wazazibar wataumia

tunatoa nafasi zanzibar wajitoe, vinginevyo hatunyanyua hata njiti ya kibiri au usufi kumwadhibu mzanzibar.
Tutawaondoa kwa njia moja tu! Serikali moja ya jmt

yaelekea wewe ni polisi zaidi ya wale polisi waliowakamata waliochoma makanisa.
Tafadhali nenda kawakamate hao uamsho na uiambie mahakama iwaachie wale watu 30 walioshutumiwa kufanya hizo shutuma unazowatumia uwamsho
 
Sisi hatulalamika kuwa ni koloni, hatujawahi kuchoma moto watu na mali zao. ....
Pili, hakuna jina lingine la UAMSHO kama si boko haram, alshabaab kwasababu matendo yao kauli zao, ubaguzi wao na mtazamo wao ni phoyocopy. Anayekataa hili akamuone Psychiatrician

Tatu, JF hakuna chuki .........

Tutawaondoa kwa njia moja tu! Serikali moja ya JMT

Kwa hiyo, ile kuchoma moto makanisa ni mbinu ya kuleta serikali moja?

Janja paka, panya ............

Pacha wako pia nasema hili. link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...tta-nyerere-na-wa-tz-bara-10.html#post3070223

Ofisi ya huyo Psychiatian iko wapi? Ulishafika huko?

Unafanya kazi nzuri mkuu Nguruvi3 ya kubuni majina.

Kwa hiyo, UAMSHO ni Al qaeda? au Boko haram?

Maumivu ya kichwa, huanza pole pole.....tumia HEDEX!
 
Me naona kuna sababu za kiusalama zilizofichika hapa...TSSA wanafahamu, na hii visit ya kiongozi wa Iran ktk kipindi crucial ina ring a bell kichwani, otherwise zanzibar haina economic advantages kwa bara zaidi ya hizo za kiusalama, nionavyo mimi
 
Back
Top Bottom