Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Hakuna haja ya kufanya mambo nusu nusu, BLM waandae muswada wa kujitenga ASP, na mchakato uanze 'yesterday' ili by 1/1/2013 Zanzibar or niseme Jamhuri ya Zanzibar iwe huru. Hili litakuwa jambo la heri kabisa.

unamuambia nani humu JF ??? Waonaje ukaweka muhadhara au ukawaona wenyewe BLM
 
Jana nimesikia BLW wakisema wanataka mgao wa 4.5 uongozwe hadi 11%. Wanasema sasa hivi wanapata mgao wa 7% kutoka hazina Dar ambayo ni Hazina ya Muungano a.k.a Tanganyika.
Hawajasema wao wanachangia nini katika hilo pato la taifa ili wadai zaidi au hata kupata tu!

BLW wanadai wapewe fungu la elimu ya juu kutoka hazina ya muungano. Hapa ndipo nasema Wazanzibar ni wanafiki sana. Siku zote wanasema Tanganyika imeongeza MAMBO 11 ya muungano hadi kufikia 22. Wanasahau kuwa elimu ya juu haikuwa suala la muungano, lakini wanapotaka pesa za elimu ya juu wanasema ni haki yao!

Hakuna hata mmoja aliyesimama na kusema hataki muungano, sasa hapa ndipo nachanganyikiwa wale wazanzibar 'wengi' wanawakilishwa na nani? UAMSHO au BLW , na je BLW ni vibaraka na wasaliti kama viongozi wa muungano kutoka Zanzibar?

Nguruvi3,

..kuhusu mgao wa mapato, kuna afisa wa TRA Zanzibar amedai kwamba makusanyo yote ya TRA Zanzibar hubakia huko huko. Hakuna wanachowasilisha makao makuu Dar-Es-Salaam. sasa mpaka hapo najiuliza, Zanzibar inachangia kiasi gani ktk shughuli za muungano?

..Pia huu mgao tunaowapa wa asilimia 4.5, na sasa unasema asilimia 7, unapatikana vipi? Mbona unapingana na vigezo vya mchango wao, na ukubwa wa uchumi wa Zanzibar?

..Kutokana na Zanzibar kushindwa kuchangia mfuko wa muungano na hivyo kuwa mzigo kwa wa-Tanganyika nadhani hakuna haja ya kuwa na muungano, au hata "mkataba". Suluhisho la kuduma la matatizo ktk mahusiano baina ya Tanganyika na Zanzibar ni nchi hizi mbili kuwa wanachama wa East Africa community au SADC.
 
Nguruvi3,..kuhusu mgao wa mapato, kuna afisa wa TRA Zanzibar amedai kwamba makusanyo yote ya TRA Zanzibar hubakia huko huko. Hakuna wanachowasilisha makao makuu Dar-Es-Salaam. sasa mpaka hapo najiuliza, Zanzibar inachangia kiasi gani ktk shughuli za muungano?

..Pia huu mgao tunaowapa wa asilimia 4.5, na sasa unasema asilimia 7, unapatikana vipi? Mbona unapingana na vigezo vya mchango wao, na ukubwa wa uchumi wa Zanzibar?

..Kutokana na Zanzibar kushindwa kuchangia mfuko wa muungano na hivyo kuwa mzigo kwa wa-Tanganyika nadhani hakuna haja ya kuwa na muungano, au hata "mkataba". Suluhisho la kuduma la matatizo ktk mahusiano baina ya Tanganyika na Zanzibar ni nchi hizi mbili kuwa wanachama wa East Africa community au SADC.
Joka Kuu, huu mgao wa asilimia 7 ni zawadi. Bajeti yao ya mwaka huu ni bilioni 307 matumizi, na bilioni 341 fedha za maendeleo kwa ujumla wa bilioni 600.

Utaona kuwa fedha zao za maendeleo ni nyingi kuliko za matumizi kwasababu
1. Hawana bajeti ya vyombo vya ulinzi na usalama
2. Hawana bajeti ya kuhudumia viongozi wao wastaafu kwa kada zote
3. Hawana bajeti ya mishahara kwasababu inatoka hazina Dar es salaam
4. Hawana bajeti ya elimu ya juu kwasababu watoto wao wanasoma kwa pesa za Muungano
5. Hawana bajeti ya wabunge wao walioko Dodoma
6. Hawana bajeti ya nishati kama umeme serikalini hadi majumbani, si Ikulu wala BLW wantumia umeme wa bureee!

Kinachosikitisha sana ni kuwa makusanyo ya TRA kwa sehemu kama wilaya ya Ilala ni makubwa kuliko Zanzibar.
Ukipata maksanyo ya soko la kariakoo kwa mwaka na kwa mwezi ni makubwa kuliko Zanzibar, sasa TRA wanakusanya nini cha kuleta katika muungano? Jibu ni kuwa Zanzibar inachangia 0 na inapata asilimia 7

Deni la umeme la bilioni 50 ambayo ni asilimia karibu 8 ya bajeti yao nzima ndiyo maana hawataki kulipa kwasababu hiyo ni sehemu kubwa sana ya bajeti yao. Anayelipa ni Mtanganyika!

Ikifika hapo ndipo wanaposema tuwe na serikali 3, mkataba au tuwe na uhusiano maalumu kwasababu tu Mtanganyika abebe mzigo wa hawa jamaa wasioisha kulalamika. Muungano ni kwa ajili yao siyo sisi na sisi hatuna cha kupoteza hata kimoja wakiondoka.

Utashangaa wanaposema tumeungana kama nchi mbili na kwahiyo kila kitu kiwe pasu pasu.
Wamegombea tume ya katiba wawe nusu kwa nusu lakini ona wanachangia nini katika muungano, hakuna, I mean ZERO.
Sasa kama wanadhani tumeungana nchi mbili nini mchango wao basi !

Kuna umuhimu wa kuwaeleza viongozi wetu hasa wabunge kusimamia masilahi yetu.
Tuwaunge UAMSHO mkono na jitihada zao ili tutue hili zigo la misumari
LET ZANZIBAR GO! Jamani hatuna cha kupoteza waacheni waende hata kesho, kwanini tubebe mzigo na matusi ikiwa ni pamoja na kumwgiwa petroli na vibiriti kwa hisani zetu?
 
Nguruvi3,

..mimi ningependekeza kwa kuanzia wajumbe wa tume ya katiba toka Zanzibar walipwe posho zao na SMZ.

..kwanini mabilioni ya pesa za wa-Tanganyika yaende kulipa wajumbe wa tume ambao hawako pale kutetea maslahi ya wa-Tanganyika??

..suala la Zanzibar kudai nusu ya wajumbe wa tume ya katiba lilipaswa kujibiwa kwamba SMZ watawajibika kulipia nusu ya gharama za posho ya wajumbe wa tume ya katiba.

..kwenye bunge la muungano kuna wabunge toka Zanzibar wanalipwa[according to uamsho] mil 12 kila mwezi kutokana na kodi za wa-Tanganyika.

..umefika wakati sasa wanasheria wakae pembeni ktk kuujadili muungano huu. nafasi hiyo wachukue wachumi na wataalamu wa fedha. u will never hear Prof.Shivji and the likes discussing jinsi muungano unavyowadhulumu kiuchumi wa-Tanganyika. kila siku ni makelele ya hati ya muungano, hati ya muungano...

..LET ZANZIBAR GO!!!
 
na waende wakapewe misaada na ndugu zao wa Oman!lkn for sure watatukumbuka na ukalimu wetu!!
not ukalimu bali ni ukarimu, anyway,,,,,,, sisi hatutakukumbukeni kwa lolote bali kwa maovu na ufisadi na unyonyaji wa visiwa vidogo vya zanzibar,
mimamo wetu uko palepale tunataka zanzibar huru tumechoka na ukoloni wa watanganyika. TUACHWE TUPUMUWEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE
 
Joka Kuu, huu mgao wa asilimia 7 ni zawadi. Bajeti yao ya mwaka huu ni bilioni 307 matumizi, na bilioni 341 fedha za maendeleo kwa ujumla wa bilioni 600.

Utaona kuwa fedha zao za maendeleo ni nyingi kuliko za matumizi kwasababu
1. Hawana bajeti ya vyombo vya ulinzi na usalama
2. Hawana bajeti ya kuhudumia viongozi wao wastaafu kwa kada zote
3. Hawana bajeti ya mishahara kwasababu inatoka hazina Dar es salaam
4. Hawana bajeti ya elimu ya juu kwasababu watoto wao wanasoma kwa pesa za Muungano
5. Hawana bajeti ya wabunge wao walioko Dodoma
6. Hawana bajeti ya nishati kama umeme serikalini hadi majumbani, si Ikulu wala BLW wantumia umeme wa bureee!

Kuna umuhimu wa kuwaeleza viongozi wetu hasa wabunge kusimamia masilahi yetu.
Tuwaunge UAMSHO mkono na jitihada zao ili tutue hili zigo la misumari
LET ZANZIBAR GO! Jamani hatuna cha kupoteza waacheni waende hata kesho, kwanini tubebe mzigo na matusi ikiwa ni pamoja na kumwgiwa petroli na vibiriti kwa hisani zetu?

Kwa nini hatudai Tanganyika yetu kama hawa jamaa wanafaidi kutunyonya?

Hivi hatuwezi kuwafundisha njia rahisi watanganyika kama tulivyowaeleza njia rahisi wazanzibari kutoka katika Muungano?

Tuanzishe Rebirth of Tanganyika movement 2012.

Mwanakijiji, Nguvuri3, Mag3,FJM, Mkandara, Zinadine, Chilisosi, Raj Patel, JokaKuu,Taso,Masopakyindi, na kila menye uchungu na mama Tanganyika, sasa kampeni ihamie katika kudai Tanganyika.
Mtu laki 1.5 inayotoka Zanzibar iliyopo Tanganyika tunaweza kuipa uraia wa Tanganyika na hii kelele ya" tunanyonywa" itakuwa tumeipatia dawa yake.

It is so simple! Tunaogopa nini? Sasa ni wakati wa ukweli na uwazi.

Ni kwa watanganyika kuidai Tanganyika tu ndio njia rahisi ya kutatua kero hii ya Muungano.

Kwa nini hatuidai Tanganyika? Tunaogopa kuwa land-locked country? Mbona Ethiopia, Zambia zimeweza?

Kwa nini tunaendelea na Muungano unaotutia hasara?

Let Tanganyika be born again! Let us have our Tanganyika back! Let us reclaim her! Can't we?
 
Kwa nini hatudai Tanganyika yetu kama hawa jamaa wanafaidi kutunyonya?

Hivi hatuwezi kuwafundisha njia rahisi watanganyika kama tulivyowaeleza njia rahisi wazanzibari kutoka katika Muungano?

Tuanzishe Rebirth of Tanganyika movement 2012.

Mwanakijiji, Nguvuri3, Mag3,FJM, Mkandara, Zinadine, Chilisosi, Raj Patel, JokaKuu,Taso,Masopakyindi, na kila menye uchungu na mama Tanganyika, sasa kampeni ihamie katika kudai Tanganyika.
Mtu laki 1.5 inayotoka Zanzibar iliyopo Tanganyika tunaweza kuipa uraia wa Tanganyika na hii kelele ya" tunanyonywa" itakuwa tumeipatia dawa yake.

It is so simple! Tunaogopa nini? Sasa ni wakati wa ukweli na uwazi.

Ni kwa watanganyika kuidai Tanganyika tu ndio njia rahisi ya kutatua kero hii ya Muungano.

Kwa nini hatuidai Tanganyika? Tunaogopa kuwa land-locked country? Mbona Ethiopia, Zambia zimeweza?

Kwa nini tunaendelea na Muungano unaotutia hasara?

Let Tanganyika be born again! Let us have our Tanganyika back! Let us reclaim her! Can't we?

Nonda,

..zingatia hapo kwenye RED.

..Tanganyika iliyoungana na Zanzibar haikuwa landlocked.

..sasa tutakuwa vipi landlocked ikiwa muungano utavunjika??

NB:

..the 10 mile coastal strip, pamoja na eneo la Mombasa, Sultani waliokuwa madarakani waliyauza na kutia pesa mfukoni.
 
Nguruvi3,

..kwanini mabilioni ya pesa za wa-Tanganyika yaende kulipa wajumbe wa tume ambao hawako pale kutetea maslahi ya wa-Tanganyika??

..suala la Zanzibar kudai nusu ya wajumbe wa tume ya katiba lilipaswa kujibiwa kwamba SMZ watawajibika kulipia nusu ya gharama za posho ya wajumbe wa tume ya katiba.

..kwenye bunge la muungano kuna wabunge toka Zanzibar wanalipwa[according to uamsho] mil 12 kila mwezi kutokana na kodi za wa-Tanganyika.

..umefika wakati sasa wanasheria wakae pembeni ktk kuujadili muungano huu. nafasi hiyo wachukue wachumi na wataalamu wa fedha. u will never hear Prof.Shivji and the likes discussing jinsi muungano unavyowadhulumu kiuchumi wa-Tanganyika. kila siku ni makelele ya hati ya muungano, hati ya muungano...

..LET ZANZIBAR GO!!!

JokaKuu
Kama Tanganyika haipo, watanganyika wametoka wapi?

Hili ndio kosa tunalolifanya!
Tudai kwanza Tanganyika iwepo, hapo itakuwa rahisi kushughulikia mambo haya. Leo Tanganyika inasemwa haipo, halafu utasikia serikali ya Zanzibar inajadiliana na serikali ya Muungano. Tuache utani huu.

Hivi tunaufahamu huu Muungano? Mimi naona huu Muungano ni kama monster, wa-tanganyika(wabara) wanalalama kunyonywa na Muungano, wazanzibari wanalalama kunyonywa na Muungano?

Kwa nini kuendelea na huu mzimu?

Kwa nini kauli za mtu laki 9.5 zinasikika zinapiga kelele kuwa hazitaki Muungano lakini sauti 40 milioni zimebana kimya? Kama vile ziko katika usingizi ile ya samaki. Mtu 40 milioni zimelala fofofo? Mtu milioni 40 hazijitambui?
Mtu milioni 40 haziwezi kuhoji mazingaombwe haya(muungano)?

We are vely zaifu! Mnyika ameliona hili.

Tanganyika first, Mazingaombwe(muungano) basi! Enough is enough!
 
Kwa nini hatudai Tanganyika yetu kama hawa jamaa wanafaidi kutunyonya?

Hivi hatuwezi kuwafundisha njia rahisi watanganyika kama tulivyowaeleza njia rahisi wazanzibari kutoka katika Muungano?

Tuanzishe Rebirth of Tanganyika movement 2012.

Mwanakijiji, Nguvuri3, Mag3,FJM, Mkandara, Zinadine, Chilisosi, Raj Patel, JokaKuu,Taso,Masopakyindi, na kila menye uchungu na mama Tanganyika, sasa kampeni ihamie katika kudai Tanganyika.
Mtu laki 1.5 inayotoka Zanzibar iliyopo Tanganyika tunaweza kuipa uraia wa Tanganyika na hii kelele ya" tunanyonywa" itakuwa tumeipatia dawa yake.

It is so simple! Tunaogopa nini? Sasa ni wakati wa ukweli na uwazi.

Ni kwa watanganyika kuidai Tanganyika tu ndio njia rahisi ya kutatua kero hii ya Muungano.

Kwa nini hatuidai Tanganyika? Tunaogopa kuwa land-locked country? Mbona Ethiopia, Zambia zimeweza?

Kwa nini tunaendelea na Muungano unaotutia hasara?

Let Tanganyika be born again! Let us have our Tanganyika back! Let us reclaim her! Can't we?

Bw, Nonda

Muungano una maana kubwa zaidi kwa hao watu uliyowataja hapo (kwenye red) . Kwao wao wananufaika moja kwa moja kwa sababu ni watumishi wa kitengo cha propaganda cha Muungano. Wanalipwa mishahara kufaya shughuli zao. Vile vile ni sehemu ya ibada kwa Bwana Mungu wao (Nyerere) .
 
Nonda,

..zingatia hapo kwenye RED.

..Tanganyika iliyoungana na Zanzibar haikuwa landlocked.

..sasa tutakuwa vipi landlocked ikiwa muungano utavunjika??

NB:

..the 10 mile coastal strip, pamoja na eneo la Mombasa, Sultani waliokuwa madarakani waliyauza na kutia pesa mfukoni.
Nilifikiri tunaogopa kivuli cha maili 10?
Sasa tunaogopa nini kudai kuirudisha Tanganyika?
Kwa nini tunapigizana kelele na mtu laki 9.5?

Nani mwenye nguvu na sauti baina ya mtu laki 9.5 na mtu 40 milioni?

Kama mtu 40 milioni zinataka Tanganyika back nani atazuia hili?
Mimi mpaka mida hii nashindwa kuelewa kwa nini tumeweka mkazo kuwa wazanzibari wajikate wakati tutakapoirudisha Tanganyika tutakuwa tumemaliza mazingaombwe ya muungano.

Vitu/mambo yatakuwa wazi, wala mtu hatahitaji darubini, mipaka, mamlaka, sheria zitakuwa wazi. Sio kama sasa mkorogo tu, tirigivyogo, shagala bagala!

Muungano, mambo ya Muungano, mambo ya Zanzibar, mambo ya bara(Tanganyika), Zanzibar ipo, Tanganyika haipo, Serikali ya Zanzibar ipo, serikali ya muungano ipo, serikali ya mambo ya Tanganyika haipo.
Serikali ya muungano ndio hiyo hiyo wakala wa serikali ya Tanganyika, mgongano wa kimaslahi na ulalamishi.

Tanzania nchi moja lakini kila upande una mambo yake halafu kuna mambo ya pamoja! Unaelewa chochote hapo?

Upande mmoja unadai unachangia/unatoa kila kitu na upande mwengine "unapokea" unaopokea mgao unadai unanyonywa! Unaelewa chochote hapo?

Ya nini mazingaombwe yote haya? Hatujachoka nayo?

Miaka 48 tunajitahidi uongeza mambo ya muungano ili Tanzania iwe nchi moja na pia tunataka kuleta serikali moja. Kwa miaka isiyopungua 46 upande mmoja unalia unafanyiwa rafu. Tunajifanya kuziba masikio,

Mpaka mida hii kuna mambo hayajawa ya muungano, yet tunasema Tanzania ni nchi moja. Kweli Tanzania ni mazingaombwe tu, usanii.

Warioba kapewa hadidu rejea za katiba mpya, juzi amesema watu wajadili wanavyotaka,waseme watakayo kuhusu Muungano. Huyu mzee anatania watu 40milioni na laki 9.5?

Mtu 40 milioni zitamke ,tunataka Tanganyika yetu, zimwambie Warioba achukue bara yake, arudishe Tanganyika yetu!
Mzee wa mazingaombwe anapewa jukumu la kukusanya maoni yetu.
Utani kwenye vitu vya msingi utatumaliza.
 
JokaKuu
Kama Tanganyika haipo, watanganyika wametoka wapi?

Hili ndio kosa tunalolifanya!
Tudai kwanza Tanganyika iwepo, hapo itakuwa rahisi kushughulikia mambo haya. Leo Tanganyika inasemwa haipo, halafu utasikia serikali ya Zanzibar inajadiliana na serikali ya Muungano. Tuache utani huu.

Hivi tunaufahamu huu Muungano? Mimi naona huu Muungano ni kama monster, wa-tanganyika(wabara) wanalalama kunyonywa na Muungano, wazanzibari wanalalama kunyonywa na Muungano?

Kwa nini kuendelea na huu mzimu?

Kwa nini kauli za mtu laki 9.5 zinasikika zinapiga kelele kuwa hazitaki Muungano lakini sauti 40 milioni zimebana kimya? Kama vile ziko katika usingizi ile ya samaki. Mtu 40 milioni zimelala fofofo? Mtu milioni 40 hazijitambui?
Mtu milioni 40 haziwezi kuhoji mazingaombwe haya(muungano)?

We are vely zaifu! Mnyika ameliona hili.

Tanganyika first, Mazingaombwe(muungano) basi! Enough is enough!

Nonda,

..Tanganyika ipo, na wa-Tanganyika wapo. Kilichotokea, na kinachowanganya watu akili, ni kwamba shughuli za utawala ktk Tanganyika zilikasimiwa kwa serikali ya muungano mwaka 1964.

..Inawezekana kabisa kujadili haki za wa-Tanganyika ndani ya muungano huu. Wahusika wanajitia vichwa maji tu lakini sina shaka kabisa kwamba hilo linawezekana.

..Wazanzibari wanatunyonya wa-Tanganyika ndani ya muungano huu. Tunawalipia umeme. Mishahara ya watumishi inalipwa na wa-Tanganyika. Jambo lolote lile la muungano wanaochangia ni wa-Tanganyika wakati wa-Zanzibari hawatoi chochote. Hebu wewe niambie ni lini umesikia SMZ imetoa fedha fulani kwenye suala lisilohusiana na yale yaliyobainishwa kuwa ni masuala ya muungano kuwasaidia wa-Tanganyika.

..Kwanini wa-Tanganyika hawalalamiki?? Kwanza ni kwasababu tunaamini ktk UNDUGU na UMOJA WA WAAFRIKA na ktk makuzi yetu tumefundishwa kwamba muungano ni jambo jema. Pili, Zanzibar ni sehemu ndogo sana kulinganisha na Tanganyika. Hicho tunachotoa kwa wa-Zanzibari hakina athari kubwa kwetu sisi.

..Unakosea kusema kwamba wa-Tanganyika hatujitambui. wa-Tanganyika tunajitambua. Tunaamini ktk UMOJA wa Waafrika. Kwa wa-Tanganyika heshima na umoja wa wa-Afrika ni juu ya u-Tanganyika wetu. Kutokana na imani hiyo ndiyo maana ilikuwa rahisi kwetu ku-embrase utaifa mpya wa TANZANIA.

..Muungano kama muungano siyo mazingaombwe. Tell me what is wrong kwa wa-Tanganyika na wa-Zanzibar kuwa kitu kimoja. Kwa mtizamo wangu unayoyaita mazingaombwe yanaletwa na tamaa za wanasiasa.

..Tunachokataa sisi siyo muungano bali ubaguzi na chuki zinaopandikizwa ktk muungano huu. Hali hiyo imeachwa iendelee kwa upande wa Zanzibar kwa muda mrefu. Tumefika mahali tumekata tamaa kwamba kuna uwezekano wa kuwa na muungano unaozingatia udugu, heshima, haki, na usawa, baina ya wa-Tanganyika na wa-Zanzibar, ktk kizazi chetu.

..WE TRIED, BUT CAME UP SHORT.

..LET ZANZIBAR GO!!

NB:

..Hata kama wa-Tanganyika ktk wingi wetu tutapinga muungano, sitapendelea tuige attitudes na matendo ya UAMSHO. Let us oppose this union for the right reasons na siyo kupandikiza chuki, ubaguzi, udini, urongo, na uzushi.

..Pia siamini ktk kuwafukuza au kuwasumbua wa-Zanzibar walioko ktk ardhi ya Tanganyika. I am on the record hapa JF kupendekeza kwamba wa-Zanzibar walioko Tanganyika wapewe nafasi ya kuwa wakazi wa kudumu kwa kipindi maalum wakisubiri kuamua wanataka kuwa raia wa upande gani -- Tanganyika au Zanzibar.
 
Nonda said:
Nilifikiri tunaogopa kivuli cha maili 10?
Sasa tunaogopa nini kudai kuirudisha Tanganyika?
Kwa nini tunapigizana kelele na mtu laki 9.5?

Nonda,

..Hivi unafikiri ni nani huku Tanganyika anajua masuala ya hizo maili 10 unazozingumzia?

..Hata wana uamsho wanajua kwamba it is futile kwa wao kuanza kuhangaika na hizo maili 10. Shekhe wa uamsho aliulizwa suala hilo na kusema bayana kwamba nia yao ni Zanzibar ile iliyokuwa admitted kwenye UN mwaka 63.

..Kwanza sidhani kama kuna legal grounds kwa Zanzibar kuidai pwani ya Tanganyika na Kenya. Zaidi sidhani kama ni busara kwa utawala wowote ule wa Zanzibar kuleta chokochoko na kuwa na mahusiano mabaya na majirani zake.
 
Back
Top Bottom