Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mama husna kiboko yako๐ ๐
Leo ntalala mbavu zinauma, hiyo scene yโa mzenga shuhulini nimekuonea had huruma ๐คฃ๐คฃ๐คฃKwanza rangi yenyewe ilikuwa mbaya, nyeupe na dhambarau. Alafu nimelivaa juu ya t shirt yangu. Hata kwa bunduki wasingeweza kunipiga picha
Ndio uachane na mabonge mfyuuu ๐คฃ๐คฃ๐คฃSasa je, unamkwepa tu. Zipo sehemu za kupatia ajali ila sio chumbani ๐
batiki la CCM unalijua?Batiki wanavaa ACT Wazalendo, sio Mimi aisee. Ntakukimbia ๐ ๐
Ila wewe jamaa kila unapoenda unaharibu tu, ingawa nikushukuru mana nilikuwa najiona malaya ila kwa hii story mm ni mtu poa tu.Portion 11.
.... Ikabidi nirudi mpaka pale mlangoni, nikajaribu kuufungua nikakuta umefungwa kwa ndani. Nikamwambia aufungue, akagoma. Badala yake akaendelea kuniongelesha kwa sauti ya juu:
Mama Husna: "Kipi kimekurudisha? Au ndio umeijia mivuzi yako?. Unamfuko nikuwekee?"
Nilijaribu sana kumsihi lakini wapi, ndio kwanza alizidi kupayuka:
Mama Husna: "Umezoea kuvua chupi za watoto wenzako na kuondoka ukijisikia, sasa safari hii utasimulia"
Japo ilikuwa usiku, ila nilikuwa naona aibu kuliko kawaida. Wale majirani zake nao walikuwa busy madirishani kuniangalia Mimi. Waliacha hata shughuli zao, maana walizima taa za ndani, wakajikusanya madirishani. Nikahofia watu wanaweza kujaa alaf nikazidi kujichoresha, nikaamua kuondoka.
Akili ikawa inanizunguka, yule mwanamke kwa akili yake ilivyo, anaweza kunifanyia jambo baya. Na kwa upande wangu nilivyomweupe sasa, kwa Mungu sipo na kwa waganga sijawahi kwenda.
Ila nikajisemea ngoja apoe, kisha nitaongea nae vizuri ili tuweke mambo sawa. Maana sikujua amedharia kufanya nini na yale mavuzi, atanifanya nimpende yeye tu? Itakuwaje akinifanya nisidindishe?. Zilivyokuja fikra za kutodindisha hapo ndio akili ikazidi kukosa utulivu kabisa. Kesho yake nilivyoenda job, kuna jamaa mmoja anaitwa Jumanne ikabidi nimuulize vitu kadhaa kuhusu hiyo issue. Sikutaka kumwambia kama ni Mimi ndio napitia hiyo hali, bali nilitolea kama mfano japo ndani kwa ndani nilijua kuwa sio mfano:
Analyse: "Hivi broh Juma, mtu anaweza kukuroga kwa kutumia nywele zako?"
Juma: "Vipi tena mdogo wangu, asubuhi yote hii unaanza kuzungumzia ushirikina?"
Analyse: "Wewe nijibu, shida iko wapi ukijibu?"
Juma: "Nywele na kucha ndio zenyewe mdogo wangu, tena anaweza kukupoteza kabisa kwenye ramani. Unavyoonaga kwenye bongo movie waganga wanamwambia mtu, leta kucha na nywele zake unahisigi masihara? Japo wale wanaigiza, ila uhalisia nao upo hivyo hivyo"
Analyse: "Sasa nywele zinawezaje kumfanya mtu arogwe? Hizo ni imani tu"
Juma (akacheka sana): "Mdogo wangu, nywele zako ni wewe. Yani mtu akiamua kuzitumia vibaya anakuharibia kabisa. Tena mfano zikiwa za kwapa au mavuzi, hapo ndio kabisaa hakuna mganga atakayeweza kukuagua"
Wakati Mimi na Juma tunaongea, tulikuwa tumesimama pembeni ya gari la ofisi. Ila baada ya kuniambia kauli ile, tumbo lilinikata ghafla alafu nikahisi kama miguu inakosa nguvu. Nikachuchumaa chini.
Juma: "Mdogo wangu vipi, unaumwa au?"
Analyse: "Tokea jana tumbo linasumbua, linakata na kutulia"
Juma: "Omba ruhusa ukapumzike mdogo wangu, hii ofisi sio yako mpaka ufie hapa"
Analyse: "Hapana broh, nitamudu tu"
Juma: "Mdogo wangu, sisi masikini likizo yetu ni mpaka tuumwe, likizo yako imefika nenda kaongee na HR upate hata siku mbili za kupumzika"
Nikajaribu kujitetea pale, jamaa ikabidi aniitikie tu. Story zikaisha, tukaendelea na mambo mengine, lakini sikuwa na furaha kabisa. Wenzangu wakawa wanahisi sababu naumwa, ila ukweli nilikuwa naujua mwenyewe. Mida ya mchana Mama Husna akaniambia niende kwake, nikamwambia nitaenda jioni maana bado nipo job, ila akanikazia kuwa kama siendi mchana, basi na jioni asinione.
Ikabidi niende kuomba ruhusa job kuwa najisikia vibaya, hapakuwa na complications maana sikuwa nimeajiriwa, hivyo nikapewa ruhusa ya siku 3. Nikaondoka. Nilipitia kwanza home, nikaoga na kubadili nguo kisha ndio nikaamua kwenda kwa Mama Husna.
Nilikuwa naona aibu jinsi majirani zake watakavyoniona. Ila sikuwa na namna, nikafika mpaka pale ila mlango nikakuta umefungwa. Nikajaribu kumpigia simu, akaniambia amepata dharura ametoka, ila mpaka saa kumi atakuwa amesharudi.
Nikaondoka eneo lile. Njia nzima nafikiria najitoa vipi kwa huyu Mama bila kupata madhara, maana kwa akili zake nilijua hashindwi kunifanyia jambo. Sikurudi ghetto, nilienda sehemu nikakaa natafakari mambo yangu. Kuna wazo likanijia na Mimi nitafute mganga kabla mambo hayajawa magumu. Nikakumbuka kuna matangazo nilishawahi kuyaona kwenye nguzo, kwavile sina mganga ninayemjua, basi acha nianzie hapo.
Mara nyingi nilikuwa nikipita, hayo matangazo kwa siku ningeweza kuyaona hata mara 10, ila ajabu siku hiyo sikuwa nayaona kabisa. Ili nilazimu kupanda gari mpaka maeneo ya buguruni, pale ndio nikabahatika kuyaona. Nika nakili zile namba, kisha nikaondoka.
Kumbe wakati naziandika japo ilikuwa kwa kuibia ibia, wadau wa ofisini walikuwa site maeneo yale, wakaniona. Hawakunishtua, walinipiga picha tu, alaf wakaniacha. Inaonekana nilivyotoka lile eneo, wakaenda kuangalia nilichokuwa na copy, ndio wakakuta namba ya mganga. Siku niliyorudi kazini walinicheka sana wale jamaa. Na mpaka natoka kwenye ile ofisi, walikuwa hawaachi kunitania. Haya yote nilikuja kuyajua baadae kabisa.
Nilivyoondoka eneo lile (buguruni), wakati narudi home nikaona tangazo la mganga mwingine, nalo nikachukua maana niliamini waganga wanatofautiana uwezo. Mbele tena nikaona la mwingine. Yani kiufupi mpaka nafika home, nikawa na list ya majina kama Saba au nane. Kuna wawili niliona matangazo yao sehemu nyingi zaidi, nikawa nahisi hao ndio watakuwa wazuri zaidi. Nikajisemea mmoja kati yao ndio atanipambania.
Mpaka naingia ghetto kabisa mida ya saa kumi na mbili jioni, Mama Husna hakuwa amenicheki kabisa. Nikiwa ghetto pale nikawa najiuliza kati ya wale waganga wawili, nani niende nae?. Wakati naendelea na ilo zoezi, kwenye radio nako kikaingia kipindi cha dini yakaanza mahubiri. Wazo jipya likaja, au niokoke?. Nikamsikiliza kwa makini sana yule mchungaji, nikajawa na faraja kiasi kwamba nikaona Mama Husna haniwezi, na nikadhamiria kesho yake inabidi niende kanisani.
Yani kwa hali niliyokuwa nayo, kila wazo lililokuwa linakuja, nililipokea. Nilikuwa nachanganyikiwa huku najiona aisee. Yani pole pole.
Wakati najiandaa kulala,Mama Husna ndio akanipigia na kuniambia niende kwake. Muda ilikuwa kama saa tatu usiku hivi, tulibishana kidogo ila mwishowe nikaenda. Sikuwahi kulala kwake kabla ya hiyo siku, ila nikalazimika kulala. Asubuhi wakati anaondoka kwenda kwenye mishe mishe zake, na Mimi ndio nikaondoka.
Kuna muda nikawa najiambia haya yote yametokana na kujifanya nayajua mapenzi na kuyaendekeza. Wenzangu wanaovua na kugonga direct, hawakutani na hizi mambo. Yani kwa hizo siku mbili, hali yangu ilibadilika kabisa maana hata hamu ya kula ilikata. Na mtu angeniona, nikimwambia naumwa anakubali. Na hata usiku niliolala kwa Mama Husna, nae nilimwambia akakubali. Maana shoo ilikuwa ya kufosi, na hata muonekano wangu haukuwa sawa.
Muda wa ruhusa niliopewa ulivyoisha, nikarudi kazini. Kazi nikaiona chungu, maana wadau waliponiona tu wakaanza kunicheka. Wanacheka bila kujua kinachowachekesha. Na hata nilipowauliza, nilijibiwa kwa mafumbo tu.
Mapenzi kwa Mama Husna ni kama yalikata kabisa, tena ghafla. Ila niliendelea kuwa nae sababu ya uoga tu. Leo hii nikikumbuka jinsi ilivyokuwa, hadi najishangaa kwamba nilikuwa naogopa nini haswa?
Nilikuja kuokolewa na Juma. Wik end moja nikiwa zangu ghetto sijatoka siku nzima, mida ya jioni akanipigia simu:
Juma: "Mdogo wangu uko wapi?"
Analyse: "Nipo ghetto kaka, vipi?"
Juma: "Nataka tuongee, nakuja maeneo hayo"
Analyse: "Poa kaka tukutane wapi?"
Juma: "Nisubirie hapo hapo nakuja, ningependa tuongelee kwako"
Analyse: "Aina noma"
Nilisubiria kwa muda kadhaa, akanipigia tena. Nikamfata alipo. Tukarudi mdogo mdogo mpaka ghetto.
Juma: "Mdogo wangu hivi unasumbuliwa na nini, tokea wiki iliyopita?"
Analyse: "Tumbo tu kaka, hakuna jipya"
Juma: "Kweli?"
Analyse: "Huamini kama naumwa au?. Huoni muda wote nashinda ghetto tu"
Juma: "Amna nimeuliza tu. Hebu niambie ile siku uliyopewa ruhusa kazini maeneo ya buguruni ulienda kufanya nn?"
Analyse: "Misele tu kawaida, umejuaje kama nilikuwa kule?"
Juma: "Kuna watu wa ofisini walikuona"
Analyse: "Waliniona wapi?"
Juma: "Kuna sehemu ulikuwa unaandika namba, wanahisi ulikuwa unachukua namba ya mganga. Wamekupiga na picha"
Analyse: "Mganga? Picha? Picha gani?"
Juma: "Tuachane na hayo, hebu niambie unashida gani haswa?"
Analyse: "Shida ipi kaka?"
Juma: "Unajua zile story tulizokuwa tunapiga ile siku uliyoanza kuumwa, nimejaribu kuvuta picha isijekuwa unatatizo"
Analyse: "Hapana kaka, zilikuwa story tu. Nilishawahi kumsikia jamaa yangu akiongea hizo habari kipindi cha nyuma, ndio nikaona tuziongelee muda ule"
Juma: "Huyo jamaa yako alipata suluhu ya ilo jambo?"
Analyse: "Itakuwa alipata tu, maana hakuliongelea tena ilo jambo"
Juma: "Kwavile alipata suluhu, basi sawa. Ila angekuwa hajapata, ningemsaidia, maana haya mambo ukichelewa unaweza kupoteana mazima"
Akanyanyuka akiwa anataka kuondoka, nikawahi kumdaka:
Analyse: "Unaenda wapi sasa kaka. Niambie kwanza anapoteanaje mazima?"
Juma: "Hizo story tutapiga siku nyingine, leo acha niwahi mdogo wangu"
Analyse: "Siku nyingine ipi tena kaka? Akipoteana kweli je??"
Juma: "Atapoteanaje na umesema alipata suluhu?"
Nikabaki kimya kidogo.
Juma: "Sikia mdogo wangu, umepata suluhu au bado?"
Analyse: "Kwani ni Mimi kaka?. Mbona unauliza kama vile ni mimi ndio ninashida?"
Juma: "Sawa, tufanye ni jamaa yako, vipi amepata suluhu?"
Analyse : "Tufanye hajapata"
Juma ikabidi akae tena kwenye kiti. Na kuniambia "Hebu kuwa muwazi basi mdogo wangu."
Sikuwa na namna, ikabidi nimuelezee hali halisi. Alinisikiliza mpaka mwisho, ila aliishia kunicheka tu. Kiasi kwamba nikaanza kupata hasira. Akaniambia:
"Sikia mdogo wangu, hapo hakuna cha kuogopa. Kuanzia sasa mpotezee kabisa. Muache afanye anachotaka kufanya, alaf tutaenda nae sawa"
Analyse: "Kwamba unamaanisha tusubirie aninyooshe kwanza, alafu ndio tumfate?. Kuwa serious basi Juma"
Juma: "Wewe kuwa na amani, fanya ninachokwambia"
Analyse: "Nakuwaje na amani wakati umesema naweza kupotea kwenye ramani mazima?"
Juma: "Niamini Mimi"
Analyse: "Hivi unajisikia unachoongea lakini? Nikuamini wewe kwa lipi?"
Juma: "Mdogo wangu mwenzako nishatembea sana, vingi navijua kwenye haya mambo. Cha msingi......."
Analyse: "Hata kama broh, ila mavuzi aliyonayo ni yangu na sio yako. Hivyo siwezi kurelax kama wewe"
Juma: "Nisikilize basi, au nikuache na jambo lako?"
Analyse: "Amna broh, ni vile wewe humjui yule mwanamke. Akili zake anazijua mwenyewe "
Juma: "Wewe relax, kuna mambo yangu nayaweka sawa. Alafu nitakupeleka sehemu"
Analyse: "Sawa broh"
Hakuendelea kukaa, akawa ameondoka. Nikabaki peke yangu pale ghetto nikiwa nimejawa na confidence za kutosha. Na hata Mama Husna aliponicheki, nilimwambia sitoenda. Alinitisha, lakini nikakaza. Muda wote nilikuwa natembelea confidence ya Juma.
Ila usiku wote sikulala vizuri. Mara kwa mara nashtuka naangalia kobilo kama inafanya kazi au la. Nikiona sielewi, nacheki porn nione kama itaitika. Then ikiitika nalala.
Ilipita kama wiki hivi, hakuna cha ajabu kilichonitokea. Lakini haikuwa nyepesi kwa upande wangu, maana nilikuwa najikagua kila muda. Pia niliambulia sana matusi toka kwa Mama Husna. Nilipoona fujo zimekuwa nyingi, nikaamua kuhama mitaa ile, na huo ndio ukawa mwisho wa kuonana na Mama Husna. Juma aliniambia mwenye nia mbaya haongei sana, hivyo hata aliposema atanipeleka hatukwenda.
Nilivyohama pale nikahamia mitaa ya Tabata Liwiti, mitaa opposite na shule, nyuma ya zilipokuwa ofisi za Tanesco.
Nikiwa kwenye hii mitaa, ndipo nilipofahamiana na Mama Bahati pamoja na Binti yake aitwaye Bahati. Sitoelezea kwa kina habari zao kwenye hii story, labda kwenye story zijazo kama nitaandika.
Hii nyumba niliyoamia, ilikuwa na wapangaji tupu, mwenye nyumba hakuwa akiishi pale. Wapangaji tulikuwa wanne tu. Kati ya hao wapangaji wanne, ni mmoja tu ndio alikuwa kaoa, sisi wengine wote tulikuwa mabachela.
Kati ya sisi ambao hatujaoa palikuwa na jamaa ambae alikuwa ni dereva malori, mtu wa mademu sana yule jamaa. Hatukuwahi kuzoeana sana, japo tulikuwa tunapiga story mara chache chache ambazo wote tutakuwa home. Na kilichochangia tuweze kupiga hizo story, ni kwavile jamaa alikuwa muongeaji sana. Alizoea kuniita "mtani" hii ni kwavile yeye upande wa Mama ni kutokea Kigoma, na Baba ni kutokea Mara, hivyo alikuwa mtani wangu pande zote mbili. Jamaa alikuwa mbishi kuliko watu wote ambao nimeshawahi kufahamiana nao.
Hii nyumba sikuweza kuishi muda mrefu sana, nikalazimika kuhama na kusamehe Kodi yangu. Maana ni kwenye hii nyumba ndio nilifumaniwa...
Mwenyekiti ๐Ila una dhambi wewe mwenzio bonge kaishiwa nguvu kalegea kutokana na nyegge ukamuacha pale pale amechuchumaa hata kumsapot anyanyuke apostle huendi mbinguni walai!
Cc Smart911