Life style yangu ilinipotezea mwanamke mzuri

Life style yangu ilinipotezea mwanamke mzuri

Tatizo k zenye amani hazitaki we mtu ushaambiwa binti na mali zake havigusiki nae akaenda hapohapo ngoja tusubiri ya kesho tumnyambue mpk mbupu ziwe ndefu kuzidi kobilo[emoji28][emoji28][emoji28]

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
[emoji1787][emoji1787] Yaani huyu kiumbe kuvumilia hawezi ili aishi kwa amaniii jamaniii nyege zimezidi si apige puchu tu mbona anajiendekeza sanaaa
Kupiga puli ni matumizi mabaya ya muda 😅😅
 
Wote njia yetu ni hiyo hiyo mbona. Hakuna atakayebaki 😅😅
Mi napenda ila sijafikia hata nusu ya robo yako au ni vile sijasimulia ya kwangu😂😂 na watu aina yako anguko lako liko hapo hapo kwenye mapaja ya kina k, achana na k za mafungu zitakuua au labda uniambie ulishaacha
 
Sasa hivi nimeshaokoka, nasubiria Kalpana anipatie mdogo wake, nitulie 😅
😅😅😅 kwa k ambazo umeshaona labda mdogo wangu aww nazo mbili au tatu ndo utaridhika, nilimwambia hivyo jirani yangu huyu😂😂😂wakati anachumbia alicheeka sana
 
Portion 16:

...... Safari haikuboa. Mpaka tunafika, Mimi na yule Mzee aliyekuwa pembeni yangu tulikuwa tunapiga story kana kwamba tulifahamiana siku nyingi. Nilikuja kufahamu jina lake, anaitwa Mr. B. Alikuwa ni mtu mwenye ufahamu na mambo mengi sana. Japo taaluma yake ilikuwa ni tofauti kabisa na ya kwangu, ila wote tulifanya kazi kwenye taasisi zilizopo chini ya wizara moja. Mtu wa kariba yake ni kama dhahabu endapo ukiwa karibu yake. Nadhani ndio maana hata Mzee wa Kongowe alitaka niwe nae karibu.

Mr. B alikuwa nimpenda kusoma vitabu, na hicho ndio kilisaidia Mimi na yeye kuelewana. Katika vitabu vyote ambavyo nimeshasoma, kila nilichomtajia, alikuwa nae ameshakisoma. Alifurahishwa na tabia yangu ya kupenda kusoma vitabu. Akaniandikia list ya vitabu 10 ambavyo alisema angependa niwe nimevisoma ndani ya mwaka mmoja. Na tokea siku ile, amekuwa na utaratibu wa kunipa list ya vitabu vya kusoma kila tunapouanza mwaka. Tokea nimefahamiana nae, nimejikuta nasoma vitabu vingi sana tofauti na kipindi cha nyuma.

Kwa kiasi kikubwa amenisaidia sana kuibadilisha akili yangu.

Siku moja tukiwa short break wakati wa training, ulikuwa muda wa chakula. Kuna picha moja nilimpiga Mr. B wakati anakula. Ilikuwa ni picha nzuri, hivyo akahitaji nimtumie.

Baada ya kuipata picha, akaamua kusave namba yangu. Whatsap wanamtindo ukitaka kusave namba ya mtu, basi sehemu ya kuandika jina wataweka jina ambalo huyo mtu ndio ameliweka Whatsapp. Mimi Kwa upande wangu niliandika "Amphibian" hivyo Mr. B alivyokuwa anasave namba yangu, likakaa ilo jina.

Mr. B: "Amphibian? Seriously?"

Nilijisikia noma sana, sikuwahi zingatia ile sehemu na sikuona kama ni kitu kikubwa. Ila Kwa mtu wa heshima kama yule, niliona kama ameniona miyeyusho.

Ila na yeye kwenye kuisave namba yangu, akaamua kuisave hivyo hivyo Amphibian. Na ndio jina ambalo amekuwa akiniita tokea siku hiyo. Mpaka kuna muda huwa nahisi akitajiwa jina langu halisi anaweza asinitambue kwa haraka.

Training ilikuwa ni ya siku 30 kisha tukarudi nchini na kutawanyika, maana tulienda watu wa taaluma tofauti tofauti, japo karibia wote tulikuwa chini ya wizara moja.

Ile siku ambayo ndio tulirudi, mida ya usiku Mzee wa Kongowe akanipigia simu:

Mzee: "Vipi mambo yameendaje huko?"

Mimi: "Vizuri tu, hata Mr. B tunaelewana vizuri sasa hivi"

Mzee: "Nimefarijika kuona unaenda vizuri nae"

Analyse: "Ndio Mzee, tunaelewana kwa kiasi fulani"

Mzee: "Ukielewana nae vizuri, ni mtu mzuri sana huyu. Anaweza kukusaidia pakubwa"

Analyse: "Nitajitahidi kuendana nae"

Mzee: "Unajua kwenye maisha kila kitu huwa kina zeeka. Kitu pekee ambacho hakizeeki ni connection na watu. Na hicho ndio kila mtu anapambania. Kwa Mr. B upo sehemu sahihi. Anaweza kukusaidia zile sehemu zote ambazo Mimi sikuweza".

Analyse: "Mzee ni mkarimu na muelewa sana, nina imani nitaenda nae vizuri"

Mzee: "Pamoja na kumuona muelewa, ila hanaga uvumilivu kwenye mambo mawili, mali zake na binti yake wa mwisho. Kuwa mwangalifu na hivyo vitu"

Analyse: "Ilo lisikupe shaka Mzee"

Mzee: "Unajua sisi ambao familia zetu sio popular kwenye siasa, tunatumia nguvu kubwa ili kuweza kukaa level za juu. Na ndio maana tukistaafu ni rahisi kusahaulika. Kesho yako inategemea na mambo utakayofanya leo, jitahidi kila nafasi unayoipata unaitumia vizuri, huwezi jua siku moja itakuweka kwenye level gani"

Analyse: "Nitajitahidi sana kwenye ilo Mzee"

Mzee: "Nakukumbusha tena huyo sio ndugu yako, hivyo jitahidi kumfanya awe karibu nawe. Jitahidi usivuke mipaka"

Baada ya hapo tukaagana, akakata simu.

***** ***** ***** ******

Tokea niondoke Dar kwa kiasi fulani nimekuwa na amani, japo imekuwa ngumu kuzoea life la huku nilipo. Ofisi anayofanyia kazi Mr. B ipo mkoa huu huu niliopo hivyo imekuwa rahisi sana Mimi na yeye kuinteract. Amekuwa ni mtu wa kunishauri na kunipa facts za hapa na pale ambazo zimekuwa msaada kwangu.

Kwa muda mrefu nimekuwa nikijaribu kubadilisha vitu kwenye maisha yangu , ila nimekuwa nafeli mara zote. Hii inatokana na kwamba nilikuwa najaribu kubadilisha kila kitu, ila nasahau kubadilisha fikra zangu. Tokea nimefahamiana na Mr. B, nimekuwa napigania sana kubadili fikra zangu, na Kwa kiasi fulani nauona mwanga.

Siku zote amekuwa akijaribu kunipa mwongozo kwenye vitu kadha wa kadha. Kawaida huwa nikishatoka kazini kuna sehemu napendaga kwenda kukimbia kimbia na kucheza mpira kidogo. Jioni moja nikiwa natoka mazoezini, nikakuta missed calls za Mr. B, ikabidi nimpigie:

Mr. B: "Amphibian hujambo?"

Analyse: "Sijambo Mzee. Shikamoo"

Mr. B: "Marahaba. Mbona hupokei simu zangu?"

Analyse: "Nilikuwa mazoezini kidogo Mzee, hivyo simu sikuwa nayo"

Mr. B: "Mazoezi gani ya muda huu, mbona unaleta ujanja ujanja kijana?"

Analyse: "Muda huu ndio narudi, ila nilienda mapema tu"

Mr. B: "Wik end ratiba yako ipoje?"

Analyse: "Usafi tu mida ya asubuhi, na jioni ndio kama hivi nakuja kupunguza mafuta ambayo sina"

Mzee akacheka:

Mr. B: "Basi kama utaweza, ukitoka kwenye hayo mazoezi yako, uje nyumbani kwangu"

Analyse: "Siku gani haswa ambayo utahitaji nije?"

Mr. B: "Jumapili itakuwa vizuri zaidi"

Analyse: "Sawa Mzee"

Baada ya kukata simu, nikabaki najiuliza "Huyu Mzee ananiitia nini?". Sikupata jibu, na sikuona haja ya kuendelea kujiuliza maswali mengi wakati nikienda nitajua.

Hiyo siku tuliyokuwa tunaongea ilikuwa ni alhamisi. Ilipofika jumapili, mida ya saa moja nikawa njiani kuelekea kwake. Nilikaribishwa vizuri, nikakuta msosi umeshaandaliwa nikajumuika nao mezani. Nikiangalia mezani, naona mboga ni nyingi kuliko vyakula vingine. Kibaya zaidi nikaambiwa Mimi ndio nianze kupakua. Nikapakua aste aste, lakini nilivyoanza kula nashangaa wali umeisha, nimebaki na mboga tu kwenye sahani. Nilikuwa naona aibua wakati hakuna hata aliyekuwa na muda na Mimi.

Baada ya kula, tukawa tunapiga story na Mr. B pale sebuleni:

Mr. B: "Vipi mambo yako yanaendaje sasa hivi?"

Analyse: "Mungu ni mwema Mzee, yanaenda"

Mr. B: "Nafurahia sana kuona jinsi ulivyosharp. Usipoteteleka, utafika mbali sana"

Analyse: "Mungu anisimamie"

Mr. B: "Hivi ukiachana na hii kazi yako, unajishughurisha na kitu gani kingine?"

Nikataka nimwambie namiliki bodaboda kuna mtu nimempa mkataba, ila nikasita. Maana Mshua wangu mwenyewe nilivyomwambiaga nimenunua bodaboda, aliniambia nitafute kitu kingine maana hiyo sio biashara, muda wowote naweza kupigiwa simu niambiwe chombo kipo chini ya fuso, mtaji na faida vinapotea ndani ya sekunde chache. Hivyo kama Mshua alinikataa, huyu Mzee itakuwaje?

Analyse: "Sina chochote zaidi ya kazi yangu Mzee"

Mr. B: "Seriously?. Una nguvu, una muda, inakuwaje unakubali vyote vipotee hivyo?"

Analyse: "Kitu cha kufanya ndio sikioni"

Mr. B: "Mbona vya kufanya vipo vingi sana?. Anzisha hata kampuni, kuna watu wanakampuni za (....) au (....) mambo yao yanaenda vizuri tu. Commitment na dedication ndio kila kitu"

Analyse: "Ni kweli unachosema, ila mtaji wa kuanzisha hiyo kampuni ndio ugumu ulipo"

Mr. B: "Ugumu? Kwani kampuni ni nini mpaka iwe ngumu kuanzisha?"

Nikamulezea uelewa wangu juu ya kampuni. Akacheka:

Mr. B: "Kuna tofauti kati ya kampuni na ofisi Amphibian. Hapo wewe umeelezea ofisi za kampuni, na sio kampuni yenyewe. Kuna watu wanamiliki kampuni na hawana hata physical office, wana laptop na briefcase tu na mambo yao yanaenda. Acha kuniangusha kijana"

Analyse: "Sikuwahi fikiria hivyo, nitajaribu kuyafanyia kazi mawazo yako"

Mr. B: "Unajua kwa umri ulionao sasa hivi, hiki ndio kipindi cha kujaribu sana uwekezaji. Kuna wakati utafika hela yako itakuwa inaisha kabla hata haijakufikia mkononi. Ukishafika kipindi hicho kama hujawekeza popote, basi sahau kabisa kuhusu uwekezaji wowote wa maana"

Analyse: "Ni kweli Mzee"

Mr. B: "Kwa sisi Watanzania, mpaka kufika hapa tulipo tunakuwa tumepitia kwenye mikono ya watu wengi. Hivyo na sisi tunamadeni ya watu wengi hata kama hawatokuja kutudai. Hivyo ukiona kipato chako kinakutosha wewe tu, basi jua haupo salama. Maana pia kuna dharura ambazo zikija, zinahitaji uwe na uwezo wa kuhudumia hata familia kumi ndio huweze kuzitatua".

Akakaa kimya kidogo, kisha akaniuliza:

"Hivi unawekaga akiba?"

Analyse: "Mara chache chache"

Mr. B: "Ukiwa mwanaume kati ya vitu unavyotakiwa kuviogopa sana, ni kutokuwa na akiba. Otherwise, you're not safe"

Nikabaki kimya kwa muda, maana kulikuwa na uzito mkubwa kwenye vitu alivyoongea. Nilihitaji kufanya maamuzi kutoka kwenye jambo aliloniambia. Nilikaa kimya kwa muda mrefu mpaka pale aliponishtua:

Mr. B: "Naona akili yako ipo mbali sana kwasasa. Take your time, plan kitu kizuri. Alafu nisije nikawa nimekubana hapa, ukitaka kwenda kupumzika niambie tu. Maana najua kesho unahitajika kazini mapema"

Analyse: "Sikuwa nimeangalia saa kabisa, kumbe muda ndio umeenda hivi. Basi acha niwakimbie Mzee"

Mr. B: "Uwe unakuja tunapiga story kama hivi, hapo ni nyumbani pia"

Analyse: "Sawa Mzee, nitajitahidi niwe nakuja. Maana ninavingi sana vya kuchukua toka kwako"

Mr. B: "Anytime Amphibian"

Analyse: "Basi utaniagia kwa Mama ndani"

Mr. B: "Huyo atakuwa ameshaenda kulala, nitakuagia usijali"

Tukatoka nje, akawa ananisindikiza. Wakati tunataka kutoka getini, kuna mdada amevaa tight, raba na vesta akawa ameingia:

Mr. B: "Amphibian, huyu ni Binti yangu anaitwa Katrina, sidhani kama ushawahi kumuona"

Analyse: "Hapana, ndio mara ya kwanza hii"

Mr. B: "Huyu bwana ndio last born wangu, tena na yeye ni mpenda mazoezi kama wewe, hapo alipo anatoka evening walk"

Tukasalimiana na Katrina. Manzi mwenyewe ni ananata kuliko hata gundi, yani super glue ikasome. Maana tulisalimiana lakini alikuwa kama vile hana time na mimi. Kwa muda mchache niliomuona, ni kama aliishika akili yangu. Lakini kwa ule unataji wake, nikayafuta akilini mawazo yoyote juu yake maana sikuwa tayari kurudia makosa yaliyonifanya niondoke Jiji la Chalamila.

Lakini kumbe haikuwa rahisi kama nilivyodhani. Sijui ni Mimi ndio niliingia kwenye kumi na nane zake, au ni yeye ndio aliingia kwenye zangu, maana nilijikuta kwenye mazingira ambayo sikupenda kabisa niingie. Katrina alikuja kuwa kikwazo kwangu. Na hii ni baada ya kushindwa kufuata ushauri wa Mzee wa Kongowe kuhusiana na vitu vya Mr. B ambavyo ni untouchable.

Niliteleza padogo sana.....
Qwiiiiiiisheeeerrrr
 
Mzeee nimesoma story zako zote non stop,,,,nikupe 🌸🌸🌸💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐💐 yako.

Ninapenda usimuliaji wako na vile unavyoandika vizuri,,,🫡🫡🫡🫡🫡…….
Keep up mzeee 💪🏿💪🏿💪🏿💪🏿…..
 
Back
Top Bottom