Acha inyeshe tuone panapovuja-
Tatizo la Simba sio kocha, Kama wengi tunavyoaminishwa! Kwa mtazamo wangu tatizo la Simba ni Uongozi, hasa kipindi hiki Cha Try again na Babra.
Wanasajili wachezaji wa viwango vya kawaida Sana, nadhani wanaangalia Sana gharama kuliko ubora, Mambo yakiwa magumu zigo anaangushiwa kocha, mpaka Sasa ni kocha wa tatu huyu kuachana na timu katika uongozi wao! Mfano Try again aliahidi mwaka huu watavunja bank ili kumpata Adabayo mwisho wa Siku haikuwezekana, hivyo hivyo kwa Manzuki.
Hivi viongozi wamewezaje kufunga usajili huku kukiwa hakuna mshambuliaji no 9, na mkabaji wa chini! Unaendaje kwenye mashindano huku timu haijakamilika!
Wachezaji , Banda, Agpani, Onyango, Okwa na Mzungu wote hawa ni mapro, lakini hawana nafasi ya uhakika kikosi Cha Kwanza, hili ni tatizo, pro anakaa benchi! na wanaoanza baadhi yao viwango vyao vinatia mashaka! Matokeo yake wale tuliodhani wamechoka wanapata nafasi
Mm nashauri uongozi wangetengeneza idara ya kurungenzi ya ufundi, waajiri mtu au watu, wataalamu wa mpira ili wawe wanawashauri hasa kipindi Cha usajili! La sivyo tutakuwa tunapoteza Sana mabegi Airport.
Msimu uliopita hatukufanya vizuri! Kwa sababu hatukusajili vizuri- Kuna viashiria msimu huu pia hatujasajili vizuri,. Viongozi wajitafakali.