Ligi Kuu Bara: Simba SC vs Mwadui FC

Hongera zako julio na mwadui..
 
Hongera zako julio na mwadui..

Karibu sana ndetichia Tulikumiss sana ukipotea wewe na Azam habari zake humu zinapotea. Tumepokea pongezi zako. Na kwa kuwa umeonyesha nidhamu tutawafunga kombe la shirikisho then kwa Hisani ya watu wa jangwani tutawatuma mkashiriki kombe la
Shirikisho kwa niaba ya wababe wenu
 
Ndio hivyo mifupa wanagombea wengine nyama tumechukua sie.
Hamna lolote!, Yanga inabebwa Tu!, bila kubebwa Yanga haina lolote, acheni kubebwa, kwa mfano Leo Yanga imebebwa kuwa bingwa!. "Na SIMBA lakini!".
 
Bora kuwa wa kimataifa,kuliko mchangani
Simba huyu kabakia kufa,anakula jalalani
Mjomba hiyeeee
Mjomba mlipofungwa na coastal,mkasema haijawauma sana kwani hao ni waarabu wa tanga
Mlipopigwa na toto mlisema imewauma sana kwani hao ni watoto wa hasimu wenu yanga
Mjomba football is a performance na sio historia
Ooh tuliwafunga 5 mpaka wazirudishe
Unaishia kushangilia historia
Huku kwetu tuna methali Mjomba
Msiba hauji peke yake
Haya sasa musoti anadai chake
Hamjakaa sawa Julio huyo
Mjomba akija mo
Mpe akunusuru vinginevyo utaendelea kuwa wa mchangani mjomba natania tu ilaaaa.
 


Heheeeeeeee!!!!!!!!!!!!
Mambo bado mtani, mtalia na kusaga meno.

Tunajisikia raha tu!!!!!!!

Yebo!!!!! twende kazi mtani wangu.
 
Sasa simba wameamua ubingwa watupe tuu
Daaaah!!!
 
MBWEMBWE ZA JULIO (PART 1)





Kocha Mkuu wa MWadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema ana kikosi bora kabisa ambacho hakiwezi kulinganishwa na kile cha Simba.
Mwadui FC watakuwa wageni wa Simba katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo.
Julio anasema atashangazwa sana kama wao watapoteza mechi dhidi ya Simba hii leo.
“Kweli mechi itakuwa na ushinda, huenda inaweza ikawa ngumu. Lakini nitashangazwa sana kama nitafungwa na Simba.

“Nasema hivyo kwa kuwa nina kikosi bora kabisa ambacho huwezi ukakilinganisha na Simba. Tunachotakiwa ni kupambana na kushinda na hilo liko wazi,” alisema Julio aliyewahi kuwa beki wa kati wa Simba, kocha msaidizi na kocha mkuu.
 
MBWEMBWE ZA JULIO (PART 2)


Kocha Mkuu wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amejingaza kuwa kocha bora wa Tanzania.
Julio amesema hayo mara tu baada ya mechi kati yao dhidi ya Simba kwisha na Mwadui FC kushinda kwa bao 1-0.
“Mimi ndiye kocha bora hapa Tanzania. Nilitaka sana kuifunga Simba ili kuwaonyeshea kuwa mimi ninaweza kuwafunga kwa kuwa nina uwezo.
“Hawa Simba walitufukuza mimi na kocha Kibadeni, hii ni laana yetu kwa kuwa nilianza kumfunga kocha wao wa zamani (Patrick Liewig wa Stand United). Leo nimewafunga tena leo kupitia kocha wao sijui nani, sijui Mayanja.
“Nataka wajue makocha wazalendo pia wanapaswa kuthaminiwa. Waache mambo yao ya kizamani kuwa wanaona makocha wazalendo hawana maana. Waache majungu, waache kutudharau,” alisema Julio akionyesha kujiamini.

KIkosi cha Mwadui kilionyesha soka safi na kuizidi Simba ambayo licha ya kucheza vizuri lakini ilishindwa kuonyesha kuwa ingeifunga Mwadui FC.
 
UTAMU MCHUNGU KWA SIMBA SC



Azam FC imeifunga kwa Kagera Sugar kwa mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. Ushindi huo unairejesha Azam FC katika nafasi ya pili ya Ligi Kuu Bara baada ya Simba kupoteza kwa kuchapwa bao 1-0 na Mwadui FC, leo. Kwani Azam FC imefikisha 70 baada ya kucheza mechi 28 na Simba inaendelea kubaki na pointi 68 ikiwa na mechi 27. Tayari bingwa wa Bara ameishapatikana ambaye ni Yanga na sasa itakuwa ni vita ya Azam na Simba kuwania nafasi ya pili ambayo ni kama heshima tu au wingi wa fedha kutoka Vodacom.
 
" ikifika May niulizeni , nawahakikishia Simba
SC kubeba vikombe vyote vya ligi kuu na FA.
Tumejipanga vyema "
Haji Manara
February
 
...yaondoke yale matapeli kwanza ndio tuanze kutengeneza timu,majitu yanayopiga panga mpk mishahara ya wachezaji!,bila yale matapeli kuondoka,tutaendelea kusindikiza wengine tu!
 

Umedesa kwa Saleh Jembe blog.
Kakosea.
Azam INA 60 sasa hivi na sio 70. Na mikia wana 58, sio 68.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…