Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) - Mkapa Stadium | Yanga SC v Simba SC

Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) - Mkapa Stadium | Yanga SC v Simba SC

Yanga huwa hatuna maneno mengi, kazi kazi.
Tafadhalini sana Mikia hatutaki kuwatafuta baadae, tumechoka tabia yenu ya kukimbia kila muonapo mambo magumu kama inavyoenda kuwa hii leo.
.Unataka unidai nini
 
Hawa mwanitesa united (man u) mbona wanataka kunitisha, kwa rekodi zangu za haraka haraka simba na man u wakicheza kwa siku moja lazima mmoja apoteze pointi, kama sikosei ni mara moja simba alishinda na man u akashinda.
 
Hawa mwanitesa united (man u) mbona wanataka kunitisha, kwa rekodi zangu za haraka haraka simba na man u wakicheza kwa siku moja lazima mmoja apoteze pointi, kama sikosei ni mara moja simba alishinda na man u akashinda.
Ngapi ngapi huko?
 
Hello Tanzania na Ulimwengu kwa Ujumla...

Karibu katika Patashika ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL ) Jumamosi ya leo November 7, 2020 kunako Uwanja wa Benjamin Mkapa ambapo Yanga SC kutoka mitaa ya Jangwani wanakwaruzana na Mabingwa wa Nchi Simba SC, kutoka mitaa ya Msimbazi.

Ni mchezo ambao utarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90 za mchezo, huku Yanga ikijivunia rekodi ya kutopoteza mchezo wowote hadi sasa huku ikiwa imeshinda saba na imetoka sare mara mbili kwa michezo tisa, ambapo Simba SC imepoteza michezo miwili na kutoka sare mchezo mmoja huku ikiwa imeshinda mchezo sita.

Kocha wa Yanga SC, Cedric Kaze amesema "Tunajua tutakabiliana na hali ngumu kesho (leo), lakini tumejiandaa kukabiliana na hali hiyo ngumu, pia mechi dhidi ya Simba SC ni kipimo kikubwa cha kwanza cha ubora wa kikosi cha Yanga SC" amesema Kaze.

Na upande wake Kocha wa Simba SC Sven Vanderbroeck amesema " Ni mchezo wa watani wa Jadi, lakini pia ni mchezo ambao tunapaswa kuwa makini zaidi ili kushinda na hatimaye kukusanya alama tatu muhimu" amesema Sven.

Nani kuibuka na alama tatu muhimu leo? timu kutoka JF sambamba nami nahodha Ghazwat ipo nawe mpaka mwisho... Usikose Ukaambiwa!

Kumbuka mtanange huu wa VPL ni kuanzia saa 11:00 jioni.

View attachment 1621429
Baadaye msimulaumu Manula
FB_IMG_1604756397823.jpg
 
Wakati wowote mpira utaanza uwanja wa Mkapa

Naaaam mpira umeanza hapa uwanja wa Benjamin Mkapa, dakika 90 za jasho na damu

Yanga SC 0-0 Simba SC
 
Yanga leo anapigwa kuanzia tatu
Na Luis a.k.a konde boy lazma awe man of the match
 
05' kwenye Ligi Kuu Tanzania VPL hakuna bao kwa pande zote mbili

Mpira unachezwa sana katikati huku kila timu ikijaribu kupenya kufikia lango la timu pinzani

Yanga SC 0-0 Simba SC
 
10' Yanga wa tatu ambazo hazikuzaa mabao

Ni Free Kick kuelekea Yanga SC ngoja tuone. Inapigwaaaa inaokolewa.
 
Kama kawaida yangu nataka nibane pumbu Yanga wasipate goli.
mliopo uko uwanjani Yanga wapo upande upi kaskazi au kusi?
 
15, Yanga wanakosa nafasi ya wazi baada ya mpira wa krosi kuzagaaa na kuokolewa na Manula

Yanga SC 0-0 Simba SC
 
20' Free Kick kuelekea Simba SC

Inapigwaaaa, inaokolewa na mabeki
 
Back
Top Bottom