DOKEZO Limeshafika ghorofa ya 13 na linaendelea, lakini nguzo kama njiti za kiberiti

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Haya nd majibu ya kitaalamu... Mdau katoa angalizo na ww umejibu kitaalamu
 
Hichi ndicho kilichopaswa kujadiliwa, sio mtu kaona tu gorofa. anaishia kusema hili liko chini ya kiwango.. Kufanya judgment kwa kuangalia kwa macho tu pekee bila kuwa na vivid evidence si sawa
 
Mbona limepinda?
 
Mkuu, fanya issue zako, mambo ya watu achana nayo, unaweza ukawa na very limited facts kwenye hilo jambo
Sidhani kama wanaweza kujenga jengo LA gharama kubwa kama hilo kwa wataalam wa kuokota jalalani
Dah! Nilikuwa na wasi wasi na ghorofa langu ambalo nimejengea nondo za milimita 12 sasa baada ya kuliona hili nimepata moyo. Ngoja nizichange nipandishe floor nyingine ziwe tatu!
Tungekuwa na raia kama wewe 500000 tu nchi hii ingenyooka.Kuna madudu mengi yanafanyika ila kwa vile tunaona kama hayatuhusu tunapotezea kumbe kwa namna moja ama nyingi ya naweza kutuumiza baadae
Ngoja wataalamu wa majengo waje hapa
Bila connection ni ngumu kuyajua haya
 
!
!
Teknolojia Inabadilika. Huwezi Kujua Katumia Material Gani Kwenye Hizo Nguzo. Ukubwa Na Uimara Ni Vitu Tofauti Mkuu. Punguza Ujuaji
 
Mkuu acha unoko fanya mambo yako hilo jengo tumejenga kwa kuzingatia vipimo
thibitisha, je kuna nafasi ya kupumua baina ya jengo 1 na lingine

je nguzo ni imara kiasi gani? alafu yeye kaomba mamlaka zikague wakikuta ni sahihi ujenzi utaendelea hapo unoko u wap?
 
Mbona ni ghorofa 10 sio 13
 
Kwa ufupi ni kuwa nguzo/columns za jengo zinzaweza kubadilika urefu ila upana ukabaki vile vile floor zinazofuata.
Mfano:-
Ground -3rd floor (300x600)
3rd floor- 7th floor (300x450)
7th - 10th floor (300x300)
Usanifu wa majengo pia hutegemea aina ya matumizi ya jengo,hivyo mzigo utakaosafirishwa kupitia beams baadae columns/nguzo ni lazima ukidhi ubora wa zege,kiasi na aina ya nondo,size za beams na columns/nguzo.
Kwa ufupi ni kuwa kuonekana kwa wembemba wa nguzo upande wa mbele (cx view) hakumaanishi nguzo zile ni nyembamba,pengine ungelipiga picha ubavuni mwa jengo ili tuone kama upande wa (cy view) uko vile vile?.
Hata hivyo ukubwa wa nguzo hutegemea:-
1.uzito.
2.urefu wa floor to floor.
3.ukubwa wa balcony/cantilever (kuna wakati clients hawapendi beams zichomoze/zionekana nje ya jengo)
4.Aina ya/na ubora wa Nondo.
5.Matumizi ya Jengo (mfano: Parking, Ukumbi,Kanisa n.k)
Mbali na hivyo zipo aina mbili za majengo:-
1.Framed structures (non dead walls)
2.Load bearing structures (dead walls)
Hivyo usanifu wa 2. Hapo juu husaidia kuta kubeba mizigo directly kutoka kwenye beams,hivyo kupunguza mzigo kwenye columns/nguzo.
Yawezekana,lakini sina hakika kuwa Jengo hilo ni mojawapo ya Partial-framed/load bearing structure.
Cha kufanya/kukagua ni:-
Tabia ya udongo.
Matumizi ya Jengo.
Material inayotumika,hasa Nondo,kokoto, mchanga na tofari.
Ubora wa zege iliyokwisha fanyika awali.(rebound hammer/cube tests kama zipo).
Michoro hasa beams,columns,balcony details,foundations bases/raft.
Kiwango cha maji yanayotumika kumwagilia au ni aina gani ya umwagiliaji inatumika kushibisha zege.
 
Asante kwa ufanunuzi, ila kujiridhisha ni muhimu
 
Tanzania, everything is possible. Kuna jengo lilianguka. Vibao vyote vilikuwa vya kununua. Walijenga wenye jengo kimtindo mtindo
kweli kabisa kazi zangu na deal sana na mainjinia kuna sehem site kama tatu hivi tumezivisit kumbe wamenunua jina mzee bongo nyosoo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…