Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Mbona maelekezo yameanza kuwa mengi na hata kampeni hazijaanza?
Msimamizi wa uchaguzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, Juma Mnwele amevihimiza vyama vya siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 kuhakikisha kampeni zao zinafanyika kwa kistaarabu na kwa kufuata muda uliowekwa ambao ni Novemba 20 na kumalizika Novemba 26, 2024.
Akizungumza na Mashujaa FM, Mnwele alibainisha kuwa uchaguzi huo unajumuisha wagombea 3,115 wanaowania nafasi mbalimbali kutoka vyama saba vya siasa, ambavyo ni ACT Wazalendo, CCM, CUF, CHAUMA, CHADEMA, TLP, na NCCR-Mageuzi.
Pitia Pia: CHADEMA na ACT Wazalendo nendeni mahakamani mkausimamishe Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Mnwele amesisitiza umuhimu wa kufuata muongozo wa kampeni, akiwataka wagombea kujikita katika kunadi sera zao kwa hekima na kuepuka lugha za matusi au kampeni za kumvunjia heshima mtu binafsi.
Wananchi wa Manispaa ya Lindi, kwa upande wao, wameeleza matarajio yao ya kupata viongozi waadilifu, wenye maono ya kuwaunganisha, kusikiliza kero zao, na kuzitafutia suluhisho kwa maslahi ya jamii.
Mbona maelekezo yameanza kuwa mengi na hata kampeni hazijaanza?
Msimamizi wa uchaguzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, Juma Mnwele amevihimiza vyama vya siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 kuhakikisha kampeni zao zinafanyika kwa kistaarabu na kwa kufuata muda uliowekwa ambao ni Novemba 20 na kumalizika Novemba 26, 2024.
Akizungumza na Mashujaa FM, Mnwele alibainisha kuwa uchaguzi huo unajumuisha wagombea 3,115 wanaowania nafasi mbalimbali kutoka vyama saba vya siasa, ambavyo ni ACT Wazalendo, CCM, CUF, CHAUMA, CHADEMA, TLP, na NCCR-Mageuzi.
Pitia Pia: CHADEMA na ACT Wazalendo nendeni mahakamani mkausimamishe Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Mnwele amesisitiza umuhimu wa kufuata muongozo wa kampeni, akiwataka wagombea kujikita katika kunadi sera zao kwa hekima na kuepuka lugha za matusi au kampeni za kumvunjia heshima mtu binafsi.
Wananchi wa Manispaa ya Lindi, kwa upande wao, wameeleza matarajio yao ya kupata viongozi waadilifu, wenye maono ya kuwaunganisha, kusikiliza kero zao, na kuzitafutia suluhisho kwa maslahi ya jamii.