Uchaguzi 2020 Lissu alishapoteza sifa za Kugombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA

Uchaguzi 2020 Lissu alishapoteza sifa za Kugombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA

Benson Mramba

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2013
Posts
648
Reaction score
1,485
Kwa mujibu wa muongozo wa watia nia wa nafasi mbalimbali wa CHADEMA wa mwaka 2012, Mtiania kwa nafasi ya Urais anapaswa kutangaza nia yake katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja kabla ya tarehe ya Uchaguzi.

Muongozo huu uliandikwa ili kumdhibiti Zitto Kabwe ambaye mwaka 2010 wakati Dr Slaa anagombea Urais yeye akiwa Kigoma akatangaza kugombea Urais 2015. Sasa wakubwa wakaamua kumdhibiti mapema.

Mwaka 2013 Zitto akaingia kwenye mgogoro baada ya kunaswa kwa mkakati wa mabadiliko 2013 ulioandikwa na Mwigamba, Kitila na Waitara na mimi kwa mbali kidogo.

Sasa Mh. Tundu Lissu ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA ametangaza nia ya kugombea Urais mwaka 2017, 2018, 2019 na 2020 katika matamko yake mbalimbali na mikutano na waandishi wa habari ndani na nje ya nchi.

Sasa kamati kuu hii ya CHADEMA ambayo iko chini ya Mbowe ambaye pia nia yake ya kuutaka Urais imeonekana kwa vitendo mara zaidi ya maneno itampitisha Lissu? Hawawezi kumpitisha. Nia wanayo na sababu wanayo

Nilisema kuwa mgogoro unaofuata CHADEMA sasa ni kati ya Mbowe na Lissu! Huu ndio utakuwa hatma ya Chama hicho au ufufuko wake. Muda utatuambia.

Mimi naamini Lissu atagombea kwa tiketi ya NCCR
 
Wewe ni kama fisi anayemfuata binadamu kwa nyuma akitegemea binadamu atadondosha mkono.

Mbona chadema inawaumiza sana vichwa hata wakitulia?
Yeyote chadema itakayempitisha sisi ndo tutamwunga mkono kwahiyo wewe huo upupu wako hauna mantiki
 
Hakuna mahali katika hiyo miaka Lissu alitangaza kugombea urais bali alisema kama"Chama kitampa nafasi ya kugombea" halafu kuna mtu kama Zitto anasema "Nitagombea urais kwa tiketi ya Chadema 2015"hizi ni kauli zenye maana tofauti kabisa.

Inaonekana ccm wanamuogopa sana Lissu.Lakini kitu cha msingi ni kuangalia ilani ya chama iliyo bora. Hatuangalii mtu in personal bali tunaangalia atatufanyia nini huyo mtu tukimchagua.
 
Asante sana kiongozi
Wewe ni kama fisi anayemfuata binadamu kwa nyuma akitegemea binadamu atadondosha mkono.

Mbona chadema inawaumiza sana vichwa hata wakitulia?
Yeyote chadema itakayempitisha sisi ndo tutamwunga mkono kwahiyo wewe huo upupu wako hauna mantiki
 
Wewe ni kama fisi anayemfuata binadamu kwa nyuma akitegemea binadamu atadondosha mkono.

Mbona chadema inawaumiza sana vichwa hata wakitulia?
Yeyote chadema itakayempitisha sisi ndo tutamwunga mkono kwahiyo wewe huo upupu wako hauna mantiki
Mkuu, huwezi kujikita kwenye hoja Tu ukaacha kutweza Utu wa mtu?
 
Lissu anatafuta sababu ya kufukuzwa ahamie ACT
Halafu sheria za uchaguzi zinataka muombaji achumue fomu mwenyewe,lissu anaogopa kurudi kwa usaliti alioufanya
 
Wewe ni kama fisi anayemfuata binadamu kwa nyuma akitegemea binadamu atadondosha mkono.

Mbona chadema inawaumiza sana vichwa hata wakitulia?
Yeyote chadema itakayempitisha sisi ndo tutamwunga mkono kwahiyo wewe huo upupu wako hauna mantiki


Kwani chadema ni mali yako au ya Babako hadi ukataze watu kuiongelea?
 
Kwahiyo hoja zenu nizakumimina tu. Kweli ushindani wa hoja hamuwezi.
Hapo kuna hoja gani????

Refer comments za mhe Sumaye alipotoka chadema..

Alisema mtu akitaka kugusa nafasi ya ...... nini kinatokea....!
 
Back
Top Bottom