Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tanzania Bara na 'mgombea' wa nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Tundu Lissu amewashukia wale wote wanaodai kuwa miongoni ya watu wanaomuunga mkono katika kinyang'anyiro cha kutafuta nafasi hiyo ni wale ambao mara zote amekuwa akiwatuhumu kuwa wanajihusisha na vitendo vya rushwa ndani ya CHADEMA
Akizunguma na wanahabari kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho zilizopo Mikocheni, jijini Dar es Salaam Desemba 18.2024 ikiwa ni muda mfupi baada ya kurejesha fomu za kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa katika mchakato wa ndani wa uchaguzi unaoendelea Lissu amesema amekanusha vikali madai ya kuungwa mkono na watu wanaojihusisha na vitendo hivyo.
Pia soma: Kuelekea 2025 - Freeman Mbowe: Nitatoa uamuzi wa kugombea Uenyekiti siku ya Jumamosi saa 5 asubuhi
Amesema miongoni mwa wale anaowatuhumu mara kwa mara kujihusisha na vitendo vya rushwa mmoja wapo ametangaza dhamira ya kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (ingawa Lissu hajabainisha kama mgombea huyo anatokea upande wa Tanzania Bara au Zanzibar), na kwamba mtu huyo ametangaza hadharani kuwa anamuunga mkono Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe katika mchakato huo (ingawa Mbowe mwenyewe ameahidi kutoa msimamo wake ndani ya saa 48)
Aidha, Lissu ameenda mbali zaidi kwa kudai kuwa mtu huyo (anayemtuhumu) ndiye aliyemfuata nyumbani kwake (Tegeta, Dar es Salaam) akiwa ameambatana na mtu mmoja aliyemtaja kwa jina moja la 'Abdul' ambapo wawili hao walifika kumshawishi apokee rushwa, na kwamba walitumia nafasi hiyo kumueleza watu wengine ndani ya chama hicho waliofikiwa na 'Abdul' na 'kuchukua chao', lakini Lissu aliwakatalia
"Mtu aliyemleta Abdul nyumbani kwangu kuja kunihonga anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama, na amesema kwa maneno yake mwenyewe kuwa anamuunga Mwenyekiti (Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa) mkono, sasa hao wanaosema niliowasema mimi (kuwa wanajihusisha na rushwa) na wananiunga mkono ni kina nani?, ninajuwa aliyemleta Abdul nyumbani kwangu anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama na amesema anamuunga mkono Mwenyekiti, maana yake mimi najuwa aliyeniambia amepewa hela na Abdul na aliyeniambia wengine waliyepewa hela na Abdul, na ndiye aliyemleta Abdul nyumbani kwangu na ndiye mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama, huyo ambaye mimi nimemsema na ananiunga mkono ni nani?" -Lissu
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tanzania Bara na 'mgombea' wa nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Tundu Lissu amewashukia wale wote wanaodai kuwa miongoni ya watu wanaomuunga mkono katika kinyang'anyiro cha kutafuta nafasi hiyo ni wale ambao mara zote amekuwa akiwatuhumu kuwa wanajihusisha na vitendo vya rushwa ndani ya CHADEMA
Akizunguma na wanahabari kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho zilizopo Mikocheni, jijini Dar es Salaam Desemba 18.2024 ikiwa ni muda mfupi baada ya kurejesha fomu za kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa katika mchakato wa ndani wa uchaguzi unaoendelea Lissu amesema amekanusha vikali madai ya kuungwa mkono na watu wanaojihusisha na vitendo hivyo.
Pia soma: Kuelekea 2025 - Freeman Mbowe: Nitatoa uamuzi wa kugombea Uenyekiti siku ya Jumamosi saa 5 asubuhi
Amesema miongoni mwa wale anaowatuhumu mara kwa mara kujihusisha na vitendo vya rushwa mmoja wapo ametangaza dhamira ya kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (ingawa Lissu hajabainisha kama mgombea huyo anatokea upande wa Tanzania Bara au Zanzibar), na kwamba mtu huyo ametangaza hadharani kuwa anamuunga mkono Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe katika mchakato huo (ingawa Mbowe mwenyewe ameahidi kutoa msimamo wake ndani ya saa 48)
Aidha, Lissu ameenda mbali zaidi kwa kudai kuwa mtu huyo (anayemtuhumu) ndiye aliyemfuata nyumbani kwake (Tegeta, Dar es Salaam) akiwa ameambatana na mtu mmoja aliyemtaja kwa jina moja la 'Abdul' ambapo wawili hao walifika kumshawishi apokee rushwa, na kwamba walitumia nafasi hiyo kumueleza watu wengine ndani ya chama hicho waliofikiwa na 'Abdul' na 'kuchukua chao', lakini Lissu aliwakatalia
"Mtu aliyemleta Abdul nyumbani kwangu kuja kunihonga anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama, na amesema kwa maneno yake mwenyewe kuwa anamuunga Mwenyekiti (Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa) mkono, sasa hao wanaosema niliowasema mimi (kuwa wanajihusisha na rushwa) na wananiunga mkono ni kina nani?, ninajuwa aliyemleta Abdul nyumbani kwangu anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama na amesema anamuunga mkono Mwenyekiti, maana yake mimi najuwa aliyeniambia amepewa hela na Abdul na aliyeniambia wengine waliyepewa hela na Abdul, na ndiye aliyemleta Abdul nyumbani kwangu na ndiye mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama, huyo ambaye mimi nimemsema na ananiunga mkono ni nani?" -Lissu