Pre GE2025 Lissu: Aliyemleta Abdul kunihonga anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti na anamuunga mkono 'Mwenyekiti'

Pre GE2025 Lissu: Aliyemleta Abdul kunihonga anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti na anamuunga mkono 'Mwenyekiti'

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
1000017480.jpg
 
Ameshaonyesha hatoshi

Huko serikalini kila mtu angekuwa anamchongea mwenzake sijui ingekuwaje.

Ndio maana, mawaziri wanaapa kutunza siri za nchi.

Hakuna serikali isiyokuwa na mambo ya hovyo duniani. Huko kwenye vyama vya siasa ndio kabisa.

Sasa mtu anaetoa siri za ndani, ndio wakumuamini huyo.

Mambo mengine ni ya ku-leak wengine waseme hiyo ndio political-etiquette sio wewe muhusika kusema direct.

Hivi unadhani CCM walio madarakani au wanasiasa wa nchi zingine wangekuwa wanachongeana. Kungekuwa na chama cha kudumu kweli.

Lissu hajui siasa.
 
Fitina ndio njia kuu za siasa, hujui tu hata hilo
Shida yake hajui, mipaka.

Embu kutana na haya mabazazi ya CCM yaanze kukupa umbea wa wenzao na wao wenyewe.

Kama una akili timamu utajiuliza sasa wewe mwenye madaraka unaniadisia mimi ili iwaje.

Seuse mtu kama Lissu kwa nafasi yake anajua mangapi ya ndani ya chama.

Ni ropo-ropo hafai
 
Wakuu,


Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tanzania Bara na 'mgombea' wa nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Tundu Lissu amewashukia wale wote wanaodai kuwa miongoni ya watu wanaomuunga mkono katika kinyang'anyiro cha kutafuta nafasi hiyo ni wale ambao mara zote amekuwa akiwatuhumu kuwa wanajihusisha na vitendo vya rushwa ndani ya CHADEMA

Akizunguma na wanahabari kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho zilizopo Mikocheni, jijini Dar es Salaam Desemba 18.2024 ikiwa ni muda mfupi baada ya kurejesha fomu za kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa katika mchakato wa ndani wa uchaguzi unaoendelea Lissu amesema amekanusha vikali madai ya kuungwa mkono na watu wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Pia soma: Kuelekea 2025 - Freeman Mbowe: Nitatoa uamuzi wa kugombea Uenyekiti siku ya Jumamosi saa 5 asubuhi

Amesema miongoni mwa wale anaowatuhumu mara kwa mara kujihusisha na vitendo vya rushwa mmoja wapo ametangaza dhamira ya kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (ingawa Lissu hajabainisha kama mgombea huyo anatokea upande wa Tanzania Bara au Zanzibar), na kwamba mtu huyo ametangaza hadharani kuwa anamuunga mkono Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe katika mchakato huo (ingawa Mbowe mwenyewe ameahidi kutoa msimamo wake ndani ya saa 48)

Aidha, Lissu ameenda mbali zaidi kwa kudai kuwa mtu huyo (anayemtuhumu) ndiye aliyemfuata nyumbani kwake (Tegeta, Dar es Salaam) akiwa ameambatana na mtu mmoja aliyemtaja kwa jina moja la 'Abdul' ambapo wawili hao walifika kumshawishi apokee rushwa, na kwamba walitumia nafasi hiyo kumueleza watu wengine ndani ya chama hicho waliofikiwa na 'Abdul' na 'kuchukua chao', lakini Lissu aliwakatalia

"Mtu aliyemleta Abdul nyumbani kwangu kuja kunihonga anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama, na amesema kwa maneno yake mwenyewe kuwa anamuunga Mwenyekiti (Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa) mkono, sasa hao wanaosema niliowasema mimi (kuwa wanajihusisha na rushwa) na wananiunga mkono ni kina nani?, ninajuwa aliyemleta Abdul nyumbani kwangu anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama na amesema anamuunga mkono Mwenyekiti, maana yake mimi najuwa aliyeniambia amepewa hela na Abdul na aliyeniambia wengine waliyepewa hela na Abdul, na ndiye aliyemleta Abdul nyumbani kwangu na ndiye mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama, huyo ambaye mimi nimemsema na ananiunga mkono ni nani?" -Lissu
It is too late to catch a moving truck 🤣

atasema yote but it will not help him at all.

Political mistakes na blunders alizofanya Lisu ni pamoja na hiyo ya kuogopa kuwataja anao watuhumu kwa rushwa at first place.

saivi anaonekana anatapatapa tu kama mfa maji 🐒
 
Mbowe anaweza kuwa ni mmoja wa hao waliopewa hela na Abdul ndio maana Lissu anasita kuwataja. Lakini naamini iko siku atawataja.
Taratibu mtaanza kuelewa sasa nyuzi za Pascal Mayalla juu kirusi kilichopo ndani ya chadema.

Ndio mtaelewa kwamba sasa hata ile sign ya kwenye barua ya kuwaidhinisha kina Mdee kule bungeni haikufojiwa kama tulivyoambiwa.
 
It is too late to catch a moving truck 🤣

atasema yote but it will not help him at all.

Political mistakes na blunders alizofanya Lisu ni pamoja na hiyo ya kuogopa kuwataja anao watuhumu kwa rushwa at first place.

saivi anaonekana anatapatapa tu kama mfa maji 🐒
Lissu alipigwa risasi na Mbowe
 
Kiongozi wa siasa lazima uwe na kifua na kuweza kuchunga ndimi yako.

Lissu Mchanga wa siasa

Imagine ma-CCM yakianza kuchongeana hadharani.
 
Back
Top Bottom