Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 15,101
- 56,054
Akiwa mjini Tunduma, Tundu Lissu katika harakati zake za kutafuta wadhamini, ameongea na maelfu ya wananchi.
Amezungumza kuhusu hali ya uminywaji wa Vyombo vya Habari nchini, watumishi wa umma kutopewa maslahi yao ipasavyo, kero za wafanyabiashara ndogondogo hususan vitambulisho vya wamachinga vya sh 20000, Viongozi wa dini ya waislamu walioko jela kinyume cha haki, uonevu dhidi ya vyama vya siasa, kero ya wafanyabiashara kubambikiziwa kodi na TRA na kusema kuwa watavikomesha hivyo october 28.
Na pia, akampiga kijembe Rais Magufuli kuwa badala ya kuhangaika kuweka bando la internet ili kuwatazama wapinzani kwenye WhatsApp, afungulie vyombo vya habari ili awaone kupitia vyombo rasmi vya habari.
Hapo Tunduma OCD wa sehemu hiyo alijaribu kuwazuia wananchi kwenda mkutanoni, lakini alishindwa kuwathibiti wananchi maana walikuwa ni wengi mno.
Kwa taarifa zaidi muone yeye mwenyewe Tundu Lissu.
Amezungumza kuhusu hali ya uminywaji wa Vyombo vya Habari nchini, watumishi wa umma kutopewa maslahi yao ipasavyo, kero za wafanyabiashara ndogondogo hususan vitambulisho vya wamachinga vya sh 20000, Viongozi wa dini ya waislamu walioko jela kinyume cha haki, uonevu dhidi ya vyama vya siasa, kero ya wafanyabiashara kubambikiziwa kodi na TRA na kusema kuwa watavikomesha hivyo october 28.
Na pia, akampiga kijembe Rais Magufuli kuwa badala ya kuhangaika kuweka bando la internet ili kuwatazama wapinzani kwenye WhatsApp, afungulie vyombo vya habari ili awaone kupitia vyombo rasmi vya habari.
Hapo Tunduma OCD wa sehemu hiyo alijaribu kuwazuia wananchi kwenda mkutanoni, lakini alishindwa kuwathibiti wananchi maana walikuwa ni wengi mno.
Kwa taarifa zaidi muone yeye mwenyewe Tundu Lissu.