Uchaguzi 2020 Lissu anaendesha kampeni kivivu, siku moja anafanya jimbo moja ilhali majimbo yako 264. Itamchukua miezi 9 kuyamaliza, tume imetoa miezi miwili tu

Uchaguzi 2020 Lissu anaendesha kampeni kivivu, siku moja anafanya jimbo moja ilhali majimbo yako 264. Itamchukua miezi 9 kuyamaliza, tume imetoa miezi miwili tu

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
Lissu kaishiwa nguvu aendesha kampeni kivivu majimbo yako 264 yeye siku moja anafanya Jimbo moja itamchukua miezi 9 kuyamaliza tume imetoa miezi miwili tu kabla ya kura.

Kwa spidi hiyo hatamaliza majimbo 264 ya uchaguzi anaendesha kampeni kwa mwendo wa kuchechemea, hana stamina ya kampeni na tayari anaonyesha kuchoka hasa kimwili, kifikra, kisaikolojia na kipesa.

Kampeni ya Urais tulimwambia sio lelemama au kwa Kiingereza tunamwambia Presidential campain is not a Lele Mother. Ndio maana Magufuli akichoka hupiga push up ku boost mwili tayari kwa awamu inayofuata ya kampeni.
 
Magufuli vipi? Yeye mpak sasa ametembelea majimbo mangapi?

Yesu na Muhammad hawakuitembelea dunia nzima lkn dunia nzma leo tunawaamini. Lisu ni kusudi la Mungu. Subiri utaona.

Lissu ameshashindwa, maana anaonekana hajajiandaa na wala CDM hawajajiandaa. Nimeangalia hii ratiba ya uchaguzi kuna siku Magu anaenda hadi majimbo manne wakati Lissu inaonyesha jimbo moja tu kwa siku. Pia Magu na Makamu wake muda mwingi wapo majimbo tofauti tofauti wakati Lissu na Makamu wake wao wanafuatana majimbo karibu yote.

Kingine majimbo ya mjini saivi CDM hawana support, yote Magu atawalaza, si Dsm, Arusha wala Mwanza, yote haya Magu ataongoza sasa jiulize ngome ya Lissu ni wapi ?
 

Attachments

Kampeni za Lissu zinaenda vizuri mpaka alipo sasa hivi ameshazungumza na kujinadi kwa zaidi ya majimbo 15 sababu kampeni zake zinaenda kwa mtindo wa kanda.
 
Acha kuingilia shughuli zisizo kuhusu! Hivi wewe hujuwi kama Lissu ana Team ya Kampeni yenye wataalam? Subirini mziki wake mbona bado!
 
Back
Top Bottom