SI KWELI Lissu asema hata akibaki mwenyewe CHADEMA itasonga. Mimi ni ''One Man Army''

SI KWELI Lissu asema hata akibaki mwenyewe CHADEMA itasonga. Mimi ni ''One Man Army''

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
LISSU KWENYE UKURASA WAKE WA X (TWITTER) AMENENA MAZITO ASEMA HATA AKIBAKI MWENYEWE CHADEMA ITASONGA.

Hayo yamekuja mara baada ya viongozi mbalimbali wa Kanda wa CHADEMA kujiuzulu kwa madai ya Chama chao (CHADEMA) kukosa Muelekeo na Kwenda kujiunga na ACT wazalendo ili kuongeza nguvu kwenye chama chenye nia ya mabadiriko ya kweli sio kwa Sasa CHADEMA imejifia kifo cha asili sema viongozi taifa hawataki kusema ukweli.

SIKWELI_LISSU_21FEB25.jpg
 
Tunachokijua
Hivi karibuni kumekuwepo na mvutano kwa baadhi ya wana CHADEMA, mathalani tarehe Februari 18, 2025 mmoja wa makada wa chama hicho, Lembrus Mchome aliwasilisha pingamizi la kupinga uteuzi wa viongozi watendaji wa juu wa sekretarieti na wajumbe wa kamati kuu ya chama hicho uliofanywa na Mwenyekiti Tundu Lissu Januari 22, 2025 akidai kuwa umekiuka katiba ya chama hicho.

Ambapo baada ya taarifa hiyo katibu mkuu wa CHADEMA Taifa, John Mnyika alieleza kuhusu madai hayo kupitia ukurasa wake wa X aliandika.

"Kuna mkakati wa kuhamisha mwelekeo kutoka #NoReformsNoElection . Maamuzi ya Baraza Kuu @ChademaTz ya tarehe 22 Januari 2025 ni halali kwa kuwa Mkutano ulikuwa na wajumbe halali 234 kati ya 412 sawa na asilimia 56.8 kwa mujibu wa Katiba ibara ya 6.2.2.

Kikao hicho kilifanya uthibitishaji kwa mujibu wa Katiba ibara ya 7.7.12 (c) na (e) na hakukuwa na agenda ya uchaguzi.

Nakala ya barua tajwa kupelekwa kwa Msajili kunaashiria nia ovu iliyoko nyuma ya pazia."


Madai

Kumekuwapo picha inayoonekana kuwa chanzo chake ni mtandao wa X, ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii na kuonesha kuwa Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Lissu amechapisha akieleza kuhusu vuguvugu linaloendelea Chadema likiongozwa na Boniface Jacob. Inaonesha pia akieleza kuwa yeye ni “One Man army” na amewataka watu wajifunze kwa Ntobi.

Uhalisia wa madai hayo

JamiiCheck imefuatilia kwa njia ya mtandao ikiwemo kupitia ukurasa wa X zamani Tweeter wa Tundu Lissu na kubaini kuwa screenshot hiyo si ya kweli. Aidha aina ya mwandiko (font) uliotumika katika screenshot hiyo si unaotumika na mtandao wa X na badala yake ni ya kuhaririwa.

Madai yanayoonekana katika taarifa hiyo kuwa Lissu ameandika atawashughulikia wananchama hao kama ilivyokuwa kwa Ntobi siyo sahihi. Emmanuel Ntobi alikuwa ni mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Shinyanga ambaye alivuliwa nafasi hiyo na kamati tendaji ya chama hiko kutokana na utovu wa nidhamu wakati wa kampeni kipindi ambacho Lissu alikuwa mgombea tu na si mwenyekiti. Tazama hapa

Chadema pia haijatoa taaarifa yoyote kuhusu kuwepo kwa viongozi wa kanda wa chama hiko wanaotaka kujiuzulu.​
Mmmmmmh... dictator kawasha indicator.

Huyu jamaa angebaki kuwa makamu pengine angeaminiwa zaidi kwenye harakati.

Asiri ya Lissu ni kupinga na sio kuongoza. Wacha inyeshe tuone panapovuja.
 
LISSU KWENYE UKURASA WAKE WA X (TWITTER) AMENENA MAZITO ASEMA HATA AKIBAKI MWENYEWE CHADEMA ITASONGA.

Hayo yamekuja mara baada ya viongozi mbalimbali wa Kanda wa CHADEMA kujiuzulu kwa madai ya Chama chao (CHADEMA) kukosa Muelekeo na Kwenda kujiunga na ACT wazalendo ili kuongeza nguvu kwenye chama chenye nia ya mabadiriko ya kweli sio kwa Sasa CHADEMA imejifia kifo cha asili sema viongozi taifa hawataki kusema ukweli.
viongozi gani wa Kanda? Siyo fake kweli hii post? Antipasu anamapungufu ya kiuongozi lakini hawezi kujishusha hadi hapa!
 
LISSU KWENYE UKURASA WAKE WA X (TWITTER) AMENENA MAZITO ASEMA HATA AKIBAKI MWENYEWE CHADEMA ITASONGA.

Hayo yamekuja mara baada ya viongozi mbalimbali wa Kanda wa CHADEMA kujiuzulu kwa madai ya Chama chao (CHADEMA) kukosa Muelekeo na Kwenda kujiunga na ACT wazalendo ili kuongeza nguvu kwenye chama chenye nia ya mabadiriko ya kweli sio kwa Sasa CHADEMA imejifia kifo cha asili sema viongozi taifa hawataki kusema ukweli.
Waondoke mamluki wakubwa hao, wapuuzi wasiojitambua
 
LISSU KWENYE UKURASA WAKE WA X (TWITTER) AMENENA MAZITO ASEMA HATA AKIBAKI MWENYEWE CHADEMA ITASONGA.

Hayo yamekuja mara baada ya viongozi mbalimbali wa Kanda wa CHADEMA kujiuzulu kwa madai ya Chama chao (CHADEMA) kukosa Muelekeo na Kwenda kujiunga na ACT wazalendo ili kuongeza nguvu kwenye chama chenye nia ya mabadiriko ya kweli sio kwa Sasa CHADEMA imejifia kifo cha asili sema viongozi taifa hawataki kusema ukweli.
Huyo Boni Yai ni kirusi kinachoweza kudhoofisha uhai wa chama.

Kunatakiwa ipatikane dawa ya kupulizia, ili kirusi hiko kitokomezwe.
 
Kweni walitaka wabembelezwe?!🤔 CHADEMA kinasonga mbele.
 
Hiyo itakuwa ni fake. Lissu hawezi kuandika hayo. Kama kuna virusi watafukuzwa kwa utaratibu na sio kutishia X. Pili Kiongozi huwezi kuweka umimi kwenye chama. Hiyo ni kazi ya masalia
 
CDM inatakiwa iwe ya upinzani sio mamluki.
 
LISSU KWENYE UKURASA WAKE WA X (TWITTER) AMENENA MAZITO ASEMA HATA AKIBAKI MWENYEWE CHADEMA ITASONGA.

Hayo yamekuja mara baada ya viongozi mbalimbali wa Kanda wa CHADEMA kujiuzulu kwa madai ya Chama chao (CHADEMA) kukosa Muelekeo na Kwenda kujiunga na ACT wazalendo ili kuongeza nguvu kwenye chama chenye nia ya mabadiriko ya kweli sio kwa Sasa CHADEMA imejifia kifo cha asili sema viongozi taifa hawataki kusema ukweli.
Ni mpumbavu Tu atakayeamini huu upumbavu kutoka CCM
 
TAL siyo mjinga kwa kiwango cha kuandika huo ujinga.
 
Back
Top Bottom