Pre GE2025 Lissu ataka Ukomo wa Madaraka kwenye nafasi za uongozi CHADEMA. Asema itapunguza 'Uchawa'

Pre GE2025 Lissu ataka Ukomo wa Madaraka kwenye nafasi za uongozi CHADEMA. Asema itapunguza 'Uchawa'

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Tundu Lissu wakati akitangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa CHADEMA Taifa amesema CHADEMA haina budi kurudisha utaratibu wa ukomo wa Madaraka kwani utaondoa uwezekano wa Viongozi kung'angania madaraka na kuandaa Viongozi wapya, kupatikana kwa mawazo mapya na itapunguza upambe na uchawa ulioshamiri pale kiongozi anang'ang'ania madaraka pale ambapo hakuna ukomo wa madaraka

Ili kutekeleza majukumu yanayodaiwa na mazingira ya sasa ya mapambano ya kidemokrasia CHADEMA inatakiwa kuimarishwa katika maeneo mbalimbali ambapo kwanza ni Katiba ya Chama hicho, ambapo amesema Chama kimekuwa kikubwa na hakuna hofu ya kukosa uongozi katika nafasi mbalimbali za chama hivyo chama kinahitaji kurudisha ukomo wa mataraka kama ilivyokuwa mwanzo

Aidha, akizungumzia ukomo madaraka katika nafasi za Ubunge na Udiwani. Lissu amesema "Ukomo wa madaraka unahitajika pia katika suala nyeti la Ubunge na Udiwani wa Viti Malaamu." Amesema mchakato na namna ya kuwapata Wabunge wa Viti Maalumu umeleta mgawanyiko katika chama hicho ambapo mara baada ya uchaguzi wa 2020 ilibidi CHADEMA iwafukuze wanachama karibu Viongozi waandamizi wote wa BAWACHA waliorubuniwa ili kupewa nafasi za Viti Maalumu.

PIA SOMA

- LIVE - Tundu Lissu: Nimewasilisha kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA
 
Wakuu,

Kumbe kulikuwa na uchawa pia ndani ya CHADEMA na mlikuwa hamsemi?

Akiwa anaongea leo wakati anatangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa CHADEMA, Lissu amesema kuwa utaratibu wa sasa wa CHADEMA wa kutokuwa na ukomo wa madaraka kwa baadhi ya viongozi unatoa nafasi ya kuwepo kwa machawa ndani ya chama hicho.

================================

Kwa hiyo ndani ya CHADEMA nani ni chawa wa Mbowe?


 
Kwani wewe ulifikiri kina MMM, Boniyai na Erythrocyte ni kina nani, ni machawa kama hawa wa ccm tu tofauti ni vyama.

Lissu is right on point!
Hujui kitu, Shut Up! Boniyai ni Mwenyekiti wa Kanda, Maranja ni Ofisa wa Juu wa Chadema official, Erythrocyte ni Mfadhili wa Chama, Hakuna Tajiri awezaye kuwa Chawa
 
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Tundu Lissu wakati akitangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa CHADEMA Taifa amesema CHADEMA haina budi kurudisha...
Namuunga mkono hoja yake.

Ili chama kiendelee kuwa hai kuna ulazima wa kuwepo utaratibu wa kuachiana nafasi.. Haiingii akilini Mtu mmoja kuongoza Chama kwa Zaidi ya Miaka 20 kisha tutarajie mabadiliko..
 
Wakuu,

Kumbe kulikuwa na uchawa pia ndani ya CHADEMA na mlikuwa hamsemi?

Akiwa anaongea leo wakati anatangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa CHADEMA, Lissu amesema kuwa utaratibu wa sasa wa CHADEMA wa kutokuwa na ukomo wa madaraka kwa baadhi ya viongozi unatoa nafasi ya kuwepo kwa machawa ndani ya chama hicho.

================================

Kwa hiyo ndani ya CHADEMA nani ni chawa wa Mbowe?


View attachment 3175140
Erythrocyte Chakaza brazaj
Retired
 
Sijajua kama ni tajiri ila ni Mfadhili wa Chadema, nimeandika mara kadhaa humu kwamba mimi ni mfanyabiashara wa Kimataifa nina miliki kiwanda nchini Tanzania

Unayenifananisha naye ni wapi aliwahi kusema naye ni Tajiri? au umeamua tu kunitukana?
Unaifadhili chadema kwenye nyanja gani kama ni pesa si wanapokea ruzuku za kutosha?
 
BILA KUPEPESA MACHO MBOWE KAA PEMBENI KWA SASA,
#Asante kwa mpaka ulipo kifikisha chama.
HONGERA
N. B, mbowe atakapoondoka wengi watarejea chadema na itakuwa hai tena.


::::::::::
Ni heshima kwa mbowe kusema sigombei tena nangatuka napisha wengine!
Kuna mawili, akae pembeni chama kijijenge upya au ndio chama kife kabisa.
 
Back
Top Bottom