Pre GE2025 Lissu ataka Ukomo wa Madaraka kwenye nafasi za uongozi CHADEMA. Asema itapunguza 'Uchawa'

Pre GE2025 Lissu ataka Ukomo wa Madaraka kwenye nafasi za uongozi CHADEMA. Asema itapunguza 'Uchawa'

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, Tundu Lissu, akizungumza na wanahabari Alhamisi, Desemba 12, 2024, Mlimani City, Dar es Salaam, amesema kwamba ukomo wa madaraka utapunguza upambe na uchawa unaojitokeza pale viongozi wanaposhikilia madaraka kwa muda mrefu katika mazingira yasiyokuwa na ukomo wa madaraka.

Lissu alikumbuka kauli ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyowahi kusema: “Kila nilipokuwa nikitaka kung’atuka walikuwa wakiniambia: ‘Mwalimu endelea tu, hii nchi ni changa na umeitoa mbali. Nchi hii haitaendelea bila wewe.’ Nami niliendelea hadi pale nilipokuja kugundua kumbe nchi changa waliyoiongelea ni familia zao, na hazitaendelea bila mimi kuwepo madarakani, maana walikuwa hawana uhakika kama Rais ajaye atawaacha katika nafasi walizokuwa nazo.”

Lissu pia alieleza azma yake ya kugombea uenyekiti wa CHADEMA Taifa, akisema uamuzi huu ulitokana na hali ya kisiasa ya sasa na kuhitaji uongozi mpya ndani ya chama hicho.
 

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Tundu Lissu wakati akitangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa CHADEMA Taifa amesema CHADEMA haina budi kurudisha utaratibu wa ukomo wa Madaraka kwani utaondoa uwezekano wa Viongozi kung'angania madaraka na kuandaa Viongozi wapya, kupatikana kwa mawazo mapya na itapunguza upambe na uchawa ulioshamiri pale kiongozi anang'ang'ania madaraka pale ambapo hakuna ukomo wa madaraka
Afadhali leo ndio TL amelizungumzia hili, anashangiliwa, kama hakuna ukomo, then hakuna kung'ang'ania madaraka,hili neno kung'ang'ania madaraka ni kumsema mtu kwa mlango wa nyuma!。

Msikilize TL hapa Tundu Lissu kama JPM, ni mtu mkweli. Asema ukweli jinsi ukomo wa uongozi ulivyoyeyuka CHADEMA

Siku nilipoibua hii issue ya ukomo wa madaraka, KM wa wakati huo, Dr Slaa, aliruka kimanga na kuniparua Tuhuma Hii: CHADEMA kuendeshwa kwa Katiba "Fake" ikithibitishwa, CHADEMA inaweza kufutwa

Haya sasa leo TL kayasema, nasubiria kama ataparuliwa!。
P
 

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Tundu Lissu wakati akitangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa CHADEMA Taifa amesema CHADEMA haina budi kurudisha utaratibu wa ukomo wa Madaraka kwani utaondoa uwezekano wa Viongozi kung'angania madaraka na kuandaa Viongozi wapya, kupatikana kwa mawazo mapya na itapunguza upambe na uchawa ulioshamiri pale kiongozi anang'ang'ania madaraka pale ambapo hakuna ukomo wa madaraka

Ili kutekeleza majukumu yanayodaiwa na mazingira ya sasa ya mapambano ya kidemokrasia CHADEMA inatakiwa kuimarishwa katika maeneo mbalimbali ambapo kwanza ni Katiba ya Chama hicho, ambapo amesema Chama kimekuwa kikubwa na hakuna hofu ya kukosa uongozi katika nafasi mbalimbali za chama hivyo chama kinahitaji kurudisha ukomo wa mataraka kama ilivyokuwa mwanzo

Aidha, akizungumzia ukomo madaraka katika nafasi za Ubunge na Udiwani. Lissu amesema "Ukomo wa madaraka unahitajika pia katika suala nyeti la Ubunge na Udiwani wa Viti Malaamu." Amesema mchakato na namna ya kuwapata Wabunge wa Viti Maalumu umeleta mgawanyiko katika chama hicho ambapo mara baada ya uchaguzi wa 2020 ilibidi CHADEMA iwafukuze wanachama karibu Viongozi waandamizi wote wa BAWACHA waliorubuniwa ili kupewa nafasi za Viti Maalumu.

PIA SOMA
- LIVE - Tundu Lissu: Nimewasilisha kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA
Msigwa atajuta kusaliti Chadema!
 
Back
Top Bottom