Lissu haelewi maana ya ‘Jeshi la Akiba’?

Lissu haelewi maana ya ‘Jeshi la Akiba’?

Sheria ya mgambo ilishafutwa.

Ipo sheria mpya ya " jeshi la polisi na huduma za ziada".

Hata kwenye sheria ya JWTZ sijaona hilo jeshi la akiba.

Traditionally, tunaweza kuwa na kitu kinachoitwa jeshi la akiba, lakini sidhani kama ni jeshi rasmi.
Ilifutwa lini?
Unaweza kuweka udhibitisho wa kufutwa kwa hio sheria?
Yeye mwenyewe Lissu katamka kua kuna Jeshi la Mgambo...asichofahamu ni kua Jeshi la Akiba na Jeshi la mgambo ni kitu kile kile...
Hakuna aliemkamilifu, tunapokosea tujifunze kukubali kua tumekosea...huo ndo uungwana sio kutafta visababu vya kujustfy makosa...
 
Peoples' Militia

''Peoples Militia refers to an organized group of people of the United Republic of Tanzania operating with the authority of and under the aegis of the Government and which is receiving military training or is participating in any military training, quasi-military or law enforcement exercise for the protection of the sovereignty of the United Republic or for protection of the people or the property of the United Republic. This does not include the Police Force, any arm or branch of the Défense Force, the Prison Service or the National Service.

The Peoples Militia was introduced according to the Militia Act of 1963 to provide the military with Tanzanian citizens; the peasants and workers who were ready to defend their country as one of the components of the TPDF. The intent of the Peoples Militia was to create a sense of responsibility and national pride in the civilian population by welcoming the citizens to play a role in the Défense of the country.

The government decided to involve the people in defending their villages. The establishment of the militia was also in accordance with President Nyerere’s concept of having a small professional army supported by a majority in the militia. In traditional societies, every able-bodied man was also a fighter when the need arose. The Défense system therefore satisfied the need for Défense and security at the village level. This section provides you with roles of the Militia and the Militia training.''

TL ni mtupu sana.
 
..hili ni jeshi haramu.

..na wala siyo kati ya kamandi cha jeshi la wananchi.
 


Au kaanza kachanganyikiwa?


Swali liko wazi "jeshi la akiba liko kwa mujibu wa sheria gani?"

Msaidie jiwe kufafanua kama wewe unajua. Sisi hatujui. Jibu lako litaweka wazi aliyechanganyikiwa na kuweweseka juu ni yupi.

Kumbuka nchi huendeshwa kwa mujibu wa katiba iliyojengwa juu ya sheria. Kwamba nchi huendeshwa kwa mujibu wa sheria.

Nchi haiendekeshwi kwa kutegemea jiwe kaamkaje kama kwenye teuzi wa za kina katawi - maafisa vipenywa.
 
Jeshini kuna Active Force Na Reserve force Na maana Ya Reserve Force ni Jeshi la Akiba ambalo hapo nyuma liliitwa Mgambo ila kwa sasa ni Jeshi la akiba Na lina MKUU wao kabisa so hapo Lissu kajichanganya sana

Hakuna reserve force Tanzania! . JKT, Polisi, Magereza ndiyo yanatumika wakati wa vita hatuna jeshi la reseve Tanzania wala kisheria. Hata USA hakuna jeshi la reseve kinachotokea ni kwamba kama ulikuwa mwanajeshi zamani ukaacha jeshi unakuwa reseve lakini kuna kitengo maalumu kama Army, Navy, air force au marine ni lazima uwe kati ya hayo. Vilevile Tanzania wahitimu wa JKT ni kama reserve lakini wakihitajika wanaitwa JKT sio Jeshi la akiba!. Hili jeshi halipo kisheria na kuna mbinu zao. Polisi hawajaomba msaada sasa jeshi la akiba la nini! Nani kiongozi wake?
 
Jeshini kuna Active Force Na Reserve force Na maana Ya Reserve Force ni Jeshi la Akiba ambalo hapo nyuma liliitwa Mgambo ila kwa sasa ni Jeshi la akiba Na lina MKUU wao kabisa so hapo Lissu kajichanganya sana
Amejichanganya kivipi wewe ndio unaleta uchambuzi wako ambao na Mimi naushangaa hapa,kwa maelezo ya lisu ameyataja majeshi yaliyopo kwa mujibu wa sheria likiwepo jeshi la mgambo,,,wewe umeleta tafsi unatuaminisha mgambo ndio jeshi la akiba,mavazi yanayo valiwa na mgambo unayajua?Hilo jeshi linalo vaa t-shirt nyekundu ni la wapi mbona huku Musoma sijawahi liona?
 
Ridhiwani Kikwete kuwanunulia kombati jeshi la akiba.

Nyani Ngabu,


..hebu niambieni ni lini mmesikia mtu binafsi kamnunulia Afande Mabeyo uniform?

..huu ni UHUNI umekuwa ukifanyika sema hatukuwa na mtu mwenye ujasiri kukemea.

..sasa Tundu Lissu / Kaka wa Taifa amerudi ndiyo amekuta upuuzi huu.😂

1599093421117.png
 
Hapo ni mjanja mmoja na fisadi mmoja amechapisha T-shirt ili auze apate pesa.
Jeshi la mgambo lina Uniform zake Rasmi na mafunzo yake yanafanyika kwa uwazi bila kijali Vyama.

Lakini pia Watoto wa maskini wanaotumiwa na watawala walioshiba na kuvimbiwa wajitafakari.

Hivi kwa mfano kule Zanzibar kuna mwanajeshi wa akiba atakubali kutumika kuiba kura ili Dr. Hasani alazimishiwe ushindi???
Utakua ni ulevi ,laana ,kufuru, dhambi, uovu,uasi na dhulma kubwa sana .
Mungu hatawaacha siku ya kiyama wale walitakao lazimisha ushindi wa Huseni Mwinyi na yeye mwenyewe kwa sababu ,Mungu amempa Baba yake Urais kwa miaka wa Zanzibar na Tanganyika , Yeye mwenyewe Mungu akampa uwaziri kwa miaka zaidi ya 20 .Sasa anagombea kuomba ridhaa ya kuwa Rais kwa haki.
Akishinda kwa haki Sawa kabisa lakini asikubali kubeba laana mana Mungu amempa kila kitu na fahari zote za Dunia. Anataka nini tena kuvuruga na kuangamiza watoto wa maskini waishi maisha ya kiyatima kwa sababu anataka tena uraisi kwa nguvu. Kodi za wananchi amezila tangu utotoni na uwaziri miaka zaidi ya 20.
Hao wavaa T-shirt za Jeshi la akiba ni vijana wa familia maskini wasikubali kudhulumu ili kuwafurahisha watu wasioridhika na mema yote waliyopewa na Mungu kupitia madaraka.
CCM kwa nini Hanna shukrani hata kwa Mungu.

Hata upande wa bara.
Kuna mtu amekua waziri miaka 20 na Rais miaka mitano lakini bado hataki kutenda haki ili amwambie Mungu nakushukuru kwa uliponifikisha nami nakuahidi kusimamia uchaguzi uwe wa haki nikishinda nitakushukuru na kuendelea kuongoza kwa mapenzi yako lakini nikishindwa pia nitashukuru mana umenipa kupitia wananchi kwa wakati na sasa wananchi wako wamempa mwingine kura.
Vinginevyo kwa kweli nchi zetu maskini tutaendelea kubaki nyuma mana tunajenga na kisha tunaweka mazingira mabovu ya kulinda umoja wetu na matokeo yake tunavurugana na kuharibu hata vidogo tulivyojenga.

Jeshi la akiba ni mgambo na wana uniform zao na hawapaswi kufanya kazi za jeshi kama hakuna vita.
Hii mambo ya matishet ni miradi ya watu walafi .

Hao migambo Wakiwatumikia wananchi wanafanya kazi kwa kusimamiwa polisi.
Hawaruhusiwi kufanya chochote bila kukifisha kituo cha polisi.
Wakifanya kazi chini ya polisi wanaitwa polisi wasaidizi.

Lisu yupo sahihi.

Mkuu wa nchi anashauriwa vibaya na walevi wa madaraka wasiofuata sheria.

Ubababaishaji sasa basi.
 
Ridhiwani Kikwete kuwanunulia kombati jeshi la akiba.

Nyani Ngabu,


..hebu niambieni ni lini mmesikia mtu binafsi kamnunulia Afande Mabeyo uniform?

..huu ni UHUNI umekuwa ukifanyika sema hatukuwa na mtu mwenye ujasiri kukemea.

..sasa Tundu Lissu / Kaka wa Taifa amerudi ndiyo amekuta upuuzi huu.😂

View attachment 1557065
Lini Rizimoko kanunua hizo kombati? Au unaleta fake news?
 
Si kila kitu kinandikwa kwenye sheria...jeshi la akiba ni kamandi ya jeshi la wananchi wa tanzania ambapo majeshi mengine ni majeshi ya nchi kavu,majini na anga.

Kukuthibitishi hilo ndo maana mkuu wake ni afisa wa jwtz na linasimamiwa na jwtz na linapewa mafunzo na jwtz. Na vitambulisho vyao vinasainiwa na afisa wa JWTZ.

Sawa sawa na kusema leo jeshi la wanamaji limewnzishwa na sheria ipi...hitimisho jeshi la akiba ni moja ya kamandi ya jwtz na inasimamiwa na jwtz na linasimamiwa na sheria iliyoanzisha JWTZ
Wanapofanya kazi za ulinzi wa watu na Mali zao hawaitwi Jeshi la akiba.
Ndio maana wakishahitimu mafunzo wakati wa amani wanakua chini ya polisi na vijini wanafanya kazi za polisi mpaka kukamata. Lakini sio Jeshi la akiba na hawawi chini ya Jeshi la wananchi wakati wa amani isipokua wakati wa vita tuu.

Lisu ni Genius wa sheria tukubali wala tusimshauri vibaya Mgombea uraisi wa CCm ambaye ndiye amiri Jeshi mkuu.
Haya majeshi yakitumiwa kisiasa yataleta matatizo sana. Hakuna atakayekua salama.
Kumbuka wao nao wanahitaji kuishi kwa amani na watanzania wenzao wa vyama vya upinzani kwenye nchi yao. Japo CCM wanataka kutawala tu bila kufuata sheria kwa sababu tu wamefanikiwa kuwateka baadhi ya idara za umma kuwa Mali yao kupitia ahadi za vyeo vya kisiasa.

Kwa nini awamu hii ya tano inayomaliza muda wake imetumia muda mwingi kuwapandikiza makada wa CCM kwenye vyombp vya dola na sheria ili kuhakikisha kuwa wapinzani kwa mamilioni yao wote wanaitwa wahalifu na wanashughulikiwa kama wahalifu japo wapo kisheria?
Je, hali hiyo ya chama tawala na Serikali yake kutumia fedha na ahadi za vyeo kuwaumiza washindani wao italiunganisha taifa na kulifanya moja au italigawa taifa na kuwapa askari wa majeshi yetu shida kubwa ya kuweka mambo Sawa kwa sababu tu kuna wachache wamehongwa vyeo na ndugu au marafiki zao?
Rushwa kubwa sasa kwa CCM imebaki kwenye ahadi za vyeo na madaraka mana huko kuna ulaji na kila mtu anaokoa tumbo lake.

Ndio maana Mungu alimponya Lisu na kuondoa Korona Tanzania ili uchaguzi ufanyike kwa haki tupate viongozi watenda haki wasiojenga ukabila na udini na ubaguzi wa kivyama na kuwanyima Watanzania haki ya kuchagua viongozi wao wanaowataka.
 
Uchaguzi mwepesi sana huu
Mpaka ikifika siku ya 20,lissu na timu yake watua hawatoki majumbani mwao wanajisikilizia,kwa jinsi walivyoharibu
 
Si kila kitu kinandikwa kwenye sheria...jeshi la akiba ni kamandi ya jeshi la wananchi wa tanzania ambapo majeshi mengine ni majeshi ya nchi kavu,majini na anga.

Kukuthibitishi hilo ndo maana mkuu wake ni afisa wa jwtz na linasimamiwa na jwtz na linapewa mafunzo na jwtz. Na vitambulisho vyao vinasainiwa na afisa wa JWTZ.

Sawa sawa na kusema leo jeshi la wanamaji limewnzishwa na sheria ipi...hitimisho jeshi la akiba ni moja ya kamandi ya jwtz na inasimamiwa na jwtz na linasimamiwa na sheria iliyoanzisha JWTZ

You are very ignorant of law. Tatizo letu watanzania ni kupenda kutoa mawazo hata maeneo ambayo tu mbumbu kabisa. Ungejua walau definition ya sheria, basi usingeandika ulicho andika. Penda kujisomea na kutafuta maarifa kabla haujaandika au sema kitu. Itakujengea heshima.
 
Back
Top Bottom