Tetesi: Lissu kutua nchini na kesi nzito dhidi ya Bunge na Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Tetesi: Lissu kutua nchini na kesi nzito dhidi ya Bunge na Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Kuna kitu hapa kikizungumzwa wote mtakaa kimya coz either mnajitoa ufahamu na kujitia uchizi msiokuwa nao au hamjui hivyo mnajikuta mnaandika kishabiki zaidi.
Si vizuri kufurahia madhira ya mwenzio lakini sio vizuri vilevile kutumia madhira hayohayo kuwatia wengine ubaya.
Utaratibu mzima wa kumsafirisha TL kwenda Nairobi ulikiukwa na haukufuata sheria. Ulikuwa wakisiasa kwa dhana kwamba akienda M'mbili wabaya wake watammalizia. Rufaa iliyotakiwa ilibidi wampeleke muhimbili, kwa ubishi wa mbowe wakampeleka nairobi tofauti na utaratibu wa bunge kwamba muhimbili wakishindwa ndio bunge linagharamikia matibabu nje ya nchi.
So msifikiri bunge na serikali wamekaa kimya kwa stori zenu za mtaani mkajua hawana majibu au hawajui wanachokifanya.
Km mnakumbuka jpm alimwambia shein kwanini anamsainia maalim seif check zake za matibabu wakati hata salama hataki kupokea.
Sasa huku jeuri kakutana na kiburi/ makusudi .
Aende tu mahakamani ili vituko viendelee tuchangamke kidogo tupate cha kujadili.

..mambo ya ruhusa ya muhimbili yaweke kando kwanza.

..kuna posho ya mbunge aliyeko kwenye matibabu, pamoja na posho ya anayemuuguza.

..TL amesema bunge halijampatia posho hizo.

..zaidi, suala la matibabu ya Maalim Seif ni tofauti na matibabu ya Tundu Lissu.

..Maalim Seif anahudumiwa kwa mujibu wa sheria ya mafao ya viongozi wakuu wastaafu wa SMZ.

..Tundu Lissu masuala yake ni kwa mujibu wa sheria ya mafao na huduma za wabunge.
 
..kuna mambo nadhani manne ambayo bunge lilipaswa kumhudumia.

1. Usafiri kwenda na kurudi ktk matibabu.

2.gharama za matibabu.

3.posho ya mbunge aliyeko kwenye matibabu.

4.posho ya msaidizi anayemuuguza.

..kwa maoni yangu, serekali inaweza kumshinda ktk hoja namba 1 na 2, lakini sioni jinsi gani watamshinda ktk hoja ya 3 na 4.

..lakini ukumbuke kwamba hukumu yoyote inaathiri maamuzi yanayofuatia. Kwa hiyo wakikataa kugharimia matibabu ya TL Nairobi Bunge litakuwa limejifunga mikono kumhudumia mbunge mwingine nje ya Muhimbili na India.
Mkuu nashukuru kwa kulielewa swali langu.
Sasa hoja ya pili ni je kama ni kweli yeye na msaidizi wake wanastahili posho. watastahili kulipwa kwa rate ipi?
Ya kutibiwa TZ au Ubelgiji alikojiamulia mwenyewe kwenda?
Kama ni kwa rates za nje ya nchi, ina maana mbunge yeyote anaweza kuamua kujitibia popote duniani na kulipwa posho kwa international rates yeye na msaidizi wake ili mradi tu asidai usafiri na gharama za matibabu?
 
Sijui kawakosea nini Lissu hadi wanafikia hatua hata ya kubana hadi stahiki zake.
 
..hili suala linaweza lisifike mahakamani.

..linaweza kujadiliwa na kuamuliwa na wabunge wenyewe ktk kamati yao ya huduma na utawala.

..na huko wabunge wengi wanaweza kuwa sympathetic na situation ya mbunge mwenzao, na pia hawatapenda kutoa uamuzi ambao utawakwamisha ktk matibabu yao huko mbeleni.

..Mahakama ni hatua ya mbali na ya mwisho. Suala la Mh.Lissu ni la BUNGENI zaidi.

Na ulichosema hapa ndio busara zenyewe

lazima kuna mahali kuna sheria zao wenyewe ambazo zinakwamisha huyu bwana kulipwa! na kama ujuavyo wengi waoga kufanya maamuzi awamu hii, itahitaji mjadala na maamuzi ya pamoja ili malipo yaendane na minutes za vikao
 
Rais ccm anavunjisha Amani ya watanzania tumkemee kwa nguvu zote.



Swissme
Labda tuanze na wew unataka amani ipi kwa sasa? Ukikaa nyumba ya keyboard utaandika ujinga kaishi kongo ndio kunaamani wew tuache sisi watanzania
 
Kuna kitu hapa kikizungumzwa wote mtakaa kimya coz either mnajitoa ufahamu na kujitia uchizi msiokuwa nao au hamjui hivyo mnajikuta mnaandika kishabiki zaidi.
Si vizuri kufurahia madhira ya mwenzio lakini sio vizuri vilevile kutumia madhira hayohayo kuwatia wengine ubaya.
Utaratibu mzima wa kumsafirisha TL kwenda Nairobi ulikiukwa na haukufuata sheria. Ulikuwa wakisiasa kwa dhana kwamba akienda M'mbili wabaya wake watammalizia. Rufaa iliyotakiwa ilibidi wampeleke muhimbili, kwa ubishi wa mbowe wakampeleka nairobi tofauti na utaratibu wa bunge kwamba muhimbili wakishindwa ndio bunge linagharamikia matibabu nje ya nchi.
So msifikiri bunge na serikali wamekaa kimya kwa stori zenu za mtaani mkajua hawana majibu au hawajui wanachokifanya.
Km mnakumbuka jpm alimwambia shein kwanini anamsainia maalim seif check zake za matibabu wakati hata salama hataki kupokea.
Sasa huku jeuri kakutana na kiburi/ makusudi .
Aende tu mahakamani ili vituko viendelee tuchangamke kidogo tupate cha kujadili.
Mgonjwa mahutuji ambaye hajitambui ajiombee rufaa kwenda muhimbili, yaani mgonjwa wa hali ile kweli alihitaji hizo longolongo kweli?

Mission imefail ndio mnamalizia hasira ya kutomlipia matibabu, ingekuwa nyie ni watu wakufuata msingekuwa mnanunua bombardier kienyeji namna hiyo.
 
Mgonjwa mahutuji ambaye hajitambui ajiombee rufaa kwenda muhimbili, yaani mgonjwa wa hali ile kweli alihitaji hizo longolongo kweli?

Mission imefail ndio mnamalizia hasira ya kutomlipia matibabu, ingekuwa nyie ni watu wakufuata msingekuwa mnanunua bombardier kienyeji namna hiyo.
Nina wasiwasi na uelewa wako. Rufaa anaitoa daktari na sio mgonjwa kuomba. So kwa taratibu zilivyo hosp ya dodma ilitakiwa wamrufaa muhimbili, na ndicho kilicho fanyika. Sasa kwa ubishi wa mbowe akapelekwa nairobi. Hapo serikali itamlipa kwa rate za muhimbili au zile za nairobi na belgium alipolazimisha yeye apelekwe bila kufuata taratibu?
 
Kuna misemo miwili ya Kiswahili inayomfaa mleta hoja;
  1. Kikulacho kiko nguoni mwako.
  2. Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.
 
..mambo ya ruhusa ya muhimbili yaweke kando kwanza.

..kuna posho ya mbunge aliyeko kwenye matibabu, pamoja na posho ya anayemuuguza.

..TL amesema bunge halijampatia posho hizo.

..zaidi, suala la matibabu ya Maalim Seif ni tofauti na matibabu ya Tundu Lissu.

..Maalim Seif anahudumiwa kwa mujibu wa sheria ya mafao ya viongozi wakuu wastaafu wa SMZ.

..Tundu Lissu masuala yake ni kwa mujibu wa sheria ya mafao na huduma za wabunge.
Huwezi kuweka kando taratibu ambazo wamejiwekea wao wenyewe kwa kuwa kuna siku na mwingine akiumwa ataamua kwenda nje osp ya gharama kubwa bila kufuata taratibu na atademand alipwe.
....wanamlipa kwa rate zipi? Za ubelgiji na nairobi? Aliyetoa kibari nani cha kwenda huko?
...na kam mafao yake ni kwa mujibu wa sheria ya mafao ya bunge, ina maana kuna mfuko unaoshugulikia kwanini wasipeleke huko.
..all in all, kubali kataa, taratibu zimekikwa kwa misingi ya kutokuaminiana na mwishowe cdm wanatumia kupigwa risasi tl kama ndio sera yao mpya ya kisiasa.
 
Nadhani cha msingi Kwanza ingekuwa kumuombea afike / awasili salama nchini na hayo mengine ndiyo yatafuata kwani ya Mungu mengi na Shetani nae ana mipango yake vile vile chini ya jua hili.
Mkuu Wewe huwa una Maono na Maneno duuu...
Najaribu Tuu kutafakari maandishi yako uliosema kuwa "Ya MUNGU mengi na shetani nae ana mipango yake"
Ndo bado natafakari Unamaanisha nini?
Ila Bado naendelea kutafakari unamaanisha nini?
Kwaresma hii Ni wakati wa Kuomba,kwa MUNGU!
 
Mkuu Wewe huwa una Maono na Maneno duuu...
Najaribu Tuu kutafakari maandishi yako uliosema kuwa "Ya MUNGU mengi na shetani nae ana mipango yake"
Ndo bado natafakari Unamaanisha nini?
Ila Bado naendelea kutafakari unamaanisha nini?
Kwaresma hii Ni wakati wa Kuomba,kwa MUNGU!

Wala hujakosea Mkuu na kama ukiwa na Upeo mdogo na Mvivu wa Kufikiri siku zote maandiko / mabandiko ya GENTAMYCINE humu Jamvini unaweza usiyaelewe na ukaniona kama vile sijielewi au napoteza tu muda. Nashukuru sana tu kwamba siku hizi kuna Watu sasa wameanza kunielewa na wanaenda sawa na Mimi. Uandishi wangu siku zote ni wa Kumfikirisha Mtu na kamwe siandiki Kiuwepesi nikiamini kuwa humu wamejazana Great Thinkers tupu.
 
Ndio hapo sasa mkuu ila kwa vile tumeamua kila jambo kulifanyia siasa. Ngoja tuone maana tukielezea kiuhalisia wafuasi wa Lissu watatuona wachawi na kuitwa majina ya kifedhea.

All in all lissu akufuata utaratibu kwenye matibabu yake.
Mahakama itaamua wewe endelea kunywa kahawa kijiweni.
 
Afungue tuu maana yule mzee ndumbayi naskia yupi india anakula pesa zetu tu ila lissu kanyimwa,
Hajafa tuu
Hatutaki ushabiki katika hili. Ni jambo zito linalohusu haki na stahiki za mbunge halali. Suala zima la planned assassination ya Lissu lisichukuliwe kimzahazaha. Kuna watu/viongozi wanapaswa kuwa implicated kwenye hii assassination kwa matendo yao ya kumnyima haki zake kwa makusudi na kutoa kauli tata kwa Taifa.
 
Hahahahaaa....

Ngoja nimcheke huyu Bwana miaka michache iliyopita alikuja kuniomba idhini yangu huku mikono ikiwa nyuma na aliahidi meengi mengi mengine yalinipa hamasa na kumpa idhini aweze kuniongoza.

Hiki kichecho kitakua na mantiki Bwana huyu atakapo rejea kunitakana nimuongeze kamuda ka kuniongoza..

Swali langu kwake litakua moja Tu, nitachukua ahadi zote alizoniahidi ( niliziandika na bado naendelea na zoezi la kuzipa tick kwa zile zilizotimizwa)...iwapo hatakua na ufaulu mzuri , alama za tick zikiwa chache nadhani atakua amepoteza imani yangu.

Ngoja nitazame hizi videos tena, nakumbuka vitu vingiiiii...[emoji23][emoji23]

Mambo yako motooooo, mafurikooo sijui nyomiiii...[emoji23][emoji23]wale watu Wako wapi???
 
Back
Top Bottom