Lissu: Kwanini wananchi hawataki kutusikiliza tena

Lissu: Kwanini wananchi hawataki kutusikiliza tena

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Kwenye mahojiano na BBC namsikia Lissu anasema kuwa Mbowe aliyeenda jela sie yule aliyetoka. N watu wawili tofauti. Kwamba baada ya Mbowe kupewa alivyopewa amekuwa mkimya, mpole, Mdiplomasia, n.k. Kwamba wale wananchi waliokuwa tayari kuwafia, kuwafuata, kuwasikiliza na kukifuata chama, leo hii hawafanyi tena yale. Mbowe akiitisha maandamamo wananchi hawatikii...

Hivi kweli Lissu ni wa kusema hayo?
Hivi kweli Lissu haoni aina ya siasa inayofanyika nchini?
Hivi kweli haoni utekaji unaoendelea?
Hivi kweli haoni Mauaji yanayofanyika kwa mgongo wa wasiojulikana?
Hivi kweli haoni vijana wa CDM waliopotea hadi leo hawajapatikana?
Hivi kweli haoni vile Dola inavyotisha wananchi?

Ongezeni yenu.

Halafu Leo Lissu anakuja kusema Mbowe ni sababu ya wafuasi kupoa na kukipa chama mgongo. Inawezekana kweli Mbowe ni sababu katika mtizamo chanya. kwamba kwa sababu ya siasa zake, amesababisha serikali na chama tawala kuwa walivyo leo. Wameshindwa kuhimili upinzani na hoja za chadema. Wameshindwa kuhimili upinzani chini ya Mbowe na ndio maana leo tunaona Dola inaingia na miguu yote kunyamazisha upinzani.

Hivi kweli naona mobilizaton ya vikosi vya polisi nchi nzima na kauli za kibabe na za vitisho toka kwa wakuu wa polisi, bado niingie mtaani kuandamana? Aisee...
 
Mwambie Tundu Lissu naye afanye jinai halafu ashikwe na kuwekwa Segerea. Halafu tumpime akitoka atakuwaje.

Jitu limeharibu MARIDHIANO halafu linataka kuwa Mwenyekiti wa chama??
 
Lissu yuko sahh kabisa, mbowe kwasasa anaangalia maslahi yake...ni kama anataka kujilipa kiinua mgongo kwa kudumu madaraka miaka mingi hivyo hii miaka 5 mipya anayoitaka ya mwisho ana jambo lake maalum!!.
 
Alichosema ni cha ukweli. Lakini nao hawajajiuliza kwanini Mbowe kabadilika hivyo. Mbowe kabadilika baada ya kuwekwa ndani kwa muda mrefu na hakuna wana CHADEMA wala wananchi walioandamana kumpigania atoke ndani. Kwa hiyo ameamua kujipigania mwenyewe.

Hivyo kwasasa Mbowe sio yule wa zamani. Sasa ni Mbowe wa maslahi binafsi. Hivyo ni bora tu astasfishwe kwa heshima kwa kutompa kura.
 
Alichosema ni cha ukweli. Lakini nao hawajajiuliza kwanini Mbowe kabadilika hivyo. Mbowe kabadilika baada ya kuwekwa ndani kwa muda mrefu na hakuna wana CHADEMA wala wananchi walioandamana kumpigania atoke ndani. Kwa hiyo ameamua kujipigania mwenyewe. Hivyo kwasasa Mbowe sio yule wa zamani. Sasa ni Mbowe wa maslahi binafsi. Hivyo ni bora tu astasfishwe kwa heshima kwa kutompa kura.
Tundu Lissu: Aliyenieleza kwa undani mambo ya Rushwa ya Mama Abdul Sasa ni Marehemu
 
Lissu anakosea. Anadhani anajijenga kumbe anaendelea kujibomoa. Hata hao kina Halima Mdee na wenzake tuliona namna ambavyo walikipigania chama na nafasi zao. Tunaona jinsi walivyoporwa kura mchana kweupe. Tunaona jinsi walivyoshambuliwa kipindi wameenda Segerea, ila hatimaye waliungana na Mtesi. Tatizo sio Mbowe wala Lissu mwenyewe bali ni mfumo wa kiutawala uliopo
 
Mwambie Tundu Lissu naye afanye jinai halafu ashikwe na kuwekwa Segerea. Halafu tumpime akitoka atakuwaje.

Jitu limeharibu MARIDHIANO halafu linataka kuwa Mwenyekiti wa chama??
Hakuna maridhiano pale boss, bali ilikuwa kuchorana.
 
Lissu bado anafikiri siasa zasasa nikupiga makelele yakugombana na serikali.Yeye mwenyewe alikosa urais akakimbilia ulaya alivyorudi akawa anapiga piga porojo za hapa na pale asisahaulike.Akumbuke tu kua wenzake wana dola na asijidanganye kuna watanzania wakumpambania nyuma yake zaidi ya porojo za mitandaoni.ngoja tuone yeye atakuaje.Tuupe muda nafasi.
 
Hakuna maridhiano pale boss, bali ilikuwa kuchorana.
Maridhiano haya hapa:-
1. Wakimbizi waliomkimbia Magufuli waliruhusiwa kurudi nyumbani (Lissu & Lema)
2. Kesi za kubambikizwa ziliindolewa Mahakamani (Lissu kesi 3 Mahakama ya Kisutu na wengine wengi)
4. Waliokuwa wanashikiliwa rumande waliachiwa
5. Mikutano ya kisiasa ikaruhusiwa na inafanyika hadi leo
6. Ruzuku ya CHADEMA ikatolewa ambayo ilikuwa imesimama miaka 3
7. Waliodhulumiwa fedha wakarudishiwa including mafao ya Tundu Lissu

Hayo ni baadhi ya mengi ambayo CHADEMA walitaka. Wakati haya yanaendelea Tundu Lissu na Mdude Chadema walendelea kumtukana Rais kwenye majukwaa na kubeza MARIDHIANO ambayo wao ni wanufaika wakubwa.

Kama Tindo utakataa hizo hoja hapo juu ukasema siyo MARIDHIANO basi sina msaada na wewe
 
Lissu bado anafikiri siasa zasasa nikupiga makelele yakugombana na serikali.Yeye mwenyewe alikosa urais akakimbilia ulaya alivyorudi akawa anapiga piga porojo za hapa na pale asisahaulike.Akumbuke tu kua wenzake wana dola na asijidanganye kuna watanzania wakumpambania nyuma yake zaidi ya porojo za mitandaoni.ngoja tuone yeye atakuaje.Tuupe muda nafasi.
Mkuu gigabyte umeliweka vizuri sana. Tundu Lissu ni bingwa au shujaa wa kwenye mitandao, lakini kunako ground hakuna mtu atakayepoteza muda na kumunga mkono. Watu wapo wanaangalia maisha yao na watoto wao
 
Maridhiano haya hapa:-
1. Wakimbizi waliomkimbia Magufuli waliruhusiwa kurudi nyumbani (Lissu & Lema)
2. Kesi za kubambikizwa ziliindolewa Mahakamani (Lissu kesi 3 Mahakama ya Kisutu na wengine wengi)
4. Waliokuwa wanashikiliwa rumande waliachiwa
5. Mikutano ya kisiasa ikaruhusiwa na inafanyika hadi leo
6. Ruzuku ya CHADEMA ikatolewa ambayo ilikuwa imesimama miaka 3
7. Waliodhulumiwa fedha wakarudishiwa including mafao ya Tundu Lissu

Hayo ni baadhi ya mengi ambayo CHADEMA walitaka. Wakati haya yanaendelea Tundu Lissu na Mdude Chadema walendelea kumtukana Rais kwenye majukwaa na kubeza MARIDHIANO ambayo wao ni wanufaika wakubwa.

Kama Tindo utakataa hizo hoja hapo juu ukasema siyo MARIDHIANO basi sina msaada na wewe
Haki za watu wanazopaswa kupewa na watu wastaarabu wenye kuheshimu katiba na haki za binadamu, kweli unaita maridhiano. Kwamba wewe uwekwe chini ili uwatunze watoto wako, halafu ukakubali, utakuwa na akili timamu kujisifia mbele ya watoto kuwa ulibembelezwa kuwatunza watoto ukakubali kwa hiyo wakuheshimu!! Kwanza mfano niliotoa ni irrelevant, maana hii nchi si ya kifalme. Ni ulimbukeni wa madaraka ndio unawafanya viongozi wengi kufikiri wakiwa watawala wanamiliki na haki ya watu wengine kuwa na furaha, huzuni au kuwa hai. Hili si jambo la kujisifia hata kidogo.
Mbona makaburu wa Afrika ya kusini hatuwasikii wakitamba walimtoa Mandera jela, wakaruhusu maridhiano na baadaye wakamuachia Mandera aongoze nchi!! Tuone aibu na kinyaa tunapokunbuka kwamba kuna wakati tulitumia nafasi/dhamana za uongozi tulizopewa kuumiza watanzania wenzetu, Mungu akasikia kilio chao akaingilia kati na huo ndio ukweli.
 
Mwambie Tundu Lissu naye afanye jinai halafu ashikwe na kuwekwa Segerea. Halafu tumpime akitoka atakuwaje.

Jitu limeharibu MARIDHIANO halafu linataka kuwa Mwenyekiti wa chama??
Kwahio wahisi Mbowe kukaa jela miezi 6 na Tundu kupigiwa Risasi zaid ya 17 unaona nani alipata mateso makali?.
 
Mwambie Tundu Lissu naye afanye jinai halafu ashikwe na kuwekwa Segerea. Halafu tumpime akitoka atakuwaje.

Jitu limeharibu MARIDHIANO halafu linataka kuwa Mwenyekiti wa chama??
kumbe mbowe alipokaa ndani alifanya jinai?
 
Tundu Lissu: Aliyenieleza kwa undani mambo ya Rushwa ya Mama Abdul Sasa ni Marehemu
Nilikuwa najihoji mwenyewe bila kupata jibu. Kwamba kwanini mzee Kimbao afutwe katika uso wa walio hai. Dunia haina huruma.
 
Back
Top Bottom