Lissu: Kwanini wananchi hawataki kutusikiliza tena

Lissu: Kwanini wananchi hawataki kutusikiliza tena

Uwe unatumia akili basi ata kidogo mtu kapigwa risasi nyingi mwilini ufananishe na alienda maabusu
Sasa mtu aliyepigwa risasi na moja imebakia mwilini, unategemea atakuwa na akili nzuri
 
Mbona haya unayoyasema HAMKUYADAI kwa Magufuli?? Magufuli aliwateka, aliwaua, alinyang'anya fedha zenu na wengine akawajeruhi. Mama Samia alipokuja akataka kuponya nchi, mkamuona ni DHAIFU na kutaka kumpanda kichwani.

Kama ni haki ya Katiba mlishindwaje kumdai Magufuli??
Kumbe hujanielewa!! Ni mpumbavu peke yake ataona alichokuwa akifanya Magufuri ni cha maana. Kwa taarifa yako viongozi wengi wakatili ndani yao wamejaa uoga mwingi na wasiwasi sana.
Kitendo cha Magufuri kushinda kwa kura kiduchu 2015, tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hakukumuacha salama. Alichofanya ni kuhakikisha anazuia challenge yoyote itakayoibua madhaifu yake.
Mfano kutiliwa shaka kwa elimu yake na Ben Saanane, kwa kiongozi mwenye kujiamini kusingemnyima usingizi, maana wapo viongozi wazuri wenye digrii Moja tu na wanafanya vizuri sana.
Vyama vya upinzani vipo kwa mujibu wa katiba ambayo ndio iliyomuweka madarakani. Aliapa kwa Mungu kwa midomo yake mbele ya watanzania wote kuwa atailinda na kuitii, bahati mbaya wengi huwa tunasahau kuwa Mungu adhihakiwi.
Ni katiba hii ndio imempa na Mama Samia urais. Nimalizie kwa kumnukuu Baba Askofu Dr. Benson Bagonza,Mungu analipenda sana taifa hili,na ukitaka kuthibitisha Kuna gharama kubwa sana.
 
Back
Top Bottom