Lissu: Kwanini wananchi hawataki kutusikiliza tena

Lissu: Kwanini wananchi hawataki kutusikiliza tena

Mwambie Tundu Lissu naye afanye jinai halafu ashikwe na kuwekwa Segerea. Halafu tumpime akitoka atakuwaje.

Jitu limeharibu MARIDHIANO halafu linataka kuwa Mwenyekiti wa chama??
Jela na risasi kumi na sita kipi ni afadhari ?
 
Maridhiano haya hapa:-
1. Wakimbizi waliomkimbia Magufuli waliruhusiwa kurudi nyumbani (Lissu & Lema)
2. Kesi za kubambikizwa ziliindolewa Mahakamani (Lissu kesi 3 Mahakama ya Kisutu na wengine wengi)
4. Waliokuwa wanashikiliwa rumande waliachiwa
5. Mikutano ya kisiasa ikaruhusiwa na inafanyika hadi leo
6. Ruzuku ya CHADEMA ikatolewa ambayo ilikuwa imesimama miaka 3
7. Waliodhulumiwa fedha wakarudishiwa including mafao ya Tundu Lissu

Hayo ni baadhi ya mengi ambayo CHADEMA walitaka. Wakati haya yanaendelea Tundu Lissu na Mdude Chadema walendelea kumtukana Rais kwenye majukwaa na kubeza MARIDHIANO ambayo wao ni wanufaika wakubwa.

Kama Tindo utakataa hizo hoja hapo juu ukasema siyo MARIDHIANO basi sina msaada na wewe
Wakimbizi kurudi nyumbani ni haki yao wala sio hisani. Baada ya shetani magu kuelekea motoni, waliamua kurudi maana walikimbia kulinda uhai wao na wala sio walifukuzwa.
Nani aliwajibishwa kwa hizo kesi za kubambikiwa?
Mikutano ya kisiasa iko kisheria na sio hisani.
Ruzuku ya cdm ni haki yao, tena ilapaswa kuwa nyingi zaidi ya hiyo. Nani alichukuliwa hatua kwa kudhulumu pesa za watu? Maridhiano yalikuwa ni kupatikana kwa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi je zimepatikana? Na ikiwemo na hatua kali kwa walioshiriki kufanya ukatili chini ya dhalimu magu sio zaidi ya hapo.
 
Lissu anakosea. Anadhani anajijenga kumbe anaendelea kujibomoa. Hata hao kina Halima Mdee na wenzake tuliona namna ambavyo walikipigania chama na nafasi zao. Tunaona jinsi walivyoporwa kura mchana kweupe. Tunaona jinsi walivyoshambuliwa kipindi wameenda Segerea, ila hatimaye waliungana na Mtesi. Tatizo sio Mbowe wala Lissu mwenyewe bali ni mfumo wa kiutawala uliopo
Umenena vema. Tatizo ni mfumo wa kikandamizaji wa chama dola. Je, kwa nguvu ya mbowe ya sasa na maridhiano kati ya mbowe na samia unadhani kuna uwezekano wowote wa ku-push hoja ya mabadiliko ya mfumo na yatokee? Mimi sioni. Ndo maana kunaimbwa wimbo wa maridhiano lakini kwenye uchaguzi hakuna maridhiano.
 
Kwenye mahojiano na BBC namsikia Lissu anasema kuwa Mbowe aliyeenda jela sie yule aliyetoka. N watu wawili tofauti. Kwamba baada ya Mbowe kupewa alivyopewa amekuwa mkimya, mpole, Mdiplomasia, n.k. Kwamba wale wananchi waliokuwa tayari kuwafia, kuwafuata, kuwasikiliza na kukifuata chama, leo hii hawafanyi tena yale. Mbowe akiitisha maandamamo wananchi hawatikii...

Hivi kweli Lissu ni wa kusema hayo?
Hivi kweli Lissu haoni aina ya siasa inayofanyika nchini?
Hivi kweli haoni utekaji unaoendelea?
Hivi kweli haoni Mauaji yanayofanyika kwa mgongo wa wasiojulikana?
Hivi kweli haoni vijana wa CDM waliopotea hadi leo hawajapatikana?
Hivi kweli haoni vile Dola inavyotisha wananchi?

Ongezeni yenu.

Halafu Leo Lissu anakuja kusema Mbowe ni sababu ya wafuasi kupoa na kukipa chama mgongo. Inawezekana kweli Mbowe ni sababu katika mtizamo chanya. kwamba kwa sababu ya siasa zake, amesababisha serikali na chama tawala kuwa walivyo leo. Wameshindwa kuhimili upinzani na hoja za chadema. Wameshindwa kuhimili upinzani chini ya Mbowe na ndio maana leo tunaona Dola inaingia na miguu yote kunyamazisha upinzani.

Hivi kweli naona mobilizaton ya vikosi vya polisi nchi nzima na kauli za kibabe na za vitisho toka kwa wakuu wa polisi, bado niingie mtaani kuandamana? Aisee...
Endelea kuogopa
 
Wakimbizi kurudi nyumbani ni haki yao wala sio hisani. Baada ya shetani magu kuelekea motoni, waliamua kurudi maana walikimbia kulinda uhai wao na wala sio walifukuzwa.
Nani aliwajibishwa kwa hizo kesi za kubambikiwa?
Mikutano ya kisiasa iko kisheria na sio hisani.
Ruzuku ya cdm ni haki yao, tena ilapaswa kuwa nyingi zaidi ya hiyo. Nani alichukuliwa hatua kwa kudhulumu pesa za watu? Maridhiano yalikuwa ni kupatikana kwa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi je zimepatikana? Na ikiwemo na hatua kali kwa walioshiriki kufanya ukatili chini ya dhalimu magu sio zaidi ya hapo.
CCM huwa wanaona kila jambo ni hisani
 
Haki za watu wanazopaswa kupewa na watu wastaarabu wenye kuheshimu katiba na haki za binadamu, kweli unaita maridhiano. Kwamba wewe uwekwe chini ili uwatunze watoto wako, halafu ukakubali, utakuwa na akili timamu kujisifia mbele ya watoto kuwa ulibembelezwa kuwatunza watoto ukakubali kwa hiyo wakuheshimu!! Kwanza mfano niliotoa ni irrelevant, maana hii nchi si ya kifalme. Ni ulimbukeni wa madaraka ndio unawafanya viongozi wengi kufikiri wakiwa watawala wanamiliki na haki ya watu wengine kuwa na furaha, huzuni au kuwa hai. Hili si jambo la kujisifia hata kidogo.
Mbona makaburu wa Afrika ya kusini hatuwasikii wakitamba walimtoa Mandera jela, wakaruhusu maridhiano na baadaye wakamuachia Mandera aongoze nchi!! Tuone aibu na kinyaa tunapokunbuka kwamba kuna wakati tulitumia nafasi/dhamana za uongozi tulizopewa kuumiza watanzania wenzetu, Mungu akasikia kilio chao akaingilia kati na huo ndio ukweli.
Mbona haya unayoyasema HAMKUYADAI kwa Magufuli?? Magufuli aliwateka, aliwaua, alinyang'anya fedha zenu na wengine akawajeruhi. Mama Samia alipokuja akataka kuponya nchi, mkamuona ni DHAIFU na kutaka kumpanda kichwani.

Kama ni haki ya Katiba mlishindwaje kumdai Magufuli??
 
Mwambie Tundu Lissu naye afanye jinai halafu ashikwe na kuwekwa Segerea. Halafu tumpime akitoka atakuwaje.

Jitu limeharibu MARIDHIANO halafu linataka kuwa Mwenyekiti wa chama??
Inakuaje wanaofanya jinai wanaachiwa?
 
Kwahio wahisi Mbowe kukaa jela miezi 6 na Tundu kupigiwa Risasi zaid ya 17 unaona nani alipata mateso makali?.
Kwani aliyemuokoa Lissu asipelekwe kutibiwa Muhimbili ambako watu wa Magu wangemmmaliza ni nani? Mnowe ndiye alikataa na mipango ya kumpeleka Nairobi ikaamza kufanyika. Ndipo Mbunge Turky (RIP) wa CCM Zanzibar akakodi ndege.

Ni mtu tu ambaye hana mshipa wa shukrani kama Lissu ndiyo anaweza kusahau yote haya kwa ajili ya kugombea UWENYEKITI wa CHADEMA
 
Wakimbizi kurudi nyumbani ni haki yao wala sio hisani. Baada ya shetani magu kuelekea motoni, waliamua kurudi maana walikimbia kulinda uhai wao na wala sio walifukuzwa.
Nani aliwajibishwa kwa hizo kesi za kubambikiwa?
Mikutano ya kisiasa iko kisheria na sio hisani.
Ruzuku ya cdm ni haki yao, tena ilapaswa kuwa nyingi zaidi ya hiyo. Nani alichukuliwa hatua kwa kudhulumu pesa za watu? Maridhiano yalikuwa ni kupatikana kwa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi je zimepatikana? Na ikiwemo na hatua kali kwa walioshiriki kufanya ukatili chini ya dhalimu magu sio zaidi ya hapo.
Hamna Bwana !! Wakati wa Magufuli MULIUFYATA, akaja mama Samia mkamchukulia kuwa ni dhaifu. Daaada deeeeki.

Sasa chama chenu kinsambaratika, mnagawana mbao kama CUF ya Lipumba, yote hii ni kwa sababu ya kumshabikia MROPOKAJI Lissu
 
Mbona haya unayoyasema HAMKUYADAI kwa Magufuli?? Magufuli aliwateka, aliwaua, alinyang'anya fedha zenu na wengine akawajeruhi. Mama Samia alipokuja akataka kuponya nchi, mkamuona ni DHAIFU na kutaka kumpanda kichwani.

Kama ni haki ya Katiba mlishindwaje kumdai Magufuli??
Onyesha mahali Magufuli aliposifiwa kwa huo uovu aliokuwa anaufanya, kama watu walikaa kimya huo utekaji ulikuwa wa nini? Kama watu walikaa kimya alipora uchaguzi ili iweje? Usitake kuonyesha Samia amefanya wema sana kwasababu kipimo chake ni uovu wa Magufuli. Magufuli alikuwa ni kiongozi muovu ma mlevi wa madaraka, lakini hiyo haimaanishi kuwa Samia ni kiongozi mzuri.
 
Mwambie Tundu Lissu naye afanye jinai halafu ashikwe na kuwekwa Segerea. Halafu tumpime akitoka atakuwaje.

Jitu limeharibu MARIDHIANO halafu linataka kuwa Mwenyekiti wa chama??
Yeye alitaka aambiwe kila kitu,mtu mzima lazima ujue kuficha siri,leo hii yeye anaropoka hata siri na kukataa kufuata katiba aliyoshiriki kutunga.Jamaa anajiona wa muhimu sana
 
Maridhiano ya kijinga, huku watu wanatekwa
Mwambie Tundu Lissu naye afanye jinai halafu ashikwe na kuwekwa Segerea. Halafu tumpime akitoka atakuwaje.

Jitu limeharibu MARIDHIANO halafu linataka kuwa Mwenyekiti wa chama??
 
Onyesha mahali Magufuli aliposifiwa kwa huo uovu aliokuwa anaufanya, kama watu walikaa kimya huo utekaji ulikuwa wa nini? Kama watu walikaa kimya alipora uchaguzi ili iweje? Usitake kuonyesha Samia amefanya wema sana kwasababu kipimo chake ni uovu wa Magufuli. Magufuli alikuwa ni kiongozi muovu ma mlevi wa madaraka, lakini hiyo haimaanishi kuwa Samia ni kiongozi mzuri.
Kama kwenu hakuna mwema kati ya SAMIA na Magufuli badi nyie ni SIKIO la kufa
 
Kama kwenu hakuna mwema kati ya SAMIA na Magufuli badi nyie ni SIKIO la kufa
Samia sio mwema, bali hana tabia za kimagufuli wazi wazi, uchaguzi juzi si imefanyika kilichofanyika enzi za Magifuli. Angechukua hatua dhidi ya waliotenda uovu wakati wa Magufuli huu utetezi wako ungekuwa na maana
 
Back
Top Bottom