Uchaguzi 2020 Lissu: Mawakala wasiporuhusiwa, kura zisipigwe

Uchaguzi 2020 Lissu: Mawakala wasiporuhusiwa, kura zisipigwe

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu amesema kuna mbinu za kuweka mawakala mwaka huu zimekuwa tofauti uklinganisha na miaka iliyotangulia.

Amesema miaka yote wakala anapewa barua ya utambulisho anaenda nayo kituo cha kupigia kura. Kwenye uchaguzi huu Tume ya Uchaguzi ndio inapanga sehemu ambayo wakala atakwenda.

Amesema hali hiyo inaweza leta shida kwa kuwa wakala atapaswa kutafuta kituo chenye jina lake na hivyo kunaweza kutokea uchelewaji wa mawakala kufika vituoni kwa muda watakaotumia kutafuta.

Kutokana na hilo amewaambia wafuasi wake kuwa wahakikishe kura hazipigwi hadi mawakala watakapokuwepo katika vituo vya kupiga kura ili kudhibiti kura zao.
 
Nimemuelewa.

Hata hivyo,kuna hatari kauli hii ikafanyiwa propganda kuaminisha watu kuwa Lissu amewataka wafuasi wake wasiende kupiga kura, hivyo ni bora kauli hii itolewe maelezo ya kuelewaka katika kila mkutano kwa mikutano ya kampeni iliyobaki.
 
Utaratibu huu ukikamilika na kufanyika kwa adabu haina shida,uwezekano wa tume kupitiwa kutoa vituo vya mawakala ni mkubwa kama walivyosahau kuwakumbusha wasimamizi wa uchaguzi kutoa barua za rufaa kwa wabunge na madiwani walioshinda rufaa.
 
Nadhani kuna mahali nimesoma tume walisema watatoa wiki moja ya mawakala kuhakiki majina yao, ili wajue mapema wamepangiwa vituo gani, anyway, may be a'm wrong.
 
Je, ni kwa sababu gani NEC waliamua kubadili utaratibu uliozoeleka?

Wanaendelea kuleta maswali.Wajue tuu wanao mchango mkubwa kusababisha amani au machafuko ya nchi.Yaani pale ambapo kutatokea machafuko kwa sababu tuu eti tume haikuwa imaprtial.Sijui watakavyojisikia mioyoni mwao.

Yaani nchi inabokea mikoni mwao
 
Usanii tu wa NEC-CCM. Kwani hao wasimamizi ni wasimamizi wa Tume ya Mionzi? Wanachofanya wasimamizi, ndio inachofanya NEC. Wanafanya kwa niaba ya NEC.
Utaratibu huu ukikamilika na kufanyika kwa adabu haina shida,uwezekano wa tume kupitiwa kutoa vituo vya mawakala ni mkubwa kama walivyosahau kuwakumbusha wasimamizi wa uchaguzi kutoa barua za rufaa kwa wabunge na madiwani walioshinda rufaa.
 
Back
Top Bottom