Pre GE2025 Lissu, Mnyika na Sugu wakamatwa na Polisi usiku huu. Baadhi ya Waandishi wa habari pia wakamatwa

Pre GE2025 Lissu, Mnyika na Sugu wakamatwa na Polisi usiku huu. Baadhi ya Waandishi wa habari pia wakamatwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limewakamata watu wote waliokuwa ofisi za CHADEMA kanda ya Nyasa akiwemo Makamu Mwenyekiti CHADEMA Bara Mhe. Tundu Lissu, Katibu Mkuu. John Mnyika na Mwenyekiti wa Kanda Joseph Mbilinyi (SUGU) pamoja na viongozi wa BAVICHA.


Pia soma: Jeshi la Polisi lapiga marufuku mkutano wa BAVICHA siku ya vijana duniani

Viongozi hao wamekamatwa mda mfupi baada ya kumaliza kikao cha ndani kwenye ofisi hizo pamoja na viongozi waandamizi wa Bavicha na waandishi wa Habari wa Jambo TV Online waliokuwa wamepiga kambi kwenye ofisi hizo nao wamekamatwa


Lissu aliongea na vyombo vya habari leo ambapo alisema;

1. Kwa vile ofisi ya Kanda ya Nyasa zimetekwa nyara basi Leo atazigeuza ofisi hizo kuwa darasa ameliita ni darasa la kufundisha juu ya ukombozi ,yaani Teach in Resistance.

Pia soma: Msajili apiga Marufuku Kongamano la CHADEMA mkoani Mbeya, asema matamko yao yanahusisha vitendo vya uvunjifu wa amani

2. Kwa vile ofisi za Kanda ya Nyasa zimetekwa nyara Mh LISSU amesema atabaki hapo na ikibidi atalala hapo na amesema na yupo tayari kulala hapo na yeye amesema atakuwa Mwl wa kufundisha Hilo darasa la teach in Resistance. Ila kaomba iwepo namna ya kupasha joto mwili kwa sababu hali ya mbeya ni baridi,amewataka watu wakeshe pale.

3. Kwa vile ofisi za Kanda ya Nyasa zimetekwa nyara basi wataanzia safari Yao kuelekea Ruanda nzovwe kwenye ofisi hizo za Kanda ya Nyasa


4. Kwa vile ofisi za Kanda ya Nyasa zipo mateka amesema wananchi na vijana wasikubali kutishika na Rais Samia, amesema yeye atabaki ofisini hapo kufundisha darasa la teach in Resistance waje wankamatie pale.
Ivi Lissu si alisema atatimkia ccm kama chadema itaacha misingi yake? Nafikiri anashuhudia ccm ilivyo au tuseme huwa ni njaa tu kufuata vyeo ilhali wanajua yaliyoko ccm
Alikwambia wewe kuwa atatimkia CCM?
Alisema chadema si mama yake hivyo ccm inaweza kuwa ndio mama yake halisi, Msigwa anajua madhila ya ccm lakini katimkia huko huko sasa anavaa kijani na kumsifia mama tu muda wote, Tanganyika njaa ndio shida
 
Amiri jeshi mkuu mpaka sasa yupo kimya? Alafu unajipendekeza kudai eti ni msikivu.

Kwa huu unyama aliofanyiwa Lissu, Mnyika na Sugu kulikuwa na haja ya kujikomba na kujipendekeza?

Nia yako kubwa uitwe Ikulu ili ukalambe asali vizuri huku sisi makamanda tunaumia.

Nimesafiri kwa lori toka Mbeya mpaka huku nilipo. Lakini niliteseka sana. Alafu leo unajipendekeza?
 
Ulikua ukamataji wa kijinga sana na policcm ila yule mwanamke atafute jimbo la kugombea kama anataka kurudi bungeni kwa njia ya kura sio hapo tena. Si aliwatuma wale??
 
Ki ukweli, naumia sana kwa kitendo walichofanyiwa viongozi na wafuasi wa CHADEMA kule Mbeya.
Wale ni wafuasi wa CHADEMA lakini ni Watanzania na ni binadamu kama mtanzania na binadamu mwingine yeyote yule. Wamefanyiwa kitendo kisicho cha heshima kabisa. Wamedhalilishwa sana tena sana.
Hawakuwa na silaha yoyote ile, kwa hiyo kulikuwa na haja gani kuwatweza kiasi kile.
Mimi si mwanachama wala mkeleketwa wa CHADEMA lakini kitendo walichofanyiwa si cha kibinadamu hata kidogo.
Ili kuonesha uungwana, ni muhimu utoke hadharani na uwaombe radhi waliotendewa mambo maovu hayo.
Ndugu zangu wa CHADEMA, poleni sana, Mungu ni mkubwa, kwa hakika atawalipa. Duniani hakuna dhuluma isiyo na malipo kwa mtendwa na mtendaji. Mungu mkubwa.
 
Back
Top Bottom