Naomba unijibu hoja hii niliyoipost dakika 20 zilizopita kisha na mm nitakujibu maswali yako yote uliyoyauliza hapo juu.
Kama kweli CCM ilikua inataka kumuua Lisu, kwann haikumuua wakati wa kampeini za uchaguzi??
Na ni kwann kila anachosema Lisu wafuasi wake wote ná mataifa mnaamini??
Mtazamo wangu ni kwamba huyu anatumia taaluma yake kujihami na kesi yake na kuionyesha dunia anaonewa.
Hujui chochote ngoja nikupashe!!
Hivi unajua ni kwa nini alikua anatumia sana umati wa watu na kuzungukwa Mara kwa Mara na umati Huo!!
Hivi unajua waliokua wanamzunguka ni askari polisi waliokua wamevaa kiraia ili kumlinda wakati wa kampeni?
Unajua kuwa akifa mgombea mmoja wa Urais uchaguzi unaahirishwa na inakua ni gharama kubwa sana kwa nchi?
Hivi unajua kuwa kumuua mgombea wakati wa kampeni kungeweza kuleta visasi vikubwa sana na kuiingiaa nchi kwenye machafuko makubwa mana matumaini ya watu kwa mgombea wao ni mkubwa sana kwa kila chama?
Unafikiri ni kwa nini CCM kupitia Mwenyekiti wa UVCCM Mh.Kheri walitoa tamko la kumchoma Lisu sindano ya Sumu? Hizo hazikuwa njama za kumuua?
Hivi unajua unapotaka kuestablishi utawala wa kidikteta na kujenga hofu kwenye jamii ili watu waufyate mkia mauaji huwa yanafanywa mchana kweupe ili iwe kuwatia adabu wanaojifanya wakorofi?
Unajua Korea ya Kaskazini waziri akikosea anaoigwa Kombora akiwa kwenye gari mchana kweupe?
Unajua hata wakati wa Ukoloni wa wajerumani watu walinyongwa mchana kweupe ili kuwafanya watu watii sheria za mkoloni na kumwogopa mkoloni??
Hivi unajua hata magaidi wanapowateka watu na kuwalazimisha watii sheria zao kitu cha kwanza ni kuwaua wale wanaopingana nao kwa kuwakata vichwa mchana kweupe ili anayejaribu kuwasaliti au kukimbia na kuachana na ugaidi atiwe hofu na kubaki kuwa mtiifu?
Usifikiri kuirudisha Tanzania kwenye mfumo wa chama kimoja na kudumisha fikra za mtu mmoja litakua ni jambo la kuwalisha watu tende na halua ; Tukiamua kurudi huko nyuma kwenye chama kmoja jiandae kuona rangi na harufu ya vimiminika vyekundu vikitoka kwenye miili ya watanzania wengi wanaopinga au kukosoa wakubwa.
Itafikia mahali hata kumkosoa Mtendaji kata itakua ni vigumu kwani jioni watakuja vijana wa uvCCM na kukumiminia risasi na kusepa zao na uchunguzi utafanywa na wakereketwa wenyewe ndani ya vyombo vya ulinzi na kusema kuwa ni majambazi.
Damu za watu hua inalipwa kwa damu ndio msingi wa karma.
Usione hata Rwanda au Uganda wapo pale baada ya waliojiona wababu miaka iliyopita waliwaua watu kwa maelfu na malaki .Damu zikawa zinalilia kisasi.
Walichokosea Wanyarwanda na Waganda kupiga Kagame na Museveni ni kutoweka maridhiano badala yake wanatawala kwa damu tena . Mbaya zaidi watamwaga damu zisizo na hatia. Asil ya Mungu haitawaacha salama wajukuu zao watakapokufa wao na wale waliowaingiza kwa damu. Damu zinazomwagwa inalilia kisasi. Miaka michache ijayo Uganda italipuka na museveni atazeekea kubaya kumbe angeitisha maridhiano angekua amefaulu sana duniani na ahera.
Wamelewa kwa Mali .
Wamelewa kwa madaraka.
Wamelewa kwa ulinzi walio nao!!
Laana ya mwenyezi Mungu iwe juu yao.