Pre GE2025 Lissu: Tutazuia uchaguzi kwa njia mbalimbali ikiwemo maandamano kama hakutokuwa na mabadiliko

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Lissu amesema watatumia njia mbalimbali kuzuia uchaguzi, ameeleza pia no reform no election maana yake siyo kususia uchaguzi.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Ameeleza pia kuwa zipo njia mbalimbali za kuzuia uchaguzi ikiwemo kuitisha maandamano nk.
Your browser is not able to display this video.

Soma: Pre GE2025 - Tundu Lissu: Kauli ya No Reform No Election hatujasema tunasusia Uchaguzi. Tutaongea na Rais Samia lugha atakayoielewa
 
Sera ya vyama vingi hapa kwetu ilishinikizwa kuanzishwa kutokea huko duniani. Ila cha ajabu hawa fuatilii input yake..

Badala yake kwa sasa tunaona pesa nyingi na nguvu ya dola kutumika kwenye maigizo ya uchaguzi..

Tumetoka kwa wakoloni sasa tuna tawalana wenyewe kwa wenyewe. Asee yote kulinda matumbo Shikamooo Njaa...
 
Anaota ndoto Za mchana!! Kiherehere chote kitamuisha Ana akili Za kitoto sana!! Akili zote zimemezwa na tumbo
 
MUNGU atupe uhai tujionee hii No reform No election.
 
Bado hujajipendekeza kwa ccm, utajipendekeza sana. Kwa nongwa hii hakuna rangi utaacha kuona.
 
Lissu anahitaji kui fine tune message yake.

Kusema kwamba watazuia uchaguzi hatoeleweka.
 
Kama Chadema mna njia zaidi ya moja kushinikiza kuzuia uchaguzi, nawashauri njia ya maandano msiitumie. Mkiitumia mwe na hakika ni mtapata hasara kubwa sana ikiwemo kupoteza uungwajj mkono wa wananchi wasio wanachama wenu ambao wanatamani kuona mambo tofauti kupitia kwenu.
 
Mbowe aliandamana akajikuta yupo na binti yake tu. Mbinu ya maandamano imefeli
Na ukiona unatumia njia ya maandamano mara kwa mara na matokeo ni yale yale basi ujue una mushkel kichwani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…