Pre GE2025 Lissu: Wala rushwa au wapokea rushwa hawafai kua viongozi, wawe CCM au CHADEMA, watauza nchi

Pre GE2025 Lissu: Wala rushwa au wapokea rushwa hawafai kua viongozi, wawe CCM au CHADEMA, watauza nchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ataach
Lakini mpina kasema kuwa wafanyabiashara walihonga Ikulu 6 bill kupata vibali vya sukari

No kweli tumeathirika na vitendo vya rushwa, vinavyofanywa na serekali hii sisi wanyonge tunanunua sukari kwa sh 6000 kwa kilo

Huo ufisadi wa cdm hatuuujui na Hauna madhara kwa nchi na wananchi

Kijana kazi ya uchawa kwako ni ngumu tafuta kazi nyingine
Ataachaje mwenzio unataka afe njaa!? 😂 yupo kazini hapo
 
Lakini mpina kasema kuwa wafanyabiashara walihonga Ikulu 6 bill kupata vibali vya sukari

No kweli tumeathirika na vitendo vya rushwa, vinavyofanywa na serekali hii sisi wanyonge tunanunua sukari kwa sh 6000 kwa kilo

Huo ufisadi wa cdm hatuuujui na Hauna madhara kwa nchi na wananchi

Kijana kazi ya uchawa kwako ni ngumu tafuta kazi nyingine
Ufisadi upingwe na kila mtu
 
Lakini mpina kasema kuwa wafanyabiashara walihonga Ikulu 6 bill kupata vibali vya sukari

No kweli tumeathirika na vitendo vya rushwa, vinavyofanywa na serekali hii sisi wanyonge tunanunua sukari kwa sh 6000 kwa kilo

Huo ufisadi wa cdm hatuuujui na Hauna madhara kwa nchi na wananchi

Kijana kazi ya uchawa kwako ni ngumu tafuta kazi nyingine
Lissu ndio kasema kuna rushwa ya kutisha ndani ya Chadema, mimi nausikaje kwenye ujambazi wa Chadema mkuu?
 
Hivi mlimuona wapi Mchaga mpigania haki, wachaga ni wapigania hela. akienda huko ni kwa malengo maalum
 
Lissu ameendelea kurusha jiwe gizani.

Safari hii ameikemea rushwa wazi wazi hata iliyo ndani ya chama chake CHADEMA. Lissu hajapepesa macho wala kuangalia sura ya mramba asali.

Wataalam wa mambo ya siasa za kusini mwa jangwa la sahara wanasema huu ni muendelezo wa kukosoa tuhuma za rushwa na wizi wa kura uliofanyika kwenye chama chake.

=======
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu amewataka Watanzania kutowakubali Viongozi wanaotoa au kupokea rushwa kwakuwa hawafai, bila kujali Watu hao ni wa Chama kipi au Dini ipi.

Akiongea akiwa Itigi Mkoani Singida leo June 17,2024, Lissu amesema “Watu wanaotoa rushwa na kupokea rushwa hawafai kwenye Uongozi, wawe CCM, wawe CHADEMA wawe Dini yoyote, hawafai kwasababu akipokea au kutoa rushwa atakuuza tu, msikubali Watu wasiokuwa wa haki”

"Watu wa haki, watu wasio kula rushwa, wasiotoa rushwa, wanaotoa rushwa hawafai, wawe CCM, Wawe CHADEMA, wawe dini yoyote, watoa rushwa na wapokea rushwa hawafai kwenye uongozi kwa sababu akitoa rushwa au akipokea rushwa atakuuza tu, atakuuza tu, usikubabali watu wasiokuwa wa haki, usikubali CCM."

Pia soma: Tundu Lissu: Rushwa za CCM kujaribu kuibomoa CHADEMA ni nyingi mno
Huyu Mwamba Mungu amuweke sana
 
Asisahau pia kuueleza umma nini CHADEMA watafanya wakipewa mamlaka mbali na kutuonyesha maovu ya CCM pekee.
Hili liko wazi....kwamba Chadema hawawezi kule Wala Rushwa.....sasa unataka waseme nini ambacho huelewi
 
Huyu Lisu ni mtu wa namna gani? Natamani aweke bayana anahitaji nini? Na akipata nafasi ataifanyia nini nchi hii labda kwasababu uwasilishaji wake wa kukera umenifanya nisiwe mfuatiliaji mzuri wa mawasilisho yake hasa pale anapo weka mbele kutukana kila mtu na kuona yeye pekee ana akili kubwa.
Hatahivyo bado nina hamu ya kumpata kiongozi jasiri iwe kutoka chama chochote ambaye ataboresha kidogo kutoka kwa Tundu Lisu na kuchanganya hitikadi za Mandele,Nyerere,Magufuli,Makonda,jaji Chipeta,Jaji Mwalusanya,Gaddafi. Kwa uchache niliowataja wana vitu vizuri na vibaya lakini tuchukue mazuri yao na kusimamia utekelezaji kwa kuweka yale mazuri kuwa dira ya Taifa. Mfano Mchungaji Mtikila alikuwa anaongea mambo mazito ambayo pia yalihitaji watu sahihi wa kuyasimamia japo kuwa naye uwasilishaji wake ulikuwa kama wa huyu jamaa. Matatizo yaliyomkuta Tundu na Mtikila inawezekana yanatokana na kufanya uwasilishaji wa kukera na kuudhi ingawa katika hoja hizohizo angeweza kufikisha ujumbe kuntu bila kuleta athari kwao.
Nchi hii ni kweli tunahitaji Haki tulipo tawaliwa na wakoloni Haki ya Mwafrika na wengine wachache ilipotezwa tunalojukumu kubwa kuirejesha Haki kwa upana wake mbaya zaidi hawa jamaa walipandikiza kitu ambacho ukandamizaji wa haki umerithiwa na Sisi kwa sisi.Ubinafsi,wizi na uroho,dhuluma na upendeleo ni watoto wa baba mmoja na uvunjifu wa haki hapa ni lazima wawepo watu ambao wanaweza kujitoa na kupambana na jinamizi hilo ambalo ukikosea lazima ile kwako.Kujituma katika kazi zenye kuleta tija ndiyo mzizi wa fitina lakini ni lazima tupate viongozi wenye nia thabiti pamoja na kwamba nimemtaja Makonda miongoni mwa wanaotakiwa kuchukuliwa maarifa yao lakini sikubaliani na namna anavyofanya kwa kukashifu au kutweza watu kinyume na ile kanuni yangu ya kwanza ya kutunza na kuhifadhi Haki nafikiri nijambo jema kama kungekuwa na check and balance yeye alitakiwa kusimamia viongozi wote wasiotimiza wajibu wao na kupelekea hali kuwa mbaya ya uvunjifu wa Haki ili akina Makonda wawe kila mtaa,kitongoji,Kijiji,kata Tarafa,Wilaya,Mkoa na Taifa kwaujumla.
Mahakama ndiyo chanzo cha kupoka Haki sijui ni kwasababu hawajui majukumu yao au umungu mtu umewatawala au inawezekana kunasababu iliyojificha ingawa wapo wachache angalau wanajaribu kufanya vizuri lakini wengi wao wanaofanya ule msemo wa samaki mmoja akioza wote wameoza hawa pia wanatakiwa kuwekewa tochi kubwa ya kufuatilia vituko wanavyovifanya na maamuzi yao ya kutatanisha yawekwe hadharani ili wananchi waweze kuwajadili na kuwapa ushauri labda wataona aibu.
Kuna watu wazuri wapo katika vyama vya Siasa lakini pia wabaya wapo kinachotakiwa ni uwezo wa kuwabaini na kuwapa wanachostahili.
 
Asisahau pia kuueleza umma nini CHADEMA watafanya wakipewa mamlaka mbali na kutuonyesha maovu ya CCM pekee.
SAWA Kabisa, lakini ajenda ya kuiondoa CCM kwa maovu inayoyatendea taifa letu ni ajenda tosha kabisa, hata bila kuingia ndani kuhusu wanayotarajia kuyafanya CHADEMA.
Kwa mfano: Kukomesha rushwa - kama CHADEMA wataweza kufanya hivyo, hiyo ni ajenda yao tayari. Hali ni hiyo hiyo, hata kwa hayo mengine.
 
Umejuaje "uchungu na kuumizwa". Unacho kifaa cha kuyapima haya?
unavyo tukana tu, inaonyesha una maumivi makali mno moyoni na akilini, ukiona mtu ana maoni na mtazamo tofauti na yako 🐒
 
unavyo tukana tu, inaonyesha una maumivi makali mno moyoni na akilini, ukiona mtu ana maoni na mtazamo tofauti na yako 🐒
Kumbe. Hicho ndiyo kipimio chako?
Basi, kumbe ninayokupasha yanakuingia vizuri akilini mwako. Chukuwa muda kuyatafakari, kuna siku utaona ukweli wake ulipo.
 
Back
Top Bottom