Uchaguzi 2020 Lissu: Watanzania sio kwamba hawana akili bali Lugha ya kufundishia ndio shida, Elimu yetu inabidi ifumuliwe na lugha ya kufundishiwa iwe moja


Mkuu, kwenye swala la ubora wa elimu na mfumo mzima wa elimu nakubali ni mbovu unatakiwa kubadiliswa. Ubora wa elimu haupimwi kwa lugha inayotumika kujifunzia na kufundishia, bali unapimwa kwa mtaala. Sasa mfumo ukishabadilishwa automatically kutakuwa hakuna kukariri tena na hiyo lugha haiwezi kuwa changamoto maana zitatumika mbinu za kufundishia na kujifunzia ambazo zitamjenga mwanafunzi kuelewa zaidi na kuwa na basic life skills.
 
For the time being,vaa hata suruali zenye viraka ila mwanao mpeleke shule za english medium!
Mwanao atakushukuru baadaye!
 
For the time being,vaa hata suruali zenye viraka ila mwanao mpeleke shule za english medium!
Mwanao atakushukuru baadaye!

Kwani huko kwenye shule za medium kuna mitaala tofauti na hii ya Kayumba? Bora uniambie nifunge mkanda nimpeleke mtoto International school, sio hizi medium school hamna kitu huko zaidi ya kuongea kingereza tu ambacho nuikienda kwa Ras Simba mwezi tu nakiongea vizuri.
 
Mpeleke huko kama una uwezo,ukishindwa international school mpeleke english medium ili apate msingi mzuri!Ila ukimpeleka Kayumba,unampa zigo kubwa huko mbeleni!
Kuhitimisha tu ni kwamba Hoja iliyoko mezani ni muhimu!Tumekosa viongozi wenye uthubutu kufumua mfumo wa elimu!Walau Lissu ameanzia hapo kusight tatizo ambalo lipo!
 

Hoja kuhusu ubora wetu wa elimu ina mashiko, na sio kwamba wahusika hawajui au hawaoni..wanajua vizuri tu. Ila watunga sera ndio wamejaza siasa tu katika utendaji wao. Taasisi ya elimu Tanzania wako na mitaala mizuri tu na wamefanya review nyingi na kutoa mitaala bora kabisa ila imefungiwa kabatini tu haitumiki na hakuna anae push kuipeleka mashuleni. Tumekalia vitu vidogo kama lugha wakati tatizo la msingi lipo na hatutaki kuliona, Ukiangalia hapo ndio utajua labda kuna agenda flani iliyofichwa na tunapelekwa nje ya mstari makusudi tu.

Hata alieibui hili ni mwanasiasa tu na anachukulia advantage ya wakati na udhaifu uliopo, haja address tatizo la msingi kwenye mtaala uliopo, hajatoa mbinu zitakazo tumika kuipandisha elimu yetu. Kakomalia kipengele cha lugha tu ambacho lugha sio kitu unaweza kujifunza popote tu na wakati wowote, jambo la msingi ni yale maarifa unayoyapata shuleni unaweza vipi kuyatumia? Wachina wanasoma kichina mwanzo mwisho ila kazi wanakuja kufanya Tanzania ambako hakuna kichina, kuna kiswahili na kingereza kidogo ila kazi zinafanyika maana wana ujuzi na weledi wa kutosha kwenye kile walichosomea. Ujuzi ndio msingi wa ubora wa elimu sio lugha.
 
Sawa lakini unarudiarudia kilekile ambacho nimeshakiongea!Shida sio kiingereza!Lazima ukubali huwezi kupata maarifa bila lugha,lugha ndio msingi wa kuhamisha maarifa!Sasa hapa kinachosemwa tuchague moja!Kama ni kiswahili basi iwe kiswahili,kama ni kiingereza iwe kiingereza!Huko china unapopatolea mfano ni kwamba wao wanatumia lugha yao na wamechagua hivyo!Lakini wao wana advantage kwa maana teknolojia yao ipo juu!So hata vifaa na mitambo wanatengeneza wao na kuwa programmed kwa lugha yao!Hata mifumo ya computer wametengeneza kwa lugha yao!
Sasa tukisema tutumie kiswahili,tutakuwa tunazalisha changamoto mpya nyingi sana kuliko kutatua changamoto!
Pamoja na kwamba kuna matatizo kwenye mitaala lakini pia lugha haikwepeki!
Kama taifa dogo linalokua,tunakihitaji kiingereza!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…