Uchaguzi 2020 Lissu: Watanzania sio kwamba hawana akili bali Lugha ya kufundishia ndio shida, Elimu yetu inabidi ifumuliwe na lugha ya kufundishiwa iwe moja

Uchaguzi 2020 Lissu: Watanzania sio kwamba hawana akili bali Lugha ya kufundishia ndio shida, Elimu yetu inabidi ifumuliwe na lugha ya kufundishiwa iwe moja

Hatuendelei na kupata wasomi wakutuondolea matatizo yetu hadi tukubali kama kiswahili ni rahisi kufahamika kuliko lugha zengine.

Kiengereza kiwe ni lugha ya pili, sio ilivyo sasa hadi sheria za nchi kwa lugha ya kigeni.

Hili tatizo la kukumbatia kiengereza ni la colonial mentality.
Kusema tu ni colonial mentality haisadii. Tatizo watanzania wengi tunapinga colonial mentality kwa maneno wakati maisha yetu yote yamejengeka kwenye hiyo dhana. Kujitegemea kwa kutumia lugha yako ni jambo linalohitaji commitment ya hali ya juu ambayo hawa wanasiasa wetu uchwara hawana. Wao wamebakia kung'ang'ania madaraka tu na kuabudiwa kama miungu japo kuongoza kumewashinda.
 
Ukiona zaidi ya 90% wanakumbana na changamoto hiyo,basi jua kuna tatizo hasa la msingi linalohitaji utatuzi!
Wangekuwa wachache ndio wanakuwa wabovu,basi tungesema ni uzembe wao!Lakini tunakwepa nini,ni ukweli ulio wazi kuwa watanzania wengi wanamaliza vyuo hawajui kiingereza vizuri kile tu cha kuwasiliana!Fikiri tu PhD holder,Dr Magufuli kiingereza ni kasheshe,bado unaona ni uzembe?Kwanini huoni ni tatizo la mfumo wa elimu?
Mkuu hujaelewa mfano wangu,nimesema mwalimu alikuwa analazimika kutumia kilugha ili wanafunzi waelewe!Mwisho wa siku mpaka wanamaliza darasa la 7,unakuta mtoto kashaadopt na anajua kiswahili!Hii ni kwasababu lugha ya kufundishia ni kiswahili na anajikuta yuko mazingira ya watu wanazungumza kiswahili shuleni,ndio maana akaweza kujifunza taratibu!Hapo inamaana hata tungeweka mazingira ya kiingereza shuleni na ikawa lugha ya kufundishia,mtoto angeweza kuadopt na kujifunza kiingereza!
Tuchague moja,kama ni kiswahili basi na iwe hivyo kuanzia msingi mpaka chuo kikuu na kama ni kiswahili iwe hivyo msingi mpaka chuo kikuu!
Hapa tulipo tupo katikati!
Naunga mkono msimamo wako. Tanzania tulichokosea ni kujaribu kutumia lugha chotara e.i. kiswahili na kiingereza kufundishia. Na mbaya zaidi ikatokea hata wale wanaostahili kufundisha lugha hawajui lugha yenyewe. Sasa hivi wananchi wengi hawajui kuandika kiswahili na kiingereza ndiyo kabisa. Mbona Kenya kiingereza chao ni kizuri tu. Hata ukiangalia vikao vyao chini kabisa wanazungumza kiingereza ambacho Bunge letu haliwezi kutumia.
 
Umenena vyema Kiongozi
Mkuu shule nilizopita ni Mazengo,tukahamishwa baada ya kugeuzwa kuwa st John university,nikaenda Moshi tech,nikaenda kibaha high school na baadaye UDSM!Huko kote nilikopita hakukuwa na hayo masuala ya vibao wala speak English!Kidogo nilikuta msisitizo Kibaha!
Mkuu ukiona asilimia 90 ya wanafunzi wanaopita Kayumba wanamaliza vyuo na kiingereza kibovu au kisichoridhisha,jua kuna tatizo!
Hao akina Lissu ni kati ya wachache walioweka pengine jitihada za ziada,pia masomo yake ya sheria yakamsaidia maana kuna kujieleza kwingi na case zinakuwa kwa lugha ya kiiingereza!Hiyo inawapa advantage wanasheria ya kujifunza kiingereza kwa lazima!Mchepuo kama wa uhandisi ni majanga,huko kiingereza ni technical language ya field husika na unafaulu vizuri tu!Upewe mike ujieleze hata dakika 10,majanga!
Bado narudia,medium schools zinafanikiwa sana,hata ambao tumesoma nao unaona kabisa huyu katoka sehemu fulani tofauti na mimi japo kufaulu mnafaulu wote lakini yeue anakuwa na kitu cha ziada,lugha!
Tunaweza kukawa na tatizo kwenye mitaala,lakini hili la lugha pia halikwepeki!
Mimi napendekeza kiingereza kama lugha ya kufundishia ianzie msingi,japo tutakuwa na kazi kubwa ya kufanya maana hata walimu nao hali ni ile ile!Mfano kipindi cha Corona kuna utaratibu wa walimu kwa kushirikiana na Tv stationa walianzisha wa kufundisha kupitia luninga!Mmmh kuna siku nilijikuta naangalia ufundishaji,aisee nilijikuta aibu naona mimi nikabadili na channel!
Hoja ya Lissu ni ya msingi sana,chama kitakachochukua hatamu naomba waichukue na iwe kwenye agenda za elimu!Uanzishwe mdahalo utakaoshirikisha wadau wa elimu kwa kuzingatia na uzoefu kwa majirani zetu kama Kenya na Uganda tuamua tunashika njia ipi once up for all!
Hapa tulipo tumekwama,tusipuuze hoja hii!Tuichukue na ifanyiwe kazi tupate majibu
 
Magufuli and I like listening to Tundu lissu for there are so many things to learn as far as the history of this country's concerned. he's a history & political class on it is own. lissu doesn't speak like regular politicians do. he speak as an intellectual who's passionate about justice
Natamani ni like mara "Mia Oja"
 
Mnapo
Mkuu Chige umemaliza yote. Na zaidi alichokuwa anamaanisha Lissu ni kuwa english ni moja kati ya nyenzo za kazi ambazo majaji wetu wanatakiwa waifahamu. Mazingira ya kufanyia kazi mahakama kuu na jaji kwa ujumla yanategemea sana lugha ya kiingereza hivyo kama jaji hakijui vizuri ni shida na hataweza kutenda kazi vizuri. Hii inaonyesha kuwa jinsi tunavyoteua majaji wetu kuna walakini. Na sishangai sana kwani mambo ya uteuzi hapa Bongo siku hizi yameacha kufanyika on merit na badala yake yanatumia vigezo vya milango ya nyuma. Na hii siyo kwa upande wa majaji tu bali hata kwenye mainjinia, madaktari nk utakutana na wahitimu ambao uelewa wao ni zero kabisa. Unaweza kuamini kuna mtu amemaliza Phd na kuandika thesis za kiingereza lakini sasa hivi ukimwambia aandike insha ya karatasi moja kwa kimombo hawezi? Hapa kuna tatizo zaidi ya uelewa wa lugha...
Mnaposema Lissu anajua kuongea Kiingereza mnamaanisha nini?
 
Lugha yetu ya taifa ni kiswahili sasa anataka Kiingereza kiwe kama lugha yetu? Kwani Muingereza anaongea Kiswahili kama Mtanzania?
Sawa ila sio lugha inayotumika kwenye kuendesha mambo kikatiba! Documents nyingi za kiserikal huandaliwa kwa kingereza na kama unabisha subr uletewe nots ya mahakama ndio utaelewa zaidi kuwa pombe si chai
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua Kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka Kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu. We want to make Tanzania great nation, Kiswahili ni ajenda kuu.
Nafikiri nyie ndio walengwa haswa wa hii mada kwani inaonekana lugha ya kufundishia imekuathiri vibaya kiasi kwamba hata reasoning inakuwa ndogo.

China imefika hapo ilipo kwa sababu ya watu wake kutia bidii katika kujifunza kiingereza na ndio lugha ambayo imewasaidia katika kukuza Export Economy yao.

Ebu ingia kwenye Website ya Alibaba ujaribu kuagiza bidhaa toka China uone ni lugha gani wanatumia kisha ndio urejee humu na hizo hadithi za abunuasi.
 
Tuboreshe kiingereza kwenye mfumo wa elimu; kuacha kutumia kiingereza kuna hasara nyingi kuliko faida. Sisi tuongee kiswahili chetu, tujifunze kichina, tujifunze kihindi, kirusi na nyingine zenye faida kwetu kiuchumi na kijamii. Tanzania sio kisiwa

Yeye Tundu zile kazi anazowafanyiaga Mabeberu zinakuaga kwenye lugha gani?
 
Tundu Lissu amesema haya kuhusu lugha ya kufundishia:

Ukiniuliza mimi, honest opinion Nchi yetu haiwezi kuzungumza Kiingereza, hivyo tunahitaji kuwa na mjadala juu ya sera ya lugha, tusipokuwa na mjadala huu, hatufiki popote kwani language of instruction is everything.

Mimi ni Wakili, Majaji wengi hawajui kiingereza, ukienda Nchi za wenzetu huko Mtanzania akiongea unatamani kuingia uvunguni mwa meza, Kiingereza chetu ni kibaya, sio kwasababu hatuna akili ila ni kwasababu tumekosa Sera ya Lugha.

Tangu tumepata Uhuru tumekua na ndimi mbili kuhusiana na lugha na ndimi mbili ni hatari, ulimi mmoja tumesema Kiswahili ni lugha ya Taifa na tumeiendeleza kwelikweli, ulimi wa pili tumesema Kiswahili si lugha ya kufundishia.


Fikiria tu muda Mtu anaotumia kujifunza Kiingereza ajifunze na aelewe miaka 4 tu ya Sekondari anakuwa hajaelewa Kiingereza sawa sawa na anakwenda tena form 5 na 6 bado anakuwa vilevile, kwa kifupi Watu wetu hawajui Kiingereza.
Wakala wa beberu huyu! Mbona walipanda ndege wakaja hadi huku kuongea na jiwe kuhusu makinikia! Wajifunze wao kiswahili acheni ukoloni mamboleo! Lissu hapati kura ng'ooo
 
Ukiona zaidi ya 90% wanakumbana na changamoto hiyo,basi jua kuna tatizo hasa la msingi linalohitaji utatuzi!
Wangekuwa wachache ndio wanakuwa wabovu,basi tungesema ni uzembe wao!Lakini tunakwepa nini,ni ukweli ulio wazi kuwa watanzania wengi wanamaliza vyuo hawajui kiingereza vizuri kile tu cha kuwasiliana!Fikiri tu PhD holder,Dr Magufuli kiingereza ni kasheshe,bado unaona ni uzembe?Kwanini huoni ni tatizo la mfumo wa elimu?
Mkuu hujaelewa mfano wangu,nimesema mwalimu alikuwa analazimika kutumia kilugha ili wanafunzi waelewe!Mwisho wa siku mpaka wanamaliza darasa la 7,unakuta mtoto kashaadopt na anajua kiswahili!Hii ni kwasababu lugha ya kufundishia ni kiswahili na anajikuta yuko mazingira ya watu wanazungumza kiswahili shuleni,ndio maana akaweza kujifunza taratibu!Hapo inamaana hata tungeweka mazingira ya kiingereza shuleni na ikawa lugha ya kufundishia,mtoto angeweza kuadopt na kujifunza kiingereza!
Tuchague moja,kama ni kiswahili basi na iwe hivyo kuanzia msingi mpaka chuo kikuu na kama ni kiswahili iwe hivyo msingi mpaka chuo kikuu!
Hapa tulipo tupo katikati!

Ukweli tu ni kwamba lugha ni commitment, hata ukifikisha miaka 70, ukijifunza utaweza na utaelewa tu. Halafu kama unasema mtoto ana adopt kiswahili huko shuleni kutoka kwenye kilugha sasa mbona anashindwa ku adopt hicho kingereza kwa miaka 6 shuleni? Kitu ukiona umuhimu wake utajifunza na utaweza tu. Tukubali tunakauzembe flani.. halafu unaweza kuona kingereza cha mtu flani ni kibovu ila wewe binafsi hata huwezi kuongea kingereza kwa dakika tano mfululizo. Ndio tulivyo watanzania. Kuchekana kwingi wakati wote wabovu tu na ndio maana tunabaki kulalamika tu hapa. Lugha ni kujifunza kwa kujizoeza kuongea mara kwa mara. Sasa kama mtu anaogopa kuopngea kisa atachekwa bhas huo ndio ujinga wenyewe. Practice makes perfect. Kingereza ni lugha tu kama lugha nyingine.. sio chanzo cha maarifa au uelewa mkubwa kielimu.
 
Kwa hiyo kuwa msomi ni kujua kingereza?

Hata yule beberu wake akisikia hivi ataona aibu sana

Sidhani amezungumzia usomi. Usomi ni kiwango cha ufahamu. Anazungumzia lugha na jinsi kutoamua kwetu - kunababaisha uelewa wa lugha! Beberu unayemtaja hana kigugumizi kwenye uamuzi wa lugha ya kufundishia na wengi husoma kiingereza kwa sababu za kujumuika na mataifa mengine!!

Na sisi tunaweza kusema tutumie kiingereza kwa mawasiliano lakini lugha ya kufundishia toka elimu ya msingi hadi chuo kikuu iwe ni kishwahili. Jambo hilo hatujafanya. Kwa ukweli kabisa, ni rahisi sasa kubadilisha elimu ya msingi ikatolewa kwa kiingereza kuliko kubadilisha elimu ya juu kuwa kiswahili.
 
Ukiona zaidi ya 90% wanakumbana na changamoto hiyo,basi jua kuna tatizo hasa la msingi linalohitaji utatuzi!
Wangekuwa wachache ndio wanakuwa wabovu,basi tungesema ni uzembe wao!Lakini tunakwepa nini,ni ukweli ulio wazi kuwa watanzania wengi wanamaliza vyuo hawajui kiingereza vizuri kile tu cha kuwasiliana!Fikiri tu PhD holder,Dr Magufuli kiingereza ni kasheshe,bado unaona ni uzembe?Kwanini huoni ni tatizo la mfumo wa elimu?
Mkuu hujaelewa mfano wangu,nimesema mwalimu alikuwa analazimika kutumia kilugha ili wanafunzi waelewe!Mwisho wa siku mpaka wanamaliza darasa la 7,unakuta mtoto kashaadopt na anajua kiswahili!Hii ni kwasababu lugha ya kufundishia ni kiswahili na anajikuta yuko mazingira ya watu wanazungumza kiswahili shuleni,ndio maana akaweza kujifunza taratibu!Hapo inamaana hata tungeweka mazingira ya kiingereza shuleni na ikawa lugha ya kufundishia,mtoto angeweza kuadopt na kujifunza kiingereza!
Tuchague moja,kama ni kiswahili basi na iwe hivyo kuanzia msingi mpaka chuo kikuu na kama ni kiswahili iwe hivyo msingi mpaka chuo kikuu!
Hapa tulipo tupo katikati!

..story yako imenigusa sana.

..nili-experience something similar to what you did in school.

..asante kwa ujasiri wako wa kuelezea changamoto ulizozipitia.

..unawazungumzia malaki, kama siyo mamilioni, ya waTanzania wenzako.
 
Ukweli tu ni kwamba lugha ni commitment, hata ukifikisha miaka 70, ukijifunza utaweza na utaelewa tu. Halafu kama unasema mtoto ana adopt kiswahili huko shuleni kutoka kwenye kilugha sasa mbona anashindwa ku adopt hicho kingereza kwa miaka 6 shuleni? Kitu ukiona umuhimu wake utajifunza na utaweza tu. Tukubali tunakauzembe flani.. halafu unaweza kuona kingereza cha mtu flani ni kibovu ila wewe binafsi hata huwezi kuongea kingereza kwa dakika tano mfululizo. Ndio tulivyo watanzania. Kuchekana kwingi wakati wote wabovu tu na ndio maana tunabaki kulalamika tu hapa. Lugha ni kujifunza kwa kujizoeza kuongea mara kwa mara. Sasa kama mtu anaogopa kuopngea kisa atachekwa bhas huo ndio ujinga wenyewe. Practice makes perfect. Kingereza ni lugha tu kama lugha nyingine.. sio chanzo cha maarifa au uelewa mkubwa kielimu.
Umeelewa hoja yangu lakini?Mimi siko hapa kubishana bila mantiki!Jaribu kufikiri kabla hujaandika!
Nimekuuliza swali ambalo mara zote unalikwepa!Huko shule za English medium kwanini wanafanikiwa sana?
Nikueleze tu,mtoto mdogo anakuwa na nidhamu!Unapoweka standard ya lugha ya mawasiliano kuwa ni kiingereza,hata wenzake wakimsikia anaongea lugha tofauti watamsema kwa mwalimu!So hiyo inajenga mazingira ya wanafunzi kujitahidi kuongea kiingereza!Tofauti na huku form 1,speak english inakuwa geresha tu pale mwalimu anapokuwepo!Akiondoka kila mtu anaendelea na time yake!
Lakini pia kukifanya kiingereza kuwa lugha ya kufundishia kunawafanya watoto waadopt mapema!
Halafu jambo lingine ni kuwa hapa sisemi kuwa kiingereza sijui ndio maarifa au nini!Ninachosema tuchague njia moja,kama ni kiswahili iwe kiswahili,kama ni kiingereza iwe kiingereza!Ijulikane moja!Hapa tulipo tumekwama,hilo lazima tukiri!
Ninachoona hoja hii inapingwa kwasababu za nani kaileta na kaileta wakati gani!
Hilo ndio tatizo kubwa,siasa mbele kwa mbele hata kwenye mambo ya msingi ambayo tungeweza kujadili bila kuwa na mihemko ya kisiasa!
Mkuu ukiwa na pesa ingiza mtoto wako shule za maana,hizi kayumba unamtengenezea mwanao ugumu huko mbeleni!
Mimi nimejipanga kuhakikisha mwanangu hashindwi kutimiza ndoto zake kisa lugha!Ashindwe kwa sababu nyingine lakini si lugha!Nahitaji mwanangu aje kuwa na confidence akiwa anafanya interview,ashindwe kujibu swali kwa ujinga wake na si kwasababu ameshindwa kulielewa swali au amelielewa ila kuongea alichonacho ndio changamoto!

Hao viongozi wote,watoto wao wako kwenye shule nzuri!
 
Mnapo
Mnaposema Lissu anajua kuongea Kiingereza mnamaanisha nini?
Mjadala hapa ni jinsi baadhi ya majaji wanavyoshindwa kuimudu lugha ya kiingereza ambayo ni moja ya nyenzo zao za kazi. Lissu alitoa angalizo tu (siyo Lissu tu ila wengine tumeshaliona hili tatizo tangu zamani) jinsi baadhi ya majaji wanavyotia aibu. Kiingereza siyo lugha yetu na hatuwezi kukijua sana ila kila level ya elimu mtu anayofikia angalau inatakiwa i-reflect utendaji kazi wake.
 
Mjadala hapa ni jinsi baadhi ya majaji wanavyoshindwa kuimudu lugha ya kiingereza ambayo ni moja ya nyenzo zao za kazi. Lissu alitoa angalizo tu (siyo Lissu tu ila wengine tumeshaliona hili tatizo tangu zamani) jinsi baadhi ya majaji wanavyotia aibu. Kiingereza siyo lugha yetu na hatuwezi kukijua sana ila kila level ya elimu mtu anayofikia angalau inatakiwa i-reflect utendaji kazi wake.
Ahahahahahahahahh! Hivi unajua George Bush alikuwa hajui kuongea Kiingereza? Ilimzuia kuwa Rais wa Taifa kuwa duniani? Ahahahahahahah!!
 
Ahahahahahahahahh! Hivi unajua George Bush alikuwa hajui kuongea Kiingereza? Ilimzuia kuwa Rais wa Taifa kuwa duniani? Ahahahahahahah!!
Hivi ukiitwa idiot utalalamika? Mbona unaongea vitu vya kijiwe samli hapa! Anyways niachane na wewe kwa sababu mijadala kama hii siyo kwa kila mtu.
 
"Yes you know me sometimes photocopy together, sijui nini na nini pilot standard"........bora kiswazi tu wazee
 
Hivi ukiitwa idiot utalalamika? Mbona unaongea vitu vya kijiwe samli hapa! Anyways niachane na wewe kwa sababu mijadala kama hii siyo kwa kila mtu.
Ahahahahahahahh! Huwezi kujibu hoja kama hii. Unafikiri aliyewaita nyumbu alikosea? Ahahahahahahah!
 
Back
Top Bottom