List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

Kwa vyama vyenye sera, hiyo ilikuwa nafasi mojawapo ya kujitengeneza kwa kuandaa mikakati ya kuwasaidia wananchi wenye sifa ili wapate hizo fedha.

Matokeo yake mafisadi wa CCM wakatumia hiyo nafasi kugawa hizo pesa kwa rushwa. Je vyama vingine vya siasa vilifanya nini katika kumsaidia rais juu ya hilo? Je kule kwenye majimbo ya vyama vya upinzani hizo pesa zimetumiaka vizuri kuliko maeneo mengine?

Mtanzania;
kama JK ambaye ni raisi na pia ni mwenyekiti wa chama ameshindwa kuwadhibiti wanachama wake wa CCM ambao unadai ni mafisadi waliotumia rushwa kugawa hizo pesa (mabilioni ya JK), unadhani wapinzani watafanya nini?, raisi ndo ana dola' anauwezo wa kuwachukulia hatua mafisadi hao lakini jiulize JK amewachukulia hatua gani hao mafisadi mpaka hivi sasa?

Kazi kubwa wanayoweza kuifanya wapinzani ni kuikemea rushwa kama wanavyoikemea sasa, na pia kuwataja hao wala rushwa ili kuvipa vyombo vya usalama wakati mzuri wa kuwachunguza hao wala rushwa
 
Mkandara,

Mimi ni mwumini wa siasa za vijijini, wacha mfano wangu ulenge huko. Mapesa ya JK, yalitangazwa kwa muda mrefu na kila mmoja wetu alikuwa na nafasi ya kusaidia ili pesa ziwafikie walengwa. Mimi nilitegemea viongozi wa vyama vya siasa wangesaidia kuhakikisha hizo pesa zinawafikia wakulima na wanyonge kule vijijini. Hata mimi nilitamani ningelikuwa kule kwetu ili nisaidie kuwaandaa na kuwafundisha baadhi ya vijana ili wapate hizo pesa na ziwasaidie kwenye miradi yao. Bahati mbaya na mimi
nilishindwa kwasababu haikuwa rahisi kufanya hayo mambo ukiwa mbali.

Kwa vyama vyenye sera, hiyo ilikuwa nafasi mojawapo ya kujitengeneza kwa kuandaa mikakati ya kuwasaidia wananchi wenye sifa ili wapate hizo fedha.

Oh my goodness....Mtanzania.... heshima kwako mkuuu

Ulitegemea vyama vya upinzani warukie misguided sera ya kutoa hard cash kwa wananchi kabla ya kubuild infrasture....? then kama mkulima wa kijiji cha sabasaba akitumia pesa hizo kulima nyanya nyingi sana na bora.... atazisafirisha vipi kwenda sokoni - mjimwema wakati hakuna barabara ya uhakika ya kufika huko.....?

This was wrong na hata sasa umeona matokeo yake kuwa sio mazuri. Kwa hili mkuu... usijilaumu kwa kutosaidia (ingawa naamini bado unasapoti hii sera ya mabilioni)

Nashangaa Zitto ambaye ni kijana msomi na ana uwezo anatumia muda wote huo kuongelea rushwa tu, bila kuelezea pia sera za vyama vyao. Mungemsaidia huyo kijana kwa kumpa nyenzo nzuri ili azifikishe kwa wanachi.

umehudhuria mikutano mingapi ya Zitto na ukajua anachokisema au unasoma report ya magazeti.... Kijana anamwaga sera huko ila kina mchambuzi (ambaye kazi yake ni kummaliza Zito na wapinzani) watakufanya uamini kuwa hakuna kinachosemwa kwenye mikutano hii zaidi ya udaku..
 
Kazi kubwa wanayoweza kuifanya wapinzani ni kuikemea rushwa kama wanavyoikemea sasa, na pia kuwataja hao wala rushwa ili kuvipa vyombo vya usalama wakati mzuri wa kuwachunguza hao wala rushwa


Kama hii ndio kazi kubwa zaidi ya kujenga chama na kuwa na malengo makubwa na strategy za muda mrefu na wa kati kwa ajili ya mstakabali wa nchi yetu,,, then unatuambia vyama vya upinzani vinataka kuwa vya upinzani milele!!! in this context then we can understand what is going on now!

No wonder mzee wa kiraracha amesema amepata watu wa jinsia/namna yake wakuwapatia mikoba yake!!!
 
....in this context then we can understand what is going on now!

Unasema we ukimaanisha wewe na nani vile?

List ya wala rushwa imetoka na Kikwete yuko ndani ya nyumba..

Kwa sasa ajiandae tu kupokewa na mabango atakapofanya ziara yake hapa Marekani.... labda akwepe public appearances......
 
Hao na mtandao amba wanataka kuifanya hii issue ni ya kitoto. as I commented, You can not support if you are not one of them.

Sioni tatizo katika hili la Slaa kutoa majina. Hivi hao viongozi wa nje tunaosikia wanajiuzulu kutokana na Kashfa za rushwa wao ni tofauti na wa kwetu? au wa kwetu ni Miungu kwa hiyo haifai kuwataja?

Badala ya kujadili nini kifanyike, tunajadili eti kuwataja ni Udaku. simply kwa sababu JK yumo. kama JK yumo, tujadili kwa nini yumo, kuna connection gani kati yake na hawa wengine. mazoea ya kuwaogopa viongozi yatatufikisha pabaya.
 
Je Mchambuzi bado anataka tuamini kwamba bado serikali iliyopo kuna utawala Bora? Hivi Slaa kuanika madhambi ya Viongozi ambao mwanzoni tulisema tumepewa na Mungu ni Udaku? Nadhani alichofanya Slaa ni kuwaambia Watanzania kwamba mmdhanie siye kumbe ndiye sasa kazi kwenu.

Kikwete hakuchaguliwa kwa sera, alichaguliwa kwa sababu watu walimwamini kwamba ndiye mkombozi wao kutokana na udhalimu wa CCM wa muda mrefu na ajenda kubwa ikiwa ni kukisafisha Chama kutokana na ufisadi. kikwete alipata kura hata kutoka kwa wapinzani.

Kazi ya Vyama vya siasa ni pamoja na kuikosoa serikali pale inapofanya vibaya, vivyo hivyo preasure groups. Je ulitaka haya wayaseme Preasure groups na sio vyama vya siasa?

This is my view - Upinzani wa sasa bado haufanyi kazi nzuri na ni kwa tatizo lao wenyewe, wasilaumu mtu mwingine. In that context, we need viongozi waliopo ndani ya ccm ambao ni safi kutuongoza katika kipindi cha mpito mpaka pale generation mpya itakapokuja either kujiunga na hao wana ccm safi au kwa njia ya chama kipya. In the process, watanzania wote wenye uchungu na nchi yao wasiishie kupiga kelele kwenye internet. Kama una ndugu zako kijijini, mjomba, babu, shangazi, etc, tumia nafasi hii kuwaelimisha na over time elimu hii itasambaa. Ila tusifanye kwa kutumia njia za majigambo hata kwa ndugu zetu kwamba tunajua sana na wao hawajui lolote. That wont make any meaningful change.

Ni sahihi kabisa kusema JK hakuchaguliwa kutokana na sera and instead hopes kwamba ataleta mabadiliko. Lakini kama nilivyosema huko nyuma, mkutano mkuu ulijua wazi kwamba mwenyekiti wa kampeni ya JK ni EL na walijua fika kwamba JK amekuwa created na EL. It looks like wengi humu pia hili hawalielewi au wankataa kulielewa.

Na wajumbe wengi wa mkutano mkuu ni wale wale waliokuwa nyuma ya EL 1995 na baadae wakahamia to JK kutokana na influence ya EL.

Sasa kwa mtindo huu huu, EL bado anauwezo mkubwa sana kupita kwenye mkutano mkuu akisimama 2015 na wapiga kura watampa kura nyingi tu as long as ni mtandao umemsimamisha. EL haitaji 80%. 60% inampitisha. So hizi porojo za hapa na pale kuhusu EL 2015 hazina maana yoyote kama mkutano mkuu utaona EL ndio chaguo zuri. Wananchi wa tanzania wataichagua tu CCM, whether ni EL, mwandosya, sumaye, magufuli or any other ndie atakayesimamisha for ccm.

Kuhusu upinzani na pressure groups tanzania, what i meant ni kwamba upinzani una behave kama pressure groups, sio kama real political parties.

Hata JF wakija na azimio moja humu kuhusu suala fulani inaweza ku qualify as a pressure group. Hizi vyama vya siasa tanzania inabidi vijiangalie na kujipanga vizuri. Haviwezi kuitikisa ccm, vitaweza tu tikisa individuals in ccm kutokana na udaku on rushwa. A pressure group is not a political party.

Tafadhali angalia kwenye google etc description ya pressure groups vs politica party. Why do you think serikali huko nyuma was more concerned na siasa za mtikila kuliko za chadema? au siasa za CUF znz kuliko za chadema? Ni kwasababu CUF wanaoperate in the context of sera na ndizo hizo zinawapa nguvu na legitimacy kule znz.

Mtikila became a threat because angeweza kuleta a movement kubwa sana. Yeye hakuja na sera za wala rushwa ndani ya ccm, alikuwa anaelezea rushwa in the context of uhujumu wa uchumi na jinsi gani Tanzania can be better as Tanganyika na pia by empowering weusi over wahindi. Whether ni mbaya au nzuri, zote hizi ni sera, sio udaku.
 
Hao na mtandao amba wanataka kuifanya hii issue ni ya kitoto. as I commented, You can not support if you are not one of them.

Sioni tatizo katika hili la Slaa kutoa majina. Hivi hao viongozi wa nje tunaosikia wanajiuzulu kutokana na Kashfa za rushwa wao ni tofauti na wa kwetu? au wa kwetu ni Miungu kwa hiyo haifai kuwataja?

Badala ya kujadili nini kifanyike, tunajadili eti kuwataja ni Udaku. simply kwa sababu JK yumo. kama JK yumo, tujadili kwa nini yumo, kuna connection gani kati yake na hawa wengine. mazoea ya kuwaogopa viongozi yatatufikisha pabaya.

Kikwete naye ni mla rushwa tu na anashiriki kwenye kila kinachoendelea nchini ikiwemo hili la Buzwagi ambalo rafiki yake karamagi amehusika.

Wapambe wake kila mara wanasema kuwa hausiki na hata JF imekuwa nice to Kikwete for a while kwa kumuita nice names kama msanii na muungwana....

Honey moon is over.....now.... Kikwete ataambiwa ukweli na kwa sasa mipango inakamilika ya kumshughulikia (kisheria sio kwa mapinduzi..... )
 
Hao na mtandao amba wanataka kuifanya hii issue ni ya kitoto. as I commented, You can not support if you are not one of them.

Saharavoice,

Tangaza kote Mtanzania ni mtandao. Mimi ni Mtanzania tu ambaye naangalia shilingi kwa pande zote. Sio mtandao wala sijawahi kufaidika na system katika maisha yangu. In fact system imekuwa ikinikwamisha.

Lakini pia nitakuwa naive kuamini rushwa itakoma Tanzania CCM wakiondoka madarakani. Mapambano dhidi ya umaskini, ujinga, na afya duni ndio yatatuokoa Watanzania kutoka kwenye majanga yote yanayotukabili.
 
Rushwa ni universal enemy, enemy to man kind, Hata Hillary Clinton sasa hivi anajuta kwa zile tuhuma zake za kupokea rushwa enzi hizo "long time ago", wapinzani wake hawamuachii,yaani Hillary anaona kama uraisi wa huko States anaukosa hivi hivi, Halafu eti sisi Watanzania tuwe na huruma na wala rushwa kwa kuendelea kukaa kimya tu na kuwakumbatia na kuwaita waheshimiwa, hilo hakuna!, ukishajihusisha na rushwa watu wanakutaja,wanakuumbua! na hakuna cha uheshimiwa tena.

RUSHWA NI ADUI NA MLA RUSHWA NAYE NI ADUI.

ADUI HANA BUDI KUPIGWA VITA IN ALL FRONTS.

ADUI SI MHESHIMIWA, NA MLA RUSHWA HAFAI KUITWA MHESHIMIWA
 
Badala ya kujadili nini kifanyike, tunajadili eti kuwataja ni Udaku. simply kwa sababu JK yumo. kama JK yumo, tujadili kwa nini yumo, kuna connection gani kati yake na hawa wengine. mazoea ya kuwaogopa viongozi yatatufikisha pabaya.


Binafsi naamini mh. aliowataja hao waheshimiwa wenzake ana access na wanasheria wa nchi yetu... na anajua wahalifu wanapelekwa wapi! sio Temeke Mwembe Yanga!

Tunaomba kama tuhuma hizi ziko wazi tunaomba awasaidie vyombo/mhimili wa tatu (judiciary) ufanye kazi yake!!! kufanya kwa namna hii aliyofanya ni kukwepa majukumu... siku hizi hili ni kama kamziki au noisy ndogo kwa wala rushwa na baada ya muda wanaendelea, sheria ifuate mkondo wake, then itaoneka kuna useriouseness.. na tutaona Dr. Slaa ni Zaidi ya Mrema,,, nisingependa Dr. Slaa nimlinganishe na Mrema tafadhali

Narudia tena, mbona Mtikila ameihenyesha serikali na kushinda kesi nyingi,,, kwa nini hawa waheshimiwa wasifanye hivyo kwa uzalendo tu! ili kuisaidia nchi yetu!!! wahalifu wanapelekwa mahakamani...


Wahalifu/watuhumiwa wengine hawapelekwi Temeke mwembe yanga kwa nini hawa wa rushwa tena kubwa wapelekwe huko!!! wakati access ya wanasheria ipo, watu makini wapo, chama makini kipo?
 
Unasema we ukimaanisha wewe na nani vile?

List ya wala rushwa imetoka na Kikwete yuko ndani ya nyumba..

Kwa sasa ajiandae tu kupokewa na mabango atakapofanya ziara yake hapa Marekani.... labda akwepe public appearances......

Hayo mabango mnazungumza tu lakini sidhani kama kuna mtanzania atathubutu kufanya hilo.

Nime-miss hoja zako mwafrika wa kike.
 
This is the best thread I have read in a longtime and more or less answers my question 'What we/are you going to do about it'.

The issue here is about educating the people. Anyone who is willing to educate the people doesn't have a side (CCM, CHADEMA, CUF etc), and the onus is on them to bring the change. Since we view the opposition as the driving force that should bring change in Tanzania. There approach to bring this change, will show how mature they are politically. So far with all the loot at their disposal, they are failing the Tanzanians very much. If people are educated, change will come, like it or not.

The only other option is civil war. People are getting tired, people will get tired. That old song, sijui Tanzania is a peaceful country, Mchambuzi, you have deciphered it very well. No one in Tanzania, has pain for Tanzania. There are only 2 ways, make change through education/ballot or change by force. Lets not beat around the bush.

Thats why I asked, Mbowe, Zitto and crew are emancipating people for civil disobedience.........yes, but educate the people first. Educating the people will be the best legacy you can leave for Tanzania. Even if Mbowe or any of the opposition guys dont become president of Tanzania, their legacy will stay for generations. Thats what will make these guys great leaders. You dont have to be a president to be a great leader.

Mchambuzi, for that post, I salute you.

What loot at their (opposition parties) disposal are you talking about?We are actually back at the nasty old days when the party/government held grip of all state apparatus (security organs,bunge,courts of law,etc) in the name of hegemony.And what's the better way of educating people than telling them in black and white about how their leaders are plundering their country even worse than the the way the colonialists did?Or did you mean the Mbowes and Slaas should enrol the wananchi to school to study how they should liberate themselves?I believe what they are doing is more than educating the masses (by the way,if education was the only way to make people take action about evils in the society,then Tanzania would have been HIV/AIDS free because there's so much educating going on in this particular area).That's not to undermine the role of educating the masses,but what's needed most is opening the people's eyes by exposing our leaders' mischiefs.And that's exactly what Slaa&Co did yesterday.

I believe in the power of the ballot box,but that's long proved ineffective in a corrupt and fumbled "democracy."The on-going CCM's elections could easily tell you that the ballot doesn't always produce good leaders.Read here to see what Idd Simba thinks about the way corruption makes our nation's future so uncertain.
 
Waliowasikia wanasema Waliotajwa ni Balali, andrew chenge, basil mramba, meghji,mgonja, rutabanzibwa, mkono,lowassa, karamagi,rostam,mkapa na mkewe na jk.

na wengine wadogo wadogo walikuwa wakitajwa mara kwa mara. Hakuna gazeti ambalo limeandika hayo majina. To me huko ni kuchafuana tu. Uzushi mtupu!!!!
 
This is my view - ..... we need viongozi waliopo ndani ya ccm kutuongoza

That's good to know.

In the process, watanzania wote wenye uchungu na nchi yao wasiishie kupiga kelele kwenye internet.

Kama unavyofanya wewe hapa......

.. Sasa kwa mtindo huu huu, EL bado anauwezo mkubwa sana kupita maana Wananchi wa tanzania wataichagua tu CCM.

Umeanza lini kuwa msemaji wa wananchi wa Tanzania? hii issue kuwa EL atachaguliwa tu kwa sababu ni mkristo na mmasai bado hujaiacha tu? Endelea na ndoto zenu na wizi wa mali za watatz bila kukumbuka kuwa malipo ni hapahapa duniani...
 
Mtanzania;
kama JK ambaye ni raisi na pia ni mwenyekiti wa chama ameshindwa kuwadhibiti wanachama wake wa CCM ambao unadai ni mafisadi waliotumia rushwa kugawa hizo pesa (mabilioni ya JK), unadhani wapinzani watafanya nini?, raisi ndo ana dola' anauwezo wa kuwachukulia hatua mafisadi hao lakini jiulize JK amewachukulia hatua gani hao mafisadi mpaka hivi sasa?

Kazi kubwa wanayoweza kuifanya wapinzani ni kuikemea rushwa kama wanavyoikemea sasa, na pia kuwataja hao wala rushwa ili kuvipa vyombo vya usalama wakati mzuri wa kuwachunguza hao wala rushwa

Gamba la Nyoka,

Mimi naamini ningelikuwa kule wilayani, ningeweza kuwasaidia baadhi ya vijana ili wafaidike.

Sio rahisi mtu wa juu kupambana na mambo ya chini. Hiyo top down governance haitausaidia. Lakini pia kule chini capacity yao ni ndogo mno na hakuna watu wa kusaidia capacity building. Viongozi wote wa siasa na hata NGO wako mijini.

Ndio maana wengine tunataka kufunga virago na kurudi wilayani kwetu kwenda kujaribu kufanya baadhi ya haya ambayo tunayaongelea kila siku JF. Kwa kweli inasikitisha kwamba tunaimba siasa lakini tunashindwa issues ndogo sana.
 
Hayo mabango mnazungumza tu lakini sidhani kama kuna mtanzania atathubutu kufanya hilo.

Nime-miss hoja zako mwafrika wa kike.

Wewe endelea na assumptions zako..... huna idea of what is going kwa kuwa umefumbwa macho na Rostam Aziz.....

Hata mie nili-miss propaganda zako for a while... ulivyoondoka na nilidhani labda na wewe umekuwa cut-off kama baadhi ya mtandao waliochemsha uchaguzi wa NEC....

Karibu tena...na nafurahi kusikia kuwa umesovu issue zako za kifamilia.
 
Hayo mabango mnazungumza tu lakini sidhani kama kuna mtanzania atathubutu kufanya hilo.

So,kwa vile wewe hudhani kuwa kuna Mtanzania atakeyethubutu kufanya hivyo,then it should go without saying kuwa haitokuwa hivyo?Mawazo kama hayo yaliwapa kiburi sana makaburu kuendeleza ubaguzi wa rangi huko South Africa:hawakudhani kwamba weusi wangeweza kuung'oa mfumo wa apartheid.Na ubutu wa iana hiyohiyo ndio uliochangia kung'oka kwa mfumo wa kikomunisti huko Ulaya ya Mashariki:watawala walidhani hakuna wa kuthubutu kuwang'oa madarakani.By the way,kwanini lazima dhana yako (which is largely unscientific) iwe sahihi?Kama ushawahi kufanya research ya aina yoyote utagundua kwamba sio lazima hypotheses (ambayo hapa ni sawa na hicho unachokiita "dhana") ziwe sahihi baada ya ku-apply theory flani.
 
Gamba la Nyoka,

Ndio maana wengine tunataka kufunga virago na kurudi wilayani kwetu kwenda kujaribu kufanya baadhi ya haya ambayo tunayaongelea kila siku JF. Kwa kweli inasikitisha kwamba tunaimba siasa lakini tunashindwa issues ndogo sana.

Mkuu afadhali umegundua kuwa inabidi uende wilayani na sio kutuma mabilioni hard cash kwa wananchi... huu ni mwanzo mzuri
 
Mchambuzi,Kilitime,Mwafrika_wa_kike,....
hizi kampeni za kumsakama Lowassa zitawafanya wana CCM wamuone too risky na a liability kwao. hiyo ndiyo itafanya nomination iende kwa wengine.

kila chama kinaweza kuwa na sera nzuri, tatizo ni kupata watu wenye uwezo na nia ya kuzitekeleza. CCM ni a very diverse group lakini wengi wanaopewa nafasi za uongozi hawana uwezo wala nia ya kutekeleza sera za CCM.

huyo anayelaumu wapinzani kwa kuwaumbua walarushwa amesahau wanamtandao walifanya nini kwa miaka 10 dhidi ya Sumaye? hivi Sumaye hakulaumiwa kwa kila jambo hata kukodisha shamba la eka 7 kibaigwa?

mimi nahitaji kuelimishwa kwanini kampeni kuumbua walarushwa ili-work for Lowassa na wanamtandao, but wont work for wapinzani.
 
Back
Top Bottom