Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 308
Pengine wengine hawafahamu maana ya ufisadi na pia hatuhusianishi kati ya ufisadi na maadili ya uongozi wa umma.
Tatizo ni kwamba Watanzania wengi hawajui uhusiano uliopo kati ya Serikali au watumishi wake kutumia pesa vibaya na maisha yao ya kila siku. Ni wachache mno wanaojua mchango wao katika uendeshaji wa serikali, ukimwambia msukuma wa Bariadi kuwa Chenge ni fisadi haoni kuwa hilo ni tatizo lake. Hajui ni namna gani pesa alizoiba Chenge zinamhusu , yeye anajua hiyo ni mali ya serikali, na serikali kwake ni serikali, na haina uhusiano wowote na maisha yake tofauti na misaada ya kujengewa visima, shule, zahanati, n.k
Wao wanajua kama Halmashauri ya wilaya ikijenga barabara au zahanati kuwa ni huruma ya serikali au mbunge wao, hawajui kuwa hiyo ni haki yao.
Hawajui ni namna gani wao wanachangia uendeshaji wa serikali kupitia manunuzi na matumizi yao ya kila siku. Siku wakijua ni mchango gani wanatoa katika uendeshaji wa serikali, siku hiyo tutaanza kuona maandamano pale huduma za jamii zinapopanda, ni siku hiyo ndipo Tanzania yangu itapata uhuru wa kweli.
Bila wananchi kuoanisha maisha yao ya kila siku na mapato na matumizi ya serikali CCM wataendelea kuwalaghai na mafisadi yataendelea kushika ofisi za umma.
Natamani siku hiyo ianze 31 October 2010