Wakuu
Takriban zaidi ya miaka mitano sasa tangu ulipofanyika mkutano wa hadhara wa kihistoria ambayo umebakia katika kumbukumbu ya vitabu na rejea zingine, kama mojawapo ya hallmarks za vita dhidi ya ufisadi. Ni mkutano uliofanyika Viwanja vya Mwembeyanga, Dar es a Salaam, ambapo mbele ya vyombo vya dola vyooooooote nchini, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willbrod Slaa pamoja na Kamanda Tundu Lissu, mbele ya viongozi wakuu waandamizi wa chama hicho, akiwemo Mwenyekiti Freeman Mbowe, walitaja majina 11 ya watuhumiwa wa ufisadi mkubwa ndani ya nchi hii, akiwemo Rais na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Benjamin Mkapa na Rais na Mwenyekiti wa sasa wa CCM, Jakaya Kikwete.
Mbali ya kutaja majina hayo, CHADEMA ilitoa hadharani ushahidi wa wazi na kina wa ufisadi huo mkubwa ambao watu hao 11 walikuwa wanatuhumiwa kuhusika kushiriki. Wakaenda mbali na kuutangazia umma wa Watanzania na dunia nzima kuwa, bado wanao ushahidi mwingine na wataendelea kuutoa kadri ya muda, unaowafungamanisha watu hao na tuhuma za ufisadi mkubwa wa uporaji wa rasilimali za Taifa katika kashfa mbalimbali kubwa kubwa.
Kwa kujikumbushia na kwa faida ya mjadala, majina yaliyotajwa katika ushahidi huo wa tuhuma za ufisadi mkubwa ni pamoja na
TUJIKUMBUSHE ORODHA YA 2007
1. Dr. Daudi T.S. Balali
2. Andrew J. Chenge
3. Basil Pesambili Mramba
4. Gray S. Mgonja
5. Patrick P.R Rutabanzibwa
6. Nazir Karamagi
7. Nimrod Mkono
8. Rostam Aziz
9. Edward Lowassa
10. Benjamin W. Mkapa
11. Jakaya Mrisho Kikwete
Hakuna hata mmoja kati ya hao aliwahi kukanusha ushahidi uliotolewa, mbali ya kukimbilia kwenye vyombo vya habari na kukanusha kutohusika na ufisadi, kisha baadhi yao, mmoja mmoja kwa nyakati tofauti, wakatishia kwenda mahakamani kushtaki, kitu ambacho hakuna hata mmoja aliwahi kufanya tangu 2007 hadi leo.
Kwa nini mjadala huu ni muhimu sana
List of Shame, yaani hiyo orodha ya aibu ya watuhumiwa wa ufisadi, wakati mwingi huitwa orodha ya mafisadi, ilifungua pazia muhimu sana ambalo hadi leo limekataa katakana kujifunga au kufungwa. Mkutano huo ulifungua pazia la vita dhidi ya ufisadi kwenye Mahakama Kuu ya Umma. Ilikuwa ni baada ya akina Samuel SItta na wenzake kubana kwa hila na makeke, wakitoa maneno ya kejeli dhidi ya Dkt. Slaa, wakizuia asiwasilishe ushahidi wa ufisadi huo Bungeni na kutaja majina, ili Bunge lifanye kazi yake ya kusimamia, kushauri na kuiagiza serikali kwa niaba ya wananchi.
Ufisadi mkubwa mkubwa kama wa Tangold, Meremeta, Richmond, Dowans, Kiwira, Minara ya BOT, EPA, Rada, ndege ya rais na kila aina, ukatajwa kwa ushahidi na kuzungumzwa hadharani. Ni baada ya hapo, nchi nzima ikaitikia wimbo wa vita hiyo na kurudia rudia kibwagizo chake cha ufisadi. Bila uoga. Hadi leo mambo hayajawahi kuwa sawa tena.
Bahati mbaya sana pamoja na ukweli na uhalisia huo kuwekwa bayana, hadi leo hakuna uwajibikaji wowote ambao umefanyika. Na inawezekana ni kwa sababu, Watanzania hawajawahi kudai kwa nguvu kubwa uwajibikaji na haki kutendeka katika hili. Kwa uhakika, kama hakutakuwa na uwajibikaji na haki kuonekana ikitendeka katika jamii, ni vigumu sana watu kuweza kuhubiri amani na utulivu wakaeleweka, unless they are big jokers.
Kutokana na kukosekana kwa uwajibikaji na haki kutendeka, no wonder kuwa tumeamua kuwa Taifa la kuzalisha kashfa ya ufisadi moja baada ya nyingine. Ndiyo maana Ndugu Zitto amekuja na jina lake la Fisadistan. The Land of corrupt.
No wonder bado tunaogelea katika lindi la ufisadi, ambapo sasa tumeongeza orodha ya mafisadi, kwa kashfa ya mabilioni ya rushwa katika mafuta na gesi, yaliyofichwa huko Uswisi. Hakuna uwajibikaji. Naandika haya Nikijua kuwa Dkt. Slaa amewahi kutoa updates za orodha ile ya mafisadi kwa kuongeza majina na ushahidi mwingine hasa juu ya kashfa ya uuzwaji wa nyuma za umma na Kampuni ya Kagoda. Hakuna uwajibikaji wala uwajibishwaji.
No wonder juzi, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alipomuuliza Waziri Mkuu Pinda bungeni nini hatma ya mabilioni yaliyofichwa na nchi ya nchi katika visiwa mbalimbali Kama vile Mauritius, New Jersey, Luxemburg, Uswisi, Grenanda na maeneo mengine mengi ambayo yana favour mafisadi kufanya hivyo, hakuwa na jibu sahihi kuwaambia Watanzania. Yaani serikali haijui nini cha kufanya, if you read between lines...
Updates, hoja ya Ndugu Zitto, see the serious relationship, ooops danger...