List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

Hii kazi ni jukumuletu sote, pia naambiwa kuwa JK atakuwa na interview na watu wa CNN leo ,ila sijajua ni muda gani kama mtu akiweza kuipenyeza hukuo nao wakamuuliza itakuwa imefika na ujumbe utaanza kusambazwa dunia nzima.
 
Mzee Jasusi umepiga hadi Ikulu. Yaani unamuuliza huyo tena ? Jamaa yuko anaona moto na hana neno la ku propagate hapa . Labda ana andika kwenye blog yake sijui. Kuna wengi hapa akina Tafiti na ujadili wamelala mbele na hata Mchambuzi kaona maji yamemfunika so si yeye pakee wako wengi hapa . Hii ndiyo JF naanza kuamini .
 
Waungwana,

Inaelekea ule msemo wa kifo cha nyani miti yote huteleza unajionyesha wazi hapa nyumbani. Yaani siwezi amini kuwa baada ya ile circus ya jana ya Karamagi na waandishi ambayo kwa taarifa ni kuwa alijipeleka kinyume na ushauri wa wengi bado Mzee makini kama Mgonja naye anaweza kuingia mkenge. Angalijua bomu lingene linalokuja ambalo kamwe hawezi kujinasua sidhani kama angefanya kosa hili la kujiweka katika spotlight.

Kuna taarifa kuwa nyang'au mkuu alitaka kuwasweka kina Zitto ndani akichukulia mwanya wa mwenyenchi akiwa nje lakini kabla ya kutekelezwa mwenye nchi akamshukia na mvua na kuwaarifu waliotwa manyang'au wote wajisafishe wao bnafsi bila ya kutumiwa mabavu ya dola. Na huu ndio ulikuwa msimamo wa Karamagi jana kuwa yeye alikuwa pale kama Karamagi binafsi na anajisafisha yeye binafsi ingawa katia statement yake amejitambulisha kama Waziri wa Nishati na Madini.

Inaelekea UTATU HARIBIFU unabomoka kwa mwendokasi wa mwanga....

Tusbiri kesho nini kitajiri....maana siku hizi ni uloda tu kwetu sisi wambeya wa kisiasa...

Tanzanianjema

Mkuu Tanzanianjema, hawa Waungwana hawaendi kwenye Press Conference kwa ridhaa yao.Mkuu wa Kaya katoa Maagizo ya kufanywa hivyo!,Kawaomba Watoe maelezo kwa wananchi na kwake Binafsi kuhusu kashfa zote zilizoandikwa kwenye paper ya Dr.Slaa.Atajieleza mmoja baada ya mwingine kabla ya mwenye Nyumba kuja Hitimisha atakaporudi Bongo!.Kuna maelezo kuwa Mkuu alibanwa na watu wa World Bank alipokutana nao Washington DC.Hao Waungwana wana vigezo vyote vinavyoonesha Ubadhirifu kwenye serikali ya JK haswa issue ya BOT.Kama kuna Mkombozi wa kweli hapa basi ni Kabwe!!!kwa sababu Hoja yake Binafsi Bungeni ndio imeleta hili songombingo lote.Kuweni makini Mh.Karamagi ana press Conference Jumamosi,anajiandaa kuzungumzia issue ya Mkataba wa Buzwagi,inaweza kuwa ikawa mwisho wa Uwaziri wake siku hiyo!!!
 
Wantanzania wenzangu, natumaini yale tuliyo yasema kwenye THREAD HII JINSI YA KUWASILIANA NA WABUNGE WA UINGEREZA sasa yamepata dawa, kwa sababu tumerahisishiwa kazi ya kutafsiri nakala tuliyokuwa tunaiongelea, miye naona kila mmoja wetu akiweza anaweza kwenda kwenye KIUNGANISHI HIKI AMBACHO KINA LIST YA WABUNGE WOTE WA UINGEREZA kisha bonyeza pembeni kulia kwenye wale wenye email address na kuwapelekea ujumbe huo juu baada ya ku-copy and paste na kuandika yafuatayo kama kichwa cha habari.

WAANDIKIE TU YAFUATAYO: "Dear Sir/Madam, I am a concerned Tanzania citizen and recognise that your Government, United Kingdom is a major contributor to progress, socioeconomic and other developments in our beloved nation. I kindly ask you to take part of your precious time to read through the following article and hopefully you will be touched and take decisive measures hence to assist in the sustainability and transparency of our government. Many thanks."

Sasa kama kunawataalam wa lugha na barua naomba waisahihishe hii na kuifanya iwe fupi na nakifu zaidi kama inawezekana.

MUHIMU: Naomba kama unafanya hivyo uandikie wabunge angalau wawili tu, ukizidisha utakuwa una abuse uhuru wako wa kutoa maoni na hivyo hiyo email inaweza kuwa classified as spam, na kuwa automatically deleted.

Pia kama kuna wengine ambao wanaweza kupata contacts za nchi nyinginezo naomba mziweke hapa. Ahsanteni.


SteveD.

Heshima mkuu,Nakupa tano mkubwa.Ngoja niangalie nianze na yupi
 
Wakuu naomba Msaada hii report iwekwe kwenye pdf ili tuiwakilishe kwa urahisi sehemu mbalimbali,ni vyema zoezi hili lifanyike haraka wakati issue bado hot.
 
Mkuu Tanzanianjema, hawa Waungwana hawaendi kwenye Press Conference kwa ridhaa yao.Mkuu wa Kaya katoa Maagizo ya kufanywa hivyo!,Kawaomba Watoe maelezo kwa wananchi na kwake Binafsi kuhusu kashfa zote zilizoandikwa kwenye paper ya Dr.Slaa.Atajieleza mmoja baada ya mwingine kabla ya mwenye Nyumba kuja Hitimisha atakaporudi Bongo!.Kuna maelezo kuwa Mkuu alibanwa na watu wa World Bank alipokutana nao Washington DC.Hao Waungwana wana vigezo vyote vinavyoonesha Ubadhirifu kwenye serikali ya JK haswa issue ya BOT.Kama kuna Mkombozi wa kweli hapa basi ni Kabwe!!!kwa sababu Hoja yake Binafsi Bungeni ndio imeleta hili songombingo lote.Kuweni makini Mh.Karamagi ana press Conference Jumamosi,anajiandaa kuzungumzia issue ya Mkataba wa Buzwagi,inaweza kuwa ikawa mwisho wa Uwaziri wake siku hiyo!!!

je?wametakiwa tuu kujieleza ama na kupendekeza hatua za kuchukuliwa wao binafsi?
 
Wakuu naomba Msaada hii report iwekwe kwenye pdf ili tuiwakilishe kwa urahisi sehemu mbalimbali,ni vyema zoezi hili lifanyike haraka wakati issue bado hot.

Inafanyiwa kazi na punde itawekwa kwenye pdf mkuu.
 
Heshima mkuu,Nakupa tano mkubwa.Ngoja niangalie nianze na yupi

Mtu, naomba uzidi kuicheck barua kama utataka kuikopy, maana najitahidi kuirekebisha kadili muda unavyoenda... Pia kama ushauri tu, miye naona si vyema kwa mtu yeyote kuongezea maneno mengine zaidi ya kupiga madongo yasiyo msingi (pamoja na kwamba tungependa!) au ya kashfa, inatupasa tuwe makini na as 'diplomatic' as possible ili kusikilizwa na wengi. Ahsante.

SteveD.
 
Mimi nimesha ituma kwa MP wangu first class,kwa hiyo kesho itakuwa mezani kwake. Hakuna kulala mpaka kieleweke
 
Waheshimiwa niko kwenye jitihada ya kuiweka kwenye pdf format na kuiedit kidogo kuwa presentabla.. nimeshakamilisha nusu na in the next hour and a half hivi nitawawekea reformated and edited version.
 
Ninafurahi kuwa sehemu ya watanzania ambao sasa tunajikomboa kwa fikra kwa kujadili mambo mazito ya nchi yetu. Ninaamini joto hili litaishia mahali ambapo watu wataelewa kuwa kupewa madaraka ni kuwahudumia wananci wenzio.

Tuendelee na moto huu na kila mtu uliye naye kwenye yahoo msn, mtupie ujumbe wa JF ili ajiunge na aminini kuwa ukiw JF unapevuka mawazo.
 
Nawapongeza wakuu, kanyaga twende, timua timua vumbi, haogopi mtu hapa. sambaza, tawanya, pekenyua, chokonyoa hadi Brown na malkia waisome tu.

"But tumwonee huruma JK jamani anatia huruma kweli mwee" (Joke)
 
Ushawahi kusikia mtu anapewa kamba ya kujinyongea... ? Kuna mtu kibarua chake kinakaribia kuota mbawa!
 
Mwanakijiji nimekutumia pia kwenye mail yako ya jamboforums.

Kazi njema ila niombe isiongezwe wala kupunguzwa neno kwani tayari wanayo hard copy wasije sema kuwa ni propaganda .

Kulikomboa taifa kunahitaji moyo , sote tufanye kazi hii ili kama sio sisis basi watoto wetu walau waje wakumbuke jitihada za forumhii kwenye kulikomboa taifa hili letu.
 
Habari za kawaida
Posted Date::9/26/2007
Vigogo zaidi wajitokeza kwenda kortini kupinga kashfa ya ufisadi
Na John Stephen

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, jana alijitokeza na kusema kuwa hatajiuzulu wadhifa wake na kwamba anakusudia kumshtaki mahakamani Dk Willibrod Slaa na wenzake kwa kutoa tuhuma za uongo dhidi yake.


Akijibu tuhuma hizo katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika katika wizara hiyo, Mgonja alisema kutokana na tuhuma hizo atamshtaki Dk Slaa na wenzake kwa sababu walitoa shutuma za uongo ambazo zimemchafulia jina lake.


"Shutuma za Slaa na wenzake sio za kweli, bali ni uzushi na upotoshaji wa ukweli uliolenga kuchafua jina langu na kunishushia hadhi mbele ya umma wa Watanzania na watu wa nje, wakiwamo washirika wa Tanzania katika maendeleo ya nchi yetu," alisema Mgonja.


"Kwa kuzingatia uzito wa tuhuma zilizotolewa kwa nia mbaya ya kunipaka matope na hasa nikizingatia uadilifu wangu wa miaka 33 bila kuwa na shutuma au kashfa ya aina yoyote, ili haki itendeke nimeamua kutumia mkondo wa sheria kwa kufungua kesi mahakamani dhidi ya Dk Slaa, Gazeti la Mwana Halisi na Kiwanda cha Printech kilichochapisha matoleo hayo," alisema.


Katibu huyo alipoulizwa ni lini atafungua kesi hiyo, alisema ataifungua muda wowote kuanzia sasa baada ya kuwasiliana na wanasheria wake.


"Nitafungua kesi mapema iwezekanavyo na si lazima mjue kampuni itakayosimamia kesi yangu na wala siwezi kutaja kiasi cha fidia nitakachodai, nitasema mahakamani fidia nitakayodai," alisema Mgonja.


Pia alisema amechelewa kujibu tuhuma hizo kwa sababu alichelewa kupata nakala halisi ya tuhuma za ufisadi dhidi yake na kwamba mara baada ya kupata amejibu.


Akizungumzia kama kuna athari zilizojitokeza baada ya kuhusishwa katika ufisadi akiwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Mgonja alisema tuhuma hizo, hazijasababisha athari zozote za kukwamisha misaada kutoka kwa wafadhili.


Pia alisema hazungumzii ufisadi kutokana na shinikizo la mabalozi wa nje na kwamba yaliyosemwa na mabalozi ni maoni yao na kwamba tuhuma dhidi yake zingelikuwa za kweli basi Serikali ingelipata athari kubwa kutoka kwa wafadhili.


Juzi Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU), iliitaka Serikali kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu tuhuma za ufisadi dhidi ya viongozi wa Serikali na wafanyabiashara nchini ili kurejesha imani kwa wafadhili na wananchi.


Katika hatua nyingine, Mgonja alisema amejibu tuhuma hizo kama Gray Mgonja na wala si kwa niaba ya Serikali.


Hata hivyo, barua ya majibu ya shutuma hizo aliyoisambaza kwa vyombo vya habari, ilikuwa na nembo ya serikali na kusainiwa na yeye kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha.


Septemba 15, mwaka huu, Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk. Slaa aliwatuhumu vigogo kumi na moja, wengi wao wakiwa ni viongozi wa serikali ya awamu ya nne kwamba walihusika na ubadhirifu wa mabilioni ya fedha za umma.


My take:

Hivi hawa watu kama hawataki kuzungumza kama maofisa wa serikali kwanini wasiwaite waandishi majumbani kwao, au kwenye hoteli binafsi. Tuhuma dhidi yao si kama watu binafsi bali kama maafisa wa serikali. HIvyo wanapojibu tuhuma hizo hata waseme mara ngapi kuwa wanafanya hivyo "kama wao" ukweli ni kuwa wanajibu tuhuma kama maafisa wa serikali. Na huyo aliyewaagiza wasema vinginevyo kawadanganya.
 
M/kiji sema, sema usiogope sema, na JF msiogope vibaraka sema. kwani JF tunafichana, sisi si ndio vinara wa uwazi? au NK nini?
 
Back
Top Bottom