Zamani nilikuwa nasikiliza top ten kwenye radio mbalimbali. Mfano clouds fm, radio one, magic fm etc. Sasa kwenye hizo top ten ilikuwa vichekesho.
Wimbo ulioshika namba moja radio one( kwa maana ya wimbo ambao unakubalika zaidi kwa wasikilizaji), ukisikiliza clouds fm wimbo huo huo ulioshika namba moja radio one, kwenye top ten za clouds fm umeshika namba 10.
Sasa haya matokeo ya watu wanaokubalika ama wenye ushawishi zaidi nchini yananikumbusha top ten nilizokuwa nasikilizaga enzi hizo na zinazoendelea kwenye radio mbalimbali nchini Tanzania. Nimesoma list ya watu 50 wenye ushawishi Tanzania, nimebaki kucheka peke yangu. Hivi inawezekana kwa mtu kama Mjomba Msumari ambaye hajulikani hata mtaa wa pili kuwa na ushawishi kwa jamii?
Hawa watu AVENCE MEDIA, kuna kitu si bure aisee. Na ningeshauri vyombo husika kuwachukulia hatua za kisheria kwa kusema uongo, maana huu nao ni upikaji wa data.