List ya Wasanii 10 bora kwa sasa Tanzania

List ya Wasanii 10 bora kwa sasa Tanzania

Sijawahi isikiliza kabisa hiyo nakupenda, nimeisikia sikia nakuona clips wakati ikitrend,hivyo sijasikia mashairi yake, melody ni nzuri ila naamini UTU ni bora kote kote, kale ka biti, mistari na melody yake.

Jana nimeisikiliza vizuri mnoo, akili ikaniambia kiba HAWEZI andika mistari kuntu kama hii, hizi ni level za kina harmonize, mondi hivi.
Kiba vimashairi vyake ni ujanja ujanja, kuna baadhi ya ngoma kuna mashairi mazuri na sina hakika na mwandishiwa hizo ngoma.. Mfano mwingine ni DUSHELELE, ukisikiliza yale mashairi unaona huyu aliandika akiwa katuliza kichwa... Na siku hizi kaacha zamani ngoma nyingi alikuwa anajitaja ALI, mfano ile aje bonge la ngoma, melody ni A+ mistari ni B ama C kabisa.

Umemshusha sana 😁😁😁😁
Mbona hata mapenzi yanarun dunia ilikuwa nzuri sanaaa

Halafu nilichokijua, hizi labels mara nyingi ukiangalia nyimbo zinavyotoka, unajua kabisa kuna mkono wa mtu aliyeandika

Binafsi nikifuatilia historia ya nyimbo za harmonize kuanzia Aiyola hadi anatoka WCB, itakuwa ngumu sana kuniaminisha nyimbo kama wote na nitaubeba hazina mkono wa Ibrah..

Maana kiuandishi, Harmo hamfikii Ibrah kwenye nyimbo za mapenzi. Sikiliza nitachelewa ya Ibrah ndio utanielewa, na ndio maana nahisi harmo kaondoa wasanii wake wote konde gang ila Ibrah hamuachii. Maana Ukiachana na success, Ibrah ana kichwa cha mashairi
 
1. Marioo
2. Harmonize
3. Jay Melody
4. Mbosso
5. Jux
6. Chino
7. D. Platnumz
8. Zuchu
9. Alikiba
10. Nandy

Hizo takwimu ni kutokana na performance zao huku mtaani ndani ya miaka mitano ya hivi karibuni kulingana na mtazamo wangu.

Nipe List yako
msanii Budagala Mwanamalonja wa huku simiyu amekosekana kwenye listi kweli?🐒
 
Sikujua kama Marioo angekuja kuwa msanii mkubwa namna hii, jamaa nlikuwa namsikiliza ana style moja ya kuimba kila nyimbo analalamika na kulia, nlipokuja kumuona anaimba na amapino nikasema ohooooo!!!!

Mama amina nadhani ndio amapiano ya kwanza bongo kabla hata ya Diamond.
 
Mkuu unajua kuchambua mziki vizuri af hauna ushabiki mandazi, kudos for that.!

Mimi mziki wa Bongo naupenda sana kwa kuwa unapigwa kila kona ila ni mpenzi mkubwa sana wa Rhumba na HipHop.
Huku kwenye BongoFleva wasanii wamekua na janjajanja nyingi sana wa kutembea na upepo, Namba moja kabisa ni Ali na Shemeji yake Nasibu. Hao ni waigizaji pro max maana mashairi yao ni 0 na wengine kibao
Diamond ni siku hizi tu kaishajipata, anapiga ngoma kufata upepo, ila diamond wa zamani au hata huyu akiamua kuandika mashairi yaliyonyooka anaweza, kiba uwezo wa kuandika mistari mizuri saana hana.
 
Umemshusha sana 😁😁😁😁
Mbona hata mapenzi yanarun dunia ilikuwa nzuri sanaaa

Halafu nilichokijua, hizi labels mara nyingi ukiangalia nyimbo zinavyotoka, unajua kabisa kuna mkono wa mtu aliyeandika

Binafsi nikifuatilia historia ya nyimbo za harmonize kuanzia Aiyola hadi anatoka WCB, itakuwa ngumu sana kuniaminisha nyimbo kama wote na nitaubeba hazina mkono wa Ibrah..

Maana kiuandishi, Harmo hamfikii Ibrah kwenye nyimbo za mapenzi. Sikiliza nitachelewa ya Ibrah ndio utanielewa, na ndio maana nahisi harmo kaondoa wasanii wake wote konde gang ila Ibrah hamuachii. Maana Ukiachana na success, Ibrah ana kichwa cha mashairi
Mapenzi yanarun dunia, yes, ndio imo kwenye list ya zile ngoma chache kali kiuandishi kwa kiba.

Ibra sijamsikiliza saana, huenda akawa ana mchango kwenye uandishi ila yule KIPIPA, naamini nae ni mkali saana, mfano jana nimesikiliza na ngoma inaitwa mdomo na dharau, mule kwenye mdomo bado harmonize kaonesha ukubwa, kwenye dharau pia kaonesha ukubwa wake. Yule MJOMBA NCHUMALI ni hatari sema ndio basi tu inaonekana zaidi ya uandishi kwenye mengine ni empty set. Life skills, management nzur hana
 
Sikujua kama Marioo angekuja kuwa msanii mkubwa namna hii, jamaa nlikuwa namsikiliza ana style moja ya kuimba kila nyimbo analalamika na kulia, nlipokuja kumuona anaimba na amapino nikasema ohooooo!!!!

Mama amina nadhani ndio amapiano ya kwanza bongo kabla hata ya Diamond.
Dogo anajitahidi sana. Nimesikiliza hii "hakuna matata" nikasema dogo anapita vizuri kwenye chaki
 
Kila kitu kina peak yake, mondi aliifikiaga hiyo kitaambo, sasa anaishi kwa nguvu hiyo.
Marioo ndio kajipata yupo level hiyo,
Harmonize ana maintain bado yupo kwenye ubora wake
Tofauti yao ni namna walitumia akili zao wakiwa kwenye ubora wao, alichofanya mondi kinaonekana na ndio kinambeba hata sasa, mondi anaweza imba ukuti ukuti na bado akabamba.
Mario ni muda wake atumie vizuri.
Mmakonde yeye yupo yupo tu.
Kwenye uandishi na melodies namtoa mario hayupo daraja la kina mondi.

Harmonize na mondi ni kama masteringi wa kichina na mamasta wao, masta anamfundisha steringi, adui atakuja kumuua masta wake ila wanafunzi anaua kiboko ya masta wake.
Ukimsikiliza mjomba nchumali vizuri kuna vitu utaviona, ila ndio hivyo tena mungu hakupi vyote. Ngoma NITAUBEBA, WOTE, TENA, amelowa, zanzibar na nyingine kama 5 hivi, nimesikiliza kisha nikabaki natikisa kichwa kumuheshimu huyu mmakonde.

Mondi ni sir alex ferguson, pep guardiola afanye anavyoweza kufanya, likitajwa jina la fergie ni jambo jingine, heshima yake ni kubwa zaidi, japo takwimu zinambeba pep
Kweli mkuu mond kajua kucheza na sanaa.
Kipindi harmonize yupo wasafi alipita kwenye reli ya mondi alafu akaja kujibrand alone kwa mipigo yake.
 
Nasikiliza sana ngoma za harmonize kajamaa kana uandishi flan hivi amazing
 
Msanii namba saba jamii forum.
Cha ajabu ndiye msanii namba moja kwenye kila kitu,kuanzia tuzo za ndani na nje.
Streams mtandaoni
Deals za makampuni.
Ngoma zake kutembea sana kitaani.
Habari zake kuuza zaidi kwenye media.
Tajiri kuliko wasanii wote Tanzania.
Niliacha kumshabikia Diamond alipojigeuza adui wa wapinzani na Rafik wa watawala.
Lakini ukweli utabaki kuwa ukweli.
Tanzania kuna Diamond peke yake then hao wafuatao ndiyo top ten
Kwa hiyo mtoe hapo kwenye list
 
Umekosea diamond kumweka hiyo nafasi in short Diamond ndio SI UNIT wa mziki wa Tanzania ili uonekane bora lazima ufananishwe nae
 
1. Marioo
2. Harmonize
3. Jay Melody
4. Mbosso
5. Jux
6. Chino
7. D. Platnumz
8. Zuchu
9. Alikiba
10. Nandy

Hizo takwimu ni kutokana na performance zao huku mtaani ndani ya miaka mitano ya hivi karibuni kulingana na mtazamo wangu.

Nipe List yako
Huo ni mtiririko kwa mujibu wa ubora au,ili nijue huu ugomvi ni mkubwa kiasi gani. Naona kuna wahuni unawatafuta ugomvi.
 
Baada ya kutosikiliza muziki muda mrefuuu, usiku wa leo(kiswahili usiku wa jana) nilipata mizuka, nikaona kila siku kina tupac na bob, ngoja nile za kizazi hiki, nikanogewa na mmakonde harmonize, ngoma kama
Nitaubeba.
Wote
Tena
Kuna moja jina sikumbuki anasema hana ushamba wa hela ndio maana hagombani na masela
ZANZIBAR, bonge la ngoma, hii zanziba watumie kama goma lao la taifa kiutalii.
Inanimaliza
Falling in love
Kuna moja anasema hata simu nikikupigia utaikata,

Nyingine sikumbuki kwa majina, kwemye uandishi na melody mmakonde hatari saana kale kajamaa.

Mario nilimsikiliza ila naona melody zinaingiliana kwa mbaaali, pia kwenye uandishi hana mistari mikali kama ya MJOMBA NCHUMALI.

Jana nimekuta youtube albamu kama 4 hivi za mjomba nchumali, nimezisikiliza karibia mgoma zote ni chache sana nimeruka.

Nyongeza nimesikiliza ngoma za ali kiba, ngoma pekee ilinivutia na nikairudia rudia ni UTU aisee bonge moja la ngoma plus mistari imenyooka, sitaki kuamini hii ngoma ali KAANDIKA mwenyewe, ali si muandishi mzuri wa mistari, yaani sitaki kuamini zile lyrics kaandika yeye, wajuzi mtaniambia nijiprove mwemyewe ile ngoma ali kaandika ama kaandikiwa. Ile ngoma itakuwepo kwenye kusherehekea miaka kadhaa ya ndoa yangu, siku hiyo kama nitakuwa mzima wa afya nitamfanyia mama watoto suprise, kwanza nitamsikilizisha ngoma ya TENA, NITAUBEBA na WOTE kisha atamalizia na UTU na kijizawadi kitakuwepo, hili wazo limekuja baada ya kusikiliza ngoma za MJOMBA NCHUMALI.
Mkuu ebu fungua code hapo kwa MJOMBA NCHUMALI, nimetoka kapa ujue😅
 
List yangu kwa mtazamo wangu;

1.Diamond Platinum
2.Harmonize
3.Jay Melody
4.Mbosso
5.Zuchu
6.Marioo
7.Ali kiba
8.Lava Lava
9.Rayvanny
10.Ibrah Nation
 
Back
Top Bottom