Lita 1 ya petrol inaweza kutembeza pikipiki ya TVS kilomita ngapi?

Lita 1 ya petrol inaweza kutembeza pikipiki ya TVS kilomita ngapi?

Bei zinatofautiana kutokana na mkoa uliopo.

Kwa Dar Petrol kwa sasa ni 3200 Tsh.

TVS vina engine ndogo cc 125 vinaweza kwenda hadi kilometa 50 kwenda juu, factors zipo nyingi mfano uendeshaji, milima au tanbarare, mzigo uliobeba service history...
++
hata tvs zina injini zenye ukubwa tofauti.
-za cc110 inaenda hadi km 65-70 toleo la nyuma kidogo. shoo ya mbele kubwa sana. wanazo kwa wingi rwanda na drc
-za cc 125 zinakula 45-50
-cc 150 hadi 40

matokeo ya unywaji hutegemea mambo mtambuka: upya wa oil, chain adjustments, upepo wa matairi, gear engagement, hali ya barabara (mchanga, lami, changarawe, miinuko na tambarare), ukubwa wa mizigo na ujuzi wa dereva
 
Mi nimewahi miliki pikipiki mbili tu, KTM cc390 na CBR cc650. Nilipewa maangalizo mawili makubwa Wekeza Sana kwenye Usalama wako (Safety Gears) na kua na heshima sana barabarani.



Usichukulie poa.



Unakuta mtu anaendesha pikipiki na sendo. Aisee. Ukiangimuka unapoteza vidole vyote.



Bila kofia ngumu. Au anavaa kofia ya elfu 15 sijui zile unapewa bure ukinunua pikipiki. Siwasemi ila hamna kitu pale.



Unaendesha na vest, shati, bila koti.



Etc etc etc



Wekeza sana kwenye safety gear, kuan na heshima usiendeshe kama una haraka umeacha familia umeenda kutafuta ugali wanataka jioni urudi sio wao waje hospital kukuona.
🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom