Live Kutoka Mbinguni/ Welcome back to Heaven

Live Kutoka Mbinguni/ Welcome back to Heaven

HADITHI ZA mbinguni ni nzuri tatizo ni kwamba kabla hujaenda lazima upitie KIFO (labda kama wewe ni Henoko au Eliya).

Wahubiri wengi wanahubiri maisha baada ya kifo, hawahubiri jinsi gani tuishi kwa furaha hapa duniani.

Kama Mungu angetaka angewaweka mbinguni msiteseke lipo kusudi la kuletwa duniani tulijue na tufurahie maisha.
Ubarikiwe ndugu Girl and!!

Mtu ni ROHO Si mwili.

Unaweza kupelekwa Mbinguni na Kisha kurudishwa tena katika mwili Yesu akiamua kufanya hivyo.

Yohana aliyeandika ufunuo wa Yohana alienda Mbinguni Kisha akarudishwa kuandika kitabu Cha ufunuo.

Habari za Mbinguni Kwa watakatifu ni kuwakumbusha kuwa duniani tu wapitaji tu.

Amen
 
Kwanini?
MTU ni roho!
Na roho INA mahali inatoka unawekewa,na ukifa inatoka inarudi ilikotoka!
Ndo maana ya hiyo aya!

Futa aya ya kwanza mwanadamu hajawahi kuwepo milele huko ni kumkufuru Mungu
 
Ubarikiwe ndugu Girl and!!

Mtu ni ROHO Si mwili.

Unaweza kupelekwa Mbinguni na Kisha kurudishwa tena katika mwili Yesu akiamua kufanya hivyo.

Yohana aliyeandika ufunuo wa Yohana alienda Mbinguni Kisha akarudishwa kuandika kitabu Cha ufunuo.

Habari za Mbinguni Kwa watakatifu ni kuwakumbusha kuwa duniani tu wapitaji tu.

Amen
Yesu alisema SIWAOMBEI UWATOE DUNIANI akijua fika kuna watu wanahubiri habari za mbinguni wanasahau kwamba Mungu aliumba mbingu na nchi akamuweka INTENTIONALLY mwanadamu kwenye nchi akamwambia atawale na kuvitiisha vitu vyote!

Tusiingie huu mtego, ukisoma vizuri hata mbinguni ni kwa muda tu!!!
 
Yesu alisema SIWAOMBEI UWATOE DUNIANI akijua fika kuna watu wanahubiri habari za mbinguni wanasahau kwamba Mungu aliumba mbingu na nchi akamuweka INTENTIONALLY mwanadamu kwenye nchi akamwambia atawale na kuvitiisha vitu vyote!

Tusiingie huu mtego, ukisoma vizuri hata mbinguni ni kwa muda tu!!!
Ni sawa,

Lazima tupite duniani twende Mbinguni Kisha baada ya Dunia kuangamizwa, utateremshwa mji mpya na Nchi mpya na tutaishi milele.

Kwakuwa Dunia itaangamizwa, sisi tunapita tu, tuwekeze Mbinguni, akiba zetu hazitapotea.

Ubarikiwe. Amen
 
Ubarikiwe ndugu Girl and!!

Mtu ni ROHO Si mwili.

Unaweza kupelekwa Mbinguni na Kisha kurudishwa tena katika mwili Yesu akiamua kufanya hivyo.

Yohana aliyeandika ufunuo wa Yohana alienda Mbinguni Kisha akarudishwa kuandika kitabu Cha ufunuo.

Habari za Mbinguni Kwa watakatifu ni kuwakumbusha kuwa duniani tu wapitaji tu.

Amen
Kingine mtumishi DO NOT, I REPEAT DO NOT UNDERESTIMATE MWILI,bila huo hauwezi kufanya kazi kwenye ulimwengu unaoonekana ni SHERIA ndiyo sababu YESU alivaa MWILI.

udhaifu wa mwili ndiyo unauwezesha kustahili nguvu za Mungu kama bible isemavyo tuwapo wadhaifu NDIPO TUNA NGUVU.

kuna sababu Mungu kakupa mwili mtumishi Rabbon
 
Kingine mtumishi DO NOT, I REPEAT DO NOT UNDERESTIMATE MWILI,bila huo hauwezi kufanya kazi kwenye ulimwengu unaoonekana ni SHERIA ndiyo sababu YESU alivaa MWILI.

udhaifu wa mwili ndiyo unauwezesha kustahili nguvu za Mungu kama bible isemavyo tuwapo wadhaifu NDIPO TUNA NGUVU.

kuna sababu Mungu kakupa mwili mtumishi Rabbon
Siudharau mwili, ni instrument muhimu tuwapo duniani,

Lakini mwili ni dhaifu, hautendi mapenzi ya Mungu,

MWILI muda wote upo kushindana na Roho.

Asili ya MWILI ni udongo mavumbini, lakini Asili ya Mtu ambaye ni ROHO ni Mbinguni.

Asante Kwa mchango mzuri. Ubarikiwe.
 
Nimefurahi jamaa kufika mbinguni wengine tushafika na kupitiliza ata saivi hatuna uhakika tuko wapi ila najua tuko mbinguni kwa mbele yakee
 
Nimefurahi jamaa kufika mbinguni wengine tushafika na kupitiliza ata saivi hatuna uhakika tuko wapi ila najua tuko mbinguni kwa mbele yakee
Nawe ubarikiwe.

Siku ya HUKUMU Jina lako litajwe katika kitabu Cha Uzima, uingie Mbinguni Kwa maisha ya milele.

Amen
 
Hapa mtumishi huelewi unachokisema BIBLIA ikikwambia Mwili ambao hautendi mapenzi ya Mungu wanamaanisha EMOTIONS yaani hisia

Binadamu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu anakuwaje dhaifu?

Mungu alivyomaliza kuumba aliangalia vitu vyote akaviona kuwa ni VYEMA, wewe unakuja unataka tuamini Mwili ni dhaifu? Unapingana na uumbaji??

Ukitolewa mwili unaouita UDHAIFU unakosa sifa za kuishi duniani!! Ni passport, ya kuwa hapa duniani huko mbinguni huhitaji mwili huu kufunction.

Tuwaambie watu jinsi gani wataishi maisha yaliyoandikwa katika Kumbukumbu 8,tuwaeleze jinsi gani Muumba aliuvaa mwili ili atukomboe toka kwenye dhambi ili tuhesabiwa haki kwa KULIAMINI NENO LAKE


Siudharau mwili, ni instrument muhimu tuwapo duniani,

Lakini mwili ni dhaifu, hautendi mapenzi ya Mungu,

MWILI muda wote upo kushindana na Roho.

Asili ya MWILI ni udongo mavumbini, lakini Asili ya Mtu ambaye ni ROHO ni Mbinguni.

Asante Kwa mchango mzuri. Ubarikiwe.
 
Hapa mtumishi huelewi unachokisema BIBLIA ikikwambia Mwili ambao hautendi mapenzi ya Mungu wanamaanisha EMOTIONS yaani hisia

Binadamu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu anakuwaje dhaifu?

Mungu alivyomaliza kuumba aliangalia vitu vyote akaviona kuwa ni VYEMA, wewe unakuja unataka tuamini Mwili ni dhaifu? Unapingana na uumbaji??

Ukitolewa mwili unaouita UDHAIFU unakosa sifa za kuishi duniani!! Ni passport, ya kuwa hapa duniani huko mbinguni huhitaji mwili huu kufunction.

Tuwaambie watu jinsi gani wataishi maisha yaliyoandikwa katika Kumbukumbu 8,tuwaeleze jinsi gani Muumba aliuvaa mwili ili atukomboe toka kwenye dhambi ili tuhesabiwa haki kwa KULIAMINI NENO LAKE
Basi tusibishane.

Ubarikiwe 🙏
 
Yaani,ila wanavyoliwa Sasa huko na wasaidizi wa mtumishi,utasikia nimefunuliwa we ndio mke wangu,anahama from one place to another
Jikite kwenye mada. Tafadhari 🙏
 
INTRODUCTON:

Shalom!!

Nawakaribisha tena Mbinguni, Mbinguni ndiko tulikokuwako milele kabla ya Mungu kutuleta duniani kupitia pumzi ya uhai Kwa baba na mama zetu wa duniani.

Mbinguni ni wapi?

Hapa tunapoishi ni Mbingu ya kwanza, Mbinguni tunapoongelea Leo ni Mbingu ya tatu. Ukiigawa katika matabaka inajulikana ni Mbingu ya saba. Huko ndipo tutakapokuwa tukipaangazia katika mada hii Kwa muda mrefu sana. Ni lifetime experience, maana Yesu huwachukua watu wengi sana na kuwapeleka Mbinguni Kisha huwarudisha Ili walete shuhuda Ili kuwaimarisha WATAKATIFU walioko duniani.

MY LIFE EXPERIENCE.

Nilipokuwa mdogo sikumbuki miaka, lakini nakumbuka kumbukumbu hiyo nzuri kuwahi kuipata katika Maisha yangu hapa duniani.

Nalikuwa katika njonzi, ghafula, kufumba na kufumbua, nilikuwa katika Nchi nzuri ambayo uzuri wake hauelezeki.

Palikuwa na Nuru njema sana iliyong'aa, mwonekano wa Nuru Ile ,haukufanana na Nuru ya mchana Wala Nuru ya mbalamwezi wakati wa usiku.

Niliangaza kulia na kushoto, nyuma Ili nione asili ya Nuru Ile bila mafanikio, nilijaribu kupiga hatua nione wapi Nuru Ile njema ilikotokea, Nuru Ile haikuchoma kama mwanga wa jua, palikuwa tulivu na pazuri sana, moyoni nilijawa na furaha tele kuwapo katika Nchi Ile ambayo haikuwa na Jua Wala mwezi lakini ilijaa Nuru nzuri yenye kuvutia sana.

Kila nilipoongeza hatua kuikaribia Nuru Ile nzuri yenye RANGI nzuri ambazo kamwe Hadi Leo hii sijawahi kuziona katika Ulimwengu huu, Nuru Ile ilizidi kuwa mbali nami na nilizidi kuifuata lakini kamwe sikuweza kufika mwisho, Mahali pale na Nchi Ile nilitamani sana kuendelea kuwepo. Lakini Kwa Bahati mbaya nilistuka nikiwa nimelala kitandani na nilipatwa na huzuni kurudi katika mazingira haya ya hapa tulipo.

Katika mada hii nitakuwa nikikuletea shuhuda za Raia waliotoka Mbinguni, waliopelekwa tena Mbinguni na kuonyesha uzuri wa Mbinguni Ili kuja kuwatia moyo WATAKATIFU Duniani waendelee kuvumilia Ili siku ikifika waingie mji Ule mzuri.

LIVE KUTOKA MBINGUNI. ( Na Adam Mbaya).

Nilipokuwa katika kusoma BIBLIA, BWANA Yesu alinitokea na kuniambia kuwa, Leo nitakupeleka Mbinguni, Mahali pazuri makazi ya WATAKATIFU.

Ghafula nikajiona nimegawanyika, niliona mwili wangu Ukiwa chumbani na Mimi nikiwa naelekea juu sana Kwa Kasi ya ajabu.

Tukiendelea na safari Ile Hadi tulipofika Mahali ambapo palikuwa na mpaka kati ya uumbaji nyuma yetu, na umilele mbele yetu.

Nyuma yetu Mahali pa uumbaji niliweza kuona nyota nyingi, lakini mbele yetu katika umilele, hapakuonekana mwisho wake.

MAPOKEZI YA MBINGUNI/HUDUMA YA NYUMBANI.

Tulipofika Mahali hapa, naliona Malaika wengi sana na WATAKATIFU ambao walikuwa wanapokelewa Ili kujiandaa kupanda Mbinguni juu zaidi.

Mahali pale palikuwa pazuri sana ambapo uzuri wake Si Rahisi kuelezea,

MUZIKI.

Malaika walikuwa wakiimba huku wakipiga vifaa mbalimbali vya MUZIKI ambavyo vipo hapa duniani na vingine ambavyo SIKUWAHI kuviona kabla.

Mahali hapa palikuwa na furaha tele,WATAKATIFU waliopokelewa Mahali pale walikuwa wenye furaha tele na walipongezana na kukumbatiana Kwa furaha. Palisikika mziki mkubwa na mzuri sana wa kumsifu Mungu.

Zilisikika nyimbo nzuri za kusifu na kuabudu ambazo huimbwa hapa duniani, nilishangaa kusikia nyimbo hizo Mahali pale na nilimuuliza BWANA Yesu kuwa kwanini wanaimba nyimbo zetu.
Yesu alijibu, duniani Kuna uchafuzi mkubwa hivyo Mungu hutuma neno lake kupitia nyimbo Ili kubariki WATAKATIFU.

MIILI YA WATAKATIFU.

Mwonekano wa miili hiyo ya WATAKATIFU ilionekana kama miili ya kioo, transparent , iliyong'aa sana. Na umri wa WATAKATIFU walipofika pale mapokezi ya Mbinguni ilionekana sawa wote walionekana wenye umri sawa kama miaka 30 hivi. Hapakuwa na Mzee aliyeingia Mbinguni na uzee wake,hapakuwa na mgonjwa Wala mlemavu, walipewa miili Bora. Hapakuwa na njaa, Wala huzuni Wala DHIKI.

MIILI ya WATAKATIFU ilizidiana kungaa, wahubiri INJILI waling'aa sana miili Yao, waliotunza na kuhudumia wajane, yatima, maskini,wagonjwa Kwa pesa zao pia waling'aa sana.

NDOA.

Mmoja wa WATAKATIFU aligeuka na kumwona aliyekuwa mume wake alifika Mahali pale pa mapokezi na walikumbatiana Kwa furaha na kulia machozi ya furaha.

Hapakuwa na NDOA Mahali pale kama duniani,mke na mume waliitana kaka na dada, na tamaa za mwili hazikuwepo Mahali pale, palifunikwa na furaha na utukufu wa Mungu.

VYAKULA.

Malaika wengine walikuwa wakiwahudumia WATAKATIFU MATUNDA YA MWILI WA DHAHABU. Niliona pia Malaika wakimimina juice Kwa watakatifu ambayo ilikuwa ya kipekee.

Nilitamani kunywa juice Ile lakini Yesu aliniambia kuwa juice Ile ni spesho Kwa washindao ambao ni WATAKATIFU.

Nilimwona pia Malaika mmoja akiwa anakula EMBE!! Nilimuuliza, BWANA, Pana maembe huku?

Yesu alinijibu vyakula vyote vilivyoko duniani, vipo Mbinguni na zaidi ya hapo. Pana miti mingi ya matunda mengi ambayo mengine hayapo duniani, Mbinguni ni kizuri sana.

Yesu aliniambia huku Kuna Kila chakula Cha asili kulingana vyakula WATAKATIFU walivyokula duniani, na Malaika walihudimia WATAKATIFU, walipika na kuwahudumia maana ni Wana wa ufalme. Malaika walivutiwa sana kuwaona WATAKATIFU maana wakishinda Hila na majaribu ya mwovu duniani.

NJIA ZA MBINGUNI.

Palikuwa na njia 12 zilizokuwa na Majina ya Wana wa Israel/ Yakobo.

Njia hizo ziliandikwa, 1.REUBEN 2.SIMEON. 3.ZABULONI. 4. LAWI 5. YUDA 6. ISAKARI 7.BENJAMINI 8. YUSUPHU 9. GADI 10. ASHERI. 11. DANI 12. NAPHTALI.

MALANGO YA MBINGUNI.

Pia palikuwa na Malango 12 ya Mbinguni yaliyoandikwa Majina 12 ya Wana wa Israeli kama zilivyokuwa njia zile 12. Na Kila lango alisimama Malaika mlangoni mwenye upanga mkubwa.

MAGARI YA MBINGUNI.

Baada ya mapokezi ya mahali pale, Malaika alipuliza tarumbeta kuwaarifu WATAKATIFU waliokuwa mapokezi ya Mbinguni kupanga foleni Ili kupanda magari ya Mbinguni kuwapeleka juu zaidi Mbinguni.

Yalishika magari ya Dhahabu, yenye kuwaka moto mtakatifu yaliyokuwa yakiendeshwa na Malaika, na Malaika waliwaongoza WATAKATIFU kupanda magari hayo yaliyokokotwa na farasi. Mahali pale na uzuri Ule hauelezeki.

ITAENDELEA......
Umejitahidi sana kuandika jambo hili la safari yako ya kwenda mbinguni.
Lakini nilipokusoma na kuona error kulingana na mafunuo ya ujumla wa maandiko ya biblia nikapata shaka kwamba hili andiko ni la kiakili na kama sivyo adui alihusika kukupa hili ono.
Kilichonipa shaka ni kuona ulipozungumzia majina 12 ya wana wa Israel kule mbinguni jina la Dani likiwepo.
Majina 12 ya wana wa Israel yaliyotiwa mhuri katika ufunuo 7 jina la Dani halimo.
Halimo kwa kuwa liliondolewa na sababu ni ibaada ya sanamu.
Ukiangalia vizuri maandiko wana wa Israel ni 12 ikiwa ni pamoja na Dani ,Lawi na Yusufu. Lakini katika kitabu cha Hesabu waliopewa heshima ya kushikilia majina 12 ya kabila za Israel pana Jina la Manase na Efraim bila kuwepo na jina la Lawi na Yusufu.
Lawi na Yusufu hawakuwepo kwa sababu Lawi yeye alichukuwa uridhi wake kwa Mungu kwa kuwa hakugawiwa eneo la kuridhi. Yusufu yeye eneo la urithi wake lilishikiliwa na mwanae mmojawapo kati ya wawili waliopewa heshima hiyo yaani Efraim na Manase.
Sasa wakati Israel walipokuwa wamerudi kwenye ardhi ya wenyeji wao wakati kukiwa na mgawanyiko kati yao juu ya ufalme wa Yuda chini ya Rehoboam mwana wa Suleiman na ufalme wa Israel chini ya Yeroboam mwana wa Nebati, eneo la Dani na Efraim ndilo lililotoa nafasi ya kujengwa madhabahu watu waabudu huko ili watu wasipande Yerusalemu kuabudu katika hekalu la Bwana lililojengwa na Suleimani.
Kwa sababu ya dhambi hii ya kuruhusu madhabahu ya mungu mgeni katika ardhi ya urithi wao Mungu aliwaondoa katika heshima ya kushikilia jina la kabila Dani na Efraimu na badala yake majina yaliyotiwa mhuri ya ufunuo 7 linarejeshwa jina la Lawi na Yusufu huku nafasi ya jina la Dani ikishikiliwa na jina la Manase.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umejitahidi sana kuandika jambo hili la safari yako ya kwenda mbinguni.
Lakini nilipokusoma na kuona error kulingana na mafunuo ya ujumla wa maandiko ya biblia nikapata shaka kwamba hili andiko ni la kiakili na kama sivyo adui alihusika kukupa hili ono.
Kilichonipa shaka ni kuona ulipozungumzia majina 12 ya wana wa Israel kule mbinguni jina la Dani likiwepo.
Majina 12 ya wana wa Israel yaliyotiwa mhuri katika ufunuo 7 jina la Dani halimo.
Halimo kwa kuwa liliondolewa na sababu ni ibaada ya sanamu.
Ukiangalia vizuri maandiko wana wa Israel ni 12 ikiwa ni pamoja na Dani ,Lawi na Yusufu. Lakini katika kitabu cha Hesabu waliopewa heshima ya kushikilia majina 12 ya kabila za Israel pana Jina la Manase na Efraim bila kuwepo na jina la Lawi na Yusufu.
Lawi na Yusufu hawakuwepo kwa sababu Lawi yeye alichukuwa uridhi wake kwa Mungu kwa kuwa hakugawiwa eneo la kuridhi. Yusufu yeye eneo la urithi wake lilishikiliwa na mwanae mmojawapo kati ya wawili waliopewa heshima hiyo yaani Efraim na Manase.
Sasa wakati Israel walipokuwa wamerudi kwenye ardhi ya wenyeji wao wakati kukiwa na mgawanyiko kati yao juu ya ufalme wa Yuda chini ya Rehoboam mwana wa Suleiman na ufalme wa Israel chini ya Yeroboam mwana wa Nebati, eneo la Dani na Efraim ndilo lililotoa nafasi ya kujengwa madhabahu watu waabudu huko ili watu wasipande Yerusalemu kuabudu katika hekalu la Bwana lililojengwa na Suleimani.
Kwa sababu ya dhambi hii ya kuruhusu madhabahu ya mungu mgeni katika ardhi ya urithi wao Mungu aliwaondoa katika heshima ya kushikilia jina la kabila Dani na Efraimu na badala yake majina yaliyotiwa mhuri ya ufunuo 7 linarejeshwa jina la Lawi na Yusufu huku nafasi ya jina la Dani ikishikiliwa na jina la Manase.

Sent using Jamii Forums mobile app
Uko sawa,

Kama umesoma vizuri ni ushuhuda wa Aston Mbaya. Kosa ni langu niliyereport, naomba nisamehewe Kwa kukosea na ninarudi kubadili. USHUHUDA wake haukutaja Majina, Mimi ndiye niliyekosea kuyaandika Kwa kutumia kitabu Cha mwanzo Badala ya Ufunuo.

Ahsante Kwa ufafanuzi na ninarudi kuedit.

UBARIKIWE.

Amen
 
Huyu bwana Adam Mbaya alikua anazungumza lugha gani na Yesu?
Lugha zinazotumika Mbinguni ni lugha za Mbinguni.

Mwanadamu hupewa kuelewa tafsiri ya lugha hizo. Na akiongea wanaelewana.

Ubarikiwe.
 
Ndugu Kiby karibu sana kushare nasi shuhuda za Mbinguni ulizo nazo katika Uzi huu Ili kuwatia moyo WATAKATIFU na kuhubiri INJILI.

Ubarikiwe.
 
Ndugu mwandishi naona una ujumbe mzuri ila ubora wa uwasilishaji wako upo partial .. mfano,hujaeleza namna ulivyokutana na Yesu bali unasema ukamuuliza Yesu hatujui umekutana naye vip na umemjuaje ni Yesu?
Kuongezea je,Yesu alikuwa mzungu, mwarabu,mwafrika,muhindi ? Muonekano wake ,rangi,nywele?
 
Back
Top Bottom