Live Kutoka Mbinguni/ Welcome back to Heaven

Live Kutoka Mbinguni/ Welcome back to Heaven

Mambo ya rohoni hayana matunda kwa watu wa mwilini na mara nyingi husikika kama kufuru na ushahidi wa haya upo kibao kwa hukumu zilizowahi kutolewa na watawaba(dini) kwa manabii au wapakwa mafuta.
Ushuhuda huu uliouleta umelenga sana utawala ule wa milele na maskani yake itakavyo kuwa. Ramani yake kwa uhalisi inapatikana katika kitabu cha ufunuo 21 yaani yerusalemu ya mbinguni. Ni mji wa mraba marefu na mapana yake yakilingana kwa kipimo cha maili 1,500. Hakuna hekalu ndani yake wala kanuni za maumbile ya asili mfano wa jua la mchana na nyota za usiku wala majira ya nyakati kwa sababu uumbaji umerudishwa kwenye umilele(eternity) Ni kweli kuna mto wa maji ya uzima na pia kuna mti wa matunda ukizaa kila matunda mfululizo matunda kwa ajili ya wateule na majani yake ni uponyaji kwa wenyeji. Haya yote ni mambo ya kilindi sana maana hutambulikana kwa jinsi ya roho. Katika bustani ya Edeni palikuwa na mti wa uzima katikati yake ambapo kabla ya anguko katika ule umilele uliopotezwa na Adamu kwa kula kwenye mti wa ujuzi wa mema na mabaya uliokatazwa. Huo mti uliwekewa makerubi kuulinda hata ukombozi mkamilifu wa miili ya watakatifu. Tunayo arabuni(dhama) ya roho wa Kristo hata huo ukamilifu wa wakati.
Kwenye ulimwengu wa roho kuna tofauti ya mbingu moja kwenda nyingine hadi mbingu ya saba iliyo mbingu za mbingu.
Hivyo unapotoa ushuhuda ni lazima ujue unashuhudia mbingu ipi. Kuna ufufuo wa kwanza na ufufuo wa pili, kuna mauti ya kwanza na mauti ya pili yaani lile ziwa la moto, kuna harusi ya mwana kondoo(miaka 1,000) na umilele(eternity) vitu hivi huchanganywa sana.
Lakini uaminifu wa wateule wa Mungu wajapokuwa wajinga hawatapotea katika ile njia ila ieleweka kati ya tofauti ya wajinga na wapumbavu. Wajinga ni wanyoofu wa moyo na hufu dishika bali wapumbavu ni washupavu wasiofundishika wala kurekebishika.
Chariot ni gari la moto la farasi katika ulimwengu wa roho nalo huwabeba watakatifu walalapo mauti.
Farasi hawa wa moto mtumishi wa Elisha aliombewa macho yake yafunguke aone jeshi hili la Mungu katika farasi na alipoona hofu ya asili ya kanuni za maumbile ikamtoka na kuwaita adui waje ili waufikilie mwisho wao.
Hakuna kilicho katika maumbile ya asili ya mwili ambacho hakikuanzia rohoni kwamba ni ulimwengu wa roho wa Mungu ama ulimwengu wa roho wa upotofu wa shetani.

Barikiwa!

Sent using Jamii Forums mobile app
Ubarikiwe mtumishi Kwa ufanuzi mzuri.

Pamoja sana. Amen
 
Haya nionyeshe sehemu Ambayo imeandikwa ukifa unaenda juu direct nionyeshe kutumia Mafungu ya biblia maana imeandikwa waenende kwa ushuhuda...

Mhubiri 9:5​

kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lolote, wala hawana tuzo tena; maana hata kumbukumbu lao limesahauliwa.

Zaburi 146 :4 Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, Siku hiyo mawazo yake yapotea.
(Zaburi 115:17), “…wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu yao, husuda yao, imepotea yote pamoja…”
(Mhubiri 9:10), waliokufa “hawawezi kuitarajia kweli”

(Isaya 38:18), waliokufa “hawawezi kumwona Mungu wala kumwona mwanadamu”
(Isaya 38:10,12); roho ya mtu aliyekufa pia “huzimika”,

Ayubu 17:1 inasema, Roho yangu imezimika, siku zangu zimekoma, Kaburi i tayari kunipokea.”
Ayubu 14:10,12,21 inasema, “Lakini mwanadamu hufa…Naam, mwanadamu hutoa roho, naye yupo wapi?…Ni vivyo mwanadamu hulala chini, asiinuke; Hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka, Wala kuamshwa uzingizini…”


NAJUA KUWA MWILI NA NYAMA HAZITAURITHI UFALME KWA HIYO ROHO ZITURITHI SASA SWALI KWAKO KAMA ROHO IMESHAANZA KUURITHI UFALME YESU ANAKUJA KUFANYAJE NA ANAKUJA KUFUFUA NINI...?
WATAKATIFU waliookoka wafapo na kwenda Mbinguni, huenda kupumzika kusubiri siku ya HUKUMU.

Waliokufa katika Dhambi huenda kuzimu kusubiri HUKUMU.

Hawachanganywi pamoja.

Hujasoma Ufunuo imeandikwa Yesu atakuja akiambatana na maelfu ya WATAKATIFU?

Ndo nakwambia, kusoma BIBLIA utasoma, ila kuielewa ndipo ulipo mtihani.

Ubarikiwe.
 
WATAKATIFU waliookoka wafapo na kwenda Mbinguni, huenda kupumzika kusubiri siku ya HUKUMU.

Waliokufa katika Dhambi huenda kuzimu kusubiri HUKUMU.

Hawachanganywi pamoja.

Hujasoma Ufunuo imeandikwa Yesu atakuja akiambatana na maelfu ya WATAKATIFU?

Ndo nakwambia, kusoma BIBLIA utasoma, ila kuielewa ndipo ulipo mtihani.

Ubarikiwe.
Na ndo maan nimekuambia nionyeshe hayo mafungu unayosema 😅

Biblia inasema

Isa 8:20 SUV

Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili (Biblia), bila shaka kwa hao hapana asubuhi.

Sasa mkuu ......
Shetani bado anaendelea na msemo wake kuwadanganya na kuwaambia hakika hamtakufa ila mtafanana na yeye?

Maana ufunuo kuna Ufufuo wa kwanza na wa pili..
Ufufuo wa kwanza kwa ajili ya watakatifu na ufufuo wa pili ni kwa ajili ya wadhambi..

Sasa kama hakuna kufa anafufua nini 😅😅

Ufunuo 20:6
"Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu."


1 The 4:13-18 SUV​

Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
SASA WEWE UNATOA WAPI UNAYOFUNDISHA WATU ACHA KUPOTOSHA..

Kama hutatoa andiko nawaonya wakristo wanaokusikiliza kwa...

1 Yoh 4:1 SUV

Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
 
Na ndo maan nimekuambia nionyeshe hayo mafungu unayosema 😅

Biblia inasema

Isa 8:20 SUV

Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili (Biblia), bila shaka kwa hao hapana asubuhi.

Sasa mkuu ......
Shetani bado anaendelea na msemo wake kuwadanganya na kuwaambia hakika hamtakufa ila mtafanana na yeye?

Maana ufunuo kuna Ufufuo wa kwanza na wa pili..
Ufufuo wa kwanza kwa ajili ya watakatifu na ufufuo wa pili ni kwa ajili ya wadhambi..

Sasa kama hakuna kufa anafufua nini 😅😅

Ufunuo 20:6
"Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu."


1 The 4:13-18 SUV​

Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
SASA WEWE UNATOA WAPI UNAYOFUNDISHA WATU ACHA KUPOTOSHA..

Kama hutatoa andiko nawaonya wakristo wanaokusikiliza kwa...

1 Yoh 4:1 SUV

Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
Kumuelewesha MSABATO KAZI sana.

Tuanzie hapa.

1. Mtu ni nini?

2. Kufa ni nini?

Twende Polepole kabisa.
 
Kumuelewesha MSABATO KAZI sana.

Tuanzie hapa.

1. Mtu ni nini?

2. Kufa ni nini?

Twende Polepole kabisa.
Dah mkuu una bahati mbaya sana me sio msabato kabisa..
Nashindwa nikueleweshe kutumia hali ipi ngoja nitumie Biblia tu maana nikitumia vitu vingine ntakupoteza..

Mtu kw mujibu wa biblia ni Mwili wenye pumzi ya uhai kwa mujibu wa maandiko ya kibiblia..

Kufa ninkuondokea na Pumzi ya uhai

Nimekujibu kwa level ya chini kabisa..
 
Dah mkuu una bahati mbaya sana me sio msabato kabisa..
Nashindwa nikueleweshe kutumia hali ipi ngoja nitumie Biblia tu maana nikitumia vitu vingine ntakupoteza..

Mtu kw mujibu wa biblia ni Mwili wenye pumzi ya uhai kwa mujibu wa maandiko ya kibiblia..

Kufa ninkuondokea na Pumzi ya uhai

Nimekujibu kwa level ya chini kabisa..
3. Roho ni nini?

4. NAFSI ni nini?

Nijibu, usichoke 🙏
 
3. Roho ni nini?

4. NAFSI ni nini?

Nijibu, usichoke 🙏
maswali yako ni mazuri halafu very Important..
(MIND, BODY, SPIRIT)
(SPIRIT,SOUL AND BODY)

Holy triology

natamani Nikujibu kwa mlengo wa spirituality ila ngoja nikujibu kwa mlengo wa kibiblia...

Roho (Spirit) in maana nyingi snaa natamani niongee maana huu ni ulimwengu mpana sana..

japo kibiblia ni simply Pumzi ya uhai na ulimwengu fulan

ila nafsi (Soul) ni utambuzi wa mwili yani uwepo wa kimwili

Ila natamani nieleze zaidi
 
maswali yako ni mazuri halafu very Important..
(MIND, BODY, SPIRIT)
(SPIRIT,SOUL AND BODY)

Holy triology

natamani Nikujibu kwa mlengo wa spirituality ila ngoja nikujibu kwa mlengo wa kibiblia...

Roho (Spirit) in maana nyingi snaa natamani niongee maana huu ni ulimwengu mpana sana..

japo kibiblia ni simply Pumzi ya uhai na ulimwengu fulan

ila nafsi (Soul) ni utambuzi wa mwili yani uwepo wa kimwili

Ila natamani nieleze zaidi
Mungu aliposema, na Tuumbe mtu Kwa Mfano wetu,

Kati ya MWILI , NAFSI na ROHO, mtu aliye mfano wa Mungu ni yupi kati ya hivyo vitatu?

Tukipata jibu Hilo itakuwa Rahisi kujua nini maana ya "WAFU hawajui lolote ".
 
Mungu aliposema, na Tuumbe mtu Kwa Mfano wetu,

Kati ya MWILI , NAFSI na ROHO, mtu aliye mfano wa Mungu ni yupi kati ya hivyo vitatu?

Tulipata jibu Hilo itakuwa Rahisi kujua nini maana ya "WAFU hawajui lolote ".
Mkuu sasa huu ndo uwanja wangu Na ningetamani tuwe na maongezi marefu kuhusu hili..(Maana hili linahusu spirituality na mimi ndo mlengo wangu huko)

Ila Mungu aliumba Mwili akampulizia Pumzi (Roho) yenye Nafsi ya Uhai..
Kwahyo uliumbwa Mwili ila vilivyotoka kwke ni Nafsi na Roho...
Mkuu natamani tuwe na mjadala mkubwa sana kuhusu haya mambo
 
Mkuu sasa huu ndo uwanja wangu Na ningetamani tuwe na maongezi marefu kuhusu hili..(Maana hili linahusu spirituality na mimi ndo mlengo wangu huko)

Ila Mungu aliumba Mwili akampulizia Pumzi (Roho) yenye Nafsi ya Uhai..
Kwahyo uliumbwa Mwili ila vilivyotoka kwke ni Nafsi na Roho...
Mkuu natamani tuwe na mjadala mkubwa sana kuhusu haya mambo
Pumzi( Roho) ilipoungana na mwili ndipo ilipozaliwa NAFSI hai.

Kwahiyo jibu kuhusu "WAFU hawajui lolote" limepatikana?

Kwamba vinapotengana hivi vitatu, kipi hakijui lolote?

Kwa maana tumejua kilicho mfano wa Mungu ni Cha milele, kufa ni kutengana udongo Ulio mavumbi usojitambua, na umilele.
 
Pumzi( Roho) ilipoungana na mwili ndipo ilipozaliwa NAFSI hai.

Kwahiyo jibu kuhusu "WAFU hawajui lolote" limepatikana?

Kwamba vinapotengana hivi vitatu, kipi hakijui lolote?

Kwa maana tumejua kilicho mfano wa Mungu ni Cha milele, kufa ni kutengana udongo Ulio mavumbi usojitambua, na umilele.
Sasa hiyo nafsi ndo huifadhiwa mpaka siku ya hukumu ila kinachomrudia mungu ni roho
 
INTRODUCTON:

Shalom!!

Nawakaribisha tena Mbinguni, Mbinguni ndiko tulikokuwako milele kabla ya Mungu kutuleta duniani kupitia pumzi ya uhai Kwa baba na mama zetu wa duniani.

Mbinguni ni wapi?

Hapa tunapoishi ni Mbingu ya kwanza, Mbinguni tunapoongelea Leo ni Mbingu ya tatu. Ukiigawa katika matabaka inajulikana ni Mbingu ya saba. Huko ndipo tutakapokuwa tukipaangazia katika mada hii Kwa muda mrefu sana. Ni lifetime experience, maana Yesu huwachukua watu wengi sana na kuwapeleka Mbinguni Kisha huwarudisha Ili walete shuhuda Ili kuwaimarisha WATAKATIFU walioko duniani.

MY LIFE EXPERIENCE.

Nilipokuwa mdogo sikumbuki miaka, lakini nakumbuka kumbukumbu hiyo nzuri kuwahi kuipata katika Maisha yangu hapa duniani.

Nalikuwa katika njonzi, ghafula, kufumba na kufumbua, nilikuwa katika Nchi nzuri ambayo uzuri wake hauelezeki.

Palikuwa na Nuru njema sana iliyong'aa, mwonekano wa Nuru Ile ,haukufanana na Nuru ya mchana Wala Nuru ya mbalamwezi wakati wa usiku.

Niliangaza kulia na kushoto, nyuma Ili nione asili ya Nuru Ile bila mafanikio, nilijaribu kupiga hatua nione wapi Nuru Ile njema ilikotokea, Nuru Ile haikuchoma kama mwanga wa jua, palikuwa tulivu na pazuri sana, moyoni nilijawa na furaha tele kuwapo katika Nchi Ile ambayo haikuwa na Jua Wala mwezi lakini ilijaa Nuru nzuri yenye kuvutia sana.

Kila nilipoongeza hatua kuikaribia Nuru Ile nzuri yenye RANGI nzuri ambazo kamwe Hadi Leo hii sijawahi kuziona katika Ulimwengu huu, Nuru Ile ilizidi kuwa mbali nami na nilizidi kuifuata lakini kamwe sikuweza kufika mwisho, Mahali pale na Nchi Ile nilitamani sana kuendelea kuwepo. Lakini Kwa Bahati mbaya nilistuka nikiwa nimelala kitandani na nilipatwa na huzuni kurudi katika mazingira haya ya hapa tulipo.

Katika mada hii nitakuwa nikikuletea shuhuda za Raia waliotoka Mbinguni, waliopelekwa tena Mbinguni na kuonyesha uzuri wa Mbinguni Ili kuja kuwatia moyo WATAKATIFU Duniani waendelee kuvumilia Ili siku ikifika waingie mji Ule mzuri.

LIVE KUTOKA MBINGUNI. ( Na Adam Mbaya).

Nilipokuwa katika kusoma BIBLIA, BWANA Yesu alinitokea na kuniambia kuwa, Leo nitakupeleka Mbinguni, Mahali pazuri makazi ya WATAKATIFU.

Ghafula nikajiona nimegawanyika, niliona mwili wangu Ukiwa chumbani na Mimi nikiwa naelekea juu sana Kwa Kasi ya ajabu.

Tukiendelea na safari Ile Hadi tulipofika Mahali ambapo palikuwa na mpaka kati ya uumbaji nyuma yetu, na umilele mbele yetu.

Nyuma yetu Mahali pa uumbaji niliweza kuona nyota nyingi, lakini mbele yetu katika umilele, hapakuonekana mwisho wake.

MAPOKEZI YA MBINGUNI/HUDUMA YA NYUMBANI.

Tulipofika Mahali hapa, naliona Malaika wengi sana na WATAKATIFU ambao walikuwa wanapokelewa Ili kujiandaa kupanda Mbinguni juu zaidi.

Mahali pale palikuwa pazuri sana ambapo uzuri wake Si Rahisi kuelezea,

MUZIKI.

Malaika walikuwa wakiimba huku wakipiga vifaa mbalimbali vya MUZIKI ambavyo vipo hapa duniani na vingine ambavyo SIKUWAHI kuviona kabla.

Mahali hapa palikuwa na furaha tele,WATAKATIFU waliopokelewa Mahali pale walikuwa wenye furaha tele na walipongezana na kukumbatiana Kwa furaha. Palisikika mziki mkubwa na mzuri sana wa kumsifu Mungu.

Zilisikika nyimbo nzuri za kusifu na kuabudu ambazo huimbwa hapa duniani, nilishangaa kusikia nyimbo hizo Mahali pale na nilimuuliza BWANA Yesu kuwa kwanini wanaimba nyimbo zetu.
Yesu alijibu, duniani Kuna uchafuzi mkubwa hivyo Mungu hutuma neno lake kupitia nyimbo Ili kubariki WATAKATIFU.

MIILI YA WATAKATIFU.

Mwonekano wa miili hiyo ya WATAKATIFU ilionekana kama miili ya kioo, transparent , iliyong'aa sana. Na umri wa WATAKATIFU walipofika pale mapokezi ya Mbinguni ilionekana sawa wote walionekana wenye umri sawa kama miaka 30 hivi. Hapakuwa na Mzee aliyeingia Mbinguni na uzee wake,hapakuwa na mgonjwa Wala mlemavu, walipewa miili Bora. Hapakuwa na njaa, Wala huzuni Wala DHIKI.

MIILI ya WATAKATIFU ilizidiana kungaa, wahubiri INJILI waling'aa sana miili Yao, waliotunza na kuhudumia wajane, yatima, maskini,wagonjwa Kwa pesa zao pia waling'aa sana.

NDOA.

Mmoja wa WATAKATIFU aligeuka na kumwona aliyekuwa mume wake alifika Mahali pale pa mapokezi na walikumbatiana Kwa furaha na kulia machozi ya furaha.

Hapakuwa na NDOA Mahali pale kama duniani,mke na mume waliitana kaka na dada, na tamaa za mwili hazikuwepo Mahali pale, palifunikwa na furaha na utukufu wa Mungu.

VYAKULA.

Malaika wengine walikuwa wakiwahudumia WATAKATIFU MATUNDA YA MWILI WA DHAHABU. Niliona pia Malaika wakimimina juice Kwa watakatifu ambayo ilikuwa ya kipekee.

Nilitamani kunywa juice Ile lakini Yesu aliniambia kuwa juice Ile ni spesho Kwa washindao ambao ni WATAKATIFU.

Nilimwona pia Malaika mmoja akiwa anakula EMBE!! Nilimuuliza, BWANA, Pana maembe huku?

Yesu alinijibu vyakula vyote vilivyoko duniani, vipo Mbinguni na zaidi ya hapo. Pana miti mingi ya matunda mengi ambayo mengine hayapo duniani, Mbinguni ni kizuri sana.

Yesu aliniambia huku Kuna Kila chakula Cha asili kulingana vyakula WATAKATIFU walivyokula duniani, na Malaika walihudimia WATAKATIFU, walipika na kuwahudumia maana ni Wana wa ufalme. Malaika walivutiwa sana kuwaona WATAKATIFU maana wakishinda Hila na majaribu ya mwovu duniani.

NJIA ZA MBINGUNI.

Palikuwa na njia 12 zilizokuwa na Majina ya Wana wa Israel/ Yakobo.


MALANGO YA MBINGUNI.

Pia palikuwa na Malango 12 ya Mbinguni yaliyoandikwa Majina 12 ya Wana wa Israeli kama zilivyokuwa njia zile 12. Na Kila lango alisimama Malaika mlangoni mwenye upanga mkubwa.

MAGARI YA MBINGUNI.

Baada ya mapokezi ya mahali pale, Malaika alipuliza tarumbeta kuwaarifu WATAKATIFU waliokuwa mapokezi ya Mbinguni kupanga foleni Ili kupanda magari ya Mbinguni kuwapeleka juu zaidi Mbinguni.

Yalishika magari ya Dhahabu, yenye kuwaka moto mtakatifu yaliyokuwa yakiendeshwa na Malaika, na Malaika waliwaongoza WATAKATIFU kupanda magari hayo yaliyokokotwa na farasi. Mahali pale na uzuri Ule hauelezeki.

ITAENDELEA......
Bangi si nzuri
 
WATAKATIFU waliookoka wafapo na kwenda Mbinguni, huenda kupumzika kusubiri siku ya HUKUMU.

Waliokufa katika Dhambi huenda kuzimu kusubiri HUKUMU.

Hawachanganywi pamoja.

Hujasoma Ufunuo imeandikwa Yesu atakuja akiambatana na maelfu ya WATAKATIFU?

Ndo nakwambia, kusoma BIBLIA utasoma, ila kuielewa ndipo ulipo mtihani.

Ubarikiwe.
sasa kama wafu wakifa wanaenda mbinguni kwanini ww ukiumwa unaenda hospital si usubiri ukufe uende peponi...na kama wanaenda mbinguni basi iyo hukumu ya kiama ya kazi gan
 
WATAKATIFU waliookoka wafapo na kwenda Mbinguni, huenda kupumzika kusubiri siku ya HUKUMU.

Waliokufa katika Dhambi huenda kuzimu kusubiri HUKUMU.

Hawachanganywi pamoja.

Hujasoma Ufunuo imeandikwa Yesu atakuja akiambatana na maelfu ya WATAKATIFU?

Ndo nakwambia, kusoma BIBLIA utasoma, ila kuielewa ndipo ulipo mtihani.

Ubarikiwe.
duuu ambaye haielewi biblia anajifanya mjanja ety ukifa unaenda mbinguni na wengne waenda kuzimu duuuh.
..

.sasabkama ni hivi basi hakuna haja ya iyo hukumu maana wengne wameenda kuzimu wengne wapo mbinguni🤣😆😅
NAFSI huhifadhiwa wapi?

Na inapohifadhiwa hujitambua au haijitambui?
nafsi = roho + mavumbi kaburini maiti haijitambui iv unajua maana yabkufa? from biology pointbof view
 
sasa kama wafu wakifa wanaenda mbinguni kwanini ww ukiumwa unaenda hospital si usubiri ukufe uende peponi...na kama wanaenda mbinguni basi iyo hukumu ya kiama ya kazi gan
Hakuna Mbingu ya WAFU,

Mbingu ni ya WATAKATIFU Walio hai.

Amwaminiye Kristo Yesu hafi, analala tu.

Mbinguni watakatifu wanaenda kupumzika wakisubiri HUKUMU.

Kuna UNYAKUO, MAUTI ya kwanza na MAUTI ya pili, usichanye vitu hivyo vitatu.
 
duuu ambaye haielewi biblia anajifanya mjanja ety ukifa unaenda mbinguni na wengne waenda kuzimu duuuh.
..

.sasabkama ni hivi basi hakuna haja ya iyo hukumu maana wengne wameenda kuzimu wengne wapo mbinguni🤣😆😅

nafsi = roho + mavumbi kaburini maiti haijitambui iv unajua maana yabkufa? from biology pointbof view
Biology haijadiliwi hapa.

Hapa tunajadili spiritual realm.
 
Mbingu ya kiwaki huku kwetu kuna mbususu za kumwaga chura pro max wachana na izo fake za mloganzia
 
INTRODUCTON:

Shalom!!

Nawakaribisha tena Mbinguni, Mbinguni ndiko tulikokuwako milele kabla ya Mungu kutuleta duniani kupitia pumzi ya uhai Kwa baba na mama zetu wa duniani.

Mbinguni ni wapi?

Hapa tunapoishi ni Mbingu ya kwanza, Mbinguni tunapoongelea Leo ni Mbingu ya tatu. Ukiigawa katika matabaka inajulikana ni Mbingu ya saba. Huko ndipo tutakapokuwa tukipaangazia katika mada hii Kwa muda mrefu sana. Ni lifetime experience, maana Yesu huwachukua watu wengi sana na kuwapeleka Mbinguni Kisha huwarudisha Ili walete shuhuda Ili kuwaimarisha WATAKATIFU walioko duniani.

MY LIFE EXPERIENCE.

Nilipokuwa mdogo sikumbuki miaka, lakini nakumbuka kumbukumbu hiyo nzuri kuwahi kuipata katika Maisha yangu hapa duniani.

Nalikuwa katika njonzi, ghafula, kufumba na kufumbua, nilikuwa katika Nchi nzuri ambayo uzuri wake hauelezeki.

Palikuwa na Nuru njema sana iliyong'aa, mwonekano wa Nuru Ile ,haukufanana na Nuru ya mchana Wala Nuru ya mbalamwezi wakati wa usiku.

Niliangaza kulia na kushoto, nyuma Ili nione asili ya Nuru Ile bila mafanikio, nilijaribu kupiga hatua nione wapi Nuru Ile njema ilikotokea, Nuru Ile haikuchoma kama mwanga wa jua, palikuwa tulivu na pazuri sana, moyoni nilijawa na furaha tele kuwapo katika Nchi Ile ambayo haikuwa na Jua Wala mwezi lakini ilijaa Nuru nzuri yenye kuvutia sana.

Kila nilipoongeza hatua kuikaribia Nuru Ile nzuri yenye RANGI nzuri ambazo kamwe Hadi Leo hii sijawahi kuziona katika Ulimwengu huu, Nuru Ile ilizidi kuwa mbali nami na nilizidi kuifuata lakini kamwe sikuweza kufika mwisho, Mahali pale na Nchi Ile nilitamani sana kuendelea kuwepo. Lakini Kwa Bahati mbaya nilistuka nikiwa nimelala kitandani na nilipatwa na huzuni kurudi katika mazingira haya ya hapa tulipo.

Katika mada hii nitakuwa nikikuletea shuhuda za Raia waliotoka Mbinguni, waliopelekwa tena Mbinguni na kuonyesha uzuri wa Mbinguni Ili kuja kuwatia moyo WATAKATIFU Duniani waendelee kuvumilia Ili siku ikifika waingie mji Ule mzuri.

LIVE KUTOKA MBINGUNI. ( Na Adam Mbaya).

Nilipokuwa katika kusoma BIBLIA, BWANA Yesu alinitokea na kuniambia kuwa, Leo nitakupeleka Mbinguni, Mahali pazuri makazi ya WATAKATIFU.

Ghafula nikajiona nimegawanyika, niliona mwili wangu Ukiwa chumbani na Mimi nikiwa naelekea juu sana Kwa Kasi ya ajabu.

Tukiendelea na safari Ile Hadi tulipofika Mahali ambapo palikuwa na mpaka kati ya uumbaji nyuma yetu, na umilele mbele yetu.

Nyuma yetu Mahali pa uumbaji niliweza kuona nyota nyingi, lakini mbele yetu katika umilele, hapakuonekana mwisho wake.

MAPOKEZI YA MBINGUNI/HUDUMA YA NYUMBANI.

Tulipofika Mahali hapa, naliona Malaika wengi sana na WATAKATIFU ambao walikuwa wanapokelewa Ili kujiandaa kupanda Mbinguni juu zaidi.

Mahali pale palikuwa pazuri sana ambapo uzuri wake Si Rahisi kuelezea,

MUZIKI.

Malaika walikuwa wakiimba huku wakipiga vifaa mbalimbali vya MUZIKI ambavyo vipo hapa duniani na vingine ambavyo SIKUWAHI kuviona kabla.

Mahali hapa palikuwa na furaha tele,WATAKATIFU waliopokelewa Mahali pale walikuwa wenye furaha tele na walipongezana na kukumbatiana Kwa furaha. Palisikika mziki mkubwa na mzuri sana wa kumsifu Mungu.

Zilisikika nyimbo nzuri za kusifu na kuabudu ambazo huimbwa hapa duniani, nilishangaa kusikia nyimbo hizo Mahali pale na nilimuuliza BWANA Yesu kuwa kwanini wanaimba nyimbo zetu.
Yesu alijibu, duniani Kuna uchafuzi mkubwa hivyo Mungu hutuma neno lake kupitia nyimbo Ili kubariki WATAKATIFU.

MIILI YA WATAKATIFU.

Mwonekano wa miili hiyo ya WATAKATIFU ilionekana kama miili ya kioo, transparent , iliyong'aa sana. Na umri wa WATAKATIFU walipofika pale mapokezi ya Mbinguni ilionekana sawa wote walionekana wenye umri sawa kama miaka 30 hivi. Hapakuwa na Mzee aliyeingia Mbinguni na uzee wake,hapakuwa na mgonjwa Wala mlemavu, walipewa miili Bora. Hapakuwa na njaa, Wala huzuni Wala DHIKI.

MIILI ya WATAKATIFU ilizidiana kungaa, wahubiri INJILI waling'aa sana miili Yao, waliotunza na kuhudumia wajane, yatima, maskini,wagonjwa Kwa pesa zao pia waling'aa sana.

NDOA.

Mmoja wa WATAKATIFU aligeuka na kumwona aliyekuwa mume wake alifika Mahali pale pa mapokezi na walikumbatiana Kwa furaha na kulia machozi ya furaha.

Hapakuwa na NDOA Mahali pale kama duniani,mke na mume waliitana kaka na dada, na tamaa za mwili hazikuwepo Mahali pale, palifunikwa na furaha na utukufu wa Mungu.

VYAKULA.

Malaika wengine walikuwa wakiwahudumia WATAKATIFU MATUNDA YA MWILI WA DHAHABU. Niliona pia Malaika wakimimina juice Kwa watakatifu ambayo ilikuwa ya kipekee.

Nilitamani kunywa juice Ile lakini Yesu aliniambia kuwa juice Ile ni spesho Kwa washindao ambao ni WATAKATIFU.

Nilimwona pia Malaika mmoja akiwa anakula EMBE!! Nilimuuliza, BWANA, Pana maembe huku?

Yesu alinijibu vyakula vyote vilivyoko duniani, vipo Mbinguni na zaidi ya hapo. Pana miti mingi ya matunda mengi ambayo mengine hayapo duniani, Mbinguni ni kizuri sana.

Yesu aliniambia huku Kuna Kila chakula Cha asili kulingana vyakula WATAKATIFU walivyokula duniani, na Malaika walihudimia WATAKATIFU, walipika na kuwahudumia maana ni Wana wa ufalme. Malaika walivutiwa sana kuwaona WATAKATIFU maana wakishinda Hila na majaribu ya mwovu duniani.

NJIA ZA MBINGUNI.

Palikuwa na njia 12 zilizokuwa na Majina ya Wana wa Israel/ Yakobo.


MALANGO YA MBINGUNI.

Pia palikuwa na Malango 12 ya Mbinguni yaliyoandikwa Majina 12 ya Wana wa Israeli kama zilivyokuwa njia zile 12. Na Kila lango alisimama Malaika mlangoni mwenye upanga mkubwa.

MAGARI YA MBINGUNI.

Baada ya mapokezi ya mahali pale, Malaika alipuliza tarumbeta kuwaarifu WATAKATIFU waliokuwa mapokezi ya Mbinguni kupanga foleni Ili kupanda magari ya Mbinguni kuwapeleka juu zaidi Mbinguni.

Yalishika magari ya Dhahabu, yenye kuwaka moto mtakatifu yaliyokuwa yakiendeshwa na Malaika, na Malaika waliwaongoza WATAKATIFU kupanda magari hayo yaliyokokotwa na farasi. Mahali pale na uzuri Ule hauelezeki.

ITAENDELEA......
Mkuu kama Kuna kula na kunywa huko mbinguni, inamaana nyumba za huko Zina vyoo kama huku Duniani?
 
Back
Top Bottom