Live updates, Ligi Kuu Vodacom: Mgambo vs Yanga

Live updates, Ligi Kuu Vodacom: Mgambo vs Yanga

Results Mgambo 0 - Yanga 2 Ngoja sasa tutizame uchambuzi wa Edo na Mayai mechi hii live AZAM TV2 AZAM Media Flash Page

Simon Msuva na Amis Tambwe waunaji wa Yanga.

Kesho timu yetu ya AZAM vs Coastal inashuka hapo hapo Mkwakwani.
 
Ata Simba mara mojamoja ni raha kama hivi.


http://shaffihdauda.co.tz/okwi-aibeba-simba-taifa-aifunga-yanga-1-0/

Hata mgambo raha siku moja moja kama hivi

http://shaffihdauda.co.tz/simba-yagongwa-virungu-viwili-na-mgambo-ivo-alambwa-kadi-nyekundu/
 
Leo ni kindumbwe ndumbwe uwanja wa Mkwakwani mechi kati ya Mgambo FC ( kiboko ya vigogo) watawakabili wawakilishi pekee wa Tanzania katika mashindano ya kimataifa Dar es salaam Yanga African mnamo saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Tukumbuke Timu zote zilifanikiwa kupata matokeo katika mechi zao zilizopita Yanga wakiwasambaratisha wakata miwa wa Kagera Sugar na Mgambo akiivulumusha bila huruma Simba S.C wazee wa homa za vipindi.

Mashabiki wa MGAMBO WAKIINGIA LEO MKWAKWANI!!!
 

Attachments

  • mgambo+wakiingia+(2).JPG
    mgambo+wakiingia+(2).JPG
    6.3 KB · Views: 445
Pointi Tatu muhimu kibindoni tunaendelea kukalia kiti cha uongozi wa ligi. Na huu moto hauzimiki hadi tunachukua ubingwa wa Tanzania.

Mikia fc a.k.a wa mchangani waendelee kugaragazwa na migambo pamoja na wapiga bebe wakati sisi tunaelekea kwenye ubingwa.
 
Back
Top Bottom