Liverpool FC (The Reds) | Special Thread


Unadhani furaha yao itadumu? Keshokutwa tu watapigwa Wamtukane Arteta na Hamis77.
 
Kati ya mechi 24 tumewafunga 3 tu. Mnategemea tukae kimya? Acha ushamba. Lazima tuwatambie mtujue sisi ni nani vikuku nyie 😄😄.

Utani pembeni, utaona kwa mashabiki wa Arsenal ushindi wa jana unawapa matumaini kuwa timu inaanza kujitambua kwa kuanza kwenda jino kwa jino na kushinda dhidi ya kina Liverpool na Man City. Zimetokea mechi ambazo tumewazidi Liverpool na City au kushibana nguvu lakini wao wakashinda au kutoa sare na takwimu zinabaki kutufanya sisi tuonekane underdogs.

Ila tunataka kuamini hali inaanza kubadilika. Sasa misimu miwili EPL tumewapiga au mmeambulia sare. Kwa maana tunaanza kupata matumaini kuwa na nyie pia tutawarejesha kuwa wateja wetu kama tulivyowafanya Chelkenge. Bado Mamacita naye. Tunataka kuamini kuwa, muda si mrefu, Arsenal ile ambayo wakina Carragher walikuwa wakienda kuangalia kalenda ya msimu, wanacheki watakutana nasi lini ili wajue ni wiki gani ya kukosa usingizi kwa stress.
 
Chukueni ubingwa wazee. Siyo lazima City achukue, ameshauzoea. Sasa tumemletea ushindani.
 
Klopp aache kulalamika akubali matokeo
 
Kocha aliyechezesha ni wa arse8
Linatoa kadi sehemu sizizo za kadi
 
Manga ML tunakusalimu brother😂😂
Hapo vipi?unnaionaje timu bila ya Salah?

Kule jukwaa la Arsenal walikuwa wanalialia wanamuogopa Salah..na kweli akawatenda.

Ila Kuna watu tena Wanaliver wanakuja kusema eti bila Salah timu inacheza tu vizuri 😂😂
Nilicheka sana nikajisemea moyoni subiri mechi ije tufungwe.

Jana wote nadhani tumeona umuhimu na gap la Salah.

Salah msimu Jana ameibeba timu mabegani,timu ikiwa hoi mahututi...muda wote ni wa moto,tofauti na akina Jota ambao itategemea ameamka vipi.
 
Timu muda wote wanalia
Ni vichapo tu

Acha wasafishe nyota😂😂😂


Ukipita jukwaani kwao utaona sasa wanavyomsikiliza Hamis akichambua,anawaambia EPL wanaibeba😂
 
Jamaa yupo Slow sana
Lakini huwezi kumlaumu,bado ana muda.
Ndio kwanza hajamaliza hata msimu mmoja tangu aje.

He has room ila wasi wasi wangu ni kuondoka kwa Klopp je, ajaye atamvumulia? Silaha kubwa kwa Klopp ni uvumilivu aisee

Labde aje ajae kwenye mfumo kwa haraka anaweza kubaki.
 
Umeongea vizuri sana
Ila hujamgusa Allison mwanzo mwisho.

Hahah…!!! Bad day in a office Alisson ni moja ya siku mbaya sana kwake. Na ndivyo anacheza siku zote sema makosa yke mengi huwa anayafuta mwenyewe. Ni moja ya wachezaji kulaumiwa ni nadra mno hata akiharibu. Kazi anayopiga Alison sio kitoto, japo haiondoi aliharibu zaidi jana.

Wachezaji wanaoongoza kupokea lawama:

Nunez
Vvd
Trent
Salah
Gomez

Hawa jamaa makosa yao huwa yapo wazi mno machoni mwa mashabiki.


Ila kwa jana tukubali tu we were merely poor. Aina ya magoli tuliyofungwa unaona kama wachezaji hawakufanya warm up wamekurupuliwa humo basi tuingia tuchezeni.

Haya hivyo Arsenal hawakuwa wenye ubora huo, kama ni timu iliyokuwa bora tunge aibika sana. Mechi ya jana unakutana na Brighton unadhalilishwa,good thing tulikutana na mkubwa mwenzetu ambae hana madhara apato nafasi.

YNWA
 

Kumfunga Liverpool inabidi awe kwenye ubora wa ubovu wako ndio utamfunga. Inabidi timu iwe hovyo sana ndio inakuwa nafuu kwako.

Jana timu nzima ilikuwa mbovu, magoli tuliyofungwa yanakupa picha halisi. Mimi ninaamini tumefungwa sio kwa ubora wa Arsenal bali kwa ubovu wa wetu. Ubovu wetu umetufungusha.

Arsenal tried their best level and it paid them.
 

As long as hajaumia na maamuzi ya marefa bado odds zipo upande wake kubwa unlike their rivals.

Na imeleta ladha ya ubingwa. Atleast ni msimu bingwa atatoka jasho kweli kweli
 
City leo atataka sifa unaweza kuta anampiga mtu 5.

Sema kibonde pia hakiaminiki kinaweza kukaza.
 
Ila kiukweli mtindo wa Allison kutoka nje ya goli na kukaa karibia katikati ya uwanja ,utadhani naye ni beki aisee hii tabia inanikera sana.

Mechi vs Brighton tulifungwa na hiyo staili.
Alison hatoki tu kwa maamuzi ni maagizo kwa Klopp. Anasogea juu kuongeza idadi kubwa ya wachezaji. Anakuwa kama extra central defender ili kuruhusu kiungo (mara nyingi no. 6) kusogea juu kuongeza idadi ya wachezaji mbele. Ni risk sana sana, na hii inahitaji GK mwenye footwork nzuri ambayo Alison hana ni mdhaifu kwenye mguu. Mechi ya City alitoa pasi fyongo ikatugharimu, mechi vs Brighton staili hiyo ikatigharimu, jana pia.

Unahitaji Gk mwenye uwezo mguuni sana na hii inalipa sana kama una timu nzuri. Waangalia man city wakikutana ni mbinu ngumu na timu ngumu mathalani our last match with them (1-1) Ederson alitutesa sana na mipasi yake ile sana. Sasa unahitaji GK wa hivi kwa mbinu hiyo ina work vizuri, footwork wazuri kama Onana, Pickford, Ramsdale, Vicario na wengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…