Halafu kuna watu wanakuja kumbeza humu kwamba si lolote
Emotional vs Reality…
Unawaacha waamini kile wanachoamini but He will be remembered among the best.
Ynwa Jurgen Nobert Klopp.
Ilikuwa 24 April 2013 pale BVB Stadion Dortmund, Dortmund ilipowakutanisha timu mbili zenye daraja tofauti katika ulimwengu wa soka kati ya, Real Madrid na Borussia Dortmund kwenye michuano ya usiku wa ulaya, maarufu UEFA CHAMPIONS LEAGUE hatua ya nusu fainali.
Ilikuwa ni mechi ya pande moja on paper kutokana na Dortmund kutokuwa timu maarufu masikioni na machoni pa mashabiki wengi wa kabumbu duniani, haikua na mchezaji maarufu wala kocha maarufu wakati ule.
Ilionekana wazi Madrid atamtoa Dortmund na kutinga fainali, kutokana na uzoefu, aina ya wachezaji waliokuwepo na kocha aliye naye.
Basi majira ya saa 21:45 kama ilivyo ada ya michuano, timu zikaingia uwanjani, ikapigwa “UEFA ANTHEM” vikosi vikaoneshwq, hapo ndipo watu wakazidi kuona urahisi wa Madrid kushinda mechi ile.
Dortmund kikosi kiliundwa na:
Weidenfeller
Piszcek Subotic Hummels Schmeilzer
Bender Gundogan
Blaszczykowski Gotze Reus
Lewandowski
Higuain
Ronaldo Modric Ozil
Alonso Khedira
Contrao Pepe Varane Ramos
Lopez
Madrid iliundwa na full package.
Kipyenga kikapulizwa dk ya 9 kijana asiyetambulika na dunia ya mpira Lewandowski akaingia kambani, watu tukaona wamechokoza nyuki tu hawa ushindi kwa madrid haukwepeki. Dk ya 43 Cr7 akarejesha ikawa 1-1 mpaka HT.
Second Half ukapigwa mpira mmoja, wa fainali, HEAVY THROTTLE MENTAL, GEGGEN PRESSING, ELECTRIC FOOTBALL.
“Kipindi hicho nilikuwa shabiki pia wa Madrid, niliichukia Barca kwa mpira wake wa uonevu ule, ila kwa sasa siwapendi Madrid kwa sababu wamenionenea sana, last 5 matches they have won all, ikiwemo two CL final.”
Madrid hawakuelewa wao ndio underdog au Dortmund ndio underdog, mpaka kipyenga cha mwisho Dortmund 4-1 Madrid magoli yote manne yakafungwa na Robert Lewandowski kijana kutoka Poland, ndipo ilikuwa mechi ya kujitambulisha duniani who is he. And the rest is history.
Kwenye touchline ya Dortmund alisimama kocha mjerumani anaitwa Jurgen Norbert Klopp, jamaa aliitoa Dortmund kwenye hadhi ya chini sana na kuipa hadhi moja ya timu ngumu kukutana nayo nyakati zile. 2nd leg Madrid won 2-0 wasn’t enough for qualification with agg was 4-3, book his 1st CL final as a coach.
Wakaingia finali vs Bayern ambayo nao walitoka kumtoa muhispania Barcelona iliyokuwa bado ina ubora wake. Unfortunately Klopp and his boys didn’t win that final.
Klopp anastahili kuwa na makombe mengi zaidi ya yale aliyoyashinda ukilinganisha na idadi ya fainali alizozicheza.
Klopp ni mjenzi huru, mpe timu yako isiyojiweza kama utd ya sasa inayoishi maish ya Sir Alex kwenye zama za Pep, naye ataijenga na kuwa tishio baada ya hapo mshindwe wenyewe kuendeleza.
Your excellence will forever be at Anfield Jurgen Norbert Klopp.
Ynwa’