Livingstone Lusinde amshambulia Zitto Kabwe dhidi ya kauli yake ya wanaompenda Hayati Magufuli wakazikwe naye Chato

Livingstone Lusinde amshambulia Zitto Kabwe dhidi ya kauli yake ya wanaompenda Hayati Magufuli wakazikwe naye Chato

goroko77

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2019
Posts
8,845
Reaction score
13,072
Hbr za muda huu

Niko Hapa natazama Bunge la 12 mkutano wa saba , kikao Cha la kumi na moja , mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chini ya Waziri Jenister Muhaghama

Alipewa nafasi bwana Lusinde kuchangia katika mjadala unaoendelea badala ya kujikita katika hoja iliyopo mezani yeye amebaki kumtetea Hayati Magufuli na kusema kuwa ndugu Zitto aache upuuzi wake wa kumsema marehemu Magufuli kwani marehemu hasemwi na kumtaka kufuta kauli yake ya kusema wanaopenda sana Magufuli wakazikwe nae huko Chato, alisisitiza Sana kwa jazba bila hofu

Wakati jamaa anachangia hoja zake Bunge lilikaa kimya sana hakuna aliyempenyeza taarifa wala Mwenyekiti wa Bunge hakutoa neno la kumtaarifu ndugu Lusinde kujikita ktk hoja na kuachana Mambo ya kumjadili mtu pale jamaa alipewa muda kutoa yake ya moyoni na kumtaka ndugu Zitto kuomba msamaha kwa Mama Janeth Magufuli na familia yake kwa udhalilishaji anaoufanya.

Niliona kabisa kuwa jamaa anampenda sana Hayati Magufuli na yeye amesema wasi kabisa kuwa yeye anampenda na aachwe na Zitto afundishwe adabu. Lusinde anaongea as if kwamba hajui kuwa ktk kipindi cha Hayati Magufuli alitumika kuwatukana viongozi walioko sasa hivi madarakani haswa wa chama jamaa anaongea kwa kujiamini Sana na kutokujali

Asilimia 80 mpaka 90 ya Wabunge na Mawaziri wanamkubali sana Hayati Magufuli hata Jenister ni Magufuli forevermore yule.

Pia soma > Zitto: Wanaompenda Magufuli wakazikwe naye Chato, alikuwa Rais fisadi zaidi kuwahi kutokea Tanzania
 
Zitto, kama kweli kasema haya maneno, kachemsha vibaya sana.

Na anaweza kutafsirika kwamba anataka kuua watu asiokubaliana nao kisiasa. Au angalau yuko OK wakiuawa.

Kitu ambacho wapinzani wa Magufuli walimtuhumu Magufuli.

Nasema hayo kama mtu ambaye sijamkubali Magufuli katika utawala wake.

Hili ni somo jepesi tu katika siasa za kuishi na watu wengi wenye mawazo tofauti.

Tunatakiwa kupinga hoja za watu, bila kuwachukia wale watu tunaopingana na hoja zao.

Zitto Kabwe, kama kweli kasema maneno haya, ameonekana kuwachukia watu, badala ya kupinga hoja za watu.
 
"Zitto anatutaka tunaompenda Magufuli tukazikwe naye, Waislamu mmefunga, dini inakataza kuwasema vibaya marehemu na yeye ni Muislamu anajua, ametukosea sana, atuombe radhi Watanzania, @zittokabwe amemkosea sana Mama Magufuli na ameikosea familia"- Livingstone Lusinde
#Bungeni

3226B3B1-66B8-4ADF-A1E1-8608471E5797.jpeg
 
"Zitto anatutaka tunaompenda Magufuli tukazikwe naye, Waislamu mmefunga, dini inakataza kuwasema vibaya marehemu na yeye ni Muislamu anajua, ametukosea sana, atuombe radhi Watanzania, @zittokabwe amemkosea sana Mama Magufuli na ameikosea familia"- Livingstone Lusinde
#Bungeni

View attachment 2196330
Kwani vibajaji sivimekatazwa kuingia katikati ya mji!
 
Wakati mwengine sio lazima kujibu kila kitu unacho kisikia....kukaa kimya pia ni Jibu tosha.
 
Hbr za muda huu

Niko Hapa natazama Bunge la 12 mkutano wa saba , kikao Cha la kumi na moja , mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chini ya Waziri Jenister Muhaghama

Alipewa nafasi bwana Lusinde kuchangia katika mjadala unaoendelea badala ya kujikita katika hoja iliyopo mezani yeye amebaki kumtetea Hayati Magufuli na kusema kuwa ndugu Zitto aache upuuzi wake wa kumsema marehemu Magufuli kwani marehemu hasemwi na kumtaka kufuta kauli yake ya kusema wanaopenda sana Magufuli wakazikwe nae huko Chato, alisisitiza Sana kwa jazba bila hofu

Wakati jamaa anachangia hoja zake Bunge lilikaa kimya sana hakuna aliyempenyeza taarifa wala Mwenyekiti wa Bunge hakutoa neno la kumtaarifu ndugu Lusinde kujikita ktk hoja na kuachana Mambo ya kumjadili mtu pale jamaa alipewa muda kutoa yake ya moyoni na kumtaka ndugu Zitto kuomba msamaha kwa Mama Janeth Magufuli na familia yake kwa udhalilishaji anaoufanya.

Niliona kabisa kuwa jamaa anampenda sana Hayati Magufuli na yeye amesema wasi kabisa kuwa yeye anampenda na aachwe na Zitto afundishwe adabu. Lusinde anaongea as if kwamba hajui kuwa ktk kipindi cha Hayati Magufuli alitumika kuwatukana viongozi walioko sasa hivi madarakani haswa wa chama jamaa anaongea kwa kujiamini Sana na kutokujali

Asilimia 80 mpaka 90 ya Wabunge na Mawaziri wanamkubali sana Hayati Magufuli hata Jenister ni Magufuli forevermore yule.

Pia soma > Zitto: Wanaompenda Magufuli wakazikwe naye Chato, alikuwa Rais fisadi zaidi kuwahi kutokea Tanzania
Kwani Zitto yuko Bungeni? Mbona ile Spika iliyoharibika iltuambia Wabunge wanazuiwa na Kanuni kuwajadili watu ambao hawako Bungeni maana hawatapata nafasi ya kujitetea?
 
Uzi kama huu bila kakideo hata huwa hauvutii...bora usingeuweka
 
Wakati mwengine sio lazima kujibu kila kitu unacho kisikia....kukaa kimya pia ni Jibu tosha.
Kwani ukinyamaza ndio inakuwaje,siku hizi umatulia kama sio wewe,au baada ya kupata usajili umoja party.
 
Back
Top Bottom