Livingstone Lusinde, japo ni darasa la saba tuu, ni kichwa mbaya!, ana uwezo mkubwa na pia ana powers fulani!.

Sasa pascal hiyo ni historia ya maisha mbn umempamba ata ana uwezo mkubwa me nlijua utaongelea national issues kujenga hoja au vitu constructive
Jambo la maana analoweza kujiuliza huyo Lusinde ni: ''Je, background yake imemsaidia kuwa mbunge bora anayetetea maelefu ya maskini wanaoishi kama yeye alivyoishi ukitilia maanani ana expirience ya hayo maisha? Jibu ni HAPANA. Baada ya kupanda amewasahau walio kwenye maisha ya umaskini. Sijawahi kumwona wala kumsikia akipigania maskini wa Tanzania kama mbunge! Hili linafanya hiyo historia yake ya maisha isiwe na maana yoyote!
 
Binafsi simpendi kabisa Kibajaji ila huwezi kumng'oa Kibajaji kwa gia ya usomi wa huyo Profesa Kabudi, hiyo ni moja ya sababu iliyomngowa mzee Malecela.

Kwenye kura za maoni Kibajaji aliwauliza wapiga kura kuna mwenye degree wapiga kura kimya, kuna mwenye diploma wapiga kura kimya, kuna form six wote kimya kuna form wote kimyaa, akawaambia sasa nyinyi darasa la saba mimi ndio mwenzenu dalasa la saba mwenzenu, kupigwa kura tingatinga chali.

Kabudi aingie jimbo hilo kwa gia nyingine na siyo usomi ataduwazwa na hatoamini macho yake.
 
Watanzania wengi waliopata mafanikio kwa kutokea kwenye maisha ya chini wana tabia ya ku-exaggarate na kuongopa kuhusu maisha yao ya nyuma baada ya kupata mafanikio. Kama mtu alikuwa anakunywa chai ya rangi atasema alikuwa anakaa siku saba bila kula!
 
Maisha hayana formula.
Hii ndiyo kanuni ya Poise .

Japo, kamwe hatutafanana njia za mafanikio ndiyo maana maisha yanakosa formula katika kutoka kimaisha.
 
Hili ndio tatizo la wapiga kura wa maeneo hayo. Hawajielewi na hawajitambui!
 
kama ni drs la vii,hamna kitu,na bungen anapitisha asichokijua.Nimaneno naporojo nyingi do zinamfanya aonekane mjuaji.
 
Karne ya 21 kushabikia Darasa la 3 ni upungufu wa madini kichwani!!

Hizo ni bahati tu.... Bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi!!

Mbona matajiri wengi hii Tz ni std 7, akina Mwita Gachuma, nk. Hii haimaanishi wasomi hawana maana!! Thubutu!!

Pia hawa std 3, 4 & 7 wengi walikuwa Majambazi. Ila mtu akisha toka ata anza kusimulia ONLY the POSITIVE side.

Mf...Masanja ana hela tu nzr na sasa ni mchungaji. Mfuate sasa akusimulie, historia yake ya Maisha! Movie yake utaipenda ni zaidi ya KIKOREA.

Ww kama Mwandishi ulipaswa uchunguze kwanza kabla ya kuulisha umma na kuaminisha umma kuwa Elimu si chochote!!

Hii nchi inaendeshwa kisomi, ndio maana ipo!!
 
Maisha ni safari ndefu haijalishi una elimu au huna elimu ili mradi tu ufikie mafanikio ya malengo yako ya maisha duniani.
 
Luside huyu huyu
Huyu huyu aliyewashawishi watu wake wa Mtera kuwa wale watafiti kutoka Arusha kuwa ni wanyonya damu wakawaua na kuwachoma moto. Ndiyo huyu anayesema Paskali Mayalla kuwa ana IQ ya juu sana kiasi anafaa kuwa wa kuigwa.
Namshauri Paskali aende kwenye vijiwe atakutana na waswahili wanauelezea mpira na mbinu zake kuliko Wenger kiasi unajiuliza jee kwa nini Arsenal wasimchukue huyu na kumfukuzilia mbali Wenger!
 
Mkuu yeye ameishamaliza kusoma na mafanikio yake ni hayo kutoka machinga hadi ubunge tena wa Jamhuri katika chama cha CCM,ameoa,ana mali nyingi,alimuangusha kirahisi Waziri Mkuu mstaafu Mzee Malicela,kwenye kura za maoni tu.
 
Umeongea ukweli una uwezo mkubwa sana wa kupambanua mambo na kujenga na kuwasilisha hoja kwa lugha inayoeleweka...ni moja kati ya asset za chama tena yule alipaswa kuwa katibu mwenezi wa chama
Unamchongea, chakubanga atamroga sasa hivi.
 
Watanzania wengi wenye miaka 30+ au 35+ wametokea ktk mazingira magumu sana.
Wengi wamepambana sana kufanikiwa.

Wala haiana haja ya kumsifia sana, wengi tumetokea huko japo vikwazo vimetofautiana kidogo.

Pia wanasiasa wengi wanataka waonewe huruma.
Kichwa mtu ambae hathamini elimu na watu walio soma? Mfano alisema ama mshangaa Professor anaetaka kupima udongo wa shamba lake wakati yeye amelima hapo kwa miaka mitatu bila shida, huyu mtu hana uelewa mkubwa kiukweli.

Kwa mfano tu huo wa kupima udongo, yeye anaamini aridhi anayo lima itaendelea kuwa na rutuba miaka yote tu au ata liacha shamba na kulima sehemu nyingine na hajui kama atakuwa anafanya uharibifu wa mazingira.
 
Chakaza asante sana mpaka nimecheka wakati nina maumivu! Haya ndio maisha yetu halisi ya Bongo! Maneno na wenye maneno ndio wanathaminiwa kuliko matendo na wenye vitendo! Na mbaya zaidi ndio waliojaa kwenye siasa ambayo ndiyo inaongoza kila kitu.
 
Huyo hana uwezo wowote domo tu..bongo ukiwa na domo ndo utaishi sio smart head ya kufanya world changers decisions
 
INFACT ANATAIWA KUWA WAZIRI WA ELIMU AU SHERIA KAMA WABUNGE WALIVYOOMBA...NAAMINI MH MAGUFURI ATACHUKUA MAPENDEKEZO YA WABUNGE HAO NASISI NA WEWE TUTA MUUNGA MKONO.
Lusinde kuwa wazir wa wizara yeyote ile ni Joke hata unaibu ni mashaka...
 
Paskali hyo kibajaj ni zero kabisa tatizo humjui vizri
Mkuu Mgoloko, yes anaweza kuwa zero, pia ni kweli simjui vizuri, bali nimemsikiliza leo historia yake, alipotoka na mahali alipo sasa, wengi watakubaliana na mimi, kuwa, this man is genius!. Yes ni mropokaji na mpayukaji, hiki ndicho Watanzania wanachokitaka!.

Kipimo cha maendeleo ya kweli ni mafanikio na changing life style na doo vyeti mtu alivyohitimu. Huyu jamaa is a big success!. Being a school dropout, toka kuuza kahawa hadi kuwa mtungasheria, sio kitu kidogo!.
P
 
Huyo ana tofauti ndogo na Joseph kibwetele! Ingekuwa serikali nyingine muda huu angekuwa jela alisababisha hasara kwa serikali baada ya gari kuchomwa moto na watumishi kuuawa halafu unasema ana IQ kubwa Paskali umechanganyikiwa nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…