"Long Distance Relationship" yako ilidumu kwa muda gani au huataki hata kusikia mahusiano ya mbali?

Mkuu hata kama kuna kiapo cha ndoa distance marriage ni hatari sana. Binafsi niliwahi kuhamishwa kikazi kwenda mkoa X umbali wa 1200km kutoka mkoa Z familia yangu ilipo. Nafika kituo cha kazi nakabidhiwa mama wa makamo wa umri wangu ndio nifanye naye kazi mpaka over time saa nne usiku. Mkuu nilikuwa nasafiri kila bada ya wiki mbili kuja kuona familia nakaa siku nne narudi kazini ili kukwepa hatari kulingana na yule mama alivyo na mazingira ya kazi yalivyo lakini haikuwa rahisi kwa nguvu za kibinadamu..... .....
 
Nini kilitokea mkuu😁
 
Unaweza kuvumilia mnadanganyana kwenye simu kumbe mwenzio analiwa kila siku🤣🤣🤣
 
Mahusiano ya mbali ni ujinga tu, mnaaminishana vitu havipo, mnapeana hopes hazipo....hadi muonane mnatumia gharama kubwa, just kwa weekend moja ila gharama zake aaagr.

Binafsi naona hayana(ga) afya. Kwanza kuwekana tu mbinde 🤣🤣
Mtaalamu🤣🤣🤣
 
Tangu nayaanzaga huwa nachukua karibu na nyumbani, Imani yangu juu ya hawa malaika ni ndogo Sana
Ukivuka kibaha tu ushakuwa x
 
LONG DISTANCE RELATIONSHIP yangu ina miaka 20 sasa, japokuwa changamoto hazikosekani, ila naiappriciate sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…