Loren Japhet anahujumiwa sana, hii ni mara ya tatu sasa

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
20,137
Reaction score
26,189
Hapa bongo ninadiriki kusema hakuna bondia wa kizazi hiki anayehujumiwa wazi wazi kama Loren Japhet.

Kwa haraka haraka ninaweza nikakutajia fights tatu alizohujumiwa wazi wazi mpaka mashabiki tukabaki mdomo wazi.

Fight ya kwanza aliyohujumiwa bila aibu ni ile fight dhidi ya Muhsin Alkasus kwenye hii fight Muhsin alipigwa vibaya mno Yani kama punch bag jamaa alipochoka kumpiga akaanza kumchezea show gemu na wengi tuliiona kabisa jamaa amescore vya kutosha round zote cha ajabu Muhsin ndiye akatangazwa eti ndo kashinda.

Fight ya pili aliyohujumiwa ilikuwa dhidi ya Juma Choki ,hii fight mpaka sasa hakuna shabiki yoyote aliyekubaliana na uamuzi wa majaji.

Fight ya tatu ni hii ya jana dhidi ya Nasibu Ramadhan (Pacquiao) wengi ndo hapa tukabaki mdomo wazi.

Hii ni aibu sana, majaji watende haki kijana wana muhujumu sana

 

Chai
 
Mabondia wa Bongo ni Uchwara, wapo wapo tu...wengi Hawana sifa za kuwa mabondia.
 
Chai
 
Ila hili pambano lake na Nassib Ramadhan jamaa aliangushwa round ya 8, pale ndipo alipoteza ushindi,
Kwa maoni yangu mchezo ulipaswa uwe draw maana aliscore point nyingi sana ila ndio hivyo,
Japhet bado mdogo muda anao atajifunza zaidi...

Nje ya maada : nachukia pale bondia anapohojiwa baada ya pambano anaanza kutaja shukran na ahsante kwa Narcos sijui Mabibo Camp, mara Masenze, hazina maana
 
Aachane na mganga kwa sababu ni tapeli
 
Huyo jamaa ni bondia wa kawaida sana ana utoto utoto mwingi katika mapambano yake, kinqchokera juzi alikuwa ana cheza na crowd baada ya kuona kapigwa halaf bado mashabiki wanamuimba akaanza kucheza cheza kama msenge sasa ile ni trick anajarbu kuchukua jukwaa pengine akihisi labda majaji watampa jicho nonsense ....alinikera sana kwa staili ile hafiki kokote nasibu alishinda kihalali kabsa ni kua yupo serious ana utoto ulingoni.
 
Kushukuru ni muhimu mkuu
 
To me alipigwa.....

Bado anahitaji mambo kadhaa kuwa Bora ila ni mzuri sanaaa.... Ana jab nzuri mnooo na huenda ulihesabu hizo ila sikuona punch za kunishawish baada ya jab zake.
Anaweza kupiga hata triple jab ila mkono wa finishing hakuutendea haki.
 
Aache kutegemea shilingi, awatwange kwa knockout.
Badala ya kuombea shilingi imbebe, mngemshauri awe anamaliza kwa knockout, halafu muone jinsi majaji junsi watakavyo mnyonga.
 
Jitahidi piga mtu knock out kama ukiweza kuwe hakuna ubishi wala utata
 
Nassib alicheza faulo ngapi? kuna mbili za wazi wazi alimpiga mbupu mara mbili ile ya pili mpaka jamaa akapewa muda wa kupumzika unaisemeaje hio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…